Zanzibar kunyimwa uanachama wa FIFA na CAF ni chuki kisiasa au kukosa vigezo?

Kibosho1 Tatizo ni kuwa Tanzania Bara au Tanganyika wamejiunga ndani ya FIFA kwa kupitia mlango wa Tanzania. Walitakiwa wajisajili kama Tanzania Bara. Sasa Zanzibar ipo ndani ya Tanzania kwahiyo ni ngumu kupata uanachama kwa kuwa tayari wamo ndani ya fifa kwa kupitia mlango wa Tanzania.
Suluhisho la hili ni Tanzania Bara kubadili Jina lao na mipaka yao ndani ya Fifa kitu ambacho Serekali ya Bara haitaki kiroho mbaya tu.

Mbali na hivo TFF ikishirikiana na SMT licha ya kuwabania Zanzibar kupata uanachama pia wanagoma kuwapa Zanzibar mgao wowote unaotokana na FIFA. Kwa maana Si tu Hawataki wenzao wapate uanachama bali hata Mgao hawataki kuwapa.

Huu Muungano una madudu mengi sana
 
Ukibebwa, basi jitahidi ujishikilie! Zanzibar wamebebwa na CAF kwa kupewa nafasi mbili za klabu zao kushiriki CAF Champions League a Confederation Cup. Lakini hawa jamaa huwa wanaishia raundi ya awali, na wakijitahidi sana wanaishia raundi ya kwanza. Sasa hapo inakuwa ni vigumu hata kuweza kuishawishi CAF itoe nafasi hiyo kwa ngazi ya timu za taifa
Na Somali nao, Djibout, Malawi, Eritrea, Mauritius, Seychelles, Burundi na nyengine mfano wa hizo ulizisikia zimefika wapi.

Shida ya Zanzibar ni moja tuu imekaliwa kimabavu na Jamhuri ya Tanganyika kiasi kwamba haiwezi kufanya ya kwake hata kwenye sekta ya michezo.

Na hii ni kaana hata kwa hiyo inayoitwa Taifa Stars ikiingua kwenye mashindano ya kimataifa huwa haifiki popote hubaki kuhamasishana tuu na kujipa moyo mnajifunza.
 
Kibosho1 Tatizo ni kuwa Tanzania Bara au Tanganyika wamejiunga ndani ya FIFA kwa kupitia mlango wa Tanzania. Walitakiwa wajisajili kama Tanzania Bara. Sasa Zanzibar ipo ndani ya Tanzania kwahiyo ni ngumu kupata uanachama kwa kuwa tayari wamo ndani ya fifa kwa kupitia mlango wa Tanzania.
Suluhisho la hili ni Tanzania Bara kubadili Jina lao na mipaka yao ndani ya Fifa kitu ambacho Serekali ya Bara haitaki kiroho mbaya tu.

Mbali na hivo TFF ikishirikiana na SMT licha ya kuwabania Zanzibar kupata uanachama pia wanagoma kuwapa Zanzibar mgao wowote unaotokana na FIFA. Kwa maana Si tu Hawataki wenzao wapate uanachama bali hata Mgao hawataki kuwapa.

Huu Muungano una madudu mengi sana
Bora uvunjike tu. Mbona China na Hong Kong wote wanachama wa fifa ?
 
Na Somali nao, Djibout, Malawi, Eritrea, Mauritius, Seychelles, Burundi na nyengine mfano wa hizo ulizisikia zimefika wapi.

Shida ya Zanzibar ni moja tuu imekaliwa kimabavu na Jamhuri ya Tanganyika kiasi kwamba haiwezi kufanya ya kwake hata kwenye sekta ya michezo.

Na hii ni kaana hata kwa hiyo inayoitwa Taifa Stars ikiingua kwenye mashindano ya kimataifa huwa haifiki popote hubaki kuhamasishana tuu na kujipa moyo mnajifunza.
Asante kwa jibu zuri
 
Sisi watanzania na Waafrika kwa ujumla tuna matatizo sana ya kiakili, yani mtu yupo tayari kuua cha nyumbani na wakati huo huo anatetea cha nje. Mtu na akili zake timamu hawezi kusema Zanzibar sio nchi.
Na ndo maana huko Ulaya tunabaguliwa maana sisi wenyewe hatujitambui
 
Kibosho1 Tatizo ni kuwa Tanzania Bara au Tanganyika wamejiunga ndani ya FIFA kwa kupitia mlango wa Tanzania. Walitakiwa wajisajili kama Tanzania Bara. Sasa Zanzibar ipo ndani ya Tanzania kwahiyo ni ngumu kupata uanachama kwa kuwa tayari wamo ndani ya fifa kwa kupitia mlango wa Tanzania.
Suluhisho la hili ni Tanzania Bara kubadili Jina lao na mipaka yao ndani ya Fifa kitu ambacho Serekali ya Bara haitaki kiroho mbaya tu.

Mbali na hivo TFF ikishirikiana na SMT licha ya kuwabania Zanzibar kupata uanachama pia wanagoma kuwapa Zanzibar mgao wowote unaotokana na FIFA. Kwa maana Si tu Hawataki wenzao wapate uanachama bali hata Mgao hawataki kuwapa.

Huu Muungano una madudu mengi sana
Afadhali ww umeandika cha maana kuliko hao wanaosema Zanzibar sio nchi.
 
Afadhali ww umeandika cha maana kuliko hao wanaosema Zanzibar sio nchi.
Kaandika vizuri sana lakini bado. Mfano Kosovo ni jimbo la Serbia na Serbia ni mwanachama wa fifa, mbona imepewa uanachama juzi juzi? Hong Kong nayo ni nchi?

Bado sijaona kigezo cha zbar kunyimwa huu uanachama eti kisa ipo Tanzania
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom