Zanzibar waache majaribio yasiyo na tija kwenye mfumo wa elimu

kmbwembwe

JF-Expert Member
Aug 16, 2012
10,418
7,201
Binafsi nilishangaa kujua mfumo wa zanzibar ni kumaliza shule ya msingi darasa la sita kisha mtu anaenda form 1. Sijui wanakimbilia wapi? Au kwa vile shule zao kuna kina mama na kina baba wanalea japo wao ni watoto?

Mfumo huo pia umekua na matokeo duni ya kidato cha nne. Kila mwaka shule za Zanzibar zinashika mkia matokeo ya NECTA form IV na form VI.

Ningewashauri vigogo wa elimu Zanzibar kwa kushirikiana na bara ili kuwa na mfumo mmoja wa Jamhuri. Kwanza waondoe mfumo wa miaka 6 kwa elimu ya msingi ili mfumo uwe miaka 7 sawa na bara.

Na hili suala la watoto wazazi kuchanganyika kwenye shule japo Rais Samia kalitolea mfano liigwe huku bara ukweli linapingwa vikali na wengi. Kwa maoni yangu binafsi linachangia kukwamisha maadili na kushusha umakini wa mwanafunzi kutokana na kutangulizwa fikra zake kwenye mambo ya mapenzi na ndoa kabla ya muda muafaka.
 
Fanyatafiti vizuri kutoka mataifa mengine...mfumo wao waelimu ukoje na wanamanikio kiasi gani katika elimu ukilinganisha na Tanzania bars....mfano..Kenya ,Zambia na Nigeria...na nyenginezo...elimu bora si wingi Wa miaka , bali ni strategies bora
 
Elimu ya madrasa inatutosha sana huku Zanzibar, shule za elimu ya kizungu ni utumwa tunaovalishwa tu ili kukidhi mahitaji ya binadamu wa dunia ya sasa lakini hatuupendi kivilee.
Afadhali embu fanyeni kweli tuone madaktari, na ma engineer watakaozalishwa na ilimu ya madrasa maana nasikia wana kitabu kimoja chenye masomo yote na elimu zote duniani 😀😀😀😀🙆‍♂️🙆‍♂️
 
Huu Uzi kama umechelewa kuutoa mkuu
Nimesoma bandiko humu la waziri wa elimu Zanzibar kuubadirisha mfumo wa elimu MSINGI kutoka kuishia darasa la sita na Sasa kuwa darasa la Saba . Hata hivyo naunga mkono hoja yako mkuu.
 
Fanyatafiti vizuri kutoka mataifa mengine...mfumo wao waelimu ukoje na wanamanikio kiasi gani katika elimu ukilinganisha na Tanzania bars....mfano..Kenya ,Zambia na Nigeria...na nyenginezo...elimu bora si wingi Wa miaka , bali ni strategies bora
Jana nilikuwa naangalia Report ya UN ya elimu Afrika top 10,

nikadhani labda Zanzibar itakuwemo, lakini nikakumbuka kuwa Zanzibar inafuata Tanganyika katika Elimu ya Secondari na Juu.
Ki ukweli sisi ni washika mkia.
Ya tatu ni Maouritious, ya kwanza ni Sheli sheli na Ya Tau ni Algeria , Kenya ni ya 7 , South Afrika ni ya 4. Egypt ni ya 9., Cae vade ni ya 8

Nadhani Zanzibar inatakiwa Ijitowe kwenye masuala ya Elimu yasiwe ya Muungano ili tutafute namna ya mfumo wetu ulio bora zaidi kama zamani kabla ya Mapinduzi.
 
mleta mada umeongea pumba. hayo maamuzi ya awali yalikua ni bora zaidi kuliko haya walioyaamua sasa, na hayana mahusiano kabisa na matokeo duni ya Kidato cha nne.
 
Jana nilikuwa naangalia Report ya UN ya elimu Afrika top 10,

nikadhani labda Zanzibar itakuwemo, lakini nikakumbuka kuwa Zanzibar inafuata Tanganyika katika Elimu ya Secondari na Juu.
Ki ukweli sisi ni washika mkia.
Ya tatu ni Maouritious, ya kwanza ni Sheli sheli na Ya Tau ni Algeria , Kenya ni ya 7 , South Afrika ni ya 4. Egypt ni ya 9., Cae vade ni ya 8

Nadhani Zanzibar inatakiwa Ijitowe kwenye masuala ya Elimu yasiwe ya Muungano ili tutafute namna ya mfumo wetu ulio bora zaidi kama zamani kabla ya Mapinduzi.

Hizo taarifa si za kuaminibsana. Watayarishaji hua wana malengo yao.
 
Mtoa mada umeongea bila kufanya utafiti wa jambo husika. Nijuavyo Zanzibar mfumo wao ulikuwa darasa la kwanza hadi drs la 7, hapo kulikuwa na mtihani wa mchujo. Wanaofaulu vipaji huingia form 1. Kundi linalobaki lilikuwa likiendelea darasa la 8 hadi Form 2 (Non stop). Hii form two ndipo Elimu ya msingi ilipoishia. Hufanya mitihani ya mwisho, anaefaulu alikwenda form 3 hadi 4 na kufanya mtihani wa Taifa (NECTA). Aliyeshindwa form 2 hurudi nyumbani, sawa na aliyeshindwa darasa la 7 kwa kwetu Bara.

Miaka baadaye Bara na Zanzibar wakakubaliana elimu ya lazima iwe hadi form 4, na Elimu ya msingi iwe darasa la 1 hadi 6, kisha mtoto aingie form 1. Zanzibar ilianza kutekeleza immediately, huku bara wakimbwela mbwela hadi JPM alipokuja kufuta mfumo wa hadi darasa la 6 na kuendelea na mfumo wa awali (Bara tuliufuta ukiwa haukutekelezwa hata mwaka mmoja). Sasa wanachofanya ni kurejea mfumo wa zamani ili kuendana na mtaala wa Bara tu.

All in all, utoaji wa taarifa huko Serikalini ni sifuri. Taarifa hazitolewi zikiwa zimenyooka kiasi cha kuchanganya watu.
 
Back
Top Bottom