Ziara za Arusha na Michango:Lowassa unatafuta nini ?

Kimbembe

Senior Member
May 14, 2006
122
15
Kwa muda sana kumekuwa na ziara nyingi mikoani kwa waziri mkuu mkuu.

Katika ziara hizo kaenda mara nyingi sana Arusha kuliko mahapa pengine popote . Na kila akienda lazima kuna mkutano na michango kibao ya pesa.

Najua mtasema anaenda kwao ni sawa lakini ni kweli safari ya mapumziko lazima kuwe na mikutano na yote inahusu kuchangisha mapesa? Lowasa nasikia anachangisha pesa hata kwa wahindi sirini .Lowasa nasikia yuko kwenye ule ule mkumbo wa kuvimaliza vyama ya Upinzani.

Akifika mikoani anawaita wapinzani na kuwaonya dhidi ya kuisema vibaya serikali yao yaani wanatumia ziara za Serikali kufanya kazi Chama pia .

Kubwa zaidi namuliza Lowasa pesa unazo kusanya na ziara kibao namna hii Arusha nataka kufanya nini ? Hebu mwenye habari zaidi juu ya mwenendo wa maziara ya wakubwa hawa na matamshi yao na vyombo vya habari kufa kabisa TZ atuoe nyeti hapa il nasi tufunguke .
 
vilevile aache kuporomosha mapati kila kikao cha bunge dodoma. naomba gharama zilizotumika kuporomosha mapati kule dodoma ziwekwe wazi.
 
Lowassa, Tanzania Kubwa, Hujatembela Hata Minoa 15. Sasa Arusha Kunani? Au Ni Ukabila Na Udini Tu!

Fanya Zira Za Binafsi Kwa Gharama Binafsi, Tunakuona Usidhani Hatukumliki, Tumekuwa Tukikusikia Hata Kabla Ya Kuwa Pm Kuwa Wewe Kwa Ukabila Ni Babu Kubwa.
 
EL alikuwapo pia Rukwa juzi juzi tu.....labda kumbukumbu yangu inanidanganya
 
Mambo makubwa haya Mzee Es wanajiandaa kwamba JK ataishia miaka 5 ama kuna mabadiliko kweney Katiba yenu nyie wana CCM toka miaka 10 ? Au kulikoni badi hadi wameanza kujiandaa sasa ? Tupe ulichokisikia nasi tufunguke masikio
 
Ndugu yangu kwenye siasa hakuna permanent friends, hakuna guaranteees, Mkapa kidogo apumzishwe baada ya term moja, ni lazima maisha yake yote amshukuru JM aliyemuokoa dakika za mwisho,

CCM hakuna guarantees kuwa ukiwa rais ni lazima utawale vipindi viwili, kwa hiyo ndugu yangu usishangae 2010, ukiskia kuwa kuna wazee wanachukua fomu ndani ya CCM, maana hizi mbio za wenzetu wengine sio za bure!
 
Ina maana EL anawasaidia hao wanaojiandaa kujitokeza au anawakabili kuwanyamazisha??

Sikumbuki ratiba ya EL huko Iringa inasemaje; lakini nakumbuka huko nyuma aliwahi kuahidi kuwa angerudi Iringa kufuatilia masuala ya matumizi ya Bonde la Usangu/Mto Ruaha/Bwawa la Mtera na migongano yake ya wakulima na wafugaji na umeme.

Lakini tusisahau kuwa huko mikoani mabosi huwa wanawatembelea "mafundi" wao katika "kuimarisha" nafasi zao. Si mnajua sayansi ya Kiafrika. Sasa kwa Dar inaweza kuwa ngumu kidogo, manake, kama wanavyosema vijana wa mjini Dar kuna wanga wengi! (yaani wajuaji au watu wanaoweza kueneza au kuvujisha habari). Mmemsikia Prof Jonathan Moyo wa Zimbabwe wiki iliyopita kwenye BBC Hard Talk alipoulizwa kuhusu nguvu ya Mugabe na mambo ya ushirikina alijibu kuwa huyo Mzee hukaribisha "mafundi" (Sangoma) ikulu kwa visingizio mbalimbali na kwamba hilo ni jambo la kawaida kwa "viongozi wengi wa Kiafrika kuwa karibu na 'African cosmology'.
 
Mwanagenzi,

Huku Tanzania "tunamtumia" kijana Maarifa wa pale panapotaka kujengwa bandari, Akisaidiana na wakigeni wachache.

Niliwahi kusikia kuwa hata "MK wa Kenya" amewahi kumtembelea kijana Maarifa.

Sio mchezo, waafrika kwa usangoma!!
 
FD,
Kijana Maarifa, Mzee wa Busara, watu tumeendelea kweli kweli. Inanikumbusha kale kahirizi kalikoanguka Tabora wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka jana.
 
Jasusi,

Kijana maarifa yupo, (ndo jina lake hilo) anaitwa Maarifa. Unataka kwenda kuongea naye?

FD
 
Duh! Jasusi,
Kijana Maarifa anaweza kukusaidia jimbo lingine lakini sio Singida mjini hilo lina wenyewe tayari chagua lingine.

Mafuchila
 
Mafuchila,
He!he!he!
Sasa nigombee wapi? Au Kijana Maarifa atanitabiria kwenye darubini yake?
 
Jasusi,

Kijana Maarifa anakupa MVUTO, watu wanakupenda, wakikuona tu wanashangilia, hawasikilizi sera wao wanakuona upo handsome na mcheshi saaana, hawatajali kama una uwezo wa kutawala au lah!'
Thats Maarifa. Vipi tumtafute? Ubunge wa Temeke ndio unafaa maana kule hawaangalii mtu, kihiyo sawa, Mrema sawa, Tambwe hiza sawa next ni wewe Jasusi. Nipe kazi hiyo. Nipe na budget yako ya kuukwaa ubunge. aha hahahaaaaaaa.


FD
 
Halafu huko ZNZB tayari Mzee Shamuhuna, ameshaanza kampeni tunasikia, ila majuzi kwenye kikao cha kamati kuu Mzee JK, alimuweka sawa, na kumwambia "..........Vipi Shamuhuna nasikia toka tukupe kimuli muli imekuwa taabu huko visiwani, maana nimesikia kuwa umeanza kampeni, vipi tukunyang'anye kimuli.......", ungemuona mzee wangu wa ZNZB jasho linavyomvuja!
 
FD
Basi naona Temeke patafaa. Sasa ngoja nitafute wafadhili kwanza halafu unielekeze kwa huyo kijana. Ha!ha!ha!
 
Mzee Es kama wataka kubomoa sema badala kukalia nyeti hizo bwana .Tueleze tujue maana harakati hizi za Lowasa ni nyingi sana muda huu .Na zanzibar kuna nini hebu nieleze umeseme wachukue kimulimuli jamani kuna mtu JK anamtaka nini ?
 
Back
Top Bottom