Zanzibar ilipata UHURU mwaka 1963, kwa nini ukweli huu unafichwa?

Sr.
Uhuru ni hali ambayo kwayo wenyeji wa Taifa, Nchi ausehemu yake wana madaraka ya kujichagulia dira na viongozi wawatakao, uwezo wakuwaondoa kwa mujibu wa sheria zilizo pitishwa na vyombo halali vya kitaifa; nakwa hiyo kuwa na sovereignty juu ya Taifa au nchi yao na mstakali wake. Uhuruni tofauti na mapinduzi, kwani mapinduzi yanauondosha utawala ulopo kwa nguvuau amani; ingawa aidha mapinduzi yanaweza kuleta uhuru kutegemea mfumo, dira nauongozi uliopinduliwa. Lakini mapinduzi yanaweza kuwa na dhaira ya kuletauwiano katika kushiriki katika usimamizi wa utawala, kugawana mali n.k.Mapinduzi ya Urusi yalilenga hili, lakini vita vya mapinduzi vya Marekanivililenga kuleta uhuru. Kuhusu Zanzibar inategemea mtazamo wako; Uhuru chini ya himaya ya Sultani uliwakilisha maono ya kitaifa au la?

Kaka Kasesela heshima mbele sana.

Kwa kesi ya Zanzibar Mapinduzi ya 12, January 1964 yalifanywa na John Okello Kijana wa Kiganda aliyekuwa akiishi Pemba kwa muda mchache, huyu jamaa alikuwa na ushawishi mkubwa kwa vijana na nia yake ya kuipindua serikali ya Znz ilifanikiwa, Aliingia unguja na usiku huo wa Jan, 12, 1964 alikiteka kisiwa hicho na ikumbukwe kuwa kipindi hicho bunge la Zanzibar lilifuata mfumo wa bunge la Kiingereza, Sultani akiwa kama ni mtawala tu lakini sio mtawala mwenye maamuzi ya mwisho, kulikuwa na wanzanzibar wengi tu kwenye bunge hili waliokuwa na sauti na maamuzi, kwa kifupi wa Znz waliipindua serikali yao halali.

Swali hapa kwa nini tunakumbatia historia ya Mapinduzi ya Mganda Okello na si nguvu zetu za kudai uhuru kutoka kwa mkoloni Mwingereza?..
 
huwa nikisikia tu zanzibar napatwa na kichefuchefu siwapendi hao

hata baba ako wa taifa alisema angetamani kuona zanzibar ikizama ktk bandari ya hindi! Lakini nani aliyezama ni yeye alieko shimoni au visiwa vya zanzibar? Na wewe uko njiani kuelekea kaburini na hivyo visiwa vinawenyewe!
 
Ili mradi Maalim na Jussa wamo ndani ya serikali hii tarehe lazima itarudishwa na kutambuliwa. Nchi ipo, bendera ipo, wimbo wa taifa upo, tarehe ya uhuru itakosekanaje? Nawahurumia sana akina "Mapinduzi Daima". Amani Karume kairudisha nchi ujombani kwa kuwa yeye hakuwa mtoto halisi wa Abeid.

tafazal wildcard, kwani alikua mtoto wa nani?? dadavua kwa faida ya wengi....
 
Kaka Kasesela heshima mbele sana.

Kwa kesi ya Zanzibar Mapinduzi ya 12, January 1964 yalifanywa na John Okello Kijana wa Kiganda aliyekuwa akiishi Pemba kwa muda mchache, huyu jamaa alikuwa na ushawishi mkubwa kwa vijana na nia yake ya kuipindua serikali ya Znz ilifanikiwa, Aliingia unguja na usiku huo wa Jan, 12, 1964 alikiteka kisiwa hicho na ikumbukwe kuwa kipindi hicho bunge la Zanzibar lilifuata mfumo wa bunge la Kiingereza, Sultani akiwa kama ni mtawala tu lakini sio mtawala mwenye maamuzi ya mwisho, kulikuwa na wanzanzibar wengi tu kwenye bunge hili waliokuwa na sauti na maamuzi, kwa kifupi wa Znz waliipindua serikali yao halali.

Swali hapa kwa nini tunakumbatia historia ya Mapinduzi ya Mganda Okello na si nguvu zetu za kudai uhuru kutoka kwa mkoloni Mwingereza?..
Zanzibar haikuwa koloni la Mwingereza. Ilikuwa ni "Protectorate" tu. Sultani alikuwepo kwa miaka mingi tu chini ya uangalizi wa Uingereza. Kilichofanyika tarehe 10.12.1963 ni kumwongezea madaraka Sultani ambayo alidumu nayo chini ya mwezi mmoja tu. Akina Seif wamemsomesha Amani akawaelewa. Ipo SUK sasa kuelekea kwenye Usultani tena. Ni suala la muda tu.
 
Waingereza waliondosha majeshi yao kikiwemo kikosi maalumu cha Kiarishi ambacho kilikuwa kimewekwa karibu na uwanja wa gofu na mpaka wa Mji Mkongwe mapema mwaka 1963. Kipindi ilipopandishwa bendera ya Taifa huru la Zanzibar tarehe 12 Disemba 1963, huku kukiadhimishwa uondokaji wa Gavana wa kiingereza Zanzibar na mwisho wa ukoloni Zanzibar.

Na Taifa la Zanzibar lilikuwa mwanchana kamili wa Jumuia ya madola na mwanachana mpya wa Umoja wa Mataifa, mwaka huo 1963.

Je ni kwa nini hatusherehekei uhuru wa Zanzibar 12/Dec/1963 na dadala yake tunasherehekea mapinduzi ya mwaka 1964?


Nafikiri umesha toa jibu mwenyewe kuwa mapinduzi na uhuru ni siku mbili tofauti.

Sasa wewe ombi lako ni kuongeza na siku ya uhuru wa Zanzibar isherehekewe na kuwekwa kwenye kalenda kama siku ya mapumziko.

pasi na shaka wamekusikia.
 
Huwa nikisikia tu Zanzibar napatwa na kichefuchefu siwapendi hao
Kichefuchefu ni dalili moja ya mimba.Na nilikuwa napata tabu sana kumfahamu mke wangu anaponiambia ananichukia wakati mimba zake zikiwa changa.lakini baada ya kuona post yako nimeweka ku figure out na ahsante sana just hold on only less than nine month to go.
 
arabs are becoming powerful in zanzibar little by little..shein watch your back.
 
arabs are becoming powerful in zanzibar little by little..shein watch your back.
Waarabu wajanja sana. Wanawambia Wazanzibar weusi adui yao mkubwa ni MUUNGANO. Wasiyasahau maneno ya Mwalimu. Nje ya Muungano, hakuna Zanzibar.
 
Ndivyo tulivyofundishwa shuleni Sr. Magdalena ili kuyakubali na kuyaenzi Mapinduzi Matukufu ya 12/01/1964. Vunjeni Muungano muone kitakachotokea ambacho Mwalimu alikisema pale Kilimanjaro Hotel. Halafu eti RA anawaandaa ENL/AAAK au AAAK/ENL kuchukua serikali ya Muungano 2015! Bila shaka ulimsikia Maalim Seif na kauli yake tata ya kupokezana Urais wa Muungano tu.

Wacha kutisha Wanaume wewe! Vijana wa leo wote wapo macho na mambo yote yapo hadharani, akili ya Baba yako wa Taifa umeshashipigwa na ukuta. Hemu kitafte kitabu cha "KWAHERI UKOLONI, KWAHERI UHURU!" cha Dr. Harith Ghassany huenda kikakutoa tongo za macho na kuona Uhalisia.
 
Sr.Magdalena,

..Waziri Mkuu wa kwanza wa Zanzibar alikataa katakata kuunda serikali ya mseto wa ASP kwa madai kwamba wana ASP ni WATWANA na yeye hawezi kuchanganyika nao hata kama wangempa UTUME.

..pia majimbo ya uchaguzi yaligawanywa in such a way kwamba maeneo ambayo ASP walikuwa na wafuasi wengi basi kulipewa majimbo machache, halafu maeneo ambayo ZNP[Hizbu chama cha Sultani] walikuwa na wafuasi walipewa majimbo mengi.

..hiyo ilionekana kama hujuma ya waziwazi dhidi ya ASP[chama cha Waafrika na Washirazi] ili kisiweze kushinda uchaguzi na kuunda serikali.

..tatizo lingine la uhuru ule ni kwamba mkoloni Muingereza aliondoka na kumuachia nchi MWARABU ambaye alikuwa ni mkoloni kabla yake. Kilichopaswa kufanyika ni kukabidhi nchi kwa serikali ya waliowengi ambao walikuwa ni Waafrika. Yaani uhuru huo haukuwa na tofauti na ule uhuru wa Rhodesia chini ya utawala wa Walowezi wa Ian Smith.

..kwa uchache kabisa hicho ndicho kilichopelekea kutokea kwa MAPINDUZI YA ZANZIBAR.
 
Vile ASP(Afro Shirazi Party) was a racial party kama jina linavo ashiria ? Ie chama cha waafrika na washirazi tu?
 
Sr.Magdalena,

..Waziri Mkuu wa kwanza wa Zanzibar alikataa katakata kuunda serikali ya mseto wa ASP kwa madai kwamba wana ASP ni WATWANA na yeye hawezi kuchanganyika nao hata kama wangempa UTUME.

..pia majimbo ya uchaguzi yaligawanywa in such a way kwamba maeneo ambayo ASP walikuwa na wafuasi wengi basi kulipewa majimbo machache, halafu maeneo ambayo ZNP[Hizbu chama cha Sultani] walikuwa na wafuasi walipewa majimbo mengi.

..hiyo ilionekana kama hujuma ya waziwazi dhidi ya ASP[chama cha Waafrika na Washirazi] ili kisiweze kushinda uchaguzi na kuunda serikali.

..tatizo lingine la uhuru ule ni kwamba mkoloni Muingereza aliondoka na kumuachia nchi MWARABU ambaye alikuwa ni mkoloni kabla yake. Kilichopaswa kufanyika ni kukabidhi nchi kwa serikali ya waliowengi ambao walikuwa ni Waafrika. Yaani uhuru huo haukuwa na tofauti na ule uhuru wa Rhodesia chini ya utawala wa Walowezi wa Ian Smith.

..kwa uchache kabisa hicho ndicho kilichopelekea kutokea kwa MAPINDUZI YA ZANZIBAR.

Kwa maana nyingine Mwarabu alikuwa mkoloni, sawa na wakoloni wengine tu kutoka nchi za magharibi, tofauti ni kwamba walikuja wakati tofauti, mwarabu akiwa mtu wa kwanza kuitawala Zanzibar. Anachofanya Robert Mugabe ndio hicho kilichofanyika Zanzabar wakati wa mapinduzi ila katika style tofauti tu. Ila kwa sasa dalili zinaonyesha wazi WATWANA wamesahau bibi na babu zao walivyoteseka wanajiona wako full fredged, huku mwarabu akiwadanya kama yuko bega kwa bega nao, kuja kuvuta shuka itakuwa asubuhi, hebu tususbiri
 
Simplemind,

..AFRO SHIRAZ Party was MULTIRACIAL.

..ZNP/HIZPU ndiyo walikuwa ma-racist ambapo kiongozi alitamka kwamba hawezi kuungana na ASP[chama cha watwana] hata kama wangempa UTUME.

..pia UMMA party ilianzishwa na vijana walioukataa ubaguzi uliokuwepo ZNP/HIZBU.
 
Kwa maana nyingine Mwarabu alikuwa mkoloni, sawa na wakoloni wengine tu kutoka nchi za magharibi, tofauti ni kwamba walikuja wakati tofauti, mwarabu akiwa mtu wa kwanza kuitawala Zanzibar. Anachofanya Robert Mugabe ndio hicho kilichofanyika Zanzabar wakati wa mapinduzi ila katika style tofauti tu. Ila kwa sasa dalili zinaonyesha wazi WATWANA wamesahau bibi na babu zao walivyoteseka wanajiona wako full fredged, huku mwarabu akiwadanya kama yuko bega kwa bega nao, kuja kuvuta shuka itakuwa asubuhi, hebu tususbiri

Straatkasyambe,

..aisee jina lako gumu sana!! LOL!!

..kinachotakiwa Zanzibar ni kuondosha ubaguzi.

..Mapinduzi yalikuwa na nia nzuri, lakini walichokosea ni kuanza kulipiza kisasi.

..wana Mapinduzi nao walianzisha ubaguzi wa Mwafrika dhidi ya Muarabu kitu ambacho siyo kizuri.

..Ili Zanzibar isonge mbele wanapaswa kuukataa ubaguzi wa aina yoyote ile, uwe wa rangi,dini,kabila,au jinsia.
 
Mkuu kama ulikuwa uhuru bandia, sasa ile hotuba ya Waziri Mkuu wa Zanzibar na kuezeka bendera ya Zanzibar pale UN ilikuwa nini, maigizo pia?..

Hotuba na yenyewe ilikuwa bandia, maana "hela bandia inaweza kununua cheni bandia!"
 
Aliyeuza Uhuru wa Zanzibar alikuwa Shamte kama sii huyu kukubaliana na Sultan dhidi ya ASP Zanzibar ingekuwa huru kupitia chama cha Waafrika na Washiraz lakini yeye Shamte wa ZPPP na mjumbe mwingine wa chama wakaungana na Hizbu ZNP kwa kuahidiwa Uwaziri mkuu kama watamshinda ASP.. Na angalia basi watu wawili tu kutoka ZPPP ndio walibadilisha kura zote na kumrudisha Sultan ktk utawala. Sultan ambaye alipewa heshima zote za Mtawala kama Queen wa Uingereza leo, maana muda wote ndiye alikuwa Ikulu iwe kabla ya Uhuru ama baada ya kutangazwa Uhuru 1963..Sema tu nyuma hakuwa na Total Control ya uchumi wa Zanzibar, Waingereza walikamata naye akabakia kama King akila ruzuku tu kaegesha msuli.

Mengine kayaeleza Jokakuu, Na sii ati kweli Okello alikuwa sii mkazi Zanzibar..Okello alikuwa akiishi Pemba muda mrefu sana akifanya kazi za kibarua akipasua mawe ya kujengea nyumba...Na sii kweli mpango wa Mapinduzi aliufanya yeye bali yeye alitumiwa kuongoza Mapinduzi yale lakini waliopindua wanajulikana ni Wazanzibar na Waislaam lakini haramu kuwataja isipokuwa Okello Mjaluo na Mkr.....Oops!
 
Straatkasyambe,

..aisee jina lako gumu sana!! LOL!!

..kinachotakiwa Zanzibar ni kuondosha ubaguzi.

..Mapinduzi yalikuwa na nia nzuri, lakini walichokosea ni kuanza kulipiza kisasi.

..wana Mapinduzi nao walianzisha ubaguzi wa Mwafrika dhidi ya Muarabu kitu ambacho siyo kizuri.

..Ili Zanzibar isonge mbele wanapaswa kuukataa ubaguzi wa aina yoyote ile, uwe wa rangi,dini,kabila,au jinsia.

Lol! kweli jina refu, nitamuomba mode nitumie initials kama inawezekana maana wewe sio mtu wa kwanza kusema. Mh lakini unafikiri inawezekana wakaishi sawa? maana sasa inaoneka wazi Tanganyika inatumika kama scapegoat kwa matatizo yao. As if Mwarabu na Mwafrika Zanzibar waliishi kwa amani na upendo miaka yote then tatizo ni baada muungano ndio hali imekuwa mbaya Zanzibar.

Kwa hali ilivyo matatizo mengine ambayo yanaikumba Zanzibar hayaonekani. Mimi naona muungano ufe hata kwa majaribio ya miaka kumi ili watu waweze pima uzito kama wako full fredged Tanganyike tujitoe maana sasa tunaogopa hata kwenda Pemba tunavyosemwa vibaya.

Mimi nitakuwa huru zaidi kama nitaenda kwa visa Zanzibar huku na wao wakija kwa visa Tanganyika ili kila mtu amheshimu mwenzake
 
Yes, Zanzibar walipata uhuru 1963 lakini ulikuwa uhuru-bandia. Uhuru wa remote control uliojaa makucha ya mkoloni yule yule waliyekuwa wanamfukuza na ndio maana kukawepo na Mapinduzi. Mapinduzi maana yake unapindua kile usichokubaliana nacho.

Bado nasubiri kwa hamu kumsikia Maalim Seif akiongea kuhusu uhuru wa 1963 na Mapinduzi ya 1964. Hapa ndio kuna siri kubwa kuhusu CUF ya mtandao ya Maalim Seif.

Yaah;ni kama case ya South Africa!Walipata uhuru kama wa ZNZ mwaka 1934 lakiniuhuru wa kweli ni pale majuzi tu!!
 
Amani Karume aliwaunganish6a Wazanzibari wapate kula wote ili asipatikane wa kumnyoosh6ea kidole, kwa mazambi na dh6ulma yake na familia yake ilidh6aniwa ataning'-inizwa akitoka madarakani, sasa kila mtu ana mfupa... wooote wanaimba asanti baba karume, kweli watu ni watotot tu.
 
Back
Top Bottom