Zijui Sifa kuu tatu za Kikwete

BabaH

Senior Member
Jan 25, 2008
103
8
Mwana JF mmoja kaeleza vizuri sana sifa za Raisi wa Tanzania KIKWETE.
 
Mwana JF mmoja kaeleza vizuri sana sifa za Raisi wa Tanzania KIKWETE. Naomba sana watanzania mziangalie hizi sifa za huyu muheshimiwa wetu na mlinganishe na mambo yanayoendelea hapa Tanzania jamani, Sifa binafsi za huyu bwana ni kama zifuatazo:-

  • Mnafiki - Anawachekea watanzania lakini anawaachia rafiki zake wananyonya wananchi masikini.Historia itakuja kuonyesha kwamba, dhambi nyingi zilifanywa wakati wa Mkapa, lakini nyingi zaidi zimefichuka wakati wa Kikwete kwasababu ni kiongozi dhaifu.
  • Mwoga - Anaogopa kuchukua hatua zinazostahili kwa kuhofia atawaudhi wafadhili wake ambao sasa wanajinafasi kufidia gharama zao.Haiwezekani rais ukawa na urafiki na kila mtu anayeharibu kisha usichukue hatua kali na kuziba mianya ya wizi, labda kama na wewe unanufaika.
  • Hajui la kufanya - Pamoja na yote anayojaribu kufanya ukweli ni kuwa ameishiwa ideas za kuiongoza Tanzania, amezidiwa na ukubwa wa kazi, hakutegemea kazi ya urais ni ngumu kiasi anachoshudia.

Ebu tutafakari hizi sifa za huyu kiongozi wa Mafisadi, kisha tujiulize, Je ndani ya sifa hizi, hii nchi itapona kweli au tutaishia kufika waliko ndugu etu wa Kenya jamani
Msilale watanzania tutafika mahali pabaya tusipokataa haya mambo sasa hivi. Wenzetu Kenya sasa hivi wanajuta, maana hali ni mbaya, sasa kama mnataka tufike huko endeleeni kulala tu.

Mungu waamshe watanzania, waelewe jinsi wanavyoibiwa, Mungu ibariki Tanzania.

BABAH, USAMEHEWE MAKOSA YAKO YOTE NA HATA YALE YA 'UTOTONI' KWANI HUJUI UTENDALO

SINA HAJA YA KUJUA UWEZO WAKO WA KUFIKIRI NA KUTENDA.

MH. JAKAYA KIKWETE NI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA AMBAYE AMECHAGULIWA NA KIHALALI KWA KURA ZA WANANCHI WENGI.

MOJA YA WAJIBU WANGU KAMA RAIA WA TANZANIA NI KUMHESHIMU RAIS KAMA TAASISI (HAIJALISHI HATA KAMA ANGEKUWA NI MTIKILA, MREMA AU MWINGINE YEYOTE).

FURSA INAYOPATIKANA KUPITIA JF KUTOA MAONI YAKO KWA UHURU HAIMAANISHI UNAWEZA KUPITILIZA KIASI CHA KUTOMHESHIMU RAIS WETU.

KUMBUKA DALILI ZA MTU AMBAYE HANA HESHIMA NI KUTOKUHESHIMU WENGINE.
 
Utamheshimu kama angeweza kuheshimu zile kura zote za watanzania(more than 80%).Mfano mmojawapo....kuhusu BOT Rais yuko kimya, Marekani wametoa ofa ya kumrudisha Balali, if rais angekuwa serious hata kiduchu he was supposed to take that opportunity.
Inaonesha huo uchunguzi unaofanywa ni zuga tu.
Wewe endelea kuheshimu, wahitaji kufunguliwa macho uone ukweli.
 
BABAH, USAMEHEWE MAKOSA YAKO YOTE NA HATA YALE YA 'UTOTONI' KWANI HUJUI UTENDALO

SINA HAJA YA KUJUA UWEZO WAKO WA KUFIKIRI NA KUTENDA.

MH. JAKAYA KIKWETE NI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA AMBAYE AMECHAGULIWA NA KIHALALI KWA KURA ZA WANANCHI WENGI.

MOJA YA WAJIBU WANGU KAMA RAIA WA TANZANIA NI KUMHESHIMU RAIS KAMA TAASISI (HAIJALISHI HATA KAMA ANGEKUWA NI MTIKILA, MREMA AU MWINGINE YEYOTE).

FURSA INAYOPATIKANA KUPITIA JF KUTOA MAONI YAKO KWA UHURU HAIMAANISHI UNAWEZA KUPITILIZA KIASI CHA KUTOMHESHIMU RAIS WETU.

KUMBUKA DALILI ZA MTU AMBAYE HANA HESHIMA NI KUTOKUHESHIMU WENGINE.

Wewe ndo umekosa heshima kwa waTZ na kwa Baba H.

Ni kweli hasa ile sifa ya 3 naikubali, JK anashindwa kujua wajibu na majukumu yake kama raisi. Amejaza marafiki zake kwenye uongozi, amekuwa kiongozi wa kikundi kimoja cha wanamtandao na kuna tabaka linataka kujengwa la Watawala na watawaliwa.

JK alisema hajui kinachochangia umaskini wa familia yake, katika hali hii unafitegemea atakuwa kiongozi makini? Kule chalinze alisema wanaokula hela za miradi atawataja majina yao mbele ya wananchi, so next step baada ya kuwataja? Anayo majina ya wauza madawa ya kulevya, Je hataki kuwashughulikia hadi pale vijana wetu watakapoteketetea? JK amekumbatia kundi fulani huku akikosa kipaombele katika mambo ya Taifa.
 
Heshima ninayo sana tena inawezekana hata wewe ni 5% of mine
ila ndugu yangu, Sina haja hata kidogo ya kumueshimu mtu ambaye ana upendo hata kidogo na familia zetu, na sitakaa hata siku moja nieshimu watu kama hao ndugu yangu
Wangekuwa wanajieshimu wasingekuwa wezi namna hiyo
Mwizi anajieshimu???
Unajua maana ya Heshima wewe au unaongea tu kwa sababu ndo unakoelekea huko kwenye mafisadi wenzio??

Narudia tena
Siwezi kuheshimu mwizi,wezi tena wasio na huruma ya vizazi vya tanzania bali wanajali kuvimbisha matumbo yao na kukaa kwenye makasiri yaliyojengwa kwa nguvu zetu walala hoi

This is serious, BabaH can you read what you posted here?
 
BABAH, USAMEHEWE MAKOSA YAKO YOTE NA HATA YALE YA 'UTOTONI' KWANI HUJUI UTENDALO

SINA HAJA YA KUJUA UWEZO WAKO WA KUFIKIRI NA KUTENDA.

MH. JAKAYA KIKWETE NI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA AMBAYE AMECHAGULIWA NA KIHALALI KWA KURA ZA WANANCHI WENGI.

MOJA YA WAJIBU WANGU KAMA RAIA WA TANZANIA NI KUMHESHIMU RAIS KAMA TAASISI (HAIJALISHI HATA KAMA ANGEKUWA NI MTIKILA, MREMA AU MWINGINE YEYOTE).

FURSA INAYOPATIKANA KUPITIA JF KUTOA MAONI YAKO KWA UHURU HAIMAANISHI UNAWEZA KUPITILIZA KIASI CHA KUTOMHESHIMU RAIS WETU.

KUMBUKA DALILI ZA MTU AMBAYE HANA HESHIMA NI KUTOKUHESHIMU WENGINE.

Heshima ni kutu cha bure.

Mtu haombi kuheshimiwa ila anapewa heshima kutokana na yale aifanyiyayo jamii.
Kwa sababu tu Kikwete ni Rais basi anastahili heshima! Naona wewe unalivuruga na kuligaragaza neno hili kwenye tope.
Kuna wazee wengi pale Tanzania wanaheshiwa sana kiasi kwamba wakiingia kwenye Baraza matusi na kejeli za kijinga zinakoma, lakini wazee hao hata vyeo vya ujumbe wa nyumba 10 hawana.

Ukiona Rais wa nchi anabezwa, kitu cha maana ni kujiuliza swali kwa nini Rais anabezwa kuliko kuwaona wale wammbezao wana walakini.
Heshima kitaendelea kuwa kitu cha Bure kabisa kwa mtu yeyote bila kujali cheo chake.
 
....tunamuheshimu Rais Zaidi Kama Anakuwa Mkweli...taassisi Ya Urais Ni Ya Kuheshimika..na Zaidi Ianze Kuheshimiwa Na Anayeikalia..nina Mashaka Kuwa Jk Anaheshimu Taasisi Hii..na Kama Anajua Dhima Ya Kuwa Rais...

Leo Naona Alipoongelea Bot Anakazania Kutia Huruma Kuwa Watu Waache Uzushi.....anasahau Kuwa Hii Kashfa Ilipoibuliwa Yeye Na Spika Wake Walisema Ni Uzushi Wa Wapinzani....sasa Kama Imedhibitika Ni Kweli ..atatushawishi Vipi Tuone Maneno Yanayosemwa Na Wapinzani Ni Uzushi....wakati Mara Zote Madai Yao Yamedhibitika Kuwa Ukweli?
 
BABAH, USAMEHEWE MAKOSA YAKO YOTE NA HATA YALE YA 'UTOTONI' KWANI HUJUI UTENDALO

SINA HAJA YA KUJUA UWEZO WAKO WA KUFIKIRI NA KUTENDA.

MH. JAKAYA KIKWETE NI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA AMBAYE AMECHAGULIWA NA KIHALALI KWA KURA ZA WANANCHI WENGI.

MOJA YA WAJIBU WANGU KAMA RAIA WA TANZANIA NI KUMHESHIMU RAIS KAMA TAASISI (HAIJALISHI HATA KAMA ANGEKUWA NI MTIKILA, MREMA AU MWINGINE YEYOTE).

FURSA INAYOPATIKANA KUPITIA JF KUTOA MAONI YAKO KWA UHURU HAIMAANISHI UNAWEZA KUPITILIZA KIASI CHA KUTOMHESHIMU RAIS WETU.

KUMBUKA DALILI ZA MTU AMBAYE HANA HESHIMA NI KUTOKUHESHIMU WENGINE.

...watu kama hawa ndio matatizo makubwa kuliko hata kina kikwete wenyewe na huyu hafai hata kuitwa mpambe wala fisadi maana ni wa kumwonea huruma tuu.
 
BABAH, USAMEHEWE MAKOSA YAKO YOTE NA HATA YALE YA 'UTOTONI' KWANI HUJUI UTENDALO

SINA HAJA YA KUJUA UWEZO WAKO WA KUFIKIRI NA KUTENDA.

MH. JAKAYA KIKWETE NI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA AMBAYE AMECHAGULIWA NA KIHALALI KWA KURA ZA WANANCHI WENGI.

MOJA YA WAJIBU WANGU KAMA RAIA WA TANZANIA NI KUMHESHIMU RAIS KAMA TAASISI (HAIJALISHI HATA KAMA ANGEKUWA NI MTIKILA, MREMA AU MWINGINE YEYOTE).

FURSA INAYOPATIKANA KUPITIA JF KUTOA MAONI YAKO KWA UHURU HAIMAANISHI UNAWEZA KUPITILIZA KIASI CHA KUTOMHESHIMU RAIS WETU.

KUMBUKA DALILI ZA MTU AMBAYE HANA HESHIMA NI KUTOKUHESHIMU WENGINE.

Pole sana wewe ambaye bado ni miongoni mwa Watanzania wanaoendekeza "ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA MWENYEKITI WA CHAMA" Rais ni Binadamu kama binadamu wengine, heshima yake anaijenga au kuibomoa mwenyewe kutokana na matendo yake. Sifa zote tatu zimemkaa Kikwete. Na Bado kufikia 2010, Heshima yake itakuwa imekwenda HASI.
 
umesahau swala la uongo, ubabaikaji kwa mataifa makubwa duniani, uwezo mdogo wa fikira, na mengine mengi sana
 
Mimi nadhani ni kashfa mbaya kumtusi Mh Rais. Kipindi alichoongoza ni kifupi sana kuzidi matarajio yetu. Kwa kuwa tulimchagua sisi wenyewe kwa ridhaa yetu tusubiri huku tukitekeleza majukumu yetu katika kulijenga taifa hili lililomalizwa na mafisadi. Amen
 
Heshima ni kutu cha bure.

Mtu haombi kuheshimiwa ila anapewa heshima kutokana na yale aifanyiyayo jamii.
Kwa sababu tu Kikwete ni Rais basi anastahili heshima! Naona wewe unalivuruga na kuligaragaza neno hili kwenye tope.
Kuna wazee wengi pale Tanzania wanaheshiwa sana kiasi kwamba wakiingia kwenye Baraza matusi na kejeli za kijinga zinakoma, lakini wazee hao hata vyeo vya ujumbe wa nyumba 10 hawana.

Ukiona Rais wa nchi anabezwa, kitu cha maana ni kujiuliza swali kwa nini Rais anabezwa kuliko kuwaona wale wammbezao wana walakini.
Heshima kitaendelea kuwa kitu cha Bure kabisa kwa mtu yeyote bila kujali cheo chake.

....tunamuheshimu Rais Zaidi Kama Anakuwa Mkweli...taassisi Ya Urais Ni Ya Kuheshimika..na Zaidi Ianze Kuheshimiwa Na Anayeikalia..nina Mashaka Kuwa Jk Anaheshimu Taasisi Hii..na Kama Anajua Dhima Ya Kuwa Rais...

