Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,498
- 51,090
Kwa vyovyote vile Wazanzibari ni dhahiri wameshaamua lolote na liwe, ukisikia kauli za watu wa Zanzibar, vijana hata wazee wanaonyesha hawajali tena na roho zao zimeshakinai na wako tayari kwa lolote!.
Zanzibar ya safari hii pengine ni Zanzibar iliyo bitter (uchungu) kuliko Zanzibar ya wakati wowote tangu mapinduzi ya mwaka 1964. Wananchi wamejiapiza kusimama kulinda haki yao ya kuchagua kiongozi wamtakaye, Wamejiapiza hadi ikibidi kufa!. Haya si maneno yangu ni maneno ya wazanzibari wengi wanaongea haya bila kificho. Uongozi mzima chini ya Maalim Seif wameshatoa kauli zao kuwa wako tayari kwa lolote!
Sasa fukuto hili si la kawaida, Kama kuna watu wana akili ndani ya System, serikali na chama tawala inabidi sasa watulize akili badala ya maguvu!
Kuna haya mambo yafuatayo
1. Hatima ya muungano itategemea serikali itahandle vipi suala la uchaguzi wa Zanzibar
Mkimwaga damu hata ya watu kumi tu, hiyo ni death warrant ya muungano wenyewe!. Wazanzibar sasa badala ya kutaka muungano uliofair, Wataukataa kabisa hata muungano wenyewe. Na kiukweli hakuna atakayeweza kuulazimisha uwepo kama maelfu ya Wazanzibari wataingia mtaani non-stop kuukataa muungano wenyewe. Utaua wangapi kisha dunia ikuangalie tu?
Tendeni haki ili hiyo haki iwe kinga ya kuulinda muungano, Nje ya haki hakuna Muungano, Maana Wazanzibar watauona kama chombo cha ukoloni dhidi yao na wataukataa. Watawala fikirieni sana juu ya hili!
2. Uchaguzi huu wa Zanzibar inaweza kuwa sababu ya watu kufikishwa the Hague
Iwapo damu ya Mzanzibar itamwagika, hakuna atakayebaki salama kwa watakaohusika, wanaweza kujikuta mahali pagumu sana kisheria. Safari hii ni tofauti na zamani ambapo ilikuwa ni rahisi kuficha matukio kutokana na tekinojia ya mawasiliano kutokuwa imeendelea sana kuliko leo. Lakini kwa dunia ya leo chochote kitakachofanyika leo dakika hiyohiyo dunia itaona dhahiri. Sasa watoa amri na wenye mamlaka wachague moja, watoe haki kwa wananchi wa Zanzibar au wao wakatetee haki yao ya kuwa huru mbele ya mahakama ya uhalifu dhidi ya binadamu huko the Hague
3. Uwezo wa kutawala kwa serikali ijayo ya Zanzibar itategemea sana na jinsi watawala wa sasa watakavyohandle uchaguzi huu
Iwapo kutatokea sintofahamu katika uchaguzi huu hadi kupelekea kumwaga damu yoyote ya mwananchi wa Zanzibar, basi serikali itakayoundwa huko Zanzibar kama ni ya CCM, kamwe haitokuwa na uhalali mbele ya wananchi wa Zanzibar, wataidharau. Serikali hiyo itatafuta legitimacy zaidi kwa watawala wa bara kuliko wananchi wa Zanzibar. Itakuwa serikali isiyojiamini, ya kinyapara tu na kamwe haitoleta maendeleo yoyote ya maana kwa Wazanzibari. Kwa hivyo itakuwa serikali mzigo kwa Tanganyika maana itakuwa ni tegemezi zaidi kwa Tanganyika. Hii kitu itaathiri pia hata uchumi wa Tanganyika maana itabidi iingie hazina kuisaidia serikali hiyo ya SMZ kwa sababu serikali hiyo itakuwa hohehahe zaidi
4. Utalii unaweza kushuka sana na uchumi kuyumba sana
