Zijue TV Bora za 4k na 1080p zinazofanya vizuri kwenye soko la dunia hivi sasa

Michael Amon

JF-Expert Member
Dec 22, 2008
8,775
3,610
Kuwa TV si kazi ngumu lakini kazi ni kuchagua TV iliyo bora kulingana na bajeti yako. Kwa kuliona hilo nimeamua kufanya utafiti na kuchagua TV zilizo bora kulingana mahitaji na kipato cha Watanzania kama nitakavyoanisha hapo chini:

TV Bora za 4k UHD
1. LG EF9500
Hii ni smart tv inayotumia teknolojia ya OLED ambayo inafanya TV hii iweze kuonyesha picha yenye ubora wa hali ya juu kuliko TV zote. TV nzuri sana na inaonyesha picha vizuri sana hata kwenye giza au hata kama mtazamaji akikaa kwenye kona ya TV.

Tatizo kubwa la hii TV ni bei, hivyo TV hii inaweza isiwafae watu wengi. Lakini kama uwezo wako wa kifedha unaruhusu basi nakushauri uichukue TV hii.
medium01.jpg
BEI: Bei ya TV hii inaanzia $1800 kwa 55 inch.

2. VIZIO P SERIES

Najua wengi mtakuwa hamuifahamu kampuni ya VIZIO kwa sababu wafanyabiashara wa Tanzania bado hawajagundua ubora wa hizi TV na kuamua kuanza kuziuza huku Tanzania. Ila kwa ufupi tu, VIZIO ni kampuni ya kutengeneza TV iliyopo marekani ambayo inatengeneza TV bora na kuziuza kwa bei nafuu ukilinganisha na kampuni nyingine kama Samsung, LG, Panasonic, Sony n.k. Kampuni hii imekuwa ikijishindia tuzo ya kutengeneza TV bora na za bei nafuu karibu kila tangu nilipoanza kuzifahamu. TV ya Vizio P Series ni TV nzuri sana na inaonyesha picha vizuri sana hata kwenye giza na hii ni kutokana na hii TV kutumia teknolojia ya full array local dimming backlight na Hidh Dyanamic Range na kubwa kuliko kuliko zote, ukinununu TV unapata na tablet ndogo ambayo utaitumia kama remote ya TV yako.

front_hero_2_1_1_1.jpg


BEI: Bei ya TV hii inaanzia $999 kwa 50 inch.

3. Samsung KS8000
TV ya Samsung KS8000 ni TV nzuri sana na inaonyesha picha vizuri sana hasa kwenye sehemu zenye mwanga mkali, lakini TV hii si nzuri sana kwa kuangalia kwenye giza.

600x600.png

BEI:
Bei ya TV hii inaanzia $1,297 kwa 49 inch.

4. Sony X810C
Sony X810C ni TV inayoonyesha vizuri sana ukilinganisha na bei yake. Ni TV inayoonyesha vizuri sana kwenye mwanga na kwenye giza pia.
81yFv5%2BEOiL._SL1500_.jpg
BEI: Bei ya TV hii inaanzia $850 kwa 55 inch.

5. VIZIO D SERIES
Naam, kwa mara nyingine tena Kampuni ya Vizio imerudi kwenye list, na hii ni kutokana na ubora wa hizi TV na unafuu wake. TV hii inaonyesha picha nzuri na inauzwa kwa bei ambayo wewe mpenzi wa 4k TV unaweza kuimudu. Kwa ufupi tu naweza kusema TV hii ni the best katika ubora na bei.

duhd-front_4.jpg

BEI: Bei ya TV hii inaanzia $430 kwa 40 inch.

Baadae nikipata wasaa nitakuja kuandika TV bora za 1080p FHD.
 
Hii vizio nilikutana nayo eBay, inauzwa kwa bei nzuri sana

Naam, zinauzwa kwa bei nzuri sana sema tatizo ukiagiza nje utakuja kuumia kwenye shipping maana kusafirisha TV kwa ndege ni very expensive. Unaweza kuinunua TV kwa dola $430 lakini ikakugharimu kuisafirisha kwa $600 mpaka $1300 unless upate mtu ambaye anasafirisha mizigo yake kwa meli ndo uipachike kwenye kontena lake kuokoa gharama. Otherwise ni maumivu tu.
 
Naam, zinauzwa kwa bei nzuri sana sema tatizo ukiagiza nje utakuja kuumia kwenye shipping maana kusafirisha TV kwa ndege ni very expensive. Unaweza kuinunua TV kwa dola $430 lakini ikakugharimu kuisafirisha kwa $600 mpaka $1300 unless upate mtu ambaye anasafirisha mizigo yake kwa meli ndo uipachike kwenye kontena lake kuokoa gharama. Otherwise ni maumivu tu.
Kama hautojali kwa upande wangu naomba uniorodheshee list ya teknolojia inayotumika katika utengenezaji wa tv na sifa zake. Kuanzia zile za vichogo hadi teknolojia ya leo inayotumika. Kila nikiienda dukani kila tv ina maandishi ya LED TV 1080p au utra slim kama sijakosea. Natafuta mtu wa kunipa elimu hiyo.
 