Leo Naona Alipoongelea Bot Anakazania Kutia Huruma Kuwa Watu Waache Uzushi.....anasahau Kuwa Hii Kashfa Ilipoibuliwa Yeye Na Spika Wake Walisema Ni Uzushi Wa Wapinzani....sasa Kama Imedhibitika Ni Kweli ..atatushawishi Vipi Tuone Maneno Yanayosemwa Na Wapinzani Ni Uzushi....wakati Mara Zote Madai Yao Yamedhibitika Kuwa Ukweli?

...watu kama hawa ndio matatizo makubwa kuliko hata kina kikwete wenyewe na huyu hafai hata kuitwa mpambe wala fisadi maana ni wa kumwonea huruma tuu.

Mugo"The Great";133201 said:
Pole sana wewe ambaye bado ni miongoni mwa Watanzania wanaoendekeza "ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA MWENYEKITI WA CHAMA" Rais ni Binadamu kama binadamu wengine, heshima yake anaijenga au kuibomoa mwenyewe kutokana na matendo yake. Sifa zote tatu zimemkaa Kikwete. Na Bado kufikia 2010, Heshima yake itakuwa imekwenda HASI.

umesahau swala la uongo, ubabaikaji kwa mataifa makubwa duniani, uwezo mdogo wa fikira, na mengine mengi sana

Jazba, Chuki binafsi, husda na ukosefu wa hekima na busara vimetanda hapa JF.
Lakini kwa kifupi ni kuwa mama yako akishakwambia huyu ndiyo baba yako huna budi kumheshimu.
As long as watanzania walimchagua Mh. Kikwete kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hamna budi kumheshimu kama RAIS.

Kamwe sitakaa kimya kuona Rais wa nchi yangu anadhalilishwa kwani ni wajibu wangu kutetea taifa langu.
Nitailinda nchi yangu Tanzania na nitawaheshimu viongozi waliopewa dhamana na wananchi.
Nitailinda nchi yangu na kuitetea wakati wote dhidi ya wadhalimu wachache.
Nitajitahidi kujadiliana juu ya mustakabali wa nchi hii kwa uwazi bila ya kudharau mamlaka zote halali zilizowekwa kwa ridhaa ya wananchi
Ninaipenda nchi yangu na ninajivunia kuwa Mtanzania.

Mungu tuongeze hekima na busara watanzania na uibariki nchi yetu na wananchi wake.
 
"Flaming enthusiasm, backed by horse sense and persistence, is the quality that most frequently makes for success."
 
Usanii mwngine wa JK. Awaondoe wote wafanyabiashara,tunaanza na Karamagi na Mramba
Nataka mawaziri, wabunge wasifanye biashara-JK

Na Joseph Mwendapole

Source: NIPASHE
Rais Jakaya Kikwete, amesema anakusudia kufanya marekebisho ya Sheria ya Maadili ya Uongozi ili kuwazuia mawaziri na wabunge kujihusisha na biashara.

Amesema upo ushahidi wa kuwepo migongano ya maslahi kwa baadhi ya viongozi ambao wanajihusisha na masuala ya biashara.

Rais aliyasema hayo jana katika hotuba yake ya kila mwezi.
Aidha, alisema nchi balimbali hasa za kibepari zina taratibu nzuri za kushughulikia hali hiyo.

\"Wenzetu wanao utaratibu unaomtaka mtu mwenye shughuli za kibiashara anapokuwa Mbunge au Waziri kuacha kujishughulisha na biashara zake Ni makusudio yangu kuwa utaratibu huu tuuanzishe hapa nchini.

Viongozi wetu wachague kufanya jambo moja kwa wakati mmoja ama biashara au Ubunge na Uwaziri,`` alisema.

Alisema hata pale ambapo hakuna dalili za wazi za kiongozi kujihusisha na biashara, hisia za kupata manufaa yanayotokana na nafasi zao hutawala na matokeo ya yote hayo ni watu kupoteza imani na kutilia shaka uadilifu wa viongozi,`` alisema.

Alisema kuna haja ya kuwepo utaratibu rasmi unaotambuliwa kisheria wa wadhamini wanaoendesha shughuli za biashara bila viongozi hao kujihusisha nazo.

Alisema mbunge na waziri anapoacha uongozi wa siasa kama atapenda atachukua tena mali yake na kuendelea na shughuli zake.

``Kwa ajili hiyo ni makusudio yangu kuanzisha mchakato wa kufanya marekebisho ya Sheria ya Maadili ya Uongozi ili tuingize utaratibu huo,`` alisema.

