Zijue ratiba za kliniki kwa Mama Mjamzito

karv

JF-Expert Member
Dec 26, 2019
1,799
3,221
Wiki ya 8-12
Miadi yako ya kwanza ya kliniki inatakiwa kuchukua nafasi wiki ya 10 ya ujauzito ili mkunga wako akufanyie vipimo na uchunguzi mapema kama anahisi ni lazima. Ila inaweza fanyika kati ya wiki ya 8 na 12.
Katika miadi hii, mkunga atakuuliza:-
~Historia yako ya matibabu
~Unajisikiaje
~Mlo na maisha yako
~Kazi yako
~Wapi ungependa ujifungulie
~Kama utaendelea kumnyonyesha mwanao

Mkunga wako atakupatia taarifa nyingi. Na atakueleza:-
~Virutubisho gani unapaswa kutumia
~Faida za uzazi ambazo utakuwa nazo
~Uchunguzi wa magonjwa ya akili
~Lini utarajie kipimo cha “ultrasound”
~Faida na hatari ya baadhi ya vipimo, uchunguzi na vitendo-tiba.
~Utapata nafasi nyingi za kuuliza maswali na kuongelea tatizo lolote linalokupa wasiwasi. Ingependeza zaidi kama ukitengeneza orodha ya mambo unayotaka kuuliza kabla ya miadi yako.

Mkunga wako atakuuliza kama anaweza kuchukua damu yako, ambayo itatumika kuangalia kundi la damu yako, viwango vya madini ya chuma na pia kuangalia kama kundi lako la damu ni resusi chanya au hasi (rhesus status), na kama una antibodi au la.

Watahitaji sampuli ya mkojo wako katika miadi hii na kila miadi na mkunga wako. Atapima kama mkojo wako una protini ikiwa ni dalili ya kifafa cha mimba, na atapima maambukizi ya mkojo. Atakupima shinikizo la damu, uzito na urefu.

Mwisho wa miadi utapewa taarifa za uzazi kuenda nazo nyumbani mpaka miadi yako ijayo. Wakati huu pia unaweza ukafunguliwa kadi yako ya kliniki ya mama mjamzito.

Wiki 10-14

Picha yako ya “ultrasound” itakua tayari. Mtaalamu wa ultrasound atachunguza ukuaji wa mwanao na kuhakikisha siku ya kujifungua kwako. Atakuambia pia kama una mtoto zaidi ya mmoja.

Wiki 15-20
Utapatiwa kipimo cha damu kuangalia viwango vya protini na homoni katika damu yako ili kuangalia kama mwanao ana magonjwa ya kurithi ya akili. Kama majibu yataonyesha mtoto wako anaweza akawa na magonjwa ya akili, matibabu ya haraka yataanza kufanyika kwa mtoto aliye ndani ya tumbo.

Wiki ya 16
Mkunga wako atajadiliana na wewe matokeo ya kipimo cha damu na mkojo vilivyofanyika katika miadi yako ya kwanza (wiki ya 10). Kama kiwango cha chuma ni kidogo, anaweza kukushauri kutumia virutubisho vya chuma. Na kama ana wasiwasi wowote, atakupeleka kwa mtaalamu wa mambo ya uzazi kwa huduma ya ziada.

Mkunga wako ataangalia shinikizo lako la damu na kuchukua sampuli mpya ya mkojo wako kuangalia kama kuna uwepo wa protini,na atafanya hivi kila mara ukienda kumwona.

Na kwa kila miadi, ni muda mzuri wa kuuliza maswali na kuongea tatizo lolote linalokupa wasiwasi.

Wiki ya 18-21
Uchunguzi (scan) ya kasoro za ukuaji utafanyika. Uchunguzi utaangalia jinsi mtoto anavyokua na kwa baadhi ya hospitali zitakuambia jinsia ya mtoto wako kama ungependa kujua.

Wakati mwingine kondo la nyuma (plasenta) huziba mlango wa uzazi, na kufanya ugumu kupata vipimo sahihi wakati wa kipimo cha skani. Kama hii imetokea kwako utapangiwa muda mwingine wa kipimo.

Wiki ya 25 (kwa mimba za kwanza tu)

Kama kawaida mkunga wako ataangalia shinikizo la damu na kupima mkojo wako kama kuna protini. Pia atapima umbali kutoka mfupa wa sehemu za siri mpaka juu ya tumbo lako na tepu kuangalia kama mtoto wako anakua vizuri.

Wiki ya 28
Mkunga wako watachukua sampuli ya damu katika miadi hii. Hii itatumika kuhakikisha viwango vya chuma ni vya kawaida na kuandalia kingamwili. Iwapo una kiwango kidogo cha chuma, atashauri uchukue virutubisho vya chuma atakayokuandikia.

Kwa kila miadi kuanzia sasa, mkunga atakupima tumbo lako kuangalia kama mtoto anakua vizuri. Ataangalia pia shinikizo la damu na kupima mkojo wako kama kuna protini.

