Kamati ya Maadili ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imemfungia mgombea Urais wa @ACTwazalendo, Seif Sharif Hamad kutofanya kampeni kwa siku tano hadi Oktoba 20, 2020.
Chama cha Demokrasia Makini kiliwasilisha malalamiko kuwa mgombea huyo ameshawishi watu wapige kura Oktoba 27.
========
Katibu wa Kamati ya Maadili ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Khamis Issa Khamis amesema mbele ya waandishi wa habari kwamba Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Act-Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad amefungiwa kufanya mikutano ya kampeni kuanzia tarehe 16 Oktoba hadi tarehe 20 Oktoba Mwaka huu kutokana na kukiuka maadili ya Uchaguzi baada ya kuwasilishwa malalamiko dhidi yake na Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia chama cha Demokrasia Makini, Bwana Ameir Hassan Ameir.
Madai yaliowasilishwa mbele ya Kamati hiyo ni kuwa Maalim Seif mnamo Oktoba 13 mwaka huu katika mkutano wake uliofanyika viwanja vya Jadida Wete Pemba alitoa kauli ya kuwahamasisha wanachama wake kwenda katika vituo kupiga kura siku ya October 27 kinyume na kifungu cha 82 ambacho kimewataja watu maalumu walioruhusiwa kwenda kupiga kura siku hiyo ya uchaguzi.
Chama cha Demokrasia Makini kiliwasilisha malalamiko kuwa mgombea huyo ameshawishi watu wapige kura Oktoba 27.
========
Katibu wa Kamati ya Maadili ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Khamis Issa Khamis amesema mbele ya waandishi wa habari kwamba Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Act-Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad amefungiwa kufanya mikutano ya kampeni kuanzia tarehe 16 Oktoba hadi tarehe 20 Oktoba Mwaka huu kutokana na kukiuka maadili ya Uchaguzi baada ya kuwasilishwa malalamiko dhidi yake na Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia chama cha Demokrasia Makini, Bwana Ameir Hassan Ameir.
Madai yaliowasilishwa mbele ya Kamati hiyo ni kuwa Maalim Seif mnamo Oktoba 13 mwaka huu katika mkutano wake uliofanyika viwanja vya Jadida Wete Pemba alitoa kauli ya kuwahamasisha wanachama wake kwenda katika vituo kupiga kura siku ya October 27 kinyume na kifungu cha 82 ambacho kimewataja watu maalumu walioruhusiwa kwenda kupiga kura siku hiyo ya uchaguzi.