Ze comedi... Wanajenga, wanabomoa...?

Dr. Chapa Kiuno

JF-Expert Member
Sep 11, 2009
443
18
Wadau, jana hawa jamaa wa Ze comedi wameendeleza uhasama dhidi ya wasanii wenzao wa kutengeneza filamu baada ya kuponda kikao cha wasanii hao kilichofanyika juzi n huku wakijigamba kuwa wao hawatishiki n kwa jeuri zaidi hata wakamkaribisha Manji kwenye kipindi chao...

Je, watakapo fulia kabisa MANJI ataendelea kuwatunza?


USIMCHEKE MAMBA KABLA.........
 
Kwakweli hawa jamaa sasa wamevuka mipaka, sababu wao saiv wanahela wanajiona wamefika? alafu wanaonekana bado wana utoto,wasingewajibu wenzao badala yake wangekaa kimya tu kwani wana makosa,wao wenyewe kiingereza kinawapiga chenga,na ifike muda wajue kiingereza sio lugha yetu. wakae wakijua kuwa siku hazigandi... " what goes around comes around"
 
Mugo"The Great";586772 said:
Wao wanajiona kuwa ni zaidi ya wasanii, lakini "Time will Tell"


kwa kweli wasipojirekebisha wataangukia pabaya! wangekaa na wasanii wenzao waombane msamaha ila wao ndy kwanza wanamwagia petroli kwenye msitu.
 
Wadau, jana hawa jamaa wa Ze comedi wameendeleza uhasama dhidi ya wasanii wenzao wa kutengeneza filamu baada ya kuponda kikao cha wasanii hao kilichofanyika juzi n huku wakijigamba kuwa wao hawatishiki n kwa jeuri zaidi hata wakamkaribisha Manji kwenye kipindi chao...

Je, watakapo fulia kabisa MANJI ataendelea kuwatunza?


USIMCHEKE MAMBA KABLA.........

Wao ni wasanii, na hicho wanachokifanya ni usanii, mi naona kuzidi kuwasema ni kuwapa kichwa, bora watu wawanyamazie 2! Itafikia kipindi watajiona wajinga.
 
kwa kweli wasipojirekebisha wataangukia pabaya! wangekaa na wasanii wenzao waombane msamaha ila wao ndy kwanza wanamwagia petroli kwenye msitu.

Waombe msamaha kwa kosa gani? Mi sioni kosa walilolifanya. Wamewaigiza watu mashuri kuliko huyo Kanumba hamjasema, kusemwa Kanumba imekuwa nongwa? Kanumba alifulia kama ze komedy wanavyoelekea kufulia, hilo halina ubishi.
 
Kweli Nimehamini penye riziki hapakosi fitina, hayo sasa eti "wanahela" yanatoka wapi?? na wenye hela utawaweka wapi? Sawa hata kama "wanavisenti" mimi napenda kuita hivyo, si zao!!? Tuyaache hayo, narudi katika mada yenyewe.
Jamani, wakati tulionao huu ni wa uwazi zaidi, hivi kwanini hatukubali ukweli kwamba mwezetu kalitia haibu taifa letu kule?.Sasa Ze-comedy wanapofikisha ujumbe kwa jamii ki-urahisi zaidi ili wasanii waliopo na wengine wajifunze, tunaaza kujenga na kuweka "informal gathering" vilizojaa lugha za kashfa, chuki, majungu na fitina dhidi yao, badala ya sisi wahusika kujipanga upya katika swala hili la lugha.
Siku zote katika maisha hapa duniani ombea yule anayekukosoa maana anakuwa ana-KUJENGA na kukuimarisha sio KUBOMOA kama wengi wetu tunavyofikilia hapa.
 
Wadau, jana hawa jamaa wa Ze comedi wameendeleza uhasama dhidi ya wasanii wenzao wa kutengeneza filamu baada ya kuponda kikao cha wasanii hao kilichofanyika juzi n huku wakijigamba kuwa wao hawatishiki n kwa jeuri zaidi hata wakamkaribisha Manji kwenye kipindi chao...

Je, watakapo fulia kabisa MANJI ataendelea kuwatunza?


USIMCHEKE MAMBA KABLA.........

Nadhani hii mada haistahili kujadiliwa...

Zekomedi ni comedians. Kumwalika Manji hakuhusiani kitu na suala la Wanafilamu(wanamaigizo) kutokuwa na uelewa wa lugha ya Malkia. Hawa wanafilamu walipewa changamoto kwamba hizo nguvu walizotumia kupinga zekomedi kumuigiza Kanumba wangezihamishia kwenye mambo endelevu kama kupinga piracy, dhuluma kwa kazi zao na kujiendeleza kama wasanii.

Sioni kama Zekomedi wamefanya kosa lolote kwa mtizamo wangu.

Sasa hao wanafilamus ndio mwaona wanafanya sawa? wanajenga nini kupoteza airtime ya television kupinga ujinga?? acheni kuwaonea zekomedi.
 
Kwa mtazamo wangu ze comedy kuna baadhi ya clips wanajenga kupitia kumkosoa mhusika na kufikisha ujumbe ila kuna baadhi ya sehemu wanabomboa au kuharibu.Ile tabia ya joti ya kujambisha binafsi siifagili kabisa....Na kile kipengele cha aliyeeefulia pale wanatakiwa waangalie mbele mana siku hazigandi , ipo siku nao yatakuja kuwafika...ni sawa na kuwatukana wakunga wakati uzazi bado upo.Vijana kwa 65% huwa wanafikisha ujumbe ambao ni kuburudisha watu(kwa vituko vyao) ndo maana wakaitwa hivyo ze comedy
 
Wadau, jana hawa jamaa wa Ze comedi wameendeleza uhasama dhidi ya wasanii wenzao wa kutengeneza filamu baada ya kuponda kikao cha wasanii hao kilichofanyika juzi n huku wakijigamba kuwa wao hawatishiki n kwa jeuri zaidi hata wakamkaribisha Manji kwenye kipindi chao...

Je, watakapo fulia kabisa MANJI ataendelea kuwatunza?


USIMCHEKE MAMBA KABLA.........

Waacheni Ze Comedy wafanye kazi yao bwana,yaani kisa cha thread zote hizi kumuiga Kanumba???,WTf!!!..Anaigwa Pinda na suti zake za rangi mbili,anaigwa JK,wanaigwa waytu wengi tu lakini hamjasema kitu,leo kaigwa Kanumba akiongea PUMBA zake mbele ya mamilioni ya watu duniani wewe unaanza kuwalalamikia Ze komedi,kazi kwelikweli...kuhusu kufulia mkuu,isikusumbue sana,usidhani daima watu watu watakuwa juu...Walikuwepo watu maarufu(angalia wacheza mpira) lakini dakika ya mwisho nao huishia na kuwa chini tu..Unamkumbuka Power Mabula lakini?,jamaa alikuwa na nguvu kama nini,alikuwa anaweza hata kubeba gari ama kuzuia gari lisitembee lakini ilifikia kipindi aliugua kisukari akaokoka,aliishiwa nguvu mpaka Biblia ilikuwa tabu kuibeba,anabebewa...So usiwatishie Ze komedi kuhusu kufulia mkuu,muda ni wao saa hizi waache wautumie ili wakifulia tupate cha kuwakumbukia............
 
Kweli Nimehamini penye riziki hapakosi fitina, hayo sasa eti "wanahela" yanatoka wapi?? na wenye hela utawaweka wapi? Sawa hata kama "wanavisenti" mimi napenda kuita hivyo, si zao!!? Tuyaache hayo, narudi katika mada yenyewe.
Jamani, wakati tulionao huu ni wa uwazi zaidi, hivi kwanini hatukubali ukweli kwamba mwezetu kalitia haibu taifa letu kule?.Sasa Ze-comedy wanapofikisha ujumbe kwa jamii ki-urahisi zaidi ili wasanii waliopo na wengine wajifunze, tunaaza kujenga na kuweka "informal gathering" vilizojaa lugha za kashfa, chuki, majungu na fitina dhidi yao, badala ya sisi wahusika kujipanga upya katika swala hili la lugha.
Siku zote katika maisha hapa duniani ombea yule anayekukosoa maana anakuwa ana-KUJENGA na kukuimarisha sio KUBOMOA kama wengi wetu tunavyofikilia hapa.

Tatizo ni kwamba Ukweli daima unauma saana.
 
Waacheni Ze Comedy wafanye kazi yao bwana,yaani kisa cha thread zote hizi kumuiga Kanumba???,WTf!!!..Anaigwa Pinda na suti zake za rangi mbili,anaigwa JK,wanaigwa waytu wengi tu lakini hamjasema kitu,leo kaigwa Kanumba akiongea PUMBA zake mbele ya mamilioni ya watu duniani wewe unaanza kuwalalamikia Ze komedi,kazi kwelikweli...kuhusu kufulia mkuu,isikusumbue sana,usidhani daima watu watu watakuwa juu...Walikuwepo watu maarufu(angalia wacheza mpira) lakini dakika ya mwisho nao huishia na kuwa chini tu..Unamkumbuka Power Mabula lakini?,jamaa alikuwa na nguvu kama nini,alikuwa anaweza hata kubeba gari ama kuzuia gari lisitembee lakini ilifikia kipindi aliugua kisukari akaokoka,aliishiwa nguvu mpaka Biblia ilikuwa tabu kuibeba,anabebewa...So usiwatishie Ze komedi kuhusu kufulia mkuu,muda ni wao saa hizi waache wautumie ili wakifulia tupate cha kuwakumbukia............

......halafu vile ni vichekesho bana,kama wengine mmechoka kucheka,basi IPOTEZEE tu kivyako,subiria FUTUHII!!!(hawa ndo hamna kitu kabisa),ZE.. kiwango bana huo ndo ukweli
 
Kwa Jonas, kutokujua kiingereza ni kutia aibu taifa kivipi? kiingereza sio lugha yetu ya taifa, watanzania tunaongea kiswahili sio kiingereza. sioni aibu kwa taifa iliyotiwa na kanumba, na sidhani mafanikio ya mtu yanategemea kiingereza. watanzania tuamke sasa na tupendane tuache majungu yasio ya maana. kosa lililofanyika hapa ni kanumba kwenda bila mkalimani, lakini hana sababu ya kujua kiingereza maana sio lugha yake. wajerumani, wafaransa, wa swedish, na wengine wengi hawaongei kiingereza lakini wao wakiburuza kiingereza mnaona sawa kwa vile ni mweupe, lakini kanumba kuwa mweusi, tayari keshatia aibu taifa. hao wenye kudhani kanumba kafanya kosa, ndio wenye kutia aibu taifa, kwa kuthamini lugha za watu wengine na kudharau yao ya asili. hao ze comedi, wala hawanipi tabu, elimu waliyo nayo inasababisha wafanye hayo wanayoyafanya. hata mseme vipi watajibu tu kwa akili zao finyu.
 
Kwa issue ya Kanumba kwamba alichemsha kwenye ngeli hilo halina ubishini ni kiasi cha kujifunza tu kwani lugha yoyote ukijifunza utaimasta.ILa hawa nao inelekea wameishiwa,kwa lugha yao wameanza kufuli.Habari ya kuanza kumuonyesha huyu dogo Mhindi fisadi mara Yanga sijui imefanyaje ni mwanzo wa kufulia.Watafute vitu vingine habari ya kutuonyesha ofisi za quality group na mmiliki wake sidhani kama watanzania tulio wengi tuna interest nayo.Kama anawafadhili watafute jinsi ya kumshukuru ila sio kumuonyesha kwenye Tv ya walipa kodi kimtindo hatummaindi wala nini?
 
wafanyacho ze comedy ni kununua muda tu kwani creation zimeisha na wamejifungia ndani hawataki changamoto.

JAMII IKILALAMIKA MJUE NI SAUTI YA MUNGU. hivyo akina JOTI ambao wanajidhania wamesimama basi waangalie wasianguke
 
Kwa Jonas, kutokujua kiingereza ni kutia aibu taifa kivipi? kiingereza sio lugha yetu ya taifa, watanzania tunaongea kiswahili sio kiingereza. sioni aibu kwa taifa iliyotiwa na kanumba, na sidhani mafanikio ya mtu yanategemea kiingereza. watanzania tuamke sasa na tupendane tuache majungu yasio ya maana. kosa lililofanyika hapa ni kanumba kwenda bila mkalimani, lakini hana sababu ya kujua kiingereza maana sio lugha yake. wajerumani, wafaransa, wa swedish, na wengine wengi hawaongei kiingereza lakini wao wakiburuza kiingereza mnaona sawa kwa vile ni mweupe, lakini kanumba kuwa mweusi, tayari keshatia aibu taifa. hao wenye kudhani kanumba kafanya kosa, ndio wenye kutia aibu taifa, kwa kuthamini lugha za watu wengine na kudharau yao ya asili. hao ze comedi, wala hawanipi tabu, elimu waliyo nayo inasababisha wafanye hayo wanayoyafanya. hata mseme vipi watajibu tu kwa akili zao finyu.

Atlist mkuu wewe umeongea la maana maana wengine walikuwa wanawasuuport kwa kitendo chao cha kumsema mwenzao! Hao ndy wanao thamini lugha za nje ili hali wazungu wenyewe hawashobokei yao.
 
Kwa Jonas, kutokujua kiingereza ni kutia aibu taifa kivipi? kiingereza sio lugha yetu ya taifa, watanzania tunaongea kiswahili sio kiingereza. sioni aibu kwa taifa iliyotiwa na kanumba, na sidhani mafanikio ya mtu yanategemea kiingereza. watanzania tuamke sasa na tupendane tuache majungu yasio ya maana. kosa lililofanyika hapa ni kanumba kwenda bila mkalimani, lakini hana sababu ya kujua kiingereza maana sio lugha yake. wajerumani, wafaransa, wa swedish, na wengine wengi hawaongei kiingereza lakini wao wakiburuza kiingereza mnaona sawa kwa vile ni mweupe, lakini kanumba kuwa mweusi, tayari keshatia aibu taifa. hao wenye kudhani kanumba kafanya kosa, ndio wenye kutia aibu taifa, kwa kuthamini lugha za watu wengine na kudharau yao ya asili. hao ze comedi, wala hawanipi tabu, elimu waliyo nayo inasababisha wafanye hayo wanayoyafanya. hata mseme vipi watajibu tu kwa akili zao finyu.

Dah,bradha...Mkalimani wa nini tena ndani ya jumba la Big bradha????,cha msingi KANUMBA hakuwa na sifa za kwenda ndani ya jumba lile,period..Labda kama ingekuwa inaruhusiwa kuongea Kiswahili na Kisukuma ndo angalau angekuwa na sifa ya kuingia,swali ni nani alimruhusu KANUMBA kwenda kule ilhali wanajua kabisa kwamba ni MAIMUNA na medium ya communication ya pale ni Kiingereza???????????????????
 
Kwa Jonas, kutokujua kiingereza ni kutia aibu taifa kivipi? kiingereza sio lugha yetu ya taifa, watanzania tunaongea kiswahili sio kiingereza. sioni aibu kwa taifa iliyotiwa na kanumba, na sidhani mafanikio ya mtu yanategemea kiingereza. watanzania tuamke sasa na tupendane tuache majungu yasio ya maana. kosa lililofanyika hapa ni kanumba kwenda bila mkalimani, lakini hana sababu ya kujua kiingereza maana sio lugha yake. wajerumani, wafaransa, wa swedish, na wengine wengi hawaongei kiingereza lakini wao wakiburuza kiingereza mnaona sawa kwa vile ni mweupe, lakini kanumba kuwa mweusi, tayari keshatia aibu taifa. hao wenye kudhani kanumba kafanya kosa, ndio wenye kutia aibu taifa, kwa kuthamini lugha za watu wengine na kudharau yao ya asili. hao ze comedi, wala hawanipi tabu, elimu waliyo nayo inasababisha wafanye hayo wanayoyafanya. hata mseme vipi watajibu tu kwa akili zao finyu.

mzee mbona hukuitwa wewe kwenba BB4 kuwakaribisha wawakilishi wa nchi mbalimbali, ameitwa Kanumba kwa sababu yeye ni Celebrity na ilitamkwa kwamba jamaa anatoka Tanzania, hivyo anapochemsha ni aibu kwa Taifa kwa maana hizo ndio product zetu, sasa Ze Comedy wana Tatizo gani kuigiza yaliyojili huko bondeni, mimi nadhani hii ni changamoto kubwa kwa bwana Kanumba kutafuta kozi ya ungenge kwa sababu yeye ni Celebrity na muda wowote anaweza itwa kwenda kwenye maoccasion makubwa kama hayo ili atoe keynote, sasa kwa broken kama ile sijuhi kama jamaa watamwita tena
 
Back
Top Bottom