Alisema hilo ni jambo lenye maslahi kwa Taifa na litasaidia kujenga heshima ya viongozi wa umma mbele ya macho ya wananchi.

Alisema suala hilo pia limezungumzwa katika kikao maalum cha Kamati Kuu ya CCM kilichofanyika Dodoma.

SOURCE: Nipashe
 
Jazba, Chuki binafsi, husda na ukosefu wa hekima na busara vimetanda hapa JF.
Lakini kwa kifupi ni kuwa mama yako akishakwambia huyu ndiyo baba yako huna budi kumheshimu.
As long as watanzania walimchagua Mh. Kikwete kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hamna budi kumheshimu kama RAIS.

Kamwe sitakaa kimya kuona Rais wa nchi yangu anadhalilishwa kwani ni wajibu wangu kutetea taifa langu.
Nitailinda nchi yangu Tanzania na nitawaheshimu viongozi waliopewa dhamana na wananchi.
Nitailinda nchi yangu na kuitetea wakati wote dhidi ya wadhalimu wachache.
Nitajitahidi kujadiliana juu ya mustakabali wa nchi hii kwa uwazi bila ya kudharau mamlaka zote halali zilizowekwa kwa ridhaa ya wananchi
Ninaipenda nchi yangu na ninajivunia kuwa Mtanzania.

Mungu tuongeze hekima na busara watanzania na uibariki nchi yetu na wananchi wake.

What a joke!!!!
 
Ahsanteni kwa michango yenu mizuri. U guys are very right. Kikwete angetaka heshima angejiheshimu yeye kwanza kabla ya sisi kumheshimu. Afterall kuyasema yale mtu anayoyafanya sidhani kama ni kutomheshimu kwani ndio wasifu wake Kikwete.

Kikwete amesahau kwamba hii nchi na hiyo nafasi ya urais amepewa na watanzania kwani amefanya hii nchi ya kikundi fulani kidogo ambacho kinaweza kufanya lolote juu ya rasilimali zetu na asiwepo wa kuwafanya lolote. Kikundi hichio ni cha yeye kikwete,el,rostam,kadamage,mramba,meghji na wengine. Ni ngumu kuamini kwamba mtu kama meghji,mramba na rostam bado wanapeta. Meghji na Mramba kwa kashfa ya EPA na rostam kwa kutajwa kwenye report ya CAG kwa kuliibia taifa bil 6 kupitia makampuni yake. Hakuna wa kuwachukulia hatua kwani kikwete ni mwenzao.

Na haya maigizo ya audit report ya E&Y ndio yanazidi kumdhalilisha jk bahati mbaya kwamba yy halioni hilo.Its fun kwamba report unayo badala ya kuchukua hatua kama rais unaunda tume nyingine kuchunguza uchunguzi kwa gharama ya wale wale walioibiwa bil 133. Huu utoto na upuuzi mpaka lini jamani?

Mbali kusema atawatangaza hadharani (rais anasema utumbo kama huu sijui ni nani wa kuchukua hatua) wezi wa miradi ya wananchi alishawahi kusema anawafahamu wala rushwa anawapa muda wajirekibishe-Huyu ni rais au msanii tu fulani wandugu??. So TAKUKURU wanachofanya ni kumpelekea majina then jk anawapa muda wajirekibishe mpaka lini na nini kitakuwa kimebaki no one knows. Hv hawa vibaka mtaani nani atawapa muda?
 
Jazba, Chuki binafsi, husda na ukosefu wa hekima na busara vimetanda hapa JF.
Lakini kwa kifupi ni kuwa mama yako akishakwambia huyu ndiyo baba yako huna budi kumheshimu.
As long as watanzania walimchagua Mh. Kikwete kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hamna budi kumheshimu kama RAIS.

Kamwe sitakaa kimya kuona Rais wa nchi yangu anadhalilishwa kwani ni wajibu wangu kutetea taifa langu.
Nitailinda nchi yangu Tanzania na nitawaheshimu viongozi waliopewa dhamana na wananchi.
Nitailinda nchi yangu na kuitetea wakati wote dhidi ya wadhalimu wachache.
Nitajitahidi kujadiliana juu ya mustakabali wa nchi hii kwa uwazi bila ya kudharau mamlaka zote halali zilizowekwa kwa ridhaa ya wananchi
Ninaipenda nchi yangu na ninajivunia kuwa Mtanzania.

Mungu tuongeze hekima na busara watanzania na uibariki nchi yetu na wananchi wake.

Another Scandal,hawa ndio waliolishwa yamini,It is a symbol of Al Fasad.Mungu atuepushie Mbali watu kama hawa.Kama ungejua utumbo unaofanyika usingesema haya.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom