Zanzibar Kwanza Burundi Baadaye

Mchanya

JF-Expert Member
Jul 29, 2015
974
1,525
Vyombo vya habari hivi karibuni vimeripoti juhudi mpya za serikali yetu ya Tanzania kupitia Waziri Mahiga katika kujaribu kuleta suluhu mpya nchini Burundi. Tumeshuhudia Waziri Mahiga akianza mazungumzo na viongozi wahusika wa serikali iliyopo madarakani na wapinzani, hata viongozi wa nchi jirani. Binafsi, nakubaliana na uamuzi huu wa serikali yetu kwani sisi kama majirani tuna wajibu wa kusaidia kuleta suluhu kwa kinachoendelea Burundi, maana kwa jinsi hali inavyozidi kuwa mbaya nchini Burundi, nasi tunaathirika sana kama mtu mmoja mmoja au kama Taifa kiuchumi, kiusalama na kuendelea kubeba mzigo wa wakimbizi wanaofurika kila siku nchini mwetu. Burundi na majirani zetu wote wakiwa salama, nasi Tanzania ndio salama yetu. Burundi na majirani zetu wasipokuwa salama, tutatumbue kwamba sisi Tanzania hatuko salama. Sina shaka na uzoefu wa Balozi mkongwe Mahiga katika jukumu hili la utatuzi wa migogoro na kuleta amani maana ndio kazi zake na nina imani kwamba atafanya kazi nzuri.

Mazingira ya mzozo wa Burundi na huu wa kwetu wa Zanzibar yanalingana kwa kiasi fulani, tofauti ni kwamba Burundi kuna mauaji wakati Zanzibar hakuna mauaji, angalau kwa sasa, na pishilia mbali tuombe Mungu yasitokee. Tofauti nyingine ni kwamba wananchi walio wengi wa Burundi hawakubaliani na namna serikali ya Nkurunziza ilivyoingia madarakani, na wameamua kuchukua hatua kwa kuonyesha kutoridhishwa kwao kwa kupaza sauti zao, kwa maandamano, na njia nyingine ambazo serikali haikubaliani nazo. Polepole hadi tumefika hapa tulipofika. Mazingira yaliyopo Zanzibar ni kama yalivyoanza Burundi, yaani polepole, wananchi wanalalamika chini chini hadi kuna siku nao watapaza sauti na mwishowe hali itakuwa ngumu kuidhibiti. Tujiulize huu uvumilivu wa wananchi wa Zanzibar utadumu kwa muda gani? Na je kilichopo ni uvumilivu kweli au kitu kitu kingine?


Tanzania inajulikana kwamba ni kisiwa cha amani, juhudi za Balozi Mahiga ni ushahidi mmojawapo wa hili, hata Rais mstaafu wa awamu ya nne Rais Kikwete amefanya mengi katika kuleta amani katika eneo hili la Afrika Mashariki na Maziwa Makuu. Tuutumie uzoefu huu wa wanadiplomasia wetu kama akina Mahiga, JK, Membe, Mkapa na wengineo ili tuinusuru Zanzibar. Kwa uzoefu tulionao katika kutatua migogoro ya nchi za jirani hili la Zanzibar lisitushinde.

Chonde Chonde viongozi wote wakuu mpime nafsi zenu, mjitathimini, mumuogope Mungu na kisha mchukue hatua za haraka na za haki mmalize mgogoro na hali ya sintofahamu inayoendelea viziwani Zanzibar kwa sasa. Sioni mantiki ya kukimbilia kutatua mzozo wa Burundi ili hali Zanzibar hali ni tete.

Rais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Marais wote wastaafu wa Muungano na wale wa Serikali ya Zanzibar, Mawaziri wote wastaafu pamoja na wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na wale wawakilishi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, pamoja na Maspika waliopo na wale waliostaafu. Hii fursa ya kuuthibitishia ulimwengu na kutembea vifua mbele kwamba tatizo la Zanzibar limekuja na tumelimaliza na sasa ni historia. Tusiipoteze hii fursa.


Bunge la Jamhuri ya Muungano limeshazinduliwa na baraza jipya la mawaziri limeshaapishwa na kuanza kazi kwa kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu, sasa kauli mbiu hii sasa ielekezwe Zanzibar. Uchumi wa Zanzibar kwa kiasi kikubwa unategemea sana utalii, na tatizo linaloendelea Zanzibar limeathiri sana sekta ya utalii, Mnafamu safari ngapi za watalii zimefutwa baada ya hali hii kujitokeza? Maana yake ni kwamba wafanyakazi wa mahotelini, melini, katika ndege wachuuzi wa mitaani na wananchi wa kawaida Unguja wanalia njaa, kwa kuwa idadi ya watalii imepungua sana. Hakuna mtalii anayetaka kwenda mahali ambapo hana uhakika wa usalama wake.

Chondechonde viongozi WOTE wa nchi hii msikae kimya, kila mmoja wenu katika nafsi zenu CHUKUENI HATUA MARA MOJA KWA MASLAHI YA WATU WA ZANZIBAR NA TANZANIA KWA UJUMLA
 
Mkuu, this is by far, the best topic of 2015, on my opinion. Umezungumza kitu cha maana na chenye maslahi mapana kwa mustakbala na heshima ya Taifa letu. Heshima ya Tanzania, like it or not, imeshuka kwa kiasi kikubwa kutokana na suala la uchaguzi wa Zanzibar. Viongozi wetu hawana nguvu ya kwenda nchi jirani na kuhubiri demokrasia wakati nchini kwetu inatushinda kutekeleza. Watu tunashindwa kufahamu kwamba kila Ubalozi ina majasusi na kazi yao ni kufahamu undani wa yanayoendelea nchini, ukweli wao wanaupata kutoka sources na sio kutegemea kusoma magazeti. Wana watu wamo ndani ya serikali na vyama vyote wanawalipa kila mwezi, kwa exchange ya taarifa wanazozitaka. Nilishangaa kuona Kinana anawaandikia barua EU na USA governments kuwatia kasumba ya ugaidi na ufisadi wa Lowasa wakati references kazipata kwenye leak ya diplomatic cables za kwao!

Kwa vile uzi wako umegusua upande wa pili wa muungano, kwa ushabiki wa wana JF, hutopata hata michango 20 kwa wiki nzima. Na 15 kati ya hiyo itakuwa ya kukukejeli tu, maneno kama, "Zanzibar haituhusu, Wao si walisema ni nchi" na maneno mengine mingi tu ya kibarazuli yasiyo na mashiko. Lau kama ungeazisha uzi wa kipumbavu kama, "Kikwete anywa chai ya rangi bila sukari, au, Mkapa nguo zake za zamani hazimtoshi tena" basi ungejaza ukumbi kwa nusu saa tu.

Ahsante kwa kuliona hili na tuombe Mungu, kama ni wapenda demokrasia duniani, tulipe kipau mbele kwa mustakbala wa Taifa na kuwa mfano mwema kwa jirani zetu
 
Naunga mkono hoja,tunatowaje kibanzi kwenye jicho la mwenzetu wakati letu lina kibanzi?
 
Yote mawili yanaweza kufanywa sambamba. Kunahaja ya kutatua burundi kwanza kwa sababu ya mauwaji ya wananchi. Tatizo la Zanzibar lipo kwenye stage tofauti ukilinganisha na Burundi. Zanzibar kuna manzungumzo yanaendelea na suluhisho litapatikanika tu.
 
Genghis Khan;

Anza kwanza kutoa kibanzi jichoni mwako na kisha nenda kwa mwenzio mtolee chake!

Ni pointless kusema kuwa mgogoro wa Zanzibar haujafikia kiwango cha watu kuuwana kutokana na tofauti za kisiasa za kutengenezwa sawasawa na Burundi.


Kwa logic iliyo nyuma ya hoja yako ni kuwa tuyaache ya Zanzibar yafikie hatua kama ilivyo huko Burundi ndo tushtuke tuseme, ala kumbe kuna tatizo!!

Is that what you mean??
 
So sad huu uzi una comment 5 tu wakati unagusa ukweli halisi
 
Yote mawili yanaweza kufanywa sambamba. Kunahaja ya kutatua burundi kwanza kwa sababu ya mauwaji ya wananchi. Tatizo la Zanzibar lipo kwenye stage tofauti ukilinganisha na Burundi. Zanzibar kuna manzungumzo yanaendelea na suluhisho litapatikanika tu.

Situation in Zanzibar is very tense, unataka watu wauwane ndio ipewe attention it deserves? Wewe sijui diplomasia gani uliyokuwa nayo kichwani kwako. Huko Burundi tumevuruga sisi, kwani Tanzania ndiyo ilo facilitate kurudi kwa Nkrunziza nchini Burundi. Sisi ndio tulochafuwa Burundi kutokana na mtizamk
Yote mawili yanaweza kufanywa sambamba. Kunahaja ya kutatua burundi kwanza kwa sababu ya mauwaji ya wananchi. Tatizo la Zanzibar lipo kwenye stage tofauti ukilinganisha na Burundi. Zanzibar kuna manzungumzo yanaendelea na suluhisho litapatikanika tu.

I like your optism and let's hope for the best possible outcome. Nevertheless, the situation in Zanzibar is more tense than it looks on the surface.

Kwa hiyo tusubiri mpaka watu wauwane ndio Zanzibar ipewe attention it desrves?
Burundi mara hii tumelikoroga sisi. Tanzania ndiyo ilo facilitate kurejea kwa Nkrunziza baada ya jaribio la mapinduzi. Jumuia zote za kimataifa linajuwa hilo. Kwa sasa tunataka kujikosha tu. Position ya Tanzania kwa situation ya Burundi ni sawa na position ya Turkey kwa situation ya Syri
So sad huu uzi una comment 5 tu wakati unagusa ukweli halisi

Refer comment #2 above
 
Back
Top Bottom