Zanzibar yagoma kugharamia Katiba ya Muungano

Hivi serikali ya Muungano ni nini wakuu......? Hivi vila urojo vinakera sana na ndo maana Tundu akizungumza ukweli vinakasirika. Where's my gun?
 
Magamba walikuwa busy sana bungeni kutukana CHADEMA. Sasa nadhani wanashindwa hata namna ya kujicheka wao wenyewe. Wenzao wa CUF kama kawa wamewaingiza mkenge. Kweli CCM hamnazo. Bora Uwe chizi kuliko kuliko kuwa CCM.
 
Inawezekanaje watu wawili wawaunganishe watanganyika na wazanzibar wote kwa nguvu ya bakora? Huu muungano ni non-starter since day one.
 
Serikali ya Mapinduz ya zanzibar imesema kamwe haitachangia gharama za mchakato wa kuunda katiba mpya,imedai kuwa jukumu la kugharamia ni la Serikali ya Jamhuri ya Muungano
sosi:NIPASHE,25 N0VEMBER,2011

Sasa unashangaa nini? Kwani serikali ya muungano ililipia gharama za kutengeneza katiba ya Zanzibar?
 
Sasa ndiyo mtajua Lissu kichwa na Chadema wanaona mbali .Mliwatukana sasa mnaonyeshwa kwa matendo sasa semeni tena nyie CCM na CUF nani hautaki Muungano ?
 
Sasa unashangaa nini? Kwani serikali ya muungano ililipia gharama za kutengeneza katiba ya Zanzibar?

No ndugu,haikulipa,kumbuka kila nchi ktk muungano inatakiwa ijitegemee kwa mambo yasiyohusu muungano,sasa usichanganye mambo hapa,SMZ inatakiwa ichangie kwenye kuunda katiba ya muungano,jiulizd kwamba,kwa nini wanagombea usawa wa nafasi mbalimbali ktk mambo yote ya muungano? Mpaka kushiriki ktk mcchakato mzima wa katiba,sara wamekubaliwa kupewa a third ya nafasi na maamuzi yatategemea mashauriano ya marais hawa, swali gumu ambalo hata wao wameingia mkenge bila kujibu ni kwamba,nchi mwenza atakiwae kuchangia pia ni ipi? Tanganyika si haipo! Ni bora waelewe km mambo yataenda hv basi watachangia sana peke yao,na walifikira kukinga tu! Ss wanatakiwa kutoa which is factual to us!
 
kwani hata wangesema watachangia wangetoa wapi hela,umeme tu wanadaiwa,ni sawa na mwanao unayemlea,kila siku unampa mtaji wa biashara anakula,huwezi ukaanzisha partnership naye kwenye biashara yoyote. Waende zao na muungano uvunjike tu
 
Katiba inayo badilishwa ni JMT na si ya zanzibar sasa wao wachangie nini?
Wamo ktk huo muungano,ukisema hivyo unamaana hawastahili kuwemo kwenyo mijadala then! The equation inawapa haki ya kushiriki ktk mchakato hence kuchangia pia au ndo unamwono wa ladies first? Kwenye kula raha tu,kwenye matatizo wawe wamwisho,hakuna hiyo,wanachotakiwa ni kugombea kwamba nchi mwenza atambulike ili usawa wa kuchangia uwepo!
 
Back
Top Bottom