Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

TANESCO

Official Account
Jul 12, 2014
4,584
2,104
HATUA YA KWANZA

MAOMBI YA MWANZO


Je mteja anaweza kuchukua fomu ofisi yeyote ya tanesco?

Mteja anaweza kuchukua fomu ya maombi ya umeme katika ofisi yeyote ya shirika bila kujali kuwa eneo hilo linahudumiwa na ofisi husika. Ila atapaswa kurudisha ofisi ya maeneo ambayo makazi yake yapo ili kurahisisha kufanyiwa vipimo (service line survey)

JE KUNA GHARAMA ZOZOTE KATIKA UCHUKUAJI WA FOMU?

Fomu za maombi ya umeme zinatolewa bure kabisa kwa wateja wote.

VITU MUHIMU VYA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHUKUA FOMU

1. Hakikisha umeme umefika maeneo yako na kama ni mradi uwe umekamilika.

2. Hakikisha mtandao wa nyaya ndani ya nyumba yako (wiring) umefanyika kupitia mkandarasi aliyesajiliwa.

3. Kitambulisho kinachomtambulisha muombaji wa umeme mfano leseni ya udereva, hati ya kusafiria, kitambulisho cha kazi (hii inasaidia shirika kumtambua mteja husika)

4. Kwa mwombaji wa mita ya ziada (meter separation) jina litakalotumika ni la mwenye nyumba kama linavyosomeka katika mita ya awali. Vinginevyo mteja atapaswa kutumia uthibitisho wa ruhusa ya mwenyenyumba kama atakuwa ni mpangaji. Lazima mteja aje na namba ya mita (kama zipo zaidi ya moja aje nazo zote) ili kuhakiki kama kuna yenye deni.


5. Kwa waombaji wanaomba kwa ajili ya ofisi, makapuni au taasisi za serikali au binafsi anapaswa kuja na leseni ya biashara, tin namba, udhibitisho wa usajili wa kampuni. Au udhibitisho wa ofisi ya serikali husika.

6. Kwa wapangaji wa nyumba za taasisi au makampuni waje na barua za waliopangisha zinazoonyesha kuwe wenye nyumba hizo wameridhia mita husika iwe na jina la mpangaji husika.

7. Shirika linapenda kuwaomba wamiliki wa nyumba kupenda kufika ofisi zetu wenyewe ili kuzuia udanganyifu ambao umekuwa ukifanywa na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu

HATUA YA PILI KUWEKA MCHORO, PICHA NA KUINGIA MAKUBALIANO YA KUFUNGIWA UMEME NAKUREJESHA FOMU

Endapo mteja atakidhi vigezo na masharti ya hatua ya mwanzo na kupatiwa fomu ya maombi ya mwanzo anatakiwa afanye yafuatayo

1. Kuisoma fomu kwa umakini mkubwa na kukubailiana na vigezo namba moja mpaka kumi na mbili. Mteja akijiridhisha kuwa amekubaliana na masharti yote ataweka sahihi sehemu husika (ukurasa wa pili wa fomu ya maombi ya umeme)

2. Kumpatia mkandarasi aliyesajiliwa ili achore mchoro wa mtandao wa nyaya (wiring diagram) wa nyumba husika pamoja na kugonga muhuri. (gharama ni makubaliano baina ya mteja na mkandarasi husika), wakandarasi wanapatikana kwenye ofisi zao maeneo mbalimbali, orodha ya waliosajiliwa pia inapatikana kwenye ofisi za tanesco. Mteja anapaswa kupewa orodha na kuchagua mkandarasi anayemtaka yeye.

3. Mteja atapaswa kuweka picha moja ya mwombaji wa umeme

4. Kisha mteja atarudisha fomu hiyo iliyokamilika ofisi ya eneo ambalo makazi yake yako (inayomudumia)

HATUA YA TATU- KUFANYIWA VIPIMO (SURVEY)

Mara baada ya mteja kurejesha fomu iliyojazwa kikamilifu, mteja atapangiwa tarehe ya kufanyiwa vipimo (survey). Mafundi watafika kwenye nyumba au sehemu inayoombewa umeme ili kutathimini gharama atakazolipia mteja kwa kuzingatia umbali wa eneo ilipo miundombinu ya umeme kama nguzo na transfoma na uwezo wa umeme huo kuunganisha kwa wateja wapya.

