Zanzibar hiyooo... kidogokidogo!

Ngekewa

JF-Expert Member
Jul 8, 2008
7,705
1,288
Baraza la mawaziri kivuli Z`bar lafutwa




Na Mwinyi Sadallah



Baraza la Wawakilishi Zanzibar limetangaza mabadiliko makubwa ya muundo wake ikiwemo kufuta baraza la mawaziri kivuli na nafasi ya kiongozi wa upinzani, baada ya kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar (GNU).
Hayo yameelezwa na Katibu wa Baraza hilo, Ibrahim Mzee Ibrahim, wakati akizungumza na waandishi wa habari, Makao Makuu ya Baraza hilo Chukwani mjini Zanzibar jana.
Alisema kwamba kufuatia kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa kanuni za Baraza la Wawakilishi zinalazimika kufanyiwa marekebisho kuanzia mkutano wa pili unaotarajiwa kuanza Januari 19, mwaka huu.
Mzee alisema Baraza la Mawaziri Kivuli limefutwa na nafasi ya kiongozi wa upinzani haitokuwepo tena na badala yake kutaanzishwa nafasi ya Mnadhimu Mkuu wa Serikali katika Baraza la Wawakilishi na kila chama chenye wajumbe ndani ya baraza hilo kitakuwa na mnadhimu mmoja.
Alisema mnadhimu mkuu wa Serikali katika Baraza la Wawakilishi atateuliwa na Serikali na Makamo wa pili wa Rais ndiye atakayekuwa mtendaji mkuu wa shughuli za Serikali ndani ya baraza hilo.
Kabla ya marekebisho hayo ya kanuni, Waziri Kiongozi ndiye aliyekuwa kiongozi mkuu wa Shughuli za Serikali, mfumo ambao umebadilika baada ya marekebisho ya kumi ya Katiba ya Zanzibar yaliyokaribisha Serikali ya Umoja wa Kitaifa.
Aidha alisema kwamba kuanzia sasa wakuu wa mikoa hawatokuwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa vile marekebisho ya kumi ya Katiba ya Zanzibar yamewaondoa na watabakia watendaji tu katika mikoa yao.
Alisema kwamba kanuni za baraza la wawakilishi za mwaka 2009 zimefanyiwa marekebisho upya ili ziendane na mazingira yaliyopo sasa katika utendaji wa baraza hilo likiongozwa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa.
Katibu huyo alisema kwamba Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi hivi sasa watakaa ndani ya baraza bila ya kuzingatia tofauti za vyama vyao isipokuwa safu ya mbele itaongozwa na mawaziri na manaibu waziri na kufuatiwa na wajumbe wasiokuwa na nyadhifa katika Serikali.



CHANZO: NIPASHE JUMAPILI


Haya ndiyo wasio na macho huyabeza! Hongera Wazanzibari!
 
Kwanza walikuwa na kazi gani wakati ni nchi ya chama kimoja, ndiyo maana tunataka katiba mpya ili haya yasitokee mara kwa mara, sijui kama hata huyo Makamu wa pili anatajwa ndani ya katiba lakini wananchi tunabebeshwa mzigo wa kumhudumia.
 
Teh teh teh....CUF zanzibar kwishney...monopartism hiyooo inanukia zenj.
 
Teh teh teh....CUF zanzibar kwishney...monopartism hiyooo inanukia zenj.

Ndicho Seif Hamad alichokuwa anakitaka,tulishasema mwanzoni kuwa CUF wameolewa na CCM watu wakabisha.

Sasa hapo CUF washamezwa na kumbe shida yao ilikuwa ni vyeo tu(Umakamo wa Rais na Uwaziri).Baraza la wawaklishi sasa litaendeshwa kwa misingi ya monoparty system na hapo CCM wamepiga bao na CUF wamelipokea.

Ni vizuri kwa CUF kufanya mabadiliko ya uongozi kwa nafasi za Mwenyekiti na Katibu Mkuu ili chama kiwepo huku Tanganyika kwakuwa kinakufa Zanzibar
 
congrats z'baris for acknowledging that the cuf/ccm circus was useless for your own deed
 
Hongereni wa zanzibari,utaifa na uzalendo wa nchi kwanza mambo ya vyama badae,hakika mtapiga hatua sana ktk maendeleo mkiwa na umoja kama huo,mifano hai ipo zenj sasa ya mabadiliko yakweli yaliyoanza kujitokeza baada ya kuundwa serikali ya umoja wakitaifa.hongