Zanzibar: Watoto Wanne wafa kwa kukosa hewa baada ya Milango ya gari kujifunga

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,888
e38ced33f1dfba1c77176b2cc256e7a9.jpg

Watoto wanne wenye Umri wa Miaka kati ya Miwili na Mitatu wa Familia tofauti Mjini Unguja, wamefariki dunia baada ya kushindwa kutoka nje ya gari walilokuwemo kutokana na milango ya gari hiyo kujifunga hali iliyosababisha kukosa hewa.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mjini Magharibi Hassan Ali Nasser amethibitisha kutokea kwa tukio hilo katika eneo la Kidongo Chekundu.

======

Watoto wanne wamefariki dunia baada ya kujifungia kwenye gari kwa muda mrefu huko katika maeneo ya kidongo Chekundu Mjini Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tukio hilo Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Hassan Nassir amesema tukio hilo lilitokea hapo jana katika maeneo ya kidongo Chekundu ambapo watoto hao wamekutwa wakiwa katika Gari aina ya VITZ yenye namba za usajili Z 986 DW inayomilikiwa na Ndugu Omar ambayo ilikuwa imeegeshwa pembezoni mwa barabra katika maeneo ya kidongo chekundu mjini Zanzibar.

Akiwataja watoto hao waliofariki ni Haitham Mustafa Abuubakar miaka 2 mkaazi wa Kidongo Chekundu, Muslihi Hamza Bakari Miaka 2 Jang’ombe, Dodo Muhammed miaka miwili na miezi saba mkaazi wa Jang’ombe na Munawar Ahmed khamis Jang’ombe.

Amesema vifo vya watoto hao kinasababishwa na kukaa muda mrefu katika gari hiyo na kukosa hewa na kupelekea kushindwa kupumua katika kipindi chote ambacho wanatafutwa na familia zao.

Akizungumza juu ya Maiti hizo Mtaalamu wa Uchunguzi wa Hospital Mnazi mmoja Zanzibar Dk.Marijani Msafiri alifahamisha kuwa watoto hao walifariki dunia kutokana na kuwa na mazingira ya joto kali na ukosefu wa hewa aina ya oxgen wakiwa ndani ya gari hiyo.

Kwa mujibu wa Dk. Marijani tayari watoto hao wamechukuliwa kwa ajili ya kufanyiwa taratibu za Mazishi.

Chanzo: Zanzibar 24
 
Yaani hilo gari lilikuwa wazi watoto wa miaka mawili wakafungua mlango na kisha kujifungia?

Mwenye gari hana uhusiano wowote na watoto marehemu? Bado sielewi hayo mazingira ya vifo vyao

Anyway mlale pema watoto wazuri
 
Kuripoti taarifa kihivi ndio tunaambiwa kati ya wabongo 5, wanne ni vichaa..sasa hii ni ripoti gani,.hovyo kabisa.
 
Report ina kuja kama breaking news. Inaacha maswali mengi ya msingi hayajajibiwa
 
Back
Top Bottom