HATUA YA NNE: - KUPATIWA MAKADIRIO YA GHARAMA KIASI GANI ALIPE ILI AFUNGIWA UMEME

Mara baada ya kufanyiwa tathimini mteja anaweza kupatiwa makadirio ya gharama ya kiasi gani alipe ili kufungiwa umeme. Makadirio haya huweza kutumwa kwa njia ya nukushi, ujumbe mfupi wa meneno, barua pepe au mteja kufika ofisini na kuchukua barua. Viwango vya muda wa kutoa makadirio kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini:

MAELEZO

Muda wa makadirio

Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)

Ndani ya siku 7 za kazi

Ujenzi wa njia ya nyongeza unahitajika (mita 30- 100)

Ndani ya siku 10 za kazi

Kama mfumo mpya wa usambazaji unahitajika kujegwa au mfumo wa umeme mkubwa unahitajika kuongezwa kwa ajili ya kiwanda au biashara kubwa (kama hakuna mfumo wa kumuunganishia mwombaji) (zaidi ya mita 100)

Ndani ya siku 14 za kazi

HATUA YA TANO: - KUFANYA MALIPO

Mteja atafika ofisi ya tanesco ili kupatiwa namba ya kumbukumbu (reference number) itakayomuwezesha kufanya malipo bank, mteja atafanya malipo na atapatiwa stakabadhi ya malipo bank (risiti kwa njia ya ujumbe mfupi- sms) (kwa sasa ni bank ya nmb tu), wateja wanahimizwa kufanya malipo yote bank na si kwa mtu mwingine yeyote. Malipo yote yatakayofanyika nje ya mfumo uliwekwa hayatambulika na tanesco. Mteja akishafanya malipo bank husika hatatakiwa kurudi tena tanesco bali tanesco watakuwa na taarifa zake zote na kinachofuata ni kumfungia umeme.

HATUA YA SITA:-KUUNGANISHIWA UMEME

Mara baada ya mteja kufanya malipo viwango vya muda wa kumfungia umeme vitakuwa kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali hapo chini.

MAELEZO

Muda wa kufungiwa

Kama miundombinu iliyopo itatumika (ndani ya mita 30 kutoka kwenye nguzo iliyokaribu)

Ndani ya siku 30 za kazi

Ujenzi wa njia ya nyongeza itahitajika

(mita 30- 100)

Ndani ya siku 60 za kazi

KAMA MFUMO MPYA WA USAMBAZAJI UNAHITAJIKA KUJEGWA AU MFUMO WA UMEME MKUBWA UNAHITAJIKA KUONGEZWA KWA AJILI YA KIWANDA AU BIASHARA KUBWA (KAMA HAKUNA MFUMO WA KUMUUNGANISHIA MWOMBAJI) (ZAIDI YA MITA 100)

Ndani ya siku 90 za kazi

KWA MAULIZO WASILIANA NASI

Kituo cha huduma kwa wateja: - 0768985100/0222194400

Barua pepe: customer.Service@tanesco.Co.Tz

Facebook: www.Facebook.Com/tanesco yetu

Twitter: - www.Twitter.Com/tanesco yetu

Tovuti; www.Tanesco.Co.Tz
 
Hebu waonje sasa wameweka vionjo vipya
Wapuuzi kabisa mkuu, wamepitisha main line eneo yalipo makazi yangu leo mwaka wa tano hawataki kutandaza nyaya ndogo lakini badala wameenda kutandaza eneo la mbele.

Yaan assume starting point ni A then unaenda B, C, D etc sasa wao wameenda kutandaza point D na kuruka B na C. Hapa utawaelewa?
 
Mnazingua sana nyinyi Tanesco, niliomba kufungiwa umeme nikazungushwa kwa zaidi ya miezi sita, mara ooh kuna wateja wengi yaani visababu kibao!
Na sababu kubwa ilikuwa ni wahusika kutengeneza mazingira ya rushwa...
 
