Zanzibar itatawaliwa na Wazanzibari - Seif Sharrif

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Niliuliza hili swali huko nyuma kuwa Mzanzibari ni nani? sikupata jibu zuri la kiakili. Baada ya kumsikia Seif akiapa kuwa "hatatoka mtu mahali popote duniani kuja kutawala Zanzibar na kuwa Zanzibar itatawaliwa na Wazanzibari" nimeshindwa kuelewa anaposema "Wazanzibari" anamaanisha watu gani?

a. Wananchi wanaoishi Zanzibar na ambao wametimiza masharti ya ukazi ya Zanzibar hata kama kinasaba hawana asili ya Zanzibar?

b. Wananchi wa Zanzibar ambao wanahistoria ya muda mrefu huko Zanzibar hata kama wako nje ya eneo la jiografia la Zanzibar?

c. Wazanzibari kama watu wenye kuamini na kuitamani nchi iliyokuwepo kabla ya Uhuru wa Mwingereza?

d. Wazanzibari waliokuwa chini ya uongozi wa Serikali ya kwanza ya Shamte kabla ya Mapinduzi?

e. Wazanzibari chini ya Serikali ya Mapinduzi?

f. Wazanzibari kama watu wote wenye kujitambua kuwa wana asili ya Zanzibar hata kama hawaishi Zanzibar au hawajawahi kuishi Zanzibar hivi karibuni?

Kwa mfano, Mmakonde aliyezaliwa na kukulia Zanzibar atatambulika kama Mzanzibari? Je mmshirazi ambaye wazazi wake wametokea Zanzibar lakini amekulia Tanga na ana familia Zanzibar huyo naye ni Mzanzibari?

Bado najiuliza Mzanzibari ni nani hasa?
 
Niliuliza hili swali huko nyuma kuwa Mzanzibari ni nani? sikupata jibu zuri la kiakili. Baada ya kumsikia Seif akiapa kuwa "hatatoka mtu mahali popote duniani kuja kutawala Zanzibar na kuwa Zanzibar itatawaliwa na Wazanzibari" nimeshindwa kuelewa anaposema "Wazanzibari" anamaanisha watu gani?

a. Wananchi wanaoishi Zanzibar na ambao wametimiza masharti ya ukazi ya Zanzibar hata kama kinasaba hawana asili ya Zanzibar?

b. Wananchi wa Zanzibar ambao wanahistoria ya muda mrefu huko Zanzibar hata kama wako nje ya eneo la jiografia la Zanzibar?

c. Wazanzibari kama watu wenye kuamini na kuitamani nchi iliyokuwepo kabla ya Uhuru wa Mwingereza?

d. Wazanzibari waliokuwa chini ya uongozi wa Serikali ya kwanza ya Shamte kabla ya Mapinduzi?

e. Wazanzibari chini ya Serikali ya Mapinduzi?

f. Wazanzibari kama watu wote wenye kujitambua kuwa wana asili ya Zanzibar hata kama hawaishi Zanzibar au hawajawahi kuishi Zanzibar hivi karibuni?

Kwa mfano, Mmakonde aliyezaliwa na kukulia Zanzibar atatambulika kama Mzanzibari? Je mmshirazi ambaye wazazi wake wametokea Zanzibar lakini amekulia Tanga na ana familia Zanzibar huyo naye ni Mzanzibari?

Bado najiuliza Mzanzibari ni nani hasa?

Mbona hivyo mzee Mwanakijiji!.Zamani ulikuwa unaheshimika sana hapa Jamii Forums.Sasa naona umezeeka sana,vyenginevyo umechoka.Bora upumzike.
Nashangaa!., kwa sababu yote uliyoorodhesha ndiyo majibu,na wala hayana utata.Yawezekana una kitu umekificha lakini ujumbe unaopatikana hapa ni kuwa hekima hiyo imekushinda.
 
Mimi naona ibadilishwe Zanzibar iwe kama mikoa mingine ya TZ. Kusiwe na Double Standard.
 
Mbona hivyo mzee Mwanakijiji!.Zamani ulikuwa unaheshimika sana hapa Jamii Forums.Sasa naona umezeeka sana,vyenginevyo umechoka.Bora upumzike.
Nashangaa!., kwa sababu yote uliyoorodhesha ndiyo majibu,na wala hayana utata.Yawezekana una kitu umekificha lakini ujumbe unaopatikana hapa ni kuwa hekima hiyo imekushinda.

