Zanzibar ni nchi huru au ni sehemu ya Tanzania?

Watu waliofika Zanzibar 1734 kwa maneno yako Unawaita watu wa kuja tu Yaani ilipofika 1964 waliokua na miaka 230.
.tukiaza hivyo hata wewe usikute ni Mrundi au Mnubi wa central Africa
Kwa taarifa tu sultan Jamshid mama yake ni Mmanyema.
Alie kuwa waziri mkuu aliepinduliwa ni Mpemba wa asili.
Mgeni ni Okello alizaliwa kukulia Uganda 🇺🇬 na kuja zanzibar kuuwa wenyeji na kurudi kwao.
Hatuna tatizo lolote na Early Migrations, wenyeji asili wa Azania ni bantustans, lakini Nilotics wamehamia, Semi Nilotics, wamehamia, tuna Cushites, tuna Afroasiatic, ila kitendo cha watu kutoka Bara jingine kuhamia Africa, kulowea, kujifanya ndio kwao, wao ndio wao, kuwadharau wenyeji na hivi ndivyo wageni hawa walivyowafanya wenyeji
Kisha wenyeji wakafanya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, wakaungana na jirani zao, jee kuna mwenyeji yoyote atataka Muungano ufe?.
P
 
Hatuna tatizo lolote na Early Migrations, wenyeji asili wa Azania ni bantustans, lakini Nilotics wamehamia, Semi Nilotics, wamehamia, tuna Cushites, tuna Afroasiatic, ila kitendo cha watu kutoka Bara jingine kuhamia Africa, kulowea, kujifanya ndio kwao, wao ndio wao, kuwadharau wenyeji na hivi ndivyo wageni hawa walivyowafanya wenyeji
Kisha wenyeji wakafanya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, wakaungana na jirani zao, jee kuna mwenyeji yoyote atataka Muungano ufe?.
P

 
Zanzibar siyo nchi (Country), bali ni dola(State) inayounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Huu muungano uliwekwa kimkataba na hati idhini (Union Charter/Articles of the Union). Hivyo Zanzibar ilipunguza sehemu ya uhuru wake kujiwala (National Sovereignty) kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pili, suala la ajira lina pembe mbili. Kuna pembe ya Muungano na pembe ya Zanzibari. Watanganyika wapo Zanzibari na wanafanya kazi, lakini ni katika zile sehemu za mambo yanayohusu Muungano tu. Jambo kama hili liko hata kule Hong-Kong Uchina, na maisha yanaenda kama kawaida.

Tatu, suala la bendera siyo shida, maana bendera ni utambulisho tu (Emblem of Identity). Hata wewe ukiamua kuwa na bendera yako unaweza kuitengeneza na kuisajili kupitia HAKI-MILIKI (Intellectual Property). Nchini Marekani kila jimbo lina bendera yake na maisha yanaenda vizuri tu. Tena wananda mbali kabisa na kutumia bendera (The Confederate Flag) ya madola ya kusini (Dixie-Land) ambayo yaliasi muungano.

Nne, nadhani jina Raisi ni cheyo tu, hivyo unaweza leo ukamua kumuita Raisi wa Zanzibari wa Zanzibar Waziri Mkuu wa visiwani, Gavana,Sultani au Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Lakini muhimu kujiuliza ni hili: Je, madaraka yake ya Uraisi yanaishia wapi na ukimlinganisha na Raisi mwenzake ??? Utakuja kufahamu ni kwamba Raisi wa Zanzibari hauvuki maji ya Pemba na Unguja, lakini Raisi wa Tanganyika madaraka yake yanavuka maji na kufika Pemba hadi Unguja, katika ngazi ya kitaifa hadi kichama.

Tano, mashirikisho mengi huwa na mihimili na taasisi zinazojitegemea kama mahakama, bunge na serikali zao. Wengine kama Ethiopia walienda mbali zaidi kuwa hata vikosi vyao binafsi vya ulinzi. Nchini Marekani kuna baadhi ya majimbo yana nguvu sana hadi kumuwezesha Gavana kutoa adhabu ya kifo. Hivyo hili la Zanzibar lisikutatize kabisa mkuu.

Sita, kuhusu uwakilishi wa Zanzibari kwenye siasa za kimataifa hilo ni jambo la kawaida sana maana sheria za kimataifa hazikatazi. Tokea mwaka 1945 hadi 1991 Umoja wa Kisovieti ulikuwa una viti vitatu kule Umoja wa Mataifa ambavyo ni vya Urusi, Ukraine na Belarus ilhali wote wanatoka kwenye nchi moja iitwayo The Union of Soviets Socialist Republics (USSR). Hivyo hapa napo binafsi sioni tatizo kabisa.

Saba, kuhusu taasisi kujiendesha kwa utofauti hilo linatokana na uwepo wa madara ya ndani ya kujiendesha (Internal Sovereignty). Hata nchini Uchina, Hong-Kong inajiendesha kitofauti kabisa, nchini Marekani jimbo kama California ambalo huwa linajiendesha kitofauti kabisa na sera zake za kiliberi. Ambacho wengi kinatukera ni kwamba Tanganyika kutoweza kujiamulia mambo yake binafsi. Tunalitaka taifa letu.

Nane, hili la mikopo nakubaliana na wewe kabisa. Zanzibari haitakiwi ipate fungu lolote lile kwenye masuala yasiyo ya muungano (Non-Union Matters) ambayo yanaihusu Tanganyika. Mbaya zaidi hili la kukopa kupitia mngongo wa Tanganyika, ilhali sheria za kimataifa zinaruhusu Zanzibar iweze kukopa yenyewe binafsi. Katiba ya Ujerumani inaruhusu Ujerumani Mashariki na Ujerumani Magharibi kuingia katika mikataba binafsi ya kimataifa na nchi nyingine. Hivyo Ujerumani Mashariki inaruhusiwa hadi kukopa nje, ili mradi tu itoe taarifa kwa serikali ya Muungano.

Tunataka Zanzibar nao wakope kwa jina lao, maana inaruhusiwa kabisa. Huu ujanja wa kutaka kuimiza Tanganyika, umenza kututia kinyaa watu wengi na kutukera sana. Hasahasa unapofanywa na Raisi Mzanzibari ambaye kiuhalisia hakutakuwa kabisa kugusa mambo ya Tanganyika.

Tisa, kuhusu ardhi. Wazanzibari ni watu wenye midomo sana na wanapenda kuongea siasa zao ambazo zimejaa ubaguzi wa rangi na dini. Lakini ukweli mchungu ni kwamba kuna mambo ambayo Tanganyika ikitutumua misuli, lazima wataumia sana. Mwaka 2014 ilifanyika tafiti na kufahamika kwamba kule Zanzibar (1 Square Kilometer inakaliwa na watu 200) wakati huku Tanganyika (1 Square Kilometer inaliwa na watu 20-30).

Tukisema tuanze kuwakazia, nadhani watu kama Raisi Hussein Mwinyi, Raisi Samia, Bakhresa na wapemba wengine ambao wako Dar es Salaam kisheria inabidi wamiliki ardhi kama wawekezaji kupitia kitu kiitwacho The Derivetive Right. Lakini jambo jingine kubwa utafiti wa mafuta ya Zanzibar ulifanywa kipindi cha Raisi Magufuli na kutambulika kwamba baadhi ya miamba yenye mafuta ambayo Zanzibari ingechimba imefika hadi Tanganyika, tena sehemu kubwa iko Tanganyika.

Kiukweli mimi natamani Tanganyika irudi, ikiwezekana kabisa tuvunje huu muungano.

Halafu nyie Moderators mliopo ONLINE (Boqin , Wand , BlackBold , YinYang , Active , Mhariri ) tafadhali tuheshimiane sana. Hili la mimi kuweka nukta .... ili kuwahi nafasi ya kuandika muda nitakaotaka mimi binafsi haliwahusu kabisa. Sasa kujifanya mko kichwani mwangu na kutabiri kwamba navuruga mijadala ni upigaji ramli na uchawi. Nimewavumilia sana kuna siku mkanipa BAN, leo mmefuta nilichoandika. Tafadhali sana heshimuni uhuru wangu na tusipangiane cha kuandika.

Very well said mkuu....nimekuelewa sana sanaaa
 
Historia ya Tanganyika ni kuanza kuwa koloni la Uingereza 1922, kupata uhuru 1961, na kuuliwa na mwaka 1964. Nje ya hapo hakuna Tanganyika wala haina historia. Ni sehemu tuu Mwingereza alichora mstari kwenye ramani akapaita Tanganyika. Siyo taifa hilo.
Na Zanzibar mstari ulichorwa na nani?
 
😀 Nimeshangazwa na aya👆 yako ya mwisho.

Naona unaandika unachotaka kusikia na siyo kilichopo.

Katika Muunguno, Jamhuri ya Muunguno wa Tanzania ndiyo the only sovereign State (dola huru) linalosaini mikataba ya Kimataifa.

Zanzibar siyo sovereign State since 1964. Haina sovereignty.