4K ziko poa sana, tatizo ni content tu, hakuna 4K content nyingi zinabaki kua upscaled 1080p, na bongo yetu hii hata kukiwa na 4K content, hakuna internet iliyo kasi kuweza kustream bila issues, zilizopo ni very costful. I wish mkongo wa FibreOptic ungeunganishwa nyumba hadi nyumba tupate hizo unlimited 1Gbps za kulipia once kila mwezi.
 
Ubaya wa hizo Vizio hawana ofisi bongo. Ukipata nayo tatizo itakusumbua sana.

Yep. Hilo ni kweli kabisa. Natamani sana kama wengezileta na huku bongo. Zingeuzika sana hasa kutokana na ubora wake na gharama yake nafuu.
 
1. LG EF9500 ndo TV ninayotumia, 65 inches, top of the line OLED 4K.

Halafu 4K HDR player ya Samsung, hapo ukipata movie ya 4K, umekamilisha mchezo wa 4K.
 
Hizo vizio zipo njema sana eeh?
So far nakubaliana nawe kwa mkorea LG akifuatiwa na Samsung nishazishuhudia screen zao ni kisanga!
 
4K ziko poa sana, tatizo ni content tu, hakuna 4K content nyingi zinabaki kua upscaled 1080p, na bongo yetu hii hata kukiwa na 4K content, hakuna internet iliyo kasi kuweza kustream bila issues, zilizopo ni very costful. I wish mkongo wa FibreOptic ungeunganishwa nyumba hadi nyumba tupate hizo unlimited 1GBPs za kulipia once kila mwezi.
Sasa hivi zimeanza kutoka movies za 4k, halafu kuna 4K player.

Mi nina movie kadhaa za 4k na Samsung 4k player na hiyo LG ya kwanza hapo juu 65 inches.

Kwa hiyo hata kama Netflix wana matatizo naweza kuangalia 4K movie kama unavyoangalia Bluray.

Content bado, lakini movies mpya zinatoka kwenye 4k.

Kiwanja lakini, bongo nafikiri bado sana.
 
Sasa hivi zimeanza kutoka movies za 4k, halafu kuna 4K player.

Mi nina movie kadhaa za 4k na Samsung 4k player na hiyo LG ya kwanza hapo juu 65 inches.

Kwa hiyo hata kama Netflix wana matatizo naweza kuangalia 4K movie kama unavyoangalia Bluray.

Content bado, lakini movies mpya zinatoka kwenye 4k.

Kiwanja lakini, bongo nafikiri bado sana.

Pia tatizo movie za 4k kwa sasa file zake ni kubwa sana, yani movie moja inweza kwenda hata had 40 GB. But i know soon or later they will find a way to optimize 4k content ili file size yake iwe ndogo just like the way they did with 1080p content.
 
Pia tatizo movie za 4k kwa sasa file zake ni kubwa sana, yani movie moja inweza kwenda hata had 40 GB. But i know soon or later they will find a way to optimize 4k content ili file size yake iwe ndogo just like the way they did with 1080p content.
Yeah. Ukiongeza resolution na file size inaongezeka kwa sababu unabeba more data. They are probably looking for a technology to compress better.

Lakini ukinunua hizo 4K disc kama nilizozisema hapo juu unaondokana na tatizo hili kwa sababu unakuwa hu download movie. Unaicheza katika 4K player. Unatumia player ya 4k (not upscaling, actual 4k player kama hii ya Samsung niliyo nayo) una play kwenye 4k TV, ukitumia disc ya 4k. Umemaliza mchezo. Hakuna haja ya kuhofia file size kwa sababu hu download kitu kutoka kwenye internet.

Gradually kutakuwa na content zaidi online na internet soeeds zitakuwa nzuri zaidi.

By then wataleta kitu kipya kitakachotaka tu upgrade tena.
 
Pia tatizo movie za 4k kwa sasa file zake ni kubwa sana, yani movie moja inweza kwenda hata had 40 GB. But i know soon or later they will find a way to optimize 4k content ili file size yake iwe ndogo just like the way they did with 1080p content.
mbona technology zipo siku nyingi tu, vp9 na x265(HEVC). unaposearch/tafuta movie husika eka neno x265 kwa mbele, zipo movie za 4k hadi 2gb
https://kickass.immunicity.host/usearch/4k x265
 
Back
Top Bottom