Ziara ya Rais Magufuli kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Maktaba UDSM

Informer

JF-Expert Member
Jul 29, 2006
1,582
6,627
LIVE UPDATES UDSM



Yanayojiri ziara ya Magufuli chuo kikuu Dar es Salaam

Wanafungua mkutano kwa kuimba wimbo wa Taifa wa Tanzania na na wimbo wa Taifa wa China
Wengine waliohudhuria ni ya ni waziri wa elimu Joyce Ndalichako, rais msataafu Jakaya Kikwete, balozi wa china nchini Tanzania, makamo wa rais mstaafu Gharibu Bilali, waziri mkuu mstaafu Joseph Warioba na mkuu wa wilaya ya Kinondon Ally Hapi.


Hotuba ya makamu mkuu wa chuo Rwekaza Mukandara
Anamuelezea rais changamoto zinazoikabili chuo ikiwemo miundombinu bora ya kufundishia mabweni ya wanafunzi ambayo ni machache na yamechakaa ndio changamoto kuu.
Ametaja changamoto nyingine ni kusomesha wanafunzi wa Uzamivu na uhaba wa wakufunzi kwenye mafunzo ya kiufundi kuboresha maslahi ya wafanyakazi na wanafunzi.

Ameongezea mradi wa maktaba kwamba ukikamilika utakidhi mahitaji ya sasa kutokana na wanafunzi kuwa wengi ambayo ni maktaba kubwa zaidi ukanda wa afrika mashariki na kati na kuishukuru serikali ya China kwa ufadhili wao.

Mwakilishi wa kampuni ya ujenzi wa China amelezea maktaba hiyo itakavyokuwa na uwezo mkubwa na teknolojia ya juu.

Hotuba ya Balozi wa China Tanzania
Balozi wa China nchini Tanzania , amezungumzia historia ya ushirikiano kati ya China na Tanzania kukikisifia chuo hicho kwa kutoa viongozi mashuhuri Afrika pamoja na kutoa wataalamu wa fani mbalimbali.
Amesifia uhusiano mzuri wa kidiplomasia uliopo kati ya China na Tanzania na misaada mbalimbali ambayo China imeipa Tanzania na itakayozidi kuisaidia Tanzania.

Ameongezea maktaba hiyo itagharimu dola milioni 40 na ni maktaba kubwa zaidi kujengwa na China barani Afrika.

Hotuba ya waziri wa elimu Joyce Ndalichako
Amesema mradi huu umekuja kwa wakati muafaka kwa kua kipaumbele kikubwa cha serikali ya awamu ya 5 ni elimu na wizara ya elimu itafuatiia mradi hu kwa makini kuhakikisha unakamilika kwa wakati.

Hotuba ya Mwenyekiti wa chuo Jakaya Kikwete.
Rais aliyepita Jakaya Kikwete amezungumzia miundombinu ya chuo kama barabara na miundombinu ya chuo inavyohitaji kurekebishwa, maabara zilivyo na teknolojia ya zamani na ambazo hazitoshi.
Amesema ili akamilishe kazi yake vizuri kama mwenyekiti wa chuo ni vizuri rais Mghufuli akashughulikia changamoto hizo.

Hotuba ya rais Magufuli
Rais amemshukuru Kikwete kwa kuleta mradi huo na kuwashukuru China kwa misaada yao isiyo na masimango na masharti tangia enzi za uhuru na mpaka sasa hivi.

Amezungumzia ongezeko la wanafunzi wanaopata mikopo na changamoto ya wanafunzi 'hewa' wanaopata mikopo na kumtaka waziri wa elimu aendelee kupambana na tatizo hilo.
Amezungumzia pia wanafunzi walioenda chuo kikuu cha Dodoma waliofukuzwa ambao hawakuwa na vigezo vya kujiunga chuo na kushangazwa wanasiasa wanaowatetea.

Ameongezea kusema wanafunzi walioondoka wamefukuzwa na hata wanafunzi wote wangefukuzwa kama wangegoma.
Ameongezea kuwa chuo kikuu cha Dar es Salaam ndio alichosoma atakuwa anakisaidia na atatoa shilingi bilioni 10 kwa ajili ya kujenga majengo na chuo watenge eneo kwa ajili ya ujenzi huo.
Pia ameomba hifadhi za jamii kusaidia kujenga ujenzi wa majengo ya chuo badala ya kujenga majengo sehemu nyingine ambazo hakuna watu wa kuyatumia.

Amesema pia changamoto zilizotajwa na makamo mkuu wa chuo na mwenyekiti atazibeba na kuzifanyia kazi.
Amemshukuru Makamo mkuu wa chuo kwa ulezi mzuri wa chuo na kuwaasa wanafunzi wasikubali kutumiwa na wanaiasa.

