samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 213
ziara iliyofanywa na CHADEMA katika mikoa ya lindi na mtwara imegeuka kuwa mwiba mkali kwa wabunge wa ccm ambao majimbo yao yalipitiwa na kimbunga cha ziara hiyo yenye lengo la kuleta mabadiliko katika mikoa ya kusini. Wabunge wawili wa mkoa wa mtwara Abdallah Mtutula na Jerome Dismas Bwanaausi wameshambulia vikali hatua ya chadema kutembelea kwenye majimbo yao na kuwashambulia. Aidha wabunge hao wamesema hatua ya wabunge wa chadema kwenda kwenye majimbo yao na "kueneza chuki" na kuwashambulia wao inaweza kuleta machafuko na kutoweka kwa amani.
kuna msemo unasema kwamba ukirusha jiwe gizani ukasikia mtu anasema aiiii ujuwe limempata. Hivyo chadema wanapaswa kukaza mwendo kwani wabunge wa ccm katika mikoa ya kusini wameshaingiwa na hofu ya kuondolewa madarakani mwaka 2015.
kuna msemo unasema kwamba ukirusha jiwe gizani ukasikia mtu anasema aiiii ujuwe limempata. Hivyo chadema wanapaswa kukaza mwendo kwani wabunge wa ccm katika mikoa ya kusini wameshaingiwa na hofu ya kuondolewa madarakani mwaka 2015.