NB:Ninasisitiza google na usome Kesi ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania baina ya Machano Hamis and Others v. Republic, ambapo Wahe. Majaji walifanya utafiti wa kina kirefu, na kuelezea kwa undani kuhusu dhana nzima ya uraia, dola huru na uhaini.

Hivi vitu vipo kisheria, na ukitoa hoja bila rejea ya sheria na principles ni kosa. You're actually not with me(us).
Zanzibar ina uwezo wa kusaini mikataba ya kimataifa: Kama makoloni yasiyo na Sovereign yaliweza kusaini mikataba ambayo iko mpaka leo, sembuse Zanzibar! Huwa napenda kuwaambia wanasheria wa Tanzania someni sana PUBLIC INTERNATIONAL LAW ili kuelewa haya mambo, CONSTITUTIONAL AND ADMINISTRATIVE LAW hazitoshi. Sasa umeandika mambo mengi, lakini ukweli ni kwamba Zanzibar ina uwezo wa kusaini mikataba ya kimataifa.

Mkuu hutaki unaacha,....
 
Sheria za Vatican ambazo zinakuongoza wewe ni zile kidini (Canon and Ecclesiastical Laws), tena kwenye mambo machache kama ndoa, talaka na ubatizo wa watoto. Ukienda Vatican ndiyo utabanwa na sheria za huko.
.,....................

Hapa umekubaliana na mimi kwamba sheria za Vatican zinaniongoza.


Sasa hivyo vigezo vya dola ambavyo umeniwekea hapa, navyo umevichanganya sana. Vimetolewa na mkataba wa monte-video (The Monte-Video Convention of 1933) ambao ulitoa vigezo vya taifa au dola ambavyo ni: Permanent Population, Government, Defined Territory and Sovereignty.
..,...........
Sijajua hapa unapinga nini zaidi naona umetoa reference ya nilichosema


Sasa The Vatican haina idadi ya watu ya kudumu (Permanent Population) watu wa pale huja na kuondoka baada ya kumaliza utumishi wao na kurudi nchini kwao. Ndiyo maana nakwambia hivi, kukosekana kwa kigezo kimoja haimaanishi kwamba dola siyo huru.

.,.....,.....

Rejea case ya Machano na Wenzake iliyoamuliwa na Mahakama ya Rufaa. Vigezo vyote vinne ni sharti vitimie. Na Zanzibar ilikosa kimoja, sovereignty, na hivyo kuamuliwa siyo dola na hivyo basi Serikali ya Zanzibar haiwezi kufanyiwa uhaini.

Holly Chair/Vatican ina watu. Hakuna sheria inasema watu wawe permanent. Ni hivi, popote alipo Mkatoliki basi utawala wa Pope upo. Yaani, utawala wa Papa hauna territory maalum. Na hiyo ni exception kwenye general rule ya defined territory.


Kama kigezo ni SOVEREIGNTY, kuna nchi kama The Sovereign Military Order of Malta (SMOM) ambayo haina Sovereignty lakini bado inatambulika kama nchi na ina ushawishi mkubwa sana kimataifa.

..........😀

Sasa unasemaje Malta haina sovereignty huku unasema inatambulika kama huru?

Kutambulika kama huru ndiyo sovereignty yenyeweee
The Vatican is not The Holly See, nashukuru umekubali. Lakini pia wewe kubanwa na sheria za Vatican siyo jambo la ajabu kabisa. Mimi binafsi nabwanwa na sheria za Rotary Club International chombo ambacho siyo nchi wala dola. Lakini ili sheria za Rotary Club ziweze kunibana ni lazima kwanza ziruhusiwe na sheria za dola la Tanzania. Leo hii The JALA kama isingeruhusu Sheria za dini zitambulike, sidhani kama zingetambulika.

Pili, mkataba baina ya The Vatican City na Tanzania nao unachangia hayo kuwezekana. Dola la Tanzania likiamua leo lisitambue sheria za dini yako, linaweza fanya hivyo mara moja tu na zisitambulike. Huu ndiyo utaratibu ulivyo. Hutaki unaacha.

Kuhusu PERMANENT POPULATION: Narudia tena, kinachowaumiza wanasheria wa Tanzania ni kutokuwa na ufahamu wa PUBLIC INTERNATIONAL LAW. Tafasiri ya dola na vigezo vyake imetolewa na mikataba miwili mikubwa duniani. Mkataba wa kwanza Kabisa ni The Treaty of Westphalia 1648, mkataba wa pili ni The Monte-Video Conventio 1933 ambao unasema taifa lazima liwe na PERMANENT POPULATION. Mbona haya ni marahisi tu, na ulitakiwa uwe umeyasoma mwaka wa pili Chuo.

Sasa kuhusu SOMS, kuna kitu kinachoitwa THE SUI-GENERIS STATES ambacho kama walau ungekuwa ulisoma vizuri chuo mwaka wa pili ungekuwa unakifahamu vizuri na sidhani kama tungekuwa tunabishana hapa.
 
Tanganyika ni artificial state huwezi kupinga. Kwa mfano Mmasai wa Tanzania na Mmasai wa Kenya ni watu wale wale ila Uingereza ilichora mstari kwenye ramani ikawatenganisha. Huwezi kusema Mmasai wa Kenya na Mmasai wa Tanzania wana tofauti lakini Mmasai wa Tanzania na Msukuma wana utamaduni mmoja.

Artificial states huwa ni rahisi kusambaratika. Angalia nchi kama Syria, angalia Iraq, hata Marekani ilikuwa karibu kusambaratika, walishapigana vita ya wenyewe kwa wenyewe wakauwana watu zaidi ya milioni 1
Nikitumia mantiki yako, on CIVILIZATIONAL TERMS kila taifa ni Artificial, maana hakuna jamii iliyowahi kuzaliwa na kuwa taifa tu. Mataifa yote hapo mwanzo yalianza kama Fiefdoms under Feudal Lords: Makabila machache yalitawaliwa na mtu mmoja mwenye ukwasi na ardhi. Dhana ya taifa la kisasa (The Modern State) imeanza kutumika mara ya kwanza karne ya 17.
 
Hii siyo kweli. Zanzibar haiwezi kwenda kinyume na katiba ya JMT. Mfano mzuri ni Nyerere kupinga Zanzibar kujiunga na
Organisation of Islamic Cooperation (OIC). Haya ni makubaliano ya kimataifa ambayo Wazanzibari walitegemea yatasaidia kuinua uchumi. Sasa sovereignity gani hiyo?
Kisheria Zanzibar ina uwezo wa kujiunga na mashirika ya kimataifa na kuingia mikataba ya kimataifa. Hayo ya kukataliwa kujiunga na Organisatio of Islamic Cooperation (OIC) ni siasa uchwara za kitanzania ambazo mimi mtaalamu sitajihusisha nazo kabisa. Sasa niseme tu kitu rahisi ambacho kama utapenda kufuatilia, utafuatilia. Usipokubaliana na mimi, ACHA.

Union of Soviets Socialists Republics (USSR) iliundwa na nchi 15. Lakini mbali na taifa lile kuwa na kiti kwenye umoja wa mataifa kama taifa, nchi wanachama kama Ukraine na Belarus nao walikuwa na viti vyao vya kudumu kule Umoja wa Mataifa. Niende mbali zaidi, wewe Hong-Kong mbali na kuwa sehemu ya Uchina, ni mwanachama wa World Trade Organisation (WTO).

Hawana External Sovereignty lakini wameweza kusaini mkataba wa WTO na kuwa wanachama. Sembuse Zanzibar ??? Nchi kama Tanganyika ingekutana na watu wasomi wenye uelewa kama wenzetu wa huko Ulaya na Marekani, basi hizi porojo za OIC au Nyerere zisingekuwepo. Nyerere kukataa Zanzibar kujiunga na OIC hakuondoi ukweli kwamba Zanzibar inaweza kujiunga na OIC.
 
Hatuna tatizo lolote na Early Migrations, wenyeji asili wa Azania ni bantustans, lakini Nilotics wamehamia, Semi Nilotics, wamehamia, tuna Cushites, tuna Afroasiatic, ila kitendo cha watu kutoka Bara jingine kuhamia Africa, kulowea, kujifanya ndio kwao, wao ndio wao, kuwadharau wenyeji na hivi ndivyo wageni hawa walivyowafanya wenyeji
Kisha wenyeji wakafanya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, wakaungana na jirani zao, jee kuna mwenyeji yoyote atataka Muungano ufe?.
P
Rabda utufafanulie mwenyeji ni yupi?
kama jamii ina miaka 300 bado hajawa mwenyeji?
Kama wenyeji ni waafrika weusi basi ndio 80% ya wazanzibari kama sio zaidi,kuna hofu gani kuitisha kura ya maoni wakaamua hatma ya Nchi yao.

Je Jumbe alitaka serikali 3 ni muarabu wa Qatar 🇶🇦 ,Oman au Yemen 🇾🇪 ?

Tena cha ajabu huu ubaguzi unachochewa Zanzibar tu unapojadiliwa muungano ila bara kuna wahidi hata kiswahili ni chakubabaisha na wapo katikati kwenye siasa za nchi.
 
Kisheria Zanzibar ina uwezo wa kujiunga na mashirika ya kimataifa na kuingia mikataba ya kimataifa. Hayo ya kukataliwa kujiunga na Organisatio of Islamic Cooperation (OIC) ni siasa uchwara za kitanzania ambazo mimi mtaalamu sitajihusisha nazo kabisa. Sasa niseme tu kitu rahisi ambacho kama utapenda kufuatilia, utafuatilia. Usipokubaliana na mimi, ACHA.

Union of Soviets Socialists Republics (USSR) iliundwa na nchi 15. Lakini mbali na taifa lile kuwa na kiti kwenye umoja wa mataifa kama taifa, nchi wanachama kama Ukraine na Belarus nao walikuwa na viti vyao vya kudumu kule Umoja wa Mataifa. Niende mbali zaidi, wewe Hong-Kong mbali na kuwa sehemu ya Uchina, ni mwanachama wa World Trade Organisation (WTO).

Hawana External Sovereignty lakini wameweza kusaini mkataba wa WTO na kuwa wanachama. Sembuse Zanzibar ??? Nchi kama Tanganyika ingekutana na watu wasomi wenye uelewa kama wenzetu wa huko Ulaya na Marekani, basi hizi porojo za OIC au Nyerere zisingekuwepo. Nyerere kukataa Zanzibar kujiunga na OIC hakuondoi ukweli kwamba Zanzibar inaweza kujiunga na OIC.
Kwa sababu hizo ulizotoa na mifano uliyotoa ukubali kuwa huu siyo muungano, ni vamizi. Nyerere alipinga Zanzibar kujiunga na OIC kwa kusema itaenda kinyume cha katiba ya JMT na nchi kutokuwa na dini (secular state). Tunashukuru kwa ulivyoonyesha wazi kuwa huo mnaouita muungano siyo muungano wa kawaida.
 
The Vatican is not The Holly See, nashukuru umekubali. Lakini pia wewe kubanwa na sheria za Vatican siyo jambo la ajabu kabisa. Mimi binafsi nabwanwa na sheria za Rotary Club International chombo ambacho siyo nchi wala dola. Lakini ili sheria za Rotary Club ziweze kunibana ni lazima kwanza ziruhusiwe na sheria za dola la Tanzania. Leo hii The JALA kama isingeruhusu Sheria za dini zitambulike, sidhani kama zingetambulika.

Pili, mkataba baina ya The Vatican City na Tanzania nao unachangia hayo kuwezekana. Dola la Tanzania likiamua leo lisitambue sheria za dini yako, linaweza fanya hivyo mara moja tu na zisitambulike. Huu ndiyo utaratibu ulivyo. Hutaki unaacha.

Kuhusu PERMANENT POPULATION: Narudia tena, kinachowaumiza wanasheria wa Tanzania ni kutokuwa na ufahamu wa PUBLIC INTERNATIONAL LAW. Tafasiri ya dola na vigezo vyake imetolewa na mikataba miwili mikubwa duniani. Mkataba wa kwanza Kabisa ni The Treaty of Westphalia 1648, mkataba wa pili ni The Monte-Video Conventio 1933 ambao unasema taifa lazima liwe na PERMANENT POPULATION. Mbona haya ni marahisi tu, na ulitakiwa uwe umeyasoma mwaka wa pili Chuo.

Sasa kuhusu SOMS, kuna kitu kinachoitwa THE SUI-GENERIS STATES ambacho kama walau ungekuwa ulisoma vizuri chuo mwaka wa pili ungekuwa unakifahamu vizuri na sidhani kama tungekuwa tunabishana hapa.

Inaonekana upo level ya uanafunzi wakati mimi nipo level ya kitaalam.

Siyo kweli kwamba Tanzania inazitambua Sheria za Vatican (Katoliki). Kwa sheria ipi?

Halafu ni hivi, matumizi ya jina 'Vatican' au 'Holy Sea' hutumika kumaanisha 'Mamlaka Kuu ya Kanisa Katoliki' kwa hiyo sidhani kama ni kitu cha kibishania, that's how it is.

JALA hairuhusu sheria za kidini, bali inaruhusu na kutambua matumizi ya sheria za kimila, miongoni mwa mengine.
 
Zanzibar siyo nchi (Country), bali ni dola(State) inayounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Huu muungano uliwekwa kimkataba na hati idhini (Union Charter/Articles of the Union). Hivyo Zanzibar ilipunguza sehemu ya uhuru wake kujiwala (National Sovereignty) kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pili, suala la ajira lina pembe mbili. Kuna pembe ya Muungano na pembe ya Zanzibari. Watanganyika wapo Zanzibari na wanafanya kazi, lakini ni katika zile sehemu za mambo yanayohusu Muungano tu. Jambo kama hili liko hata kule Hong-Kong Uchina, na maisha yanaenda kama kawaida.

Tatu, suala la bendera siyo shida, maana bendera ni utambulisho tu (Emblem of Identity). Hata wewe ukiamua kuwa na bendera yako unaweza kuitengeneza na kuisajili kupitia HAKI-MILIKI (Intellectual Property). Nchini Marekani kila jimbo lina bendera yake na maisha yanaenda vizuri tu. Tena wananda mbali kabisa na kutumia bendera (The Confederate Flag) ya madola ya kusini (Dixie-Land) ambayo yaliasi muungano.

Nne, nadhani jina Raisi ni cheyo tu, hivyo unaweza leo ukamua kumuita Raisi wa Zanzibari wa Zanzibar Waziri Mkuu wa visiwani, Gavana,Sultani au Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Lakini muhimu kujiuliza ni hili: Je, madaraka yake ya Uraisi yanaishia wapi na ukimlinganisha na Raisi mwenzake ??? Utakuja kufahamu ni kwamba Raisi wa Zanzibari hauvuki maji ya Pemba na Unguja, lakini Raisi wa Tanganyika madaraka yake yanavuka maji na kufika Pemba hadi Unguja, katika ngazi ya kitaifa hadi kichama.

Tano, mashirikisho mengi huwa na mihimili na taasisi zinazojitegemea kama mahakama, bunge na serikali zao. Wengine kama Ethiopia walienda mbali zaidi kuwa hata vikosi vyao binafsi vya ulinzi. Nchini Marekani kuna baadhi ya majimbo yana nguvu sana hadi kumuwezesha Gavana kutoa adhabu ya kifo. Hivyo hili la Zanzibar lisikutatize kabisa mkuu.

Sita, kuhusu uwakilishi wa Zanzibari kwenye siasa za kimataifa hilo ni jambo la kawaida sana maana sheria za kimataifa hazikatazi. Tokea mwaka 1945 hadi 1991 Umoja wa Kisovieti ulikuwa una viti vitatu kule Umoja wa Mataifa ambavyo ni vya Urusi, Ukraine na Belarus ilhali wote wanatoka kwenye nchi moja iitwayo The Union of Soviets Socialist Republics (USSR). Hivyo hapa napo binafsi sioni tatizo kabisa.

Saba, kuhusu taasisi kujiendesha kwa utofauti hilo linatokana na uwepo wa madara ya ndani ya kujiendesha (Internal Sovereignty). Hata nchini Uchina, Hong-Kong inajiendesha kitofauti kabisa, nchini Marekani jimbo kama California ambalo huwa linajiendesha kitofauti kabisa na sera zake za kiliberi. Ambacho wengi kinatukera ni kwamba Tanganyika kutoweza kujiamulia mambo yake binafsi. Tunalitaka taifa letu.

Nane, hili la mikopo nakubaliana na wewe kabisa. Zanzibari haitakiwi ipate fungu lolote lile kwenye masuala yasiyo ya muungano (Non-Union Matters) ambayo yanaihusu Tanganyika. Mbaya zaidi hili la kukopa kupitia mngongo wa Tanganyika, ilhali sheria za kimataifa zinaruhusu Zanzibar iweze kukopa yenyewe binafsi. Katiba ya Ujerumani inaruhusu Ujerumani Mashariki na Ujerumani Magharibi kuingia katika mikataba binafsi ya kimataifa na nchi nyingine. Hivyo Ujerumani Mashariki inaruhusiwa hadi kukopa nje, ili mradi tu itoe taarifa kwa serikali ya Muungano.

Tunataka Zanzibar nao wakope kwa jina lao, maana inaruhusiwa kabisa. Huu ujanja wa kutaka kuimiza Tanganyika, umenza kututia kinyaa watu wengi na kutukera sana. Hasahasa unapofanywa na Raisi Mzanzibari ambaye kiuhalisia hakutakuwa kabisa kugusa mambo ya Tanganyika.