Ameongezea mikopo ilichelewa kutolewa kwa kuwa walikuwa wanahakiki majina ya wapokeaji wa mikopo yao na hata UDOM bado hawajapata lakini hawajagoma.
Amemsifu profesa Mgaya kwa kusimamia ukweli na akasema japokuwa ametolewa kwenye bodi ya TCU atampa kazi nyingine.
Amemaliza kwa kuishukuru nchi ya China kwa ushirikiano wao na kuahidi kuendeleza uhusiano kati ya Tanzania na China




==========

Juni 02, 2016

UONGOZI wa chuo kikuu cha Dar es salaam umetangaza kufuta ratiba zote za masomo chuoni hapo katika siku ya leo ambapo Rais Magufuli anatarajiwa kufika chuoni hapo kwa lengo la kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa maktaba ya kisasa.

Sambamba na hilo pia ratiba ya ziara hiyo ya rais Magufuli imebadilishwa sasa na baada ya kumaliza uwekaji wa jiwe la msingi katika maenwo ya Yombo ataelekea katika uwanja wa mpira wa Chuo hicho ili kuweza kuwahutubia wanafunzi hao na taifa kiujumla.

9a10f2b36bdf78d7e65044998e24700a.jpg


Taarifa za chinichini toka chuoni hapo zinasema kuwa huenda rais Magufuli akapokelewa na mabango yenye jumbe mbalimbali kutoka kwa wanafunzi hao huku suala la uhaba wa mabweni chuoni kufikia hata wanafunzi 10 kulala chumba kimoja kilichotengenezwa kwaajili ya wnafunzi wanne tu kulala.

Aidha, suala la kurudishwa nyumbani kwa wanafunzi wa UDOM, kusitishwa kwa matangazo ya moja kwa moja ya bunge pamoja na kuchelewa kwa fedha za mikopo ya wanafunzi na kupelekea migomo yakitarajiwa kujitokeza katika mabango.
 
Mkandara na Maboko wajiandae kutumbuliwa...

Japo Mkandara amefanikiwa kuituliza sana chuo na kupunguza kwa iasi kikubwa rushwa ya ngono baina ya waalimu na wanafunzi ila anapwaya sana kwa sasa.

Kifupi umri umemtupa, inahitajika damu mpya inayoweza kuendana na kasi ya sasa.

Wanachuo wambane Magufuli awajengee hostel mpya maana Kikwete alikuwa na mpango huo toka zamani, waachane na mambo ya student center kwanza kwa sasa.
 
057fd0fc9fb0d7a74cccdc5d94193fcb.jpg

Wanafunzi wameanza kuwasili eneo ambalo Rais Magufuli atahutubia
 
Mkandara na Maboko wajiandae kutumbuliwa...

Japo Mkandara amefanikiwa kuituliza sana chuo na kupunguza kwa iasi kikubwa rushwa ya ngono baina ya waalimu na wanafunzi ila anapwaya sana kwa sasa.

Kifupi umri umemtupa, inahitajika damu mpya inayoweza kuendana na kasi ya sasa.

Wanachuo wambane Magufuli awajengee hostel mpya maana Kikwete alikuwa na mpango huo toka zamani, waachane na mambo ya student center kwanza kwa sasa.
Hao hawagusi mzee maana ni wakuu wa chuo alichopatia udaktari. Ni ngumu mno na mkandara ni kada mzuri san wa lumumba. Wengine washalipwa fadhila za ukatibu.
 
ROHO YA MWENYE ENZI MUNGU itawale....AMANI, HEKIMA, BUSARA, UFAHAMU NA FURAHA
 
Nataka nione leo tofauti ya wasomi na wale wa mitaani ,kama wataanza kupiga makofi kama UVCCM bila sababu nitawadharau
 
Nataka nione leo tofauti ya wasomi na wale wa mitaani ,kama wataanza kupiga makofi kama UVCCM bila sababu nitawadharau
nimewataadharisha wasiwe kama UVCCM kupiga makofi hewa.hao wanaojiita wasomi wajipange ni wamuulize sukari hiko wapi lugumi na mambo yenye mantiki.


swissme
 
Jamaa anajiamini sana huyo. Haya tuone wasomi wetu watakavyompokea na kumsikiliza.
 
Mgeni rasmi ni Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli.
Wengine waliopo katika uwekaji wa jiwe la Msingi la Ujenzi wa Maktaba ya kisasa kabisa ni Mkuu wa Chuo, Rais Mstaafu, Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais wa awamu ya nne, Mohamed Ghalib Bilal. Waziri Mkuu Mstaafu , Joseph Sinde Waryoba, Vice Chansellor wa Kwanza wa UDSM, Pius Msekwa, Balozi wa China Nchini na wengine wengi
 
Back
Top Bottom