Ziara ya Rais Kikwete Hazina na 'Long Room' (leo)

Kumbe anakumbuka kufanya ziara nchini?? mi nilifikiri yupo Ughaibuni anakula gud tym.
Big up Kikwete kwa kuanza kufanya ziara nchini!
Hii siyo ziara. Kutoka ofisi yake Ikulu kwenda Hazina ni kama mita 300 hivi. Kwenda TRA/Long Room ni kama nusu kilometa. Hata bila yeye kwenda huko angeweza kuwaita wahusika wakaenda ofisini kwake na taarifa alizozitaka. Ni zuga zake za kila siku.
 
Ziara uchwara tu hizi .Hazina manufaa makubwa kwa Watanzania. Amehisi reputation yake imepotea kidogo akaamua ajitokeze ili vyombo vya habari viandike watu wajue yupo.
Hebu tujiulize ile ziara alifanya bandarini kwaka jana kama sio juzi, je ina mafanikio???????????? Jibu ni hapana. Zile zilikuwa nguvu za soda tu. Maana ukifika bandarini utajionea jinsi usumbufu wa kutoa mizigo bandarini ulivyo! Pia fuatilia Miundo mbinu mingine kwishny!
 
Mapato ya taifa yameongezeka kwa shilingi bilioni 205 tangu mwaka 2005 alipochanguliwa kuongoza taifa la Tanzania. Miaka ya nyuma mapato yaliyokuwa yanakusanywa ya shilingi bilioni 215 kwa mwezi yaliwezesha kujenga miradi mingi ya maendeleo iliyofadhiliwa na mapato yetu ya ndani na miradi imejengwa kwa ufanisi mkubwa.

Inakuwaje mapato yaongezeke mara mbili kisha miradi mingi ya maendeleo isimame? na hakuna mradi mwingine wowote mpya ambao umeanzishwa na serikali yake anaoweza kujivunia.

Tunataka jibu, pesa zetu zinapelekwa wapi?

Nakubaliana na wewe mkuu. Kama mapato yameongezeka kwa mara mbili kwanini huduma za jamii ndo zinazidi kuwa mbovu? Umeme, maji, hospitali, shule za kata n.k. Watuambie hizo pesa zetu zinakwenda wapi?
 
Anatafuta cavarage katika magazeti , TV na radios baada ya kuona ''Babu'' kafunika
Jk ni mchumi, sasa anaposema watafute njia za kupunguza inflation, anazungumza kwa nadharia, nilitegemea angetumia uchumi wake kushauri njia ipi itumike kupunguza inflation rate lakin jamaa yetu anatoa matumain mahali panapohitaji kutenda. Wakati huu si muda wakupeana matumaini alisha toa matumaini 5yrs ago hakuna alichotimiza aache ukilaza afanye maamuzi magumu.
 
JK anapaswa kutowasikiliza wakuu wa idara tu bali ashuke kwa akina kayumba wampe physical data za yanayojiri kwa wateule wake kiutendaji na UOZO uliopo.
 
Kwa hali ya Tanzania ilivyo hivi sasa Rais anatakiwa awe sites muda wote, sio anasubiri wakati ambao hana safari za kwenda nje ya nchi tu ndio anakwenda kukagua.

Hivi mkuu wa kampuni kama atakuwa muda mwingi anafuatilia mambo ya nje ya kampuni na kuacha ya ndani si kampuni itakufa kabisa. Hii ni hivyo hivyo na rais wa nchi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom