Elections 2010 Zanzibar yapingana na ZEC-CCM kura ya maoni na Mseto kabla ya uchaguzi mkuu

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
Date::2/18/2010
Mseto Zanzibar baada ya miezi 3

MUUNDO wa Serikali ya Mseto visiwani Zanzibar utajulikana katika kipindi cha miezi mitatu ijayo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Idd Hassan Pandu, amesema.

Alisema hayo jana alipokuwa akizungumza katika mahojiano maalumu na Shirika la Utangazaji Tanzania TBC1.

"Ofisi yangu imekwisha pokea rasimu ya muundo wa Serikali ya Mseto, lakini pamoja na majukumu iliyonayo Zec, itabidi ifanye kazi ya kupokea kura za maoni ndani ya miezi mitatu kuanzia sasa na kisha itoe majibu ya kura hizo za maoni,"alisema Pandu.

Alisema baada ya kupokea muswada huo anaufanyia kazi kabla ya kuuwasilisha Nec kwa ajili ya utekelezaji.

Kwa mujibu wa Pandu, kazi ya Zec itakuwa ni kusimamia mchakato wa kura za maoni kuhusu uanzishwaji wa serikali hiyo.

Hata hivyo Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alisema hakuna umuhimu wa kupiga kura za maoni kuhusu suala hilo kwa kuwa Wanzazibar wamekwisharidhia mfumo huo mpya wa serikali.

Alisema hayo alipokuwa akihojiwa na kituo hicho jana kama ilivyokuwa kwa mwanasheria mkuu huyo wa serikali.

"Kwa kawaida majibu katika kura zozote za maoni ni ndio au hapana. Sasa kwa Zanzibar hili halina umuhimu wowote kwa kuwa tayari wamekwishakubali suala hili,"alisema Dk Bana.

Dk Bana ambaye ni mkuu wa Idara ya Sayansi ya Siasa chuoni hapo pia alieleza sababu za kupinga kura za maoni kuwa ni kuondoa gharama zisizokuwa za lazima katika mchakato huo.

Katika mkutano wa siku mbili wa Nec uliofanyika Jumapili na Jumatatu iliyopita mjini Dodoma chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, pamoja na mambo mengine Nec iliridhia rasmi kuwa mara baada ya matokeo ya uchaguzi visiwani Zanzibar iundwe Serikali ya Mseto.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM John Chiligati alisema NEC imefanya hivyo kwa maslahi ya Zanzibar na Wazanzibar ili kuondoa malumbano na chuki iliyodumu kwa muda mrefu visiwani humo. Alisema tangu NEC iliyokutana Butiama walikubaliana Zanzibar kuwe na Serikali ya Mseto, lakini CUF walisusia mazungumzo hivyo jambo hilo likakosa msukumo.
 
Tuelewe lipi? Huku mseto baada ya uchaguzi ,kule mseto kabla ya uchauzi.
 
Tuelewe lipi? Huku mseto baada ya uchaguzi ,kule mseto kabla ya uchauzi.

Mara pia aina ya huo mseto... naambiwa aina ya mseto wanaotaka CCM si ule ambayo CUF na Karume waliokubaliana.

Kwa kweli tusubiri tuone.
 
J.K.angeulizwa kama ule mseto alioupendekeza kule Kenya, alipendekeza na kura ya maoni pia!! Wanategemea wakati wa uchaguzi wataiba kura ili CCM ishinde kwa asilimia nyingi, waghairi kura za maoni!!
 
J.K.angeulizwa kama ule mseto alioupendekeza kule Kenya, alipendekeza na kura ya maoni pia!! Wanategemea wakati wa uchaguzi wataiba kura ili CCM ishinde kwa asilimia nyingi, waghairi kura za maoni!!

I trust Zanzibaris wakiamua kitu huwa hawaangalii nyani usoni hakuna cha ZEC wala Msekwa najua itaundwa kabla ya uchaguzi ngonjera ziko huku bara
 
Date::2/18/2010
Mseto Zanzibar baada ya miezi 3

Katika mkutano wa siku mbili wa Nec uliofanyika Jumapili na Jumatatu iliyopita mjini Dodoma chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, pamoja na mambo mengine Nec iliridhia rasmi kuwa mara baada ya matokeo ya uchaguzi visiwani Zanzibar iundwe Serikali ya Mseto.

Mimi naona kama CCM bara ndiyo inayoendeleza mvurugano kwa Wanzibar. Kama wamekubaliana kuanzisha serikali ya mseto, kwa nini kuipeleka hadi baada ya uchaguzi halafu yawe magumu kutekeleza baada ya kuingia kiongozi mpya? Je, wanauhakika wa kushinda ili wawashirikishe wapinzani? Je wasiposhiwashirikisha wapinzani sasa na upinzani ukitokea kushinda na wakikataa kuanzisha hiyo srikali ya kitaifa itakuwa je?
Kweli ccm kinakuwa chama cha kuvuruga maendeleo ya Mtanzania. Ndio maana naamini kuwa ccm inafurahia kiwango kidogo cha uelewa wa watanzania ili waendelee kutawala!

Lowasa aliwahi kusema Morogoro kuwa watawala kwa zaidi ya miaka 100 ijayo, lkn sasa naona anashuhudia jinsi ilivyovigumu kufikia mategemeo yake!
 
asanteni wa znz, toeni somo la umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu, maana kama mkiungana, mtaweza kufika pale ambapo wengi huku bara tunaona kama ndoto.
 
J.K.angeulizwa kama ule mseto alioupendekeza kule Kenya, alipendekeza na kura ya maoni pia!! Wanategemea wakati wa uchaguzi wataiba kura ili CCM ishinde kwa asilimia nyingi, waghairi kura za maoni!!

Nafikiri sasa umefika wakati wa mambo ya Tanzania kujadiliwa na NEC-CCM, I mean yale yanayohusu muungano tu na mambo ya Zanzibar kujadiliwa na CCM-Zanzibar with mwenyekiti wa CCM Taifa only akiwa kutoka bara kama Mtazamaji tu.

Unajua watu wengi wa NEC-CCM wanatoka bara na hawana ujuzi wowote kuhusu Zanzibar bali wanaenda kishabiki tu. Hawa hawapaswi kuhusishwa katika mustakabali wa Zanzibar kwani ni wavurugaji (Tukianza na Makamba No. 1)

Wapenda madaraka wa bara wanaliangalia hili kwa mtazamo wa likianzia Zanzibar likafanikiwa basi na bara kutawaka moto na sisi kulazimishwa kufuata huko. Dawa hapa ni divide and rule strategy, wazanzibar wakipingana kwa misingi ya CUF na CCM basi bara tunanawiri kwani tutakuwa na nguvu ya kuwaburuza CCM Zanzibar kwani wanahitaji ulinzi wetu ili wawadhibiti CUF
 
Re: Zanzibar yapingana na ZEC-CCM kura ya maoni na Mseto kabla ya uchaguzi mkuu

Hiki kichwa cha habari ni cha kifitina na cha kupotosha. Ni wapi pameandikwa kuwa Zanzibar inapingana na ZEC-CCM?
 
Tuelewe lipi? Huku mseto baada ya uchaguzi ,kule mseto kabla ya uchauzi.

Hili linaeleweka bila shida. Kura za Maoni zitafanyika kabla ya uchaguzi kwa nia ya kuamua ni upi utakuwa mfumo wa serikali ya mseto utakavyokuwa baada ya uchaguzi.
 
Hiki kichwa cha habari ni cha kifitina na cha kupotosha. Ni wapi pameandikwa kuwa Zanzibar inapingana na ZEC-CCM?

Kubwajinga jaribu kusoma tena Zanzibar wamesemaje na Zec-CCM ilisemaje Zanzibar wamesema kura ya maoni ndani ya miezi mitatu wakati Zec CCM walisema kula ya maoni ni baada ya uchaguzi kweli huoni tofauti
Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Idd Hassan Pandu, amesema.
"Ofisi yangu imekwisha pokea rasimu ya muundo wa Serikali ya Mseto, lakini pamoja na majukumu iliyonayo Zec, itabidi ifanye kazi ya kupokea kura za maoni ndani ya miezi mitatu kuanzia sasa na kisha itoe majibu ya kura hizo za maoni,"alisema Pandu.

kama bado huoni tofauti basi kweli wewe ni Kubwajinga
 
Kubwajinga jaribu kusoma tena Zanzibar wamesemaje na Zec-CCM ilisemaje Zanzibar wamesema kula ya maoni ndani ya miezi mitatu wakati Zec CCM walisema kula ya maoni ni baada ya uchaguzi kweli huoni tofauti


Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Idd Hassan Pandu, amesema.


"Ofisi yangu imekwisha pokea rasimu ya muundo wa Serikali ya Mseto, lakini pamoja na majukumu iliyonayo Zec, itabidi ifanye kazi ya kupokea kura za maoni ndani ya miezi mitatu kuanzia sasa na kisha itoe majibu ya kura hizo za maoni,"alisema Pandu.


kama bado huoni tofauti basi kweli wewe ni Kubwajinga
Luteni umezoea uchochezi na ndio maana hata vitu unavyobandika mtandaoni husomi badala yake unajitungia tu vichwa vya habari vya kifitina. Sasa ngojea nikufundishe kwa kutumia maandiko yako mwenyewe.

CCM-ZNZ said:
"Ofisi yangu imekwisha pokea rasimu ya muundo wa Serikali ya Mseto, lakini pamoja na majukumu iliyonayo Zec, itabidi ifanye kazi ya kupokea kura za maoni ndani ya miezi mitatu kuanzia sasa na kisha itoe majibu ya kura hizo za maoni,"alisema Pandu.

CCM-TZ said:
Katika mkutano wa siku mbili wa Nec uliofanyika Jumapili na Jumatatu iliyopita mjini Dodoma chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, pamoja na mambo mengine Nec iliridhia rasmi kuwa mara baada ya matokeo ya uchaguzi visiwani Zanzibar iundwe Serikali ya Mseto.

Tafsiri ya huo mchakato ni kuwa kunakuwa na kura za maoni (kama alivyosema Pandu)----halafu-----Uchaguzi (Kama walivyosema CCM-NEC)-----halafu------Serikali ya Mseto Inaundwa (Kama wote walivyosema).

Sasa ni nini kisichoeleweka mpaka kuandika fitina?
 
Maamuzi ya Zanzibar yanaamuliwa na wazanzibari wenyewe, NEC hawana mpango wowote ni wazushi tuu.

Aliyosema Mwanasheria mkuu Zanzibar ni sawa na makubaliano yaliyopitishwa ndani ya BLW.Sasa kama NEC/Chiligati wana uwezo wa kubatilisha maamuzi ya chombo cha wazanzibari...tutaona..only time will tell!
 
Luteni umezoea uchochezi na ndio maana hata vitu unavyobandika mtandaoni husomi badala yake unajitungia tu vichwa vya habari vya kifitina. Sasa ngojea nikufundishe kwa kutumia maandiko yako mwenyewe.


Tafsiri ya huo mchakato ni kuwa kunakuwa na kura za maoni (kama alivyosema Pandu)----halafu-----Uchaguzi (Kama walivyosema CCM-NEC)-----halafu------Serikali ya Mseto Inaundwa (Kama wote walivyosema).

Sasa ni nini kisichoeleweka mpaka kuandika fitina?

Kubwajinga nenda kwenye tovuti ya CCM uone tamko la Nec kuhusu serikali ya Mseto Zanzibar si kubisha tu wakati Zanzibar wanasisitiza ni kabla ya uchaguzi mchochezi ni nani CCM mmezoea mtu akisema ukweli anakuwa mchochezi soma kipengele chenu cha tamko la Nec


(v) Halmashauri Kuu ya Taifa imetoa maelekezo kwa Kamati Maalumu (Zanzibar) na viongozi wa CCM wa ngazi zote Tanzania Zanzibar wafanye kazi ya kutoka elimu kwa umma kuhusu maana na manufaa ya Serikali Shirikishi inayotarajiwa kuundwa baada ya Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba, mwaka huu.
 
Kubwajinga nenda kwenye tovuti ya CCM uone tamko la Nec kuhusu serikali ya Mseto Zanzibar si kubisha tu wakati Zanzibar wanasisitiza ni kabla ya uchaguzi mchochezi ni nani CCM mmezoea mtu akisema ukweli anakuwa mchochezi soma kipengele chenu cha tamko la Nec


(v) Halmashauri Kuu ya Taifa imetoa maelekezo kwa Kamati Maalumu (Zanzibar) na viongozi wa CCM wa ngazi zote Tanzania Zanzibar wafanye kazi ya kutoka elimu kwa umma kuhusu maana na manufaa ya Serikali Shirikishi inayotarajiwa kuundwa baada ya Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba, mwaka huu.
Luteni,
Usifanye mambo kwa chuki na fitina bila ya sababu. CCM wamesema wazi kwenye hilo tamko lao ulilobandika hapo juu na kwenye original posting yako kuwa serikali ya mseto ni baada ya uchaguzi.

Sasa kama huelewi kuwa kura za maoni ni kabla ya huo uchaguzi basi jaribu kuuliza wengine maana naona mimi sitaweza kukutafunia zaidi ya nilivyofanya hapo awali na kwa mara ya mwisho hapa chini.

Kura za maoni (in 3months)====>Uchaguzi Mkuu (Oct,2010)====>Serikali ya Mseto(baada ya Oct,2010)

Je, umeelewa?
 
Maamuzi ya Zanzibar yanaamuliwa na wazanzibari wenyewe, NEC hawana mpango wowote ni wazushi tuu.

Aliyosema Mwanasheria mkuu Zanzibar ni sawa na makubaliano yaliyopitishwa ndani ya BLW.Sasa kama NEC/Chiligati wana uwezo wa kubatilisha maamuzi ya chombo cha wazanzibari...tutaona..only time will tell!
Endelea kuota ndoto za mchana.
 
Luteni,
Usifanye mambo kwa chuki na fitina bila ya sababu. CCM wamesema wazi kwenye hilo tamko lao ulilobandika hapo juu na kwenye original posting yako kuwa serikali ya mseto ni baada ya uchaguzi.

Sasa kama huelewi kuwa kura za maoni ni kabla ya huo uchaguzi basi jaribu kuuliza wengine maana naona mimi sitaweza kukutafunia zaidi ya nilivyofanya hapo awali na kwa mara ya mwisho hapa chini.

Kura za maoni (in 3months)====>Uchaguzi Mkuu (Oct,2010)====>Serikali ya Mseto(baada ya Oct,2010)

Je, umeelewa?

Tatizo lako unajibu kwa ukereketwa zaidi kwanza mlisema haitawahi tokea serikali ya mseto kati ya CCM na CUF halafu mkasema kura ya maoni baada ya uchaguzi mkaona zanzibar ni moto Nec yenu imenywea imebadili tena kura ya maoni kabla ya uchaguzi hata mseto utakuwa kabla ya uchaguzi wale jamaa hawatishwi eti na NEC wao wana NEC yao wamesema Mseto kabla ya uchaguzi hakuna cha Msekwa Makamba wala nani Period
 
Tatizo lako unajibu kwa ukereketwa zaidi kwanza mlisema haitawahi tokea serikali ya mseto kati ya CCM na CUF halafu mkasema kura ya maoni baada ya uchaguzi mkaona zanzibar ni moto Nec yenu imenywea imebadili tena kura ya maoni kabla ya uchaguzi hata mseto utakuwa kabla ya uchaguzi wale jamaa hawatishwi eti na NEC wao wana NEC yao wamesema Mseto kabla ya uchaguzi hakuna cha Msekwa Makamba wala nani Period
Vipi, Mbona huongelei tena kichwa cha habari nilichokwambia ni cha kichochezi?
 
Niliwahi kusema katika thread nyuma kuwa ukisikia changa la macho ndio hili hivi inawezekana kweli ukasimamia daftari la uchaguzi huku serikali ya mseto na maandalizi ya uchaguzi mkuu!!! I doubt it wanachofanya CCM ni delaying tactics kwasababu wanajua wameshawazidi kete CUF katika daftari wanabuy time uchaguzi upite waitishe hiyo serikali ya mseto but CUF wakati huo itakuwa weak waseme hawana nafasi ya kuunda serikali mwisho wa siku inarudi serikali ile ile..
 
Back
Top Bottom