Uchaguzi 2020 Zijue sababu kuchelewa vikao Kamati Kuu ya CCM kupitisha Wagombea wa Ubunge

Awamu hii ya Magufuli hakuna kopo litakalouzika upinzani. Yote yamebakia machakavu. Sasa unategemea Chadema wamchukue mtu kama Makonda? Waitara? Gambo? Sahau awamu hii. Kama tulimkataa Membe nani mwingine tutachukua?
Wewe na nani mlimkataa Membe?

Membe hataki kuja kwenu au nyie mmemkataa?

Katika wote uliowataja hata sasa hivi akiamua kuhamia huko anakuja kupata jimbo na kugombea huku nyie mkihamasishwa kuwa madodoki ya kuwasafisha!

Chadema haijawahi kuwa serious!
Ni juzi tu ndio mmekuja kigundua kwamba kumbe Lowasa hakuwa mtaji!
Tena baada ya kukaza shingo na kuvunjika ndio mkakubali.
 
Safi Sana PCCB Kufanya Kazi Yao Na Kumimina Majaro Matata Sana Ndani Ya CCM, Uamuzi Utapaki Kwa
Chama Dola!!! Kusuka Ama Kunyoa!!!!

Nitapambana Na Rushwa Bila Kigugumizi Chochote Na Dawa Ya Jipu Ni Kulitumbua
Nimejipa Kazi Ya Mtumbua Jipu!!
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
 
Kumbe? Mimi pia nilikuwa najiuliza kunani pale CCM makao makuu? Huku polepole akijigamba kuwashikisha waheshimiwa wakubwa adabu mwaka huu. Hivi mwenyekiti akimgeuka atajiuzulu kwa msimamo wake kutosikilizwa?

Ajiuzulu akale wapi? Hizo kelele za kwamba anachukia rushwa ni kelele za kuwazuga wananchi. Yeye mwenyewe na mwenyekiti wake hawana uwezo wa kumnyooshea yoyote kidole, maana ndio walikuwa wanatoa rushwa ili kuwanunua wapinzani kwenye ile project ya kuunga juhudi. Hilo ndio lilisukuma watia nia wa ccm kugawa rushwa waziwazi, maana wanajua hamna vita serious ya rushwa zaidi ya siasa.
 
Sababu nyingine ya kuchelewa ni kwamba

Watakaokatwa wasiweze kwenda kwenye vyama vingine,kwani mchakato wa tume ya uchaguzi ya uchukuaji wa fomu utakuwa umeisha.
Siku moja inatosha mtu kuhama chama na kuchukua fomu, acha wajidanganye.
 
Back
Top Bottom