Wanabodi,
Kwa muda mrefu tumeshuhudia mashambulizi ya wahafidhina dhidi ya mbunge wa jimbo la Ubungo Mh. John John Mnyika.
Thread nyingi zilikuwa za "kimkakati wa kipropaganda" kwani zilishindwa kutoa ushahidi kama tatizo la maji linahusu jimbo zima la Ubungo, au ni asilimia ngapi ya wakazi wa jimbo hilo wana matatizo ya maji. Uhalisia ni kuwa zaidi ya nusu ya maeneo ya jimbo hilo huwa yanapata maji walau mara tatu kwa juma.
Kiukweli yapo maeneo kadhaa katika jimbo hilo (sio yote) ambayo yamekuwa na matatizo ya uhaba wa maji kwa muda mrefu, hasa wakati jimbo hilo linaongozwa na mbunge kwa tiketi ya ccm. Hata baada ya "mradi wa wachina" bado kuna maeneo ambayo bado yalikuwa na tatizo hilo, safari hii sababu kubwa zikiwa ni za kiufundi, uharibifu na uhujumu wa miundombinu ya maji. Sababu nyingine zaweza kuwa ni kumhujumu kwa makusudi mbunge Mnyika kunakofanywa na wahusika na wadau wa maji.
Naelewa jitihada kubwa zilizofanywa na zinazofanywa na Mh. Mnyika katika kutatua kero za wapiga kura wake hasa tatizo la maji.
Mh. Mnyika amekuwa akichukua maoni ya wapiga kura wake kupitia makongamano, mikutano ya hadhara, mitandao ya kijamii n.k. Vilevile amekuwa akitoa mara kwa mara mrejesho wa kazi zake kupitia njia hizo tajwa. Kwa mtu ambaye amekuwa akimfuatilia vizuri hawezi kupinga kuwa Mh. Mnyika amepiga hatua kubwa sana katika kuhakikisha kero za wapiga kura wake zinatatuliwa.
Wiki iliyopita mbunge Mnyika alianza ziara jimboni kwake katika ule mwendelezo wa kuwasiliana na wananchi wake.
Tangu alipotangaza kuanza ziara, maeneo karibu yote ya jimbo lake yamekuwa yakipata maji kwa kiwango kikubwa.
Hata yale maeneo ambayo hayajawahi kuona tone la maji ya bomba yamepata maji kuanzia jumamosi mfululizo hadi leo hii. Na haya ndio matunda ya mbunge anayejua nini anapaswa kufanya kwa wale anaowawakilisha.
Hongera Mh. John Mnyika.
Wale waliokuwa wanakubeza nadhani sasa aibu imewakumba.
Kwa muda mrefu tumeshuhudia mashambulizi ya wahafidhina dhidi ya mbunge wa jimbo la Ubungo Mh. John John Mnyika.
Thread nyingi zilikuwa za "kimkakati wa kipropaganda" kwani zilishindwa kutoa ushahidi kama tatizo la maji linahusu jimbo zima la Ubungo, au ni asilimia ngapi ya wakazi wa jimbo hilo wana matatizo ya maji. Uhalisia ni kuwa zaidi ya nusu ya maeneo ya jimbo hilo huwa yanapata maji walau mara tatu kwa juma.
Kiukweli yapo maeneo kadhaa katika jimbo hilo (sio yote) ambayo yamekuwa na matatizo ya uhaba wa maji kwa muda mrefu, hasa wakati jimbo hilo linaongozwa na mbunge kwa tiketi ya ccm. Hata baada ya "mradi wa wachina" bado kuna maeneo ambayo bado yalikuwa na tatizo hilo, safari hii sababu kubwa zikiwa ni za kiufundi, uharibifu na uhujumu wa miundombinu ya maji. Sababu nyingine zaweza kuwa ni kumhujumu kwa makusudi mbunge Mnyika kunakofanywa na wahusika na wadau wa maji.
Naelewa jitihada kubwa zilizofanywa na zinazofanywa na Mh. Mnyika katika kutatua kero za wapiga kura wake hasa tatizo la maji.
Mh. Mnyika amekuwa akichukua maoni ya wapiga kura wake kupitia makongamano, mikutano ya hadhara, mitandao ya kijamii n.k. Vilevile amekuwa akitoa mara kwa mara mrejesho wa kazi zake kupitia njia hizo tajwa. Kwa mtu ambaye amekuwa akimfuatilia vizuri hawezi kupinga kuwa Mh. Mnyika amepiga hatua kubwa sana katika kuhakikisha kero za wapiga kura wake zinatatuliwa.
Wiki iliyopita mbunge Mnyika alianza ziara jimboni kwake katika ule mwendelezo wa kuwasiliana na wananchi wake.
Tangu alipotangaza kuanza ziara, maeneo karibu yote ya jimbo lake yamekuwa yakipata maji kwa kiwango kikubwa.
Hata yale maeneo ambayo hayajawahi kuona tone la maji ya bomba yamepata maji kuanzia jumamosi mfululizo hadi leo hii. Na haya ndio matunda ya mbunge anayejua nini anapaswa kufanya kwa wale anaowawakilisha.
Hongera Mh. John Mnyika.
Wale waliokuwa wanakubeza nadhani sasa aibu imewakumba.