Tisa, kuhusu ardhi. Wazanzibari ni watu wenye midomo sana na wanapenda kuongea siasa zao ambazo zimejaa ubaguzi wa rangi na dini. Lakini ukweli mchungu ni kwamba kuna mambo ambayo Tanganyika ikitutumua misuli, lazima wataumia sana. Mwaka 2014 ilifanyika tafiti na kufahamika kwamba kule Zanzibar (1 Square Kilometer inakaliwa na watu 200) wakati huku Tanganyika (1 Square Kilometer inaliwa na watu 20-30).

Tukisema tuanze kuwakazia, nadhani watu kama Raisi Hussein Mwinyi, Raisi Samia, Bakhresa na wapemba wengine ambao wako Dar es Salaam kisheria inabidi wamiliki ardhi kama wawekezaji kupitia kitu kiitwacho The Derivetive Right. Lakini jambo jingine kubwa utafiti wa mafuta ya Zanzibar ulifanywa kipindi cha Raisi Magufuli na kutambulika kwamba baadhi ya miamba yenye mafuta ambayo Zanzibari ingechimba imefika hadi Tanganyika, tena sehemu kubwa iko Tanganyika.

Kiukweli mimi natamani Tanganyika irudi, ikiwezekana kabisa tuvunje huu muungano.

Halafu nyie Moderators mliopo ONLINE (Boqin , Wand , BlackBold , YinYang , Active , Mhariri ) tafadhali tuheshimiane sana. Hili la mimi kuweka nukta .... ili kuwahi nafasi ya kuandika muda nitakaotaka mimi binafsi haliwahusu kabisa. Sasa kujifanya mko kichwani mwangu na kutabiri kwamba navuruga mijadala ni upigaji ramli na uchawi. Nimewavumilia sana kuna siku mkanipa BAN, leo mmefuta nilichoandika. Tafadhali sana heshimuni uhuru wangu na tusipangiane cha kuandika.
Za ndani kabisa siku tukivunja muungano Zanzibar anachukua km 16 kutoka usawa wa bahari piga kutoka feri na kama ubungo
 
Nikitumia mantiki yako, on CIVILIZATIONAL TERMS kila taifa ni Artificial, maana hakuna jamii iliyowahi kuzaliwa na kuwa taifa tu. Mataifa yote hapo mwanzo yalianza kama Fiefdoms under Feudal Lords: Makabila machache yalitawaliwa na mtu mmoja mwenye ukwasi na ardhi. Dhana ya taifa la kisasa (The Modern State) imeanza kutumika mara ya kwanza karne ya 17.
Hujaelewa bado maana ya taifa? Ngoja nirudie tena

A nation is a large group of people who inhabit a specific territory and are connected by history, culture, or another commonality.

Mataifa yapo mengi. WaIrish ni taifa, WaBritish ni taifa, WaJapan ni taifa, WaIran ni taifa n.k. Zanzibar ni taifa ukisoma vizuri hiyo maana ya taifa, ukijua historia ya Zanzibar utaona Zanzibar ni taifa. Tanganyika ilivyokuwepo haikuwa taifa. Ilikuwa ni nchi bandia.
 
Mkuu Bepari2020, naomba nikurejeshe kwenye historia kwa kifupi
1. Naanza na Physical Geography da Formation ya Visiwa vyote vya bahari ya Hindi vilikuwa sehemu ya nchi kavu, vikamegeka, vikazungukwa na maji. Hivyo Zanzibar, Pemba Mafia ilikuwa ni sehemu ya Bara. Uthibitisho wa hoja hii ni mchoro huu View attachment 2125554
2. Visiwa vya Zanzibar vilikuwa ni sehemu ya bara miaka milioni nyuma!, vikamegeka na eneo la kati likasombwa na mmomonyoko!,
3. Baada ya miaka mingi watu wa bara ndio wakaazi asili wa visiwa vya Zanzibar na Pemba, simulizi za kale za Fumo Liongo Karne 8 na Ibin Batuta karne ya 12 zilieleza. Kiongozi wao aliitwa Mwinyi Mkuu.
4. Karne ya 15, Mreno Vasco Da Gama alipopita ndipo akapeleka Ureno sifa ya visiwa vya Zanzibar na Pemba.
5. Karne ya 16, Ureno ikaivamia Zanzibar, ndipo mtawala wa asili wa Zanzibar, MwinyiMkuu kuwaomba Waarabu wa Oman wamsaidie kuwatimua Wareno.
6. Baada ya kazi ya kuwatimua Wareno kukamimika, Karne ya 17, hakuna anayekijua kilichomkuta Mwinyimkuu maana hakijaandikwa popote, ila mara ghafla mwaka 1734, Sultan Sayyed Said, akaihamisha Sultanet yake kutoka Oman na kuihamishia Zanzibar kwa
kuvivamia visiwa hivyo na kuvitwaa as if havina wenyewe, wakakulia, wakazaliana, wakalowea na sasa baadhi yao wameanza kujisahau kwa kudhania visiwa hivyo ni mali yao ilhali wao ni watu wa kuja tuu!.
7. Mkutano wa Berlin wa mwaka 1884, ukamtambua rasmi Sultan wa Zanzibar kama mtawala na mmiliki halali wa visiwa vya Zanzibar na akapewa a 10 miles za costal stip ya Bara ilikuwa chini ya himaya ya Sultan wa Zanzibar.
8. Tanganyika ilikuwa koloni la Ujerumani, Kenya ilikuwa Koloni la Uingereza, nchi hizi zote mbili hazikuwa na access ya bahari kwasababu a 10 miles ya costal stipe ya pwani yote ya Africa Mashariki ilikuwa chini ya himaya ya Sultan, ila Zanzibar ilikuwa chini ya uangalizi wa Uingereza, ndipo mwaka 1890, Waingereza na Wajerumani
wakaingia mkataba, wa Hellingoland, (The Zanzibar Treaty) Sultan wa Zanzibar aziachie zile 10 miles kwa matumizi ya German East Africa.
9. Tarehe 10 Desemba, 1963, Uingereza ikatoa uhuru wa bandia kwa Zanzibar kuendelea kuwa chini Sultan na serikali kibaraka wa Sultan.
10. Ndipo tarehe 12 January 1964 wanaume wakaingia kazini wakafanya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya 1964, vilirudisha heshima ya visiwa hiyo iliyoporwa na madhalimu wale na muungano ukavirudisha visiwa hivyo kwa wenyewe halisi.

Mapinduzi Daima!
Muungano Udumishwe!
Mungu ibariki Tanzania.

P.
Watu wa bara walivukaje bahari mpaka Zanzibar? Ukisema walikuwepo wakati visiwa vinamegeka siyo kweli. Modern human hakuwepo enzi hizo.
 
Mkuu Bepari2020, kwenye mijadala ya kuhusu maslahi ya Taifa kama hoja hii, ni vema tuwe wakweli toka ndani ya nafsi zetu kwa kwanza kuukubali ukweli uliopo hata kama hatukubaliani nao .
Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar uliounda Tanzania, ni kitu ambacho kipo na kina exist, hivyo huwezi kuita "huo mnaouita Muungano" as if ni kitu ambacho hakipo ila kinaitwa tuu!. Hakuna huo mnaouita Muungano, hatuuiti Muungano, bali Muungano upo una exist.

Pili waasisi wa Muungano, Nyerere na Karume, waheshimiwe, usianze kumyooshea kidole mmoja na kumuita kwa majina mabaya kama "hili vamizi la Zanzibar alilofanya Nyerere".

Muungano wetu adhimu sio vamizi!. The Initiator wa Muungano ni Karume ndio alikuja bara kumuomba Nyerere ulinzi wa kuyalinda Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, dhidi ya manowari za Uingereza zilizokuwa zimetia nanga Mombasa tayari kwa kuja kuivamia Zanzibar, kuigomboa na kumrejesha Sultan aliyepinduliwa.

Ndipo Nyerere akapendekeza tuungane, Karume akakubali pale pale "tuungane, wewe rais, mimi Makamo". Usimtwishe Nyerere uzushi wa uvamizi!. Zile story za Kipumbwi ni hadithi tuu za uongo na ukweli.

Tuujadili Muungano in good faith kuwa una kero ambazo zimeendelea kutatuliwa na mwisho wa siku kero zote zitaondoshwa, tutakuwa na Muungano shwari bila kero ila pia kama ilivyo kwenye penzi, mahasidi hawakosekani hivyo tunaiendeleza nadhiri zote mbili, kwa Zanzibar "Naapa na naahidi, Mbele ya Mungu, Mapinduzi nitakulinda mpaka kifo". Na kwa JMT, "Muungano tutaulinda kwa gharama yoyote".
P
Miaka yote mmeshindwa kutatua kero kwa nini tuamini mnaweza? Miaka karibu 58 mmeshindwa kuondoa kero. Zanzibar umaskini umeongezeka, haki za binadamu zinaminywa, damu za Wazanzibari mnazimwaga kama damu za kuku. Mikopo mnapiga kelele. Mgao wa kipato cha taifa mnapiga kelele. Sasa mambo gani haya? Acheni tuu Zanzibar ipate uhuru tubaki tuu kama nchi jirani.
 
Back
Top Bottom