Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Niliuliza hili swali huko nyuma kuwa Mzanzibari ni nani? sikupata jibu zuri la kiakili. Baada ya kumsikia Seif akiapa kuwa "hatatoka mtu mahali popote duniani kuja kutawala Zanzibar na kuwa Zanzibar itatawaliwa na Wazanzibari" nimeshindwa kuelewa anaposema "Wazanzibari" anamaanisha watu gani?
a. Wananchi wanaoishi Zanzibar na ambao wametimiza masharti ya ukazi ya Zanzibar hata kama kinasaba hawana asili ya Zanzibar?
b. Wananchi wa Zanzibar ambao wanahistoria ya muda mrefu huko Zanzibar hata kama wako nje ya eneo la jiografia la Zanzibar?
c. Wazanzibari kama watu wenye kuamini na kuitamani nchi iliyokuwepo kabla ya Uhuru wa Mwingereza?
d. Wazanzibari waliokuwa chini ya uongozi wa Serikali ya kwanza ya Shamte kabla ya Mapinduzi?
e. Wazanzibari chini ya Serikali ya Mapinduzi?
f. Wazanzibari kama watu wote wenye kujitambua kuwa wana asili ya Zanzibar hata kama hawaishi Zanzibar au hawajawahi kuishi Zanzibar hivi karibuni?
Kwa mfano, Mmakonde aliyezaliwa na kukulia Zanzibar atatambulika kama Mzanzibari? Je mmshirazi ambaye wazazi wake wametokea Zanzibar lakini amekulia Tanga na ana familia Zanzibar huyo naye ni Mzanzibari?
Bado najiuliza Mzanzibari ni nani hasa?
a. Wananchi wanaoishi Zanzibar na ambao wametimiza masharti ya ukazi ya Zanzibar hata kama kinasaba hawana asili ya Zanzibar?
b. Wananchi wa Zanzibar ambao wanahistoria ya muda mrefu huko Zanzibar hata kama wako nje ya eneo la jiografia la Zanzibar?
c. Wazanzibari kama watu wenye kuamini na kuitamani nchi iliyokuwepo kabla ya Uhuru wa Mwingereza?
d. Wazanzibari waliokuwa chini ya uongozi wa Serikali ya kwanza ya Shamte kabla ya Mapinduzi?
e. Wazanzibari chini ya Serikali ya Mapinduzi?
f. Wazanzibari kama watu wote wenye kujitambua kuwa wana asili ya Zanzibar hata kama hawaishi Zanzibar au hawajawahi kuishi Zanzibar hivi karibuni?
Kwa mfano, Mmakonde aliyezaliwa na kukulia Zanzibar atatambulika kama Mzanzibari? Je mmshirazi ambaye wazazi wake wametokea Zanzibar lakini amekulia Tanga na ana familia Zanzibar huyo naye ni Mzanzibari?
Bado najiuliza Mzanzibari ni nani hasa?