Ziara ya Rais Samia Ufaransa: Tanzania yasaini Mkataba wa Mkopo wa Masharti nafuu wa Euro Milioni 178

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Utiaji Saini wa Mikataba na Makubaliano hiyo unalenga kuendeleza Uhusiano kati ya Mataifa hayo mawili. Miongoni mwa Makubaliano hayo ni Mkataba wa Mkopo wa Masharti nafuu wa Euro Milioni 178 kwa ajili ya kugharamia mradi wa ujenzi wa barabara wa mabasi yaendayo haraka

Vilevile, Tanzania na Ufaransa zimesaini Mkataba wa Mkopo wa Masharti nafuu wa Euro Milioni 80 kuimarisha Benki ya Maendeleo ya Kilimo

Nchi hizo pia zimesaini tamko la dhamira ya kushirikiana katika Uchumi wa Buluu na Usalama wa Bahari

761C8B0D-7916-463D-990D-AED79B9F08CE.jpeg
 
Utiaji Saini wa Mikataba na Makubaliano hiyo unalenga kuendeleza Uhusiano kati ya Mataifa hayo mawili. Miongoni mwa Makubaliano hayo ni Mkataba wa Mkopo wa Masharti nafuu wa Euro Milioni 178 kwa ajili ya kugharamia mradi wa ujenzi wa barabara wa mabasi yaendayo haraka

Vilevile, Tanzania na Ufaransa zimesaini Mkataba wa Mkopo wa Masharti nafuu wa Euro Milioni 80 kuimarisha Benki ya Maendeleo ya Kilimo

Nchi hizo pia zimesaini tamko la dhamira ya kushirikiana katika Uchumi wa Buluu na Usalama wa Bahari

View attachment 2116841
Euro mil 178 za Barabara ya mwendokasi,

Zikifika bongo hakuna cha Barabara ni mgao tu!

ZANZIBAR yenye watu milioni2 inapata mgao wa Euro mil 78!

TANGANYIKA yenye zaidi watu miloni 60 inapata mgao wa Euro mil 100!

Mlipaji; TANGANYIKA!

Hutaki; HAMA NCHI!!
 
Kukopa sio mafanikio wala deal anyway. Wazungu wamejaliwa kuthink beyond their noses. Huo tunaouita unafuu wanajua vema namna ya kuu compensate.
Hii kufungwa safari kwenda Kukopa kila saa Ni dalili ya viongozi wetu kukosa mbinu mbadala za kushawishi na kuvutia uwekezaji Tanzania.

Serikali haifanyi biashara, Ni hatari Kukopa ili upeleke kwenye ugavi. Tukitumia style ya administration ya kutawala Zanzibar tukaiapply kwenye Serikali Pana ya Muungano tutafeli. Zanzibar Raisi anaweza akaamua akiamka asubuhi aagize wazenj wote wanywe chai na ikawezekana.

Huyu Mama mafanikio yake yapo kwenye kukopa. Mikopo yake atakayoiacha na aliyoiacha mwendazake itavunja rekodi ya miaka 60 ya Uhuru.

Sina hakika Kama Kukopa Ni Mafanikio au Utumwa.
 
Hii Benki ya Maendeleo ya Kilimo mpaka sasa inaendeleaje na ishatoa / hudumia wakulima wangapi....

Hizo Barabara si ndio hizi tunazigharamia na Tozo ya kwenye Miamala !!!, Nadhani tunakwenda kinyume; Ni bora kwanza tukatenga hizo barabara za kujenga, tukajua tunahitaji kiasi gani ili tukope hizo pesa ili kufanikisha..., Au tupate hio Mikopo nafuu tumalizie hii Miradi ambayo huenda ikawa White Elephant
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom