abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
Spika wa baraza la wawakilishi Pandu Ameir Kificho amewaambia wajumbe wa baraza hilo kwamba tayari rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed Sheni ametia saini miswaada mitatu iliyopitishwa na wajumbe hao katika kipindi cha Baraza la Wawakilishi kilichopita na sasa kuwa sheria kamili.
Kificho alisema miswaada mitatu iliyotiwa saini na rais ni pamoja na mswaada wa kuanzishwa kwa maabara ya mkemia mkuu wa serikali, mswaada wa kuanzishwa kwa shirika la taifa la biashara Zanzibar (ZSTC) pamoja na usanifu wa kuendesha mazao mengine na mswada wa kurekebisha baadhi ya sheria na kuweka kanuni za baraza.
‘Wajumbe wa baraza la wawakilishi nafurahi kuwajulisha kwamba miswaada mitatu iliyopitishwa na baraza hili tayari imekuwa sheria baada ya kutiwa saini na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi' alisema Spika.
Aidha Spika aliwajulisha Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu mabadiliko yaliyofanywa na rais wa Zanzibar Dk Sheni ya kumuondowa katika nafasi ya katibu wa baraza, Ibrahim Mzee Ibrahim.
Kificho alisema kwamba Ibrahim ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa mashtaka wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kusema huo ni wadhifa mkubwa hata kuliko nafasi yake ya awali.
‘Nataka wajumbe wa baraza la wawakilishi kukujulisheni mabadiliko hayo ambapo sasa mwenzetu Katibu wa Baraza Ibrahim hayupo tena na sisi baada ye kuteuliwa kushika wadhifa wa Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar (DPP)' alisema Kificho.
Kificho aliwafahamisha wajumbe wa baraza la wawakilishi na kusema kwamba wadhifa huo ni mkubwa wenye hadhi ya kimataifa ikiwa ni sawa na Jaji wa Mahakama Kuu.
chanzo: Zanzibar yetu
Kificho alisema miswaada mitatu iliyotiwa saini na rais ni pamoja na mswaada wa kuanzishwa kwa maabara ya mkemia mkuu wa serikali, mswaada wa kuanzishwa kwa shirika la taifa la biashara Zanzibar (ZSTC) pamoja na usanifu wa kuendesha mazao mengine na mswada wa kurekebisha baadhi ya sheria na kuweka kanuni za baraza.
‘Wajumbe wa baraza la wawakilishi nafurahi kuwajulisha kwamba miswaada mitatu iliyopitishwa na baraza hili tayari imekuwa sheria baada ya kutiwa saini na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi' alisema Spika.
Aidha Spika aliwajulisha Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu mabadiliko yaliyofanywa na rais wa Zanzibar Dk Sheni ya kumuondowa katika nafasi ya katibu wa baraza, Ibrahim Mzee Ibrahim.
Kificho alisema kwamba Ibrahim ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa mashtaka wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kusema huo ni wadhifa mkubwa hata kuliko nafasi yake ya awali.
‘Nataka wajumbe wa baraza la wawakilishi kukujulisheni mabadiliko hayo ambapo sasa mwenzetu Katibu wa Baraza Ibrahim hayupo tena na sisi baada ye kuteuliwa kushika wadhifa wa Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar (DPP)' alisema Kificho.
Kificho aliwafahamisha wajumbe wa baraza la wawakilishi na kusema kwamba wadhifa huo ni mkubwa wenye hadhi ya kimataifa ikiwa ni sawa na Jaji wa Mahakama Kuu.
chanzo: Zanzibar yetu