Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 121,601
- 94,726
Huu ni muendelezo wa viongozi wetu waliopewa madaraka ya kutuongoza kujichukulia madaraka yasiyo yakwao.
Walianza kututandika viboko na sasa wameamua kutuamulia tunyoe mitindo gani
==
'Vijana wa chini ya miaka 18 marufuku kufuga rasta'
Mkuu wa Wilaya ya Mjini huko visiwani Zanzibar, Rashid Msaraka ametangaza kuanza operesheni ya kuwanyoa nywele vijana wenye umri chini ya miaka 18, waliofuga rasta au kunyoa mtindo wa 'panki.'
Amesema kama wanazitaka wakafugie sehemu nyingine na endapo wazazi wao wameshindwa kuwakata hizo nywele, atawakata yeye.
''Vijana wote wenye umri chini ya miaka 18 kama huyu, kama wazee wao wameshindwa kuwakata hizi nywele tutawakata sisi'' alitahadharisha kiongozi huyo.
Picha ya video imesambaa katika mitandao ya kijamii ikionesha msaidizi wa kiongozi huyo akimkata nywele kijana aliyekuwa amezisokota nywele zake.
Kitendo hicho kimeibua mjadala kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, watu wakihoji ni sheria ipi iliyomuongoza kiongozi huyo kutoa agizo la kumkata nywele kijana huyo.
Walianza kututandika viboko na sasa wameamua kutuamulia tunyoe mitindo gani
==
'Vijana wa chini ya miaka 18 marufuku kufuga rasta'
Mkuu wa Wilaya ya Mjini huko visiwani Zanzibar, Rashid Msaraka ametangaza kuanza operesheni ya kuwanyoa nywele vijana wenye umri chini ya miaka 18, waliofuga rasta au kunyoa mtindo wa 'panki.'
Amesema kama wanazitaka wakafugie sehemu nyingine na endapo wazazi wao wameshindwa kuwakata hizo nywele, atawakata yeye.
''Vijana wote wenye umri chini ya miaka 18 kama huyu, kama wazee wao wameshindwa kuwakata hizi nywele tutawakata sisi'' alitahadharisha kiongozi huyo.
Picha ya video imesambaa katika mitandao ya kijamii ikionesha msaidizi wa kiongozi huyo akimkata nywele kijana aliyekuwa amezisokota nywele zake.
Kitendo hicho kimeibua mjadala kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, watu wakihoji ni sheria ipi iliyomuongoza kiongozi huyo kutoa agizo la kumkata nywele kijana huyo.