Naomba nitoke kidogo nje ya mada nitoe malalamiko yangu,Mimi Niko Iringa nimeandika barua kuomba kuomba Tanesko waondoe waya za umeme zilizopita juu ya nyumba yangu mpaka Leo ni danadana tu.pili niliwataarifu kuwa nguzo ilioshika waya hizo si salama kwa kuwa eneo lake kubwa limechimbwa.mpaka leo hakuna kilichoendelea.Haya no baadhi ya mambo ambayo yanalichafua shirika la umeme.

Sent from my TECNO_N9 using JamiiForums mobile app
 
Wapuuzi kabisa mkuu, wamepitisha main line eneo yalipo makazi yangu leo mwaka wa tano hawataki kutandaza nyaya ndogo lakini badala wameenda kutandaza eneo la mbele.

Yaan assume starting point ni A then unaenda B, C, D etc sasa wao wameenda kutandaza point D na kuruka B na C. Hapa utawaelewa?
Fika ofisin tafadhali mpendwa mteja
 
Naomba usikimbie. Tujibu baadhi ya maswali japo machache:

1. Ni meter angapi maximum mtu atahitaji nguzo? (Yaani nguzo iliyopo hadi kufika ktk nyumba). Naomba maelezo hapa, kwani hapa ndio mafundi wa TANESCO hutupigia hela. mf ni 30m -70m au 30m to 100m? au 30-70m ni kile chuma tu bila nguzo kati ya 30m -100m?
2. Je ni sahihi ktk mfumo wa leo mtu kufunga/kuweka Cut-Out ktk meter kabla ya umeme kuingia ndani? (Japo ndani kutafungwa Circuit Breaker)
3. Naskia sijui Two Phases au Single Phase. Je ni mfumo upi ni mzr kwa matumizi ya nyumba ya makazi?

Note: Umesema Jedwali, lipo wapi sasa?
 
Gharama ya separeti mita za chumba kimoja zipo, na kama zipo ni kiasi gani mteja anatakiwa kulipa ila afanye matumizi ya kiwango cha chini cha nyumbani?
 
Asanteni kwa ufafanuzi mzuri, naombeni mnisaidie swali hili hapa chini,
Kwasasa mimi nipo dodoma, ila nina nyumba ipo dar nimeshafanya wire-ring tayari ila process za mchoro bado, je kama process za kuomba umeme nikizifanyia uku dodoma, na mambo ya mchoro nikayafanyia uku uku itawezekana?
 
HATUA YA KWANZA-:- MAOMBI YA MWANZO

JE MTEJA ANAWEZA KUCHUKUA FOMU OFISI YEYOTE YA TANESCO?

MTEJA ANAWEZA KUCHUKUA FOMU YA MAOMBI YA UMEME KATIKA OFISI YEYOTE YA SHIRIKA BILA KUJALI KUWA ENEO HILO LINAHUDUMIWA NA OFISI HUSIKA. ILA ATAPASWA KURUDISHA OFISI YA MAENEO AMBAYO MAKAZI YAKE YAPO ILI KURAHISISHA KUFANYIWA VIPIMO (SERVICE LINE SURVEY)

JE KUNA GHARAMA ZOZOTE KATIKA UCHUKUAJI WA FOMU?

FOMU ZA MAOMBI YA UMEME ZINATOLEWA BURE KABISA KWA WATEJA WOTE.

VITU MUHIMU VYA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHUKUA FOMU

1. hakikisha umeme umefika maeneo yako na kama ni mradi uwe umekamilika.

2. hakikisha mtandao wa nyaya ndani ya nyumba YAKO (wiring) UMEFANYIKA KUPITIA mkandarasi aliyesajiliwa.

