CUF Habari
JF-Expert Member
- Dec 12, 2019
- 239
- 234
ZIARA YA SIKU NNE (4) YA MWENYEKITI WA CHAMA TAIFA MHE. PROF. IBRAHIM LIPUMBA HUKO PEMBA IMELETA HAMASA KUBWA NA KUPOKEA ZAIDI YA WANACHAMA WAPYA 723.
Ziara hiyo imekijengea Chama Heshima Kubwa kwa kukiwezesha Kurejesha Ngome yake huko Pemba na kukiwezesha Chama kuwarudishia Hamasa wanachama wake pamoja na kupokea wanachama zaidi ya 723 waliokabidhiwa Kadi za CUF-Chama Cha Wananchi, idadi hiyo ikijumuisha waliokuwa wanachama wa ACT-Wazalendo 604 waliorudisha Kadi za Chama hicho na kuamua kurejea CUF-Chama Cha Wananchi.
Wengi wao walidhihirisha kujutia Maamuzi yao waliyoyafanya bila kutafakari ya kufuata Maalim Seif aliyewadanganya muda mrefu. Matawi mapya kadhaa yalizinduliwa kwenye Ziara hiyo muhimu.