Wiki ya 31 (wenye ujauzito wa mara ya kwanza)
Mkunga atakupima tumbo lako kuangalia kama mtoto anakua vizuri. Ataangalia pia shinikizo la damu na kuima mkojo wako kama kuna protini. Atakupatia majibu ya vipimo vya damu vilivyochukuliwa wiki ya 28. Upate pia mda wa kuuliza maswali, kama unayo na kujadiliana masuala yanayohusiana na afya yako.

Wiki ya 32

Uchunguzi wa kasoro (anomaly scan) uliofanyika wiki ya 18 lakini majibu hayakuonekana vizuri kwasababu wakati mwingine kondo la nyuma au kirutubisho mimba (plasenta) ilikuwa inaziba mlango wa uzazi, na kufanya ugumu kupata vipimo sahihi wakati wa kipimo cha skani unaweza ukarudiwa tena kipindi hiki. Sasa ni wakati mwingine wa kufanya kipimo hichi.

Wiki ya 34
Mkunga atakupima tumbo lako kuangalia kama mtoto anakua vizuri. Ataangalia pia shinikizo la damu na kupima mkojo wako kama kuna protini na kupima ukubwa wa tumbo lako kuangalia kama mtoto anakua vizuri ndani ya tumbo lako.

Kama huu ni ujauzito wako wa pili, mkunga wako atakupa majibu ya vipimo vilivyochukuliwa wiki ya 28. Kama atakua na wasiwasi atajadiliana na wewe. Pata nafasi ya kuongea na mkunga wako kuhusu matayarisho ya uchungu na kuzaa. Mkunga atakuelezea hatua za kujifungua na lini utapata uchungu.

Wiki ya 36
Mkunga wako atafanya vipimo na uchunguzi wa kawaida. Atashika tumbo lako kwa mkono kuangalia mlalo wa mtoto wako.
Baadhi ya watoto wengi watakua wamegeuka kichwa chini katika wiki ya 36, tayari kwa kuzaliwa. Kama mtoto wako bado hajageuka, mlalo wa kutanguliza matako. Mkunga wako atakupa miadi mingine ili huduma ya kumgeuza mtoto huku mimba ikiwa inaendelea kukua ifanyike.

Sasa umekaribia miezi tisa, mkunga wako ataanza kuzungumzia nini kitatokea baada ya mtoto kuzaliwa. Ataelezea vipimo na uchunguzi vitakavyofanywa kwa mtoto wakati ukiwa hospitali na wakati ukienda nyumbani.

Wiki ya 38
Mkunga atakupima tumbo lako kuangalia kama mtoto anakua vizuri. Ataangalia pia shinikizo la damu na kupima mkojo wako kama kuna protini na kupima ukubwa wa tumbo lako kuangalia kama mtoto anakua vizuri ndani ya tumbo lako. Mkunga wako ataanza kukuelezea kwa undani kama mimba yako itachukua mpaka wiki 41.

Utaanza kupata hofu na wasiwasi ukifikiria siku ya kwenda kujifungua. Ondoa shaka kwasababu mkunga wako atafurahi sana kuongea na wewe kuhusu wasiwasi wako na kujibu maswali yote.

Wiki ya 40 (wajawazito wa mara ya kwanza)

Mkunga wako atakupima ukubwa wa tumbo lako na kupima shinikizo la damu na kipimo cha mkojo kama kawaida. Ni wakati mzuri kuongelea wakati gani ni wa kwenda hospitali kujifungua na nini kitatokea baada ya mtoto kuzaliwa.

Kama uchungu wako haujaanza ni wakati mzuri wa mkunga kukufanyia huduma itakayosaidia kuanzisha uchungu kwa kuingiza vidole vyake ukeni taratibu na kuvizungusha kwa ukakamavu (membrane sweep)

Wiki ya 41
Kama hakuna dalili yeyote ya uchungu mpaka wiki ya 41, mkunga wako atakupatia huduma ya “membrane sweep” (kuingiza vidole taratibu ndani ya uke wako na kuvizungusha kwa ukakamavu) ili kuuanzisha uchungu.

Kama ulifanyiwa huduma hii wiki ya 40 unaweza kuchagua kama unataka kufanyiwa mara ya pili au la. Mkunga wako atakupima shinikizo la damu na vipimo vya mkojo kama kawaida, pia atapima ukubwa wa tumbo.

Kufikia wakati huu mkunga wako atakuandalia huduma nyingine ya kuanzisha na kuchochea uchungu iitwayo “induction” (hii inasaidia kuchochea mikazo ya ukuta wa kizazi wakati wa kujifungua badala ya kusubiria uchungu kuja, mkunga atakupatia dawa au huduma ya kimatibabu) huduma hii itafanyika pale “membrane sweep” imeshindikana.

Ikiwa umechagua kuendela kusubiri na ujauzito wako ukafika wiki ya 42 au zaidi,utaangaliwa kwa karibu zaidi, ikiwemo kufanyiwa kipimo cha “ultrasound” na kusikiliza mapigo ya moyo ya mtoto.

Source: MAHALA PASIPO NA DAKTARI.

JamiiForums1404015583_658x326.jpg
 
Back
Top Bottom