3. KITAMBULISHO KINACHOMTAMBULISHA MuOMBAJI WA UMEME Mfano LESENI YA UDEREVA, HATI YA KUSAFIRIA, KITAMBULISHO CHA KAZI (HII INASAIDIA SHIRIKA KUMTAMBUA MTEJA HUSIKA)

4. KWA MWOMBAJI WA MITA YA ZIADA (METER SEPARATION) JINA LITAKALOTUMIKA NI LA MWENYE NYUMBA KAMA LINAVYOSOMEKA KATIKA MITA YA AWALI. VINGINEVYO MTEJA ATAPASWA KUTUMIA UTHIBITISHO WA RUHUSA YA MWENYENYUMBA KAMA ATAKUWA NI MPANGAJI. LAZIMA MTEJA AJE NA NAMBA YA MITA (KAMA ZIPO ZAIDI YA MOJA AJE NAZO ZOTE) ILI KUHAKIKI KAMA KUNA YENYE DENI.


5. kwa waombaji wanaomba kwa ajili ya ofisi, MAKAPUNI au taasisi za serikali au binafsi anapaswa kuja na leseni ya biashara, TIN NAMBA, UDHIBITISHO wa usajili wa kampuni. AU UDHIBITISHO WA OFISI YA SERIKALI HUSIKA.

6. kwa wapangaji wa nyumba za taasisi au makampuni waje na barua za waliopangisha zinazoonyesha kuwe wenye nyumba hizo wameridhia mita husika iwe na jina la mpangaji husika.

7. shirika linapenda kuwaomba wamiliki wa nyumba kupenda kufika ofisi Zetu wenyewe ili kuzuia udanganyifu ambao umekuwa ukifanywa na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu

HATUA YA PILI KUWEKA MCHORO, PICHA NA KUINGIA MAKUBALIANO YA KUFUNGIWA UMEME NAKUREJESHA FOMU

endapo mteja atakidhi vigezo na masharti ya hatua ya mwanzo na kupatiwa fomu ya maombi ya mwanzo anatakiwa afanye yafuatayo

1. kuisoma fomu kwa umakini mkubwa na kukubailiana na vigezo namba moja mpaka kumi na mbili. mteja akijiridhisha kuwa amekubaliana na masharti yote ataweka sahihi sehemu husika (ukurasa wa pili wa fomu ya maombi ya umeme)

2. kumpatia mkandarasi aliyesajiliwa ili achore mchoro wa mtandao wa nyaya (WIRING DIAGRAM) wa nyumba husika pamoja na kugonga muhuri. (gharama ni makubaliano baina ya mteja na mkandarasi husika), wakandarasi wanapatikana kwenye ofisi zao maeneo MBALIMBALI, ORODHA ya waliosajiliwa pia inapatikana kwenye ofisi za tanesco. mteja anapaswa kupewa orodha na kuchagua mkandarasi anayemtaka yeye.

3. mteja atapaswa kuweka picha moja ya mwombaji wa umeme

4. kisha mteja atarudisha fomu hiyo iliyokamilika ofisi ya eneo ambalo makazi yake yako (inayomudumia)

HATUA YA TATU- KUFANYIWA VIPIMO (SURVEY)

mara baada ya mteja kurejesha fomu iliyojazwa kikamilifu, mteja atapangiwa tarehe ya kufanyiwa vipimo (survey). mafundi watafika kwenye nyumba au sehemu inayoombewa umeme ili KUTATHIMINI GHARAMA ATAKAZOLIPIA MTEJA KWA KUZINGATIA UMBALI WA ENEO ILIPO MIUNDOMBINU YA UMEME KAMA NGUZO NA TRANSFOMA NA UWEZO WA UMEME HUO KUUNGANISHA KWA WATEJA WAPYA.

HATUA YA NNE: - KUPATIWA MAKADIRIO YA GHARAMA KIASI GANI ALIPE ILI AFUNGIWA UMEME

MARA BAADA YA KUFANYIWA TATHIMINI MTEJA ANAWEZA KUPATIWA MAKADIRIO YA GHARAMA YA KIASI GANI ALIPE ILI KUFUNGIWA UMEME. mAKADIRIO HAYA HUWEZA KUTUMWA KWA NJIA YA NUKUShI, UJUMBE MFUPI WA MENENO, BARUA PEPE AU MTEJA KUFIKA OFISINI NA KUCHUKUA BARUA. viwango vya muda wa kutoa MAKADIRIO KAMA INAVYOONEKANA KWENYE JEDWALI HAPO CHINI:

MAELEZO

MUDA WA MAKADIRIO

KAMA MIUNDOMBINU ILIYOPO ITATUMIKA (NDANI YA MITA 30 KUTOKA KWENYE NGUZO ILIYOKARIBU)

NDANI YA SIKU 7 ZA KAZI

UJENZI WA NJIA YA NYONGEZA UNAHITAJIKA (MITA 30- 100)

NDANI YA SIKU 10 ZA KAZI

KAMA MFUMO MPYA WA USAMBAZAJI UNAHITAJIKA KUJEGWA AU MFUMO WA UMEME MKUBWA UNAHITAJIKA KUONGEZWA KWA AJILI YA KIWANDA AU BIASHARA KUBWA (KAMA HAKUNA MFUMO WA KUMUUNGANISHIA MWOMBAJI) (ZAIDI YA MITA 100)

NDANI YA SIKU 14 ZA KAZI


HATUA YA TANO: - KUFANYA MALIPO

MTEJA ATAFIKA OFISI YA TANESCO ILI KUPATIWA NAMBA YA KUMBUKUMBU (REFERENCE NUMBER) ITAKAYOMUWEZESHA KUFANYA MALIPO BANK, MTEJA ATAFANYA MALIPO NA ATAPATIWA STAKABADHI YA MALIPO BANK (RISITI KWA NJIA YA UJUMBE MFUPI- SMS) (KWA SASA NI BANK YA NMB TU), WATEJA WANAHIMIZWA KUFANYA MALIPO YOTE BANK NA SI KWA MTU MWINGINE YEYOTE. MALIPO YOTE YATAKAYOFANYIKA NJE YA MFUMO ULIWEKWA HAYATAMBULIKA NA TANESCO. MTEJA AKISHAFANYA MALIPO BANK HUSIKA HATATAKIWA KURUDI TENA TANESCO BALI TANESCO WATAKUWA NA TAARIFA ZAKE ZOTE NA KINACHOFUATA NI KUMFUNGIA UMEME.

HATUA YA SITA:-KUUNGANISHIWA UMEME

MARA BAADA YA MTEJA KUFANYA MALIPO VIWANGO VYA MUDA WA KUMFUNGIA UMEME VITAKUWA KAMA ILIVYOONYESHWA KWENYE JEDWALI HAPO CHINI.

MAELEZO

MUDA WA KUFUNGIWA

KAMA MIUNDOMBINU ILIYOPO ITATUMIKA (NDANI YA MITA 30 KUTOKA KWENYE NGUZO ILIYOKARIBU)

NDANI YA SIKU 30 ZA KAZI

UJENZI WA NJIA YA NYONGEZA ITAHITAJIKA

(MITA 30- 100)

NDANI YA SIKU 60 ZA KAZI

KAMA MFUMO MPYA WA USAMBAZAJI UNAHITAJIKA KUJEGWA AU MFUMO WA UMEME MKUBWA UNAHITAJIKA KUONGEZWA KWA AJILI YA KIWANDA AU BIASHARA KUBWA (KAMA HAKUNA MFUMO WA KUMUUNGANISHIA MWOMBAJI) (ZAIDI YA MITA 100)

NDANI YA SIKU 90 ZA KAZI


KWA MAULIZO WASILIANA NASI

KITUO CHA HUDUMA KWA WATEJA: - 0768985100/0222194400

BARUA PEPE: customer.service@tanesco.co.tz

Facebook: www.facebook.com/Tanesco yetu

Twitter: - www.twitter.com/Tanesco yetu

Tovuti; www.tanesco.co.tz



Ndugu TANESCO nimelipia umeme Nguzo2 urefu Mita100
kuanzia mwaka jana tareh19/10/2016 mpka Leo tarehe 24/04/2017 sijaunganishiwa umeme nimekuwa mtu wakuzungushwa kila nikienda Tanesco nazungushwa nimechoka.
Niliambiwa ndani ya siku60
 
46 Reactions
Reply
Back
Top Bottom