Zanzibar: Rais Mwinyi Afanya Teuzi

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,010
9,874
Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi amemteua Kanali Azana Hassan Msingiri kuwa Mkuu wa Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo(KMKM). Kanali Makame Abdallah Daima ameteuliwa kuwa Kamishna Kikosi cha Jeshi la Kujenga Uchumi(JKU)

Kanali Rashid Mzee Abdallah ameteuliwa kuwa Kamishna Kikosi cha Zimamoto na Uokozi. Luteni Kanali Khamis Bakari Khamis ameteuliwa kuwa Kamishna wa Vyuo vya Mafunzo

Luteni Kanali Burhani Zuberi Nassoro kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Uratibu na Udhibiti na Dawa za kulevya. ACP Ahmed Hamis Makarani kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi(ZAECA)
===
1619024960317.png
 
Dah hongera sana mzee wangu msingiri jirani yangu wa zaman Lugalo barracks Mungu akutangulie kwenye madaraka mapya UDMP Basi Tena.
 
Back
Top Bottom