Zanzibar will not sustain itself without Union –Sitta: Says currently Mainland meets most of cost in

... Walikula kiapo kulinda Katiba hii na Muungano huu sasa wanapata wapi ujasiri wa kutaka Muungano uvunjwe? Au waliapa hawakujua wanachoapa ni kitu gani?
Constitutional Law 101:

KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
98.Utaratibu wa kubadilisha Katiba hii na baadhi ya sheria.

1) Bunge laweza kutunga Sheria kwa ajili ya kubadilisha masharti yoyote ya Katiba.

2) Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya ibara ndogo ya (1) kubadilisha masharti ya Katiba hii au masharti ya sheria maana yake ifahamike kuwa ni pamoja na kurekebisha au kusahihisha masharti haya au kufuta na kuweka masharti mengine badala yake au kusisitiza au kubadilisha matumizi ya masharti hayo.

Maana yake nini?

Ukiapa kulinda katiba unaapa kulinda na kuheshimu kila ibara. Moja ya ibara hizo, ya 98, imelipa ruhusa Bunge kusaili kurekebisha, kufuta kipengele chochote cha katiba kwa kufuata taratibu. Moja ya hatua za taratibu za kufuta vipengele vya Katiba ni kupigiwa kura na Wabunge. Sasa kabla ya kura huwa kuna majadiliano Bungeni. Hivyo, Mbunge anaweza kujadili chochote ikiwemo kutaka kufutwa kwa vipengele vya Katiba, ukiwemo Muungano, bila kuambiwa anavunja Katiba.

Kwa nini?


Kwa sababu, adhama moja kubwa ya Katiba hii ni kuwa imesema hakuna kitu ambacho hakizungumziki, chochote kinaweza kurekebishwa, nini kurekebishwa, kinaweza kufutwa, bila ya kusema mjadala wa kufuta masharti fulani ya Katiba unavunja kiapo cha kulinda Katiba.

Na ndio maana Rais Kikwete aliyekula kiapo cha kwanza cha kulinda Katiba aliruhusiwa na Ibara ya 98 kutangaza kuwa Katiba hii sasa tunakwenda kuifuta. Kwa sababu chochote na lolote kikatiba linaweza kufutika, na Muungano nao, kwa hiyo, unafutika.

Na sidhani kama Muungano uta survive Katiba mpya katika sura uliyo nayo sasa. Thank God Katiba inaruhusu, thank God. Mzee Mwanakijiji si mwanafunzi mbaya sana wa masuala ya kikatiba na kisiasa ya Tanzania, utakuwa umeelewa.

 
[h=1][/h]Written by Hassan10 // 11/07/2011 // Habari // No comments

Sitta avaa (?) kinga wakati kachaingia mimba.

Mimi nilishangazwa sana kumuona Samul Sitta akijiona Hiro kumbe shushu lakufutia mavi, na huku wenzake wakimpigia makofi haliyakuwa anawaaibisha na kuwazalilisha, Jee Wzanzibar muko tayari kana na kuikataa Zanzibar yenu?.

Kwa hiyo opening statement mtoa mada umejidhalilisha.
Mimi sikuendelea kusoma the rest of the paragraphs.
Kimsingi uchafu ulio moyoni mwa Abdulasahaf, ni sawaswa na anachokiongelea kwenye post hii.
Hapo ni pole tu
 
kelele zote za nini? Sita kasema bila kumung'unya maneno, uwezo wenu mdogo saana, kama hamtaki tuvunje sasa kama kweli wabunge wa Zanzibar ni jabali si wangetoka majengoni? wawakilishi nao kimi huko kwenye kakiota kao. Wazanzibar mnapenda mno kubebwa kama nyumba ndogo, safari hambembellezwi ng'o mziki moja tu, hamtaki maamuzi ya bara basi nendeni. Watu hata hamjui mnachoongelea, uchumi wa Zanzibar haufikii hata nusu ya uchumi wa wilaya ya Kahama peke yake.
Watu mnashinda mmevaa taulo hamfanyi kazi leo mnasema bara inawanyonya.

Kuna mada huko nyuma inayowafananisha ndugu zetu hawa na wanawake.
Huwa wanpenda kutunzwa na si kufanya kazi.Wengine wanaona haya ni matusi lakini ndio ukweli wenyewe.
Wakitaka kuvunja muungano Wazenji ondokeni mjengoni Dodoma leo hii ilimueleweke na dunia ifahamu.
Watanganyika hatuta sikitika sana mkifanya maamuzi hayo magumu kwenu.
Na sisi gharama za kuwabeba beba zitapungua.
 
Bila Muungano Zanzibar will do better than now tuangalie facts
  • The smaller the country the easier managed, tunaona hata Rwanda sasa, tatizo la nchi za Africa ni Uongozi mbovu lakini nchi ikiwa ndogo tatizo hili linaweza kupungua
  • Free Port ya Zanzibar inaweza kuifanya Zenji iwe Business Hub ya East Africa, we might all need not go to Dubai kufata bidhaa zetu
  • Karafuu na Tourism inaweza ikasustain Wanzanibar for Free Education, Health and even manage to pay the homeless
Kwahiyo wakuu Zanzibar ikijitenga na kupata uongozi bora inaweza ikaprosper na kuwa one of the rich countries
Poor reasoning! USA is much bigger than Rwanda but excellently managed!
 
Sielewi kabisa kwanini wanaotaka Muungano uvunjike hawatoki kwanza Bungeni na kwenye Baraza la Wawakilishi na kuanzisha movement ya kutaka Muungano uvunjike? Walikula kiapo kulinda Katiba hii na Muungano huu sasa wanapata wapi ujasiri wa kutaka Muungano uvunjwe? Au waliapa hawakujua wanachoapa ni kitu gani?

Mwanakijiji,

Sita hapa aliongea kama kiongozi wa shughuli za serikali bungeni yaani kama kaimu waziri mkuu. Kwa maana nyingine hilo lilikuwa tamko la serikali ya JMT, kwa hiyo amesema peupe kama wana jambo waseme peupe wanataka nini na akwambia kama Zanzibar inataka serikali tatu tuvunje muungano. Na ametolea mifano jinsi gharama za kuiendesha serikali ya muungano zinavyo bebwa na bara, kwa mara ya kwanza tumejua Zanzibar haichangii hata senti kunedesha serikali ya muungano. Sasa kama wazanzibari walikuwa na ubavu wangetoka majengoni, mbona walikaa kimia? na huko baraza la uwakilishi wamenywea kama kuku kamwagiwa maji.

Hili hata raisi kikwete wakati wa mtafaruku juu ya kauli ya Pinda kuwa Zanzibar ni nchi au lah, aliwaambia kama kuna kitu wanataka waseme, sasa kwa nini wazanzibar wanaogopa kusema? waache unafiki,
 
Kuna mada huko nyuma inayowafananisha ndugu zetu hawa na wanawake.
Huwa wanpenda kutunzwa na si kufanya kazi.Wengine wanaona haya ni matusi lakini ndio ukweli wenyewe.
Wakitaka kuvunja muungano Wazenji ondokeni mjengoni Dodoma leo hii ilimueleweke na dunia ifahamu.
Watanganyika hatuta sikitika sana mkifanya maamuzi hayo magumu kwenu.
Na sisi gharama za kuwabeba beba zitapungua.

Mkuu bado hilo litabakia kuwa ni tusi tu.

Mara nyingi mkishindwa au mkikosa hoja, matusi ndio kimbilio lenu.

Lugha za kejeli hazisaidii maana Zanzibar ni partner katika "muungano" huu

Mlipoivamia Zanzibar, mliikuta nchi ambayo ikijitegemea kwa kila kitu. Sasa Zanzibar mmeifisidi kama mnavyoendelea kuifisidi nchi yenu tajiri lakini wananchi wake maskini.

Tutaondokaje Dodoma na nyinyi mnataka tuwepo kwa kutuvamia kijeshi?

Ondoeni majeshi yenu ya uvamizi, muone kama Zanzibar huru ikichipuka.

Mpaka umeme mnatupa bure kubembeleza "muungano" usivunjike.

Mnaofaidi ni nyinyi na nyinyi ndio mtaohasirika huu "muungano" wenu wa kulazimisha ukivunjika.

Zanzibar will rise again from Tanganyika occupation.

Keep watching these pages Mkuu.
 
Mrdash1,
Pitia historia ya Zanzibar uone kama iliwahi kuwa kama Iran au kama Saudia!

Pia Jaji Agostino Ramadhani anaweza kukusaidia katika haya mambo ya Uislamu na ukristo Zanzibar.

Muungano at any cost kulinda heshima ya mtu mweusi......Hapa Tanganyika tuna wazawa na mafisadi. Juhudi tungezifanya kuweka utawala bora ili wazawa wanufaike na rasilimali,hapo heshima ya mzawa aka mtu mweusi ingejengeka. Sasa tunawauzia,tunawagawia kila chetu wazungu,waarabu,wahindi kwa tamaa ya 10%. Heshima ya mtu mweusi iko wapi hapa ,mkuu?

Zanzibar ina mchanganyiko wa watu,weusi na weupe kama ilivyo kawaida ya visiwa. Haya mambo ya utumwa na utwana ni siasa zilizopitwa na wakati. Ni karata ya turufu kwa CCM. CCM wanapopanga wizi wa kura husema.."kulinda mapinduzi"...heshima ya mtu mweusi.

Kwa muungano huu uliopo ni suala la muda tu. Kama "kero", mimi husema mazingaombwe kama hayatasitishwa basi tunatengeneza maafa kwa siku zijazo.

Huu mjadala unaweza kuuendeleza bila kufikia mwisho sababu hutaki kuelewa sababu za msingi kama ifuatavyo:
1. hapa tanganyika ccm inagawa raslimali za nchi kwa ujinga na tamaa ya viongozi, ipo siku wananchi watapata viongozi makini na hizo raslimali zitarudi kama alivyofanya mwl JK (RIP) mwaka 1967. Hata hivyo hapa tanganyika hutajakabidhi mamlaka ya dola kwa wahindi, waarabu nk kama mnavyotaka kufanya huko zanzibar, hatukubali kamwe!!!! bora umaskini kuliko fedhea.
2. Hata kama mtalazimishia kuvunja muungano uliopo leo hii, haitachukua muda mrefu kabla ya mapinduzi ya pili ambayo yatakuwa mabaya zaidi kuliko ya mwanzo kwa familia na mali zenu, you have been warned!!!!
3. huwezi kusema utumwa na utwana ni mambo ya zamani wakati hadi hivi leo wanzanzibari wahindi waarabu na wamanga na wamangakoko wanaendelea kudharau na kukashifu watu weusi hasa wa bara. Ati wanajiona wao ni watu bora????? fikiria mwenyewe itakuwaje wakishika madaraka ya dola.
4. Muungano kulinda heshima ya mtu mweusi zanzibar na afrika kwa ujumla siyo propaganda ya ccm, it is a fact, nyie mnalijua hilo ndo maana ugomvi wenu na muungano haukomi, mnajua fika bila muungano wazanzibari weusi watakuwa dhaifu na hawata weza kuhimili harakati zenu zenye marefu kutoka uarabuni na india
5. Mnawalaghai na kuwadhoofisha watu weusi kwa kutumia imani yao ya dini ya kiislam, badala ya kuhubiri maadili ya dini misikitini, mnafundisha watu wachukie viongozi wanaodumisha muungano. Nani kakwambia kuwa mzanzibari hawezi kuwa muislam safi kama ana support muungano? Achane udanganyifu na ulaghai bana, simameni kiume kama babu zenu walivyosimama wakati wa mapinduzi na wakatolewa nyongo.
 
The Union between Tanganyika and Zanzibar is an assymetrical federation with the latter being a "de facto" autonomous republic. What I never understand is why some Tanzanians ( I mean Tanganyikans) keep supporting this loveless marriage to Zanzibar. The earlier this union is dissolved the better for everyone involved. The myth that there are security benefits from the Union are just myths and fallacies. The good thing about breaking up the Union is that Tanzania does not have to change anything, we can retain the flag, the name (United Republic of Tanzania) and everything else. Only Zanzibar will become the Republic of Zanzibar, a sovereign state. Dissolution of this Union is win for all option.
 
Each of us must speak. Each must decide what is right and what is wrong on our Union between the two nation Tanganyika and Zanzibar & Pemba and flung aside at the bullying of the pulpit, press, government, or the empty catchphrases of our politicians. In a long run there is no instance of a nation benefitting from prolonged warfare.

We have to decide now rather than later to be an unqualified and inexcusable traitor, both to yourself and to your countries (Tanganyika & Zanzibar).

So, at the end when we make a rightly decision to either break the Union or keep the Union Our loyalties must transcend our race, our tribe, our religion, and our nations; and this means we must be part of develop a World perspective.
 
Huyu samwel sitta

amekosa uspika

naona na uwaziri hautaki

na ubunge ataukosa
 
I told you before..kuna watu kukaa ktk madaraka kumewapumbza sana...like SS he is becoming irrational as days go on. Nafikiri umri ndio shida sasa hapa. He is a desperate person..,you know CCM is done with him sasa anahangaika kutafuta credits..SS muda wako umeshapita get it. Hizi kauli za mfa mja hazitakufikisha popote.

Hivi before Muungano ZNZ ilikuwa injisustain vipi? Hivi ni nani anafikiri waznz hawana resources? Na mwenye akili afuatilie aone ni visiwa vipi vilivyopo duniani vinasurvive kwa sababu ya miuungano.

I think EL is far better than SS.
 
kwani kabla ya muungano Zanzibar ilikuwa inajiendeshaje ? mpaka waziri aseme muungano ukifa znz nayo itashindwa kujiendesha kama ndio hivyo mbona wanataka muungano uvunjwe ? tuache maneno mengi rekebisheni kero za muungano

Mkuu Zanzibar haikuwahi kujiendesha kwa muda mrefu kumbuka Mapinduzi yalifanyika tarehe 12/01/1964 na Muungano ukafanyika 26/04/1964 unaweza kuona ni muda gani Zanzabar iliishi, hiyo miezi mitatu haitoshi kufahamu uelekeo kamili wa maisha ya Wazanzibari.

Maisha Zanzibar yataendelea kuwepo bila Muungano, hilo sina shaka kwa sababu maisha anatoa mwenyezi Mungu mwenyewe. Kama Wazanzibari hawaoni faida za Muungano tuwaache waende zao na tuwatakie maisha mema siku za usoni.

Ndoa ni makubaliano ya pande mbili, kama upande mmoja utaamua kuvunja ndoa hiyo hakuna jinsi, ni lazima ndoa ivunjike!
 
Mkuu bado hilo litabakia kuwa ni tusi tu.

Mara nyingi mkishindwa au mkikosa hoja, matusi ndio kimbilio lenu.

Lugha za kejeli hazisaidii maana Zanzibar ni partner katika "muungano" huu

Mlipoivamia Zanzibar, mliikuta nchi ambayo ikijitegemea kwa kila kitu. Sasa Zanzibar mmeifisidi kama mnavyoendelea kuifisidi nchi yenu tajiri lakini wananchi wake maskini.

Tutaondokaje Dodoma na nyinyi mnataka tuwepo kwa kutuvamia kijeshi?

Ondoeni majeshi yenu ya uvamizi, muone kama Zanzibar huru ikichipuka.

Mpaka umeme mnatupa bure kubembeleza "muungano" usivunjike.

Mnaofaidi ni nyinyi na nyinyi ndio mtaohasirika huu "muungano" wenu wa kulazimisha ukivunjika.

Zanzibar will rise again from Tanganyika occupation.

Keep watching these pages Mkuu.

