holy holm
JF-Expert Member
- May 6, 2017
- 4,670
- 8,670
Bata:Kujivuta vuta, kufanya kazi polepole na kuendekeza uvivu mapaka mambo ya kikundi yanazorota au kufa kabisa.
Bundi:Mtu anayefikiria ana akili kuliko wote kwenye kikundi- hutumia lugha ngumu kueleweka
Chura:Rudia rudia kitu kile kile mapaka anawachosha wenzake kundini
Kenge:Hatumii akili sawasawa, ujinga mwingi na kufanya maamuzi ya ovyo yenye kuwakatisha tamaa wenzake
Kiboko:Kulala lala na kupiga miayo, wakati wenzake wanachacharika, yeye ni kukaa tu hafanyi kazi.
Kifaru:Yeye hushambulia wengine kwenye kikundi bila sababu
Kinyonga:Kigeugeu, akiwa kwa mwanakikundi huyu anasema hili na akiwa kwa mwingine anasema tofauti
Kobe:Hujitoa akiudhiwa, hana uvumilivu kwenye changamoto zinazoikabili kikundi.
Kuku:Kuvuruga palipotengenezwa, kwenda tofauti na maono ya kikundi kwa kujali na kuzingatia mambo ya muda mfupi tu.
Mbuni:Huficha kichwa na hufikiri hakuna shida kwenye kikundi hata kama zipo shida nyingi
Nyati:Kujihami tu kwa sababu ya woga, hakosolewi, ukimgusa tu anaazisha vita vya maneno au kupigana
Nyoka:Anajificha huku akiuma bila kusema. Mchonganishi
Nyumbu:Woga na kutotumia akili kabisa.
Paka:Yeye anataka ahurumiwe tu na wenzake, hana mchango wowote kwenye kikundi.
Panya:Hachangii chochote yeye hujificha tu na kujitokeza wakati wa neema.
Popo: Hana msimamo, Kwa wanaokubali hoja yupo na kwa wanaopinga hoja yupo. Haeleweki.
Punda:Wagumu kubadilika hata umuelimishe kwa namna gani misimamo yake ni yale yale ya zamani.
Samaki:Hachangii hajibu, kazi kuteleza, kukwepa na kutoweka tu na huonekana hali ikitulia na kuwa shwari.
Simba: Hupigana kama hakubaliwi mawazo yake na wanakikundi.
Sungura:Hukimbia kama kuna dalili za hatari na kwenda kinyume na makubaliano ya kikundi
Tausi:Yeye huringisha na mambo mazuri aliyonayo ambayo wanakikundi wenzake hawana.
Tembo:Hufunga njia bila sababu watu wasipite. Huzuia mawazo, maamuzi ya kikundi yasifanikiwe bila sababu.
Tumbili:Mizaha mizaha tu wakati wote hayuko makini hata kwa mambo muhimu ya kikundi.
Bundi:Mtu anayefikiria ana akili kuliko wote kwenye kikundi- hutumia lugha ngumu kueleweka
Chura:Rudia rudia kitu kile kile mapaka anawachosha wenzake kundini
Kenge:Hatumii akili sawasawa, ujinga mwingi na kufanya maamuzi ya ovyo yenye kuwakatisha tamaa wenzake
Kiboko:Kulala lala na kupiga miayo, wakati wenzake wanachacharika, yeye ni kukaa tu hafanyi kazi.
Kifaru:Yeye hushambulia wengine kwenye kikundi bila sababu
Kinyonga:Kigeugeu, akiwa kwa mwanakikundi huyu anasema hili na akiwa kwa mwingine anasema tofauti
Kobe:Hujitoa akiudhiwa, hana uvumilivu kwenye changamoto zinazoikabili kikundi.
Kuku:Kuvuruga palipotengenezwa, kwenda tofauti na maono ya kikundi kwa kujali na kuzingatia mambo ya muda mfupi tu.
Mbuni:Huficha kichwa na hufikiri hakuna shida kwenye kikundi hata kama zipo shida nyingi
Nyati:Kujihami tu kwa sababu ya woga, hakosolewi, ukimgusa tu anaazisha vita vya maneno au kupigana
Nyoka:Anajificha huku akiuma bila kusema. Mchonganishi
Nyumbu:Woga na kutotumia akili kabisa.
Paka:Yeye anataka ahurumiwe tu na wenzake, hana mchango wowote kwenye kikundi.
Panya:Hachangii chochote yeye hujificha tu na kujitokeza wakati wa neema.
Popo: Hana msimamo, Kwa wanaokubali hoja yupo na kwa wanaopinga hoja yupo. Haeleweki.
Punda:Wagumu kubadilika hata umuelimishe kwa namna gani misimamo yake ni yale yale ya zamani.
Samaki:Hachangii hajibu, kazi kuteleza, kukwepa na kutoweka tu na huonekana hali ikitulia na kuwa shwari.
Simba: Hupigana kama hakubaliwi mawazo yake na wanakikundi.
Sungura:Hukimbia kama kuna dalili za hatari na kwenda kinyume na makubaliano ya kikundi
Tausi:Yeye huringisha na mambo mazuri aliyonayo ambayo wanakikundi wenzake hawana.
Tembo:Hufunga njia bila sababu watu wasipite. Huzuia mawazo, maamuzi ya kikundi yasifanikiwe bila sababu.
Tumbili:Mizaha mizaha tu wakati wote hayuko makini hata kwa mambo muhimu ya kikundi.