Zijue njia za kuwa tajiri au maarufu kwa kutumia nguvu za giza

Umesema baada ya kila muda mliokubaliana kutoa kafara inahitajika sasa kama ulitoa ndugu au mtoto si wataisha wote na kubaki na upweke duh hatari kweli

Sent using Jamii Forums mobile app

Ndio. Muda unaweza kuwa baada ya miaka mitano au miaka kumi, inategemea. Wengine wanatoa marafiki zao wa karibu. Someone who is very dear to you.
 
Mbwembwe zote hizo lkn mwisho wa Siku una kufa tu.....
Mfano nlikuwa Naongea na jamaa yngu mmoja anafanya kazi kwenye hotel moja maarufu arusha mmiliki wake hvi Karibuni alifariki na kuzikwa!inasemekana alikuwa mtoa kafara sana lkn ukiangalia leo hii yeye Yuko wapi ashazikwaa

Ova
Unamuomgelea Mrema wa Impala au?Sikuwahi kujua hizo inshu za ma kafara kama anapiga aisee
 
Dunia imejawa na kila aina ya mambo. Usimuone mtu ni tajiri au maarufu ukatamani utajiri wake au umaarufu wake pasipo kujua anapitia nini au alifanya nini mpaka kufikia hapo alipo.

Simaanishi kila mtu maarufu au tajiri umuonae ametumia nguvu za giza, no. Chukua mda wako uzijue njia tatu za kuwa tajiri kwa kutumia nguvu za giza.

1. KUMZIKA NG'OMBE AKIWA HAI

Amri hii ya kumzika ng'ombe akiwa hai inatolewa baada ya kufanya procedures kadhaa ya kishirikina na zenye gharama kubwa.

Zoezi hili linahusisha kununua ng'ombe aliyenona na kumtoa kafara kwa kumzika akiwa hai katikakati ya kichaka au msituni wakati wa usiku.

Kadri ng'ombe yule anavyooza na kutoa mabuu na funza, ndivyo jinsi pesa na umaarufu unavyoongezeka au kama ni biashara inazidi kupanuka. Unapoona pesa zinaanza kupungua, au biashara na umaarufu vinapungua, unarudia zoezi hili tena tena. Wanaotumia njia hii sio rahisi kukaukiwa na hela, vigezo na masharti kuzingatiwa.

2. OGBONI ABORIGINE

Hii ni fraternity au brotherhood au chama ambacho kilianza katika kabila la Yoruba nchini Nigeria. Wanaojiunga na chama hiki huwa hawafanyi kazi yoyote ya maana lakini wanakuwa na hela ya ajabu.

Pindi tu mtu akijiunga na chama hiki, pesa inaongezeka maradufu unakuwa na IQ kubwa kuliko alivyokuwa. Ogboni Aborigine ni chama chenye masharti magumu sana.

Unapojiunga nao, siku ya initiation, kunakuwa na wanachama sita wale waliokomaa, mida ya saa sita usiku, wanakufunga kitambaa cheusi machoni, kisha wanakupa sahani yenye vipande vya nyama mbichi na wanakuamuru ule kipande kimoja.

Kipande hiki ndio kitakuwa kinakuLink moja kwa moja na wao. Siku unapofariki, kabla ya kuzikwa, kile kipande cha nyama ulichokimeza awali kinarudi kwenye sahani yao kwa nguvu za giza. Chama hiki kina siri nyingi sana na za kutisha.

3. BLACK MAGIC WEALTH RITUAL

Wanaojiunga na chama hiki wanakaribishwa na wanachama waliowatangulia. Zoezi la kujiunga lina procedures nyingi.

Kwa mfano ikiwa we ni mwanchama mpya, wanachama wote wanakukaribisha na wanakuombea kwa Beelzebub (Mwakilishi wa shetani duniani) akubariki na mali na umaarufu.

Kisha wakimaliza kukuombea kwa Beelzebub, unaweka ahadi ya kafara ya kitu au mtu unayempenda. Ikiwa ni mtoto wako, mke wako, mama yako, ndugu yako, kizazi chako n.k. Ukishaweka ahadi hiyo ya kafara na kukubaliana, wanatwaa kafara yao na baada ya mwezi mmoja kila utakachofanya utaona unafanikiwa.

Chama hiki kinatoa utajiri wake kupitia biashara. Hivyo basi ikiwa hauna biashara, watakupa mtaji na utashauriwa ufungue biashara ya aina yoyote ile ambayo roho yako inapenda.

Kwa mfano ukiamua kufungua biashara ya Supermarket, kwa muda mfupi utashangaa na ukuaji na mafanikio ya biashara hiyo. Ikumbukwe kuwa baada ya kila muda mlioafikiana na chama, kafara inahitajika ili uzidi kuwa juu kimafanikio.
hiyo namba moja naona haiumizi kichwa kwa sana ebu iweke wazi tuone maandalizi yake
 
Hiyo ya 2 siyo inawahusu mapastor wetu wa hapa bongo? Maana kila mmoja wao LAZIMA apitie Nigeria kwanza kwenda kuchukua mikoba, akirudi tu anakuja na ndege binafsi au utajiri wa hajabu.
 
Hiyo ya 2 siyo inawahusu mapastor wetu wa hapa bongo? Maana kila mmoja wao LAZIMA apitie Nigeria kwanza kwenda kuchukua mikoba, akirudi tu anakuja na ndege binafsi au utajiri wa hajabu.
Unakuta mtu wa kawaida anaondoka anaenda Nigeria, akirudi pesa zimeongezeka maradufu, umaarufu unaongezeka na heshima inaongezeka pia.
 
Unakuta mtu wa kawaida anaondoka anaenda Nigeria, akirudi pesa zimeongezeka maradufu, umaarufu unaongezeka na heshima inaongezeka pia.


Mimi ndiyo maana nabaki kuwashangaa hii misukule inayokwenda kwenye haya makanisa hapa Bongo......kuna jamaa mmoja (pastor) kila akienda Nigeria anasindikizwa na misukule yake uwanja wa ndege na LAZIMA mtu au watu watakufa kwenye huo msafara bu they never learn kuwa jamaa anawafanya makafara.
 
Back
Top Bottom