Madagascar ni kisiwa kikubwa kuliko hata hivyo vijisiwa vyenu manvyoringa navyo, mbona wao hawajaendelea? Fanyeni kazi acheni uvivu mtafanikiwa tu hata kama ni ndani ya Muungano. Tanzania ni nchi maskini lakini bado kuna watu wenye shughuli zao halali wanaishi poa kuliko hata wazungu wa huko Ulaya. Badilikeni kifikra.

Usipotoshe umma, Tanganyika haikuwahi kuivamia Zanzibar bali ni upeo mdogo wa viongozi wenu walioingizwa mitini na wajanja wa bara. Fuateni taratibu za kisheria mtajitenga tu!
 
Huu mjadala unaweza kuuendeleza bila kufikia mwisho sababu hutaki kuelewa sababu za msingi kama ifuatavyo:
1. hapa tanganyika ccm inagawa raslimali za nchi kwa ujinga na tamaa ya viongozi, ipo siku wananchi watapata viongozi makini na hizo raslimali zitarudi kama alivyofanya mwl JK (RIP) mwaka 1967. Hata hivyo hapa tanganyika hutajakabidhi mamlaka ya dola kwa wahindi, waarabu nk kama mnavyotaka kufanya huko zanzibar, hatukubali kamwe!!!! bora umaskini kuliko fedhea.
2. Hata kama mtalazimishia kuvunja muungano uliopo leo hii, haitachukua muda mrefu kabla ya mapinduzi ya pili ambayo yatakuwa mabaya zaidi kuliko ya mwanzo kwa familia na mali zenu, you have been warned!!!!
3. huwezi kusema utumwa na utwana ni mambo ya zamani wakati hadi hivi leo wanzanzibari wahindi waarabu na wamanga na wamangakoko wanaendelea kudharau na kukashifu watu weusi hasa wa bara. Ati wanajiona wao ni watu bora????? fikiria mwenyewe itakuwaje wakishika madaraka ya dola.
4. Muungano kulinda heshima ya mtu mweusi zanzibar na afrika kwa ujumla siyo propaganda ya ccm, it is a fact, nyie mnalijua hilo ndo maana ugomvi wenu na muungano haukomi, mnajua fika bila muungano wazanzibari weusi watakuwa dhaifu na hawata weza kuhimili harakati zenu zenye marefu kutoka uarabuni na india
5. Mnawalaghai na kuwadhoofisha watu weusi kwa kutumia imani yao ya dini ya kiislam, badala ya kuhubiri maadili ya dini misikitini, mnafundisha watu wachukie viongozi wanaodumisha muungano. Nani kakwambia kuwa mzanzibari hawezi kuwa muislam safi kama ana support muungano? Achane udanganyifu na ulaghai bana, simameni kiume kama babu zenu walivyosimama wakati wa mapinduzi na wakatolewa nyongo.

Mkuu Mrdash1.
Nimezipenda hoja zako. Ni hoja nzito sana.
Hoja zako ni kama hoja za Sitta. Sawa tuendelee "kulinda heshima ya mtu mweusi"
Sikufahamu kuwa Lissu pia ni kimangakoko.

Kwa uzito wa lugha yako na hoja zako ni bora mjadala tusiuendeleze.Hapa iwe mwisho.
CCM...juuu! CCM....juuu! CCM........ nambari one! Mapinduziiiii....Daimaaaa!

Na wizi wa kura na kubadilisha matokea pia ni kwa ajili ya kulinda heshima ya "mtu mweusi"?

Karibu Tanganyika...Gongo la mboto!
 
Something is very wrong na hii statement ya Mh Sitta. Essentially anashauri Zanzibar ibakie kwenye Muungano maan nje ya Muungano hawataweza kujiendesha (watakufa njaa), wakati huo huo anashauri Tanganyike ibakie kwenye Muungano ili TU kuwasadia Zanzibar (charity gesture?).

Pengine ni vizuri sasa wananchi aina, faida, kasoro na umuhimu wa muungano maana kwa maelezo kama haya ya Mh.Sitta inaonekana kama hakuna hasa sababu za msingi za muungano apart from Charity...!
Duh, hatari sana!
Kwamba sababu ya muungano ni charity !!!
 
Back
Top Bottom