Iwapo kutatokea sintofahamu huko hadi maisha ya wananchi kupotea, kutatoea publicity mbaya sana kwenye media, hii itaathiri sana utalii wa Zanzibar. Hii itaathiri uchumi wa Zanzibar, na maisha kuendelea kuwa magumu sana. Kama nilivyoeleza kwenye nukta ya tatu, Tanganyika nd italazimika kuingilia kati kuinusuru Zanzibar kifedha. Hii itapelekea miradi mingi huku Tanganyika isimame etc
5. Kwako mkuu wa Majeshi, kwa unyenyekevu mkubwa, Mission ya Zanzibar ni ya kisiasa siyo ya kijeshi, usije ukalitia jeshi la wananchi lawama ya bure sababu ya wachache tu wanaotafuta shortcut ya Madaraka baada ya kukataliwa na wananchi. Jeshi haliwezi kushinda mission ya kisiasa mbele ya watu walio determined
Miaka mitatu iliyopita tuliandika hapa JF kuwa mission ya korosho kule mikoa ya kusini ni mission ya kiutawala siyo ya kijeshi, na kwamba Jeshi kujiingiza katika mission hiyo ni kulitafutia lawama tu kwa sababu biashara ya korosho si kazi yake,na halitoiweza, na ilitokea hivyo
Pia ningependa nimwambie CDF kuwa, hali iliyopo Zanzibar ni hali ya kisiasa tu, kwamba kuna watu wamezidiwa kisiasa wanataka kutumia majeshi kukaa madarakani. Sasa ni uamuzi wa CDF, kuamua jeshi litumike kwa ajili ya CCM au liwe Neutral liache wanasiasa wachuane wenyewe kwa wenyewe na lenyewe lilinde mipaka na katiba ya nchi. Uchaguzi wa Zanzibar ni issue ya kisiasa, Kupeleka Jeshi kule na kupitisha vifaru mitaani ni kuescalate tensions tu. kwani, unawezaje kwa mfano kutumia kifaru dhidi ya raia wako mwenyewe?.
Ni hatari kwa nchi iwapo Wanzanzibar wataiona JW kama occupying force!. Kwamba ipo ili kupora maamuzi yao ya kisiasa!. Jeshi lisimame imara kwenye kipindi critical kama hiki, lisiwachekee wanasiasa hata kidogo, liwe wazi na liseme kuwaambia watawala kuwa Hatukupewa silaha na Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuzigeuza silaha hizo kwao
Kwa hiyo kwa kuhitimisha ni kwamba kutokutenda haki Zanzibar kutauua hata Muungano wenyewe at one point in time.
Haki ndo njia pekee ya kuinusuru Zanzibar na muungano.
Zanzibar ya safari hii pengine ni Zanzibar iliyo bitter (uchungu) kuliko Zanzibar ya wakati wowote tangu mapinduzi ya mwaka 1964. Wananchi wamejiapiza kusimama kulinda haki yao ya kuchagua kiongozi wamtakaye, Wamejiapiza hadi ikibidi kufa!. Haya si maneno yangu ni maneno ya wazanzibari wengi wanaongea haya bila kificho. Uongozi mzima chini ya Maalim Seif wameshatoa kauli zao kuwa wako tayari kwa lolote!
Sasa fukuto hili si la kawaida, Kama kuna watu wana akili ndani ya System, serikali na chama tawala inabidi sasa watulize akili badala ya maguvu!
Kuna haya mambo yafuatayo
1. Hatima ya muungano itategemea serikali itahandle vipi suala la uchaguzi wa Zanzibar
Mkimwaga damu hata ya watu kumi tu, hiyo ni death warrant ya muungano wenyewe!. Wazanzibar sasa badala ya kutaka muungano uliofair, Wataukataa kabisa hata muungano wenyewe. Na kiukweli hakuna atakayeweza kuulazimisha uwepo kama maelfu ya Wazanzibari wataingia mtaani non-stop kuukataa muungano wenyewe. Utaua wangapi kisha dunia ikuangalie tu?
Tendeni haki ili hiyo haki iwe kinga ya kuulinda muungano, Nje ya haki hakuna Muungano, Maana Wazanzibar watauona kama chombo cha ukoloni dhidi yao na wataukataa. Watawala fikirieni sana juu ya hili!
2. Uchaguzi huu wa Zanzibar inaweza kuwa sababu ya watu kufikishwa the Hague
Iwapo damu ya Mzanzibar itamwagika, hakuna atakayebaki salama kwa watakaohusika, wanaweza kujikuta mahali pagumu sana kisheria. Safari hii ni tofauti na zamani ambapo ilikuwa ni rahisi kuficha matukio kutokana na tekinojia ya mawasiliano kutokuwa imeendelea sana kuliko leo. Lakini kwa dunia ya leo chochote kitakachofanyika leo dakika hiyohiyo dunia itaona dhahiri. Sasa watoa amri na wenye mamlaka wachague moja, watoe haki kwa wananchi wa Zanzibar au wao wakatetee haki yao ya kuwa huru mbele ya mahakama ya uhalifu dhidi ya binadamu huko the Hague
3. Uwezo wa kutawala kwa serikali ijayo ya Zanzibar itategemea sana na jinsi watawala wa sasa watakavyohandle uchaguzi huu
Iwapo kutatokea sintofahamu katika uchaguzi huu hadi kupelekea kumwaga damu yoyote ya mwananchi wa Zanzibar, basi serikali itakayoundwa huko Zanzibar kama ni ya CCM, kamwe haitokuwa na uhalali mbele ya wananchi wa Zanzibar, wataidharau. Serikali hiyo itatafuta legitimacy zaidi kwa watawala wa bara kuliko wananchi wa Zanzibar. Itakuwa serikali isiyojiamini, ya kinyapara tu na kamwe haitoleta maendeleo yoyote ya maana kwa Wazanzibari. Kwa hivyo itakuwa serikali mzigo kwa Tanganyika maana itakuwa ni tegemezi zaidi kwa Tanganyika. Hii kitu itaathiri pia hata uchumi wa Tanganyika maana itabidi iingie hazina kuisaidia serikali hiyo ya SMZ kwa sababu serikali hiyo itakuwa hohehahe zaidi
4. Utalii unaweza kushuka sana na uchumi kuyumba sana
Iwapo kutatokea sintofahamu huko hadi maisha ya wananchi kupotea, kutatoea publicity mbaya sana kwenye media, hii itaathiri sana utalii wa Zanzibar. Hii itaathiri uchumi wa Zanzibar, na maisha kuendelea kuwa magumu sana. Kama nilivyoeleza kwenye nukta ya tatu, Tanganyika nd italazimika kuingilia kati kuinusuru Zanzibar kifedha. Hii itapelekea miradi mingi huku Tanganyika isimame etc
5. Kwako mkuu wa Majeshi, kwa unyenyekevu mkubwa, Mission ya Zanzibar ni ya kisiasa siyo ya kijeshi, usije ukalitia jeshi la wananchi lawama ya bure sababu ya wachache tu wanaotafuta shortcut ya Madaraka baada ya kukataliwa na wananchi. Jeshi haliwezi kushinda mission ya kisiasa mbele ya watu walio determined
Miaka mitatu iliyopita tuliandika hapa JF kuwa mission ya korosho kule mikoa ya kusini ni mission ya kiutawala siyo ya kijeshi, na kwamba Jeshi kujiingiza katika mission hiyo ni kulitafutia lawama tu kwa sababu biashara ya korosho si kazi yake,na halitoiweza, na ilitokea hivyo
Pia ningependa nimwambie CDF kuwa, hali iliyopo Zanzibar ni hali ya kisiasa tu, kwamba kuna watu wamezidiwa kisiasa wanataka kutumia majeshi kukaa madarakani. Sasa ni uamuzi wa CDF, kuamua jeshi litumike kwa ajili ya CCM au liwe Neutral liache wanasiasa wachuane wenyewe kwa wenyewe na lenyewe lilinde mipaka na katiba ya nchi. Uchaguzi wa Zanzibar ni issue ya kisiasa, Kupeleka Jeshi kule na kupitisha vifaru mitaani ni kuescalate tensions tu. kwani, unawezaje kwa mfano kutumia kifaru dhidi ya raia wako mwenyewe?.
Ni hatari kwa nchi iwapo Wanzanzibar wataiona JW kama occupying force!. Kwamba ipo ili kupora maamuzi yao ya kisiasa!. Jeshi lisimame imara kwenye kipindi critical kama hiki, lisiwachekee wanasiasa hata kidogo, liwe wazi na liseme kuwaambia watawala kuwa Hatukupewa silaha na Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuzigeuza silaha hizo kwao
Kwa hiyo kwa kuhitimisha ni kwamba kutokutenda haki Zanzibar kutauua hata Muungano wenyewe at one point in time.
Haki ndo njia pekee ya kuinusuru Zanzibar na muungano.