Inabidi ujifunze kujibu hoja tu.. mambo ya kushambulia mtu (ad hominem) hayafanyi hoja yako iwe na nguvu. Jawabu kuwa 'Yote ni kweli" haliwezi kuwa jawabu sahihi kwani menngine yanapingana. Vitu vikipingana haviwezi vyote kuwa kweli kwa wakati mmoja.
 
wazanzibari wameelezwa vizuri kwenye katiba ya zanzibar kasome usiwe mvivu

Yale yale.. sijaelewa kwanini Maalim kauna ulazima wa kuwaambia wapiga kura kuwa hatokuja mtu "kutoka sehemu yoyote duniani kuwatawala Zanzibar"... na kuwa Zanzibar itatawaliwa na Wazanzibari? Sasa itakuwaje kama Mzanzibari huyo (sema aliyekuwa Mzanzibari kabla ya Mapinduzi) akitaka kuja kutawala? Au yeye si Mzanzibari?
 
Hawa jamaa wana elewa kitu wanacho maanisha. japo ni vigumu sana kukisema adharani, ukweli unabaki ndani ya mioyo yao.Hawataki mtu asiye kuwa na mitizamo ya kibinafsi (Zanzibar kwanza na si Tanzania kwanza).
 
Niliuliza hili swali huko nyuma kuwa Mzanzibari ni nani? sikupata jibu zuri la kiakili. Baada ya kumsikia Seif akiapa kuwa "hatatoka mtu mahali popote duniani kuja kutawala Zanzibar na kuwa Zanzibar itatawaliwa na Wazanzibari" nimeshindwa kuelewa anaposema "Wazanzibari" anamaanisha watu gani?

a. Wananchi wanaoishi Zanzibar na ambao wametimiza masharti ya ukazi ya Zanzibar hata kama kinasaba hawana asili ya Zanzibar?

b. Wananchi wa Zanzibar ambao wanahistoria ya muda mrefu huko Zanzibar hata kama wako nje ya eneo la jiografia la Zanzibar?

c. Wazanzibari kama watu wenye kuamini na kuitamani nchi iliyokuwepo kabla ya Uhuru wa Mwingereza?

d. Wazanzibari waliokuwa chini ya uongozi wa Serikali ya kwanza ya Shamte kabla ya Mapinduzi?

e. Wazanzibari chini ya Serikali ya Mapinduzi?

f. Wazanzibari kama watu wote wenye kujitambua kuwa wana asili ya Zanzibar hata kama hawaishi Zanzibar au hawajawahi kuishi Zanzibar hivi karibuni?

Kwa mfano, Mmakonde aliyezaliwa na kukulia Zanzibar atatambulika kama Mzanzibari? Je mmshirazi ambaye wazazi wake wametokea Zanzibar lakini amekulia Tanga na ana familia Zanzibar huyo naye ni Mzanzibari?

Bado najiuliza Mzanzibari ni nani hasa?

Ulichotaka ni kujenga choko choko tu.Hasa kwenye vipengele hivyo vitatu hapo juu.
Bado inabaki kuwa ni kweli na havipingani.Ikiwa kuna kipingamizi kifafanue.Fuata ushauri wa Mtu wa Pwani uepuka na kukurupuka kama Dkt.Slaa.

 
Inabidi ujifunze kujibu hoja tu.. mambo ya kushambulia mtu (ad hominem) hayafanyi hoja yako iwe na nguvu. Jawabu kuwa 'Yote ni kweli" haliwezi kuwa jawabu sahihi kwani menngine yanapingana. Vitu vikipingana haviwezi vyote kuwa kweli kwa wakati mmoja.
Mambo haya ya Zenj yalikushinda zamani, toka mazungumzo ya maridhiano yalipoanza ulikuja na chokochok nyingi, mara sultani mara wamevunja katiba, kumbe bado hujakatatamaa? na Zenj!maswali yako kuhusu Zenj yatapuuzwa kama zilivyo puuzwa chokochoko zako.
 
Yale yale.. sijaelewa kwanini Maalim kauna ulazima wa kuwaambia wapiga kura kuwa hatokuja mtu "kutoka sehemu yoyote duniani kuwatawala Zanzibar"... na kuwa Zanzibar itatawaliwa na Wazanzibari? Sasa itakuwaje kama Mzanzibari huyo (sema aliyekuwa Mzanzibari kabla ya Mapinduzi) akitaka kuja kutawala? Au yeye si Mzanzibari?


katiba ndio muongozo wa taifa lolote sasa nenda kasome wamemueleza nani mzanzibari na ukiangalia hapo alichonena huenda anakusudia kuwa hakuna mkoloni wa kiarabu au wa kokote kule kuja kutawala zanzibar zaidi ya wazanzibari wenyewe kama ilivyoeleza katiba


kama una jengine liweke wazi tulijadili
 
Apo Maalim Seif Sherrif Hamadi ,anawambia nyie mliojaa kasumba za kuwa CUF inataka kuwaludisha waalabu ,yaani mnajazwa kasumba ya eti kunataka kuludishwa sulutani ,ivi mnakujua huko waliko masulutani kukoje ? Basi wa Qatar keshasema atajenga shopping centre ya aina yake under water itakayocost 500 million dollar watu na magari vikiwemo viwanja vya michezo ,sasa sijui mtasemaje ,huko kwenu waalabu walitaka kulima mkaweka mkwala eti wenyeji watakosa pa kulima,ivi mnalima wapi ,na bado mnatumia jembe la mkono ,aloo ama kweli maendeleo ya ccm yataletwa na mawazo duni kama hayo ya kuludi kwa sulutani ,poleni sana.
 
Niliuliza hili swali huko nyuma kuwa Mzanzibari ni nani? sikupata jibu zuri la kiakili. Baada ya kumsikia Seif akiapa kuwa "hatatoka mtu mahali popote duniani kuja kutawala Zanzibar na kuwa Zanzibar itatawaliwa na Wazanzibari" nimeshindwa kuelewa anaposema "Wazanzibari" anamaanisha watu gani?

a. Wananchi wanaoishi Zanzibar na ambao wametimiza masharti ya ukazi ya Zanzibar hata kama kinasaba hawana asili ya Zanzibar?

b. Wananchi wa Zanzibar ambao wanahistoria ya muda mrefu huko Zanzibar hata kama wako nje ya eneo la jiografia la Zanzibar?

c. Wazanzibari kama watu wenye kuamini na kuitamani nchi iliyokuwepo kabla ya Uhuru wa Mwingereza?

d. Wazanzibari waliokuwa chini ya uongozi wa Serikali ya kwanza ya Shamte kabla ya Mapinduzi?

e. Wazanzibari chini ya Serikali ya Mapinduzi?

f. Wazanzibari kama watu wote wenye kujitambua kuwa wana asili ya Zanzibar hata kama hawaishi Zanzibar au hawajawahi kuishi Zanzibar hivi karibuni?

Kwa mfano, Mmakonde aliyezaliwa na kukulia Zanzibar atatambulika kama Mzanzibari? Je mmshirazi ambaye wazazi wake wametokea Zanzibar lakini amekulia Tanga na ana familia Zanzibar huyo naye ni Mzanzibari?

Bado najiuliza Mzanzibari ni nani hasa?

Mwanakijiji swali unalouliza ni kama lile la fumbo la imani la utatu mtakatifu. Jibu la nani mzanzibar inawezekana ni Seifu tu analo, kwanza uukane umakonde, usukuma, na elements zote zinazohusiana na ubara. Au kwa kifupi anaposema Zanzibar itatawaliwa na wazanzibar maana yake ni kuwa wabara au wale wazanzibara (kina Sepetu, Mwakanjuki, Mwinyi na mapuri wale sio wazanzibari wale ni wazanzibara, na ndio kwa tafsiri yake hawatakiwi kutawala zanzibar. Inawezekana kuwa katiba inatamka vizuri "mzanzibari" ni nani, lakini Seif anayo ya kwake mbali na ile iliyotamkwa. Ukiangalia kwa undani unaweza kuona kuwa Seif anataka kuifanya Zanzibar iwe kwa image yake.

Kama umenote ameshinikiza katiba ibadilishwe ikiwa ni hatua moja ya kuendeleza ajenda zake.

Na hivi juzi kuna jamaa mmoja ameanza kuingia kiujanja ujanja kwa kuwapa watu dola 100 za kubeba mizigo, ndio kabisa wanzanzibara wanatakiwa kukaa kando ile wazanzibari wanufaike.
 
Kumbe huyu ndie mwanakijiji? Yaani anafanana na jina lake vilevile kama watu wa vijijini walivyokoseshwa elimu na nyerere wakabakia kua washamba na wajinga maisha.

Mwanakijiji inavyoonekana either umechanganyikiwa au unatokea iringa kunywa ulanzi na umekua ahmada umelewa.

Kwani ukiambiwa mtanzania weye humjui? Au wale waliozaliwa kabla ya mwaka 1964 kabla ya muungano nao si watanzania? Kwani wakati huo haikuwepo hiyo munayoiita tanzania.
 
Mbona hivyo mzee Mwanakijiji!.Zamani ulikuwa unaheshimika sana hapa Jamii Forums.Sasa naona umezeeka sana,vyenginevyo umechoka.Bora upumzike.
Nashangaa!., kwa sababu yote uliyoorodhesha ndiyo majibu,na wala hayana utata.Yawezekana una kitu umekificha lakini ujumbe unaopatikana hapa ni kuwa hekima hiyo imekushinda.

samahani ni ushauri tu, je unaweza kuyarudia vizuri aliyoandika Mwanakijiji?
ukiwa umevua kofia iliyokufanya uje kwa jazba na kushindwa kumwelewa Mwanakijiji?
 
Mwanakijiji swali unalouliza ni kama lile la fumbo la imani la utatu mtakatifu. Jibu la nani mzanzibar inawezekana ni Seifu tu analo, kwanza uukane umakonde, usukuma, na elements zote zinazohusiana na ubara. Au kwa kifupi anaposema Zanzibar itatawaliwa na wazanzibar maana yake ni kuwa wabara au wale wazanzibara (kina Sepetu, Mwakanjuki, Mwinyi na mapuri wale sio wazanzibari wale ni wazanzibara, na ndio kwa tafsiri yake hawatakiwi kutawala zanzibar. Inawezekana kuwa katiba inatamka vizuri "mzanzibari" ni nani, lakini Seif anayo ya kwake mbali na ile iliyotamkwa. Ukiangalia kwa undani unaweza kuona kuwa Seif anataka kuifanya Zanzibar iwe kwa image yake.
Kama umenote ameshinikiza katiba ibadilishwe ikiwa ni hatua moja ya kuendeleza ajenda zake.

Na hivi juzi kuna jamaa mmoja ameanza kuingia kiujanja ujanja kwa kuwapa watu dola 100 za kubeba mizigo, ndio kabisa wanzanzibara wanatakiwa kukaa kando ile wazanzibari wanufaike.
mbaya zaidi ni kwamba hawa wenzetu ni kina ''mong'onyo'' hayo ya kupewa $ 100 hivi hivi ndiyo raaaha kwao
maana utamaduni wao ni kufunga msuri harafu dufu na bao asubuhi hadi jioni huku majungu kama kawa
 
Jf ni forum nzuri sana ila kuna baadhi yetu tunaishusha thamani kwa kuruhusu jazba zituongoze kwenye comment na midahalo. Aministrator wanatakiwa wajaribu kubuni mbinu kama classfication ya user.Otherwise jf itakuja kuwa kijiwe cha kubishana nakurushana roho tu badala ya kuelimishana kwa hoja

Mwanakijiji hoja yako kwa mtazamo mwingine labda wadau tujiulize Nani ambaye si mzanzibari.?

Tatizo naloliona mm baadhi ya wanzanzibari tena wanaosikilizwa na wenye "vipaza sauti" wanaona zanzibar kama ni monocluture society jambo ambalo sio kweli Wao wenyewe kwa wenyewe hawakubaliani nani ni au si raia/mkazi

Nakumbuka kuna wakati maalim seif aliwekewa pingamizi ya ukazi
 
MwanaKIJIJI, Mwiba amekujibu suala lako. Maalim Seif anazungumza na "audience" yake kuwapa imani juu ya uwezekano wa asiyerkuwa mzanzibari kuja kuitawala zanzibar. Kama unafuatilia "campaign" za Zanzibar, utafahamu kabisa kuwa kambi ya CCM wamo katika mashaka makubwa sana na njia wanaoyofikiria ya kuweza kuwatoa katika mashaka yao ni hii ya UARABU. Kwa bahati, wazanzibari wamewashitukia zamzni. Kadi hii haina nguvu tena. Sisi tunasonga mbele. Maalim Seif tutamchagua kama Raisi wa jamhuru ya wananchi wa Zanzibar.
 
MwanaKIJIJI, Mwiba amekujibu suala lako. Maalim Seif anazungumza na "audience" yake kuwapa imani juu ya uwezekano wa asiyerkuwa mzanzibari kuja kuitawala zanzibar. Kama unafuatilia "campaign" za Zanzibar, utafahamu kabisa kuwa kambi ya CCM wamo katika mashaka makubwa sana na njia wanaoyofikiria ya kuweza kuwatoa katika mashaka yao ni hii ya UARABU. Kwa bahati, wazanzibari wamewashitukia zamzni. Kadi hii haina nguvu tena. Sisi tunasonga mbele. Maalim Seif tutamchagua kama Raisi wa jamhuru ya wananchi wa Zanzibar.
Hivi hao kambi ya CCM sii Wazanzibari? au kuna Wakati Zanzibar ilitawaliwa na mtu asiyekuwa Mzanzibar? Je, Dr.Shein na Bilal sio Wazanzibar.

- Huyu Seif hakika sijui ni uzee au ni kitu gani kwa sababu sioni sababu kabisa ya kutoa maneno hayo ikiwa swala kubwa ni kupata serikali tatu ikiwa ni pamoja na ile ya Muungano...Kisha ndiye aliyeweka muafaka na CCM na kukubali serikali ya mseto, je alipokubali serikali ya mseto alikuwa akifikiria kwamba hao CCM wanaoongoza leo hii hawatakuwepo au?
 
Jf ni forum nzuri sana ila kuna baadhi yetu tunaishusha thamani kwa kuruhusu jazba zituongoze kwenye comment na midahalo. Aministrator wanatakiwa wajaribu kubuni mbinu kama classfication ya user.Otherwise jf itakuja kuwa kijiwe cha kubishana nakurushana roho tu badala ya kuelimishana kwa hoja

Mwanakijiji hoja yako kwa mtazamo mwingine labda wadau tujiulize Nani ambaye si mzanzibari.?

Tatizo naloliona mm baadhi ya wanzanzibari tena wanaosikilizwa na wenye "vipaza sauti" wanaona zanzibar kama ni monocluture society jambo ambalo sio kweli Wao wenyewe kwa wenyewe hawakubaliani nani ni au si raia/mkazi

Nakumbuka kuna wakati maalim seif aliwekewa pingamizi ya ukazi

Unajua ni jambo la kijinga kusema Zaznibar itatawaliwa na wazanzibari wakati kila mtu anajua inatakiwa kuwa hivyo. Huwezi kuzungumza na audience ya wazanzibar na kuwaambia kuwa Wazanzibari ndio watatawala Zanzibar. Itakuwa ujinga ulioje kwa JK, Slaa au Lipumba kusema Tanzania itatawaliwa na watanzania, hiyo ni kazi ya sheria za nchi na tume, si ya mgombea.

Kama ni kweli audience ilikuwa ni watu wa Zanzibar basi ni wazi kuwa alikuwa anawasema wazanzibara, yeye anaona wazanzibari ni bora zaidi kuliko wazanzibara. Kwa hiyo ni ujumbe huo ambao alikuwa anauleta.

Kweli ni ajabu sana kila mara baadhi ya wenzetu wanasema wanataka misaada, wanasema kuwa muungano umepunguza misaada, yaani bila hata aibu wanaufagilia umatonya. JK alikasirisha watu kwa kusema tuynaishi kwa misaada lakini wenzetu Zanzibar wanaoana hiyo ndio heri.

Na sasa mwarabu anaingia taratibu ameanza kwa kuwarubuni kwa dola 100, then ataleta khalua na tende, then atashika uchumi na kila kitu. Ngoja wamruhusu halafu baadaye aanze kuwachapa mikwaju ndio wataamka.
 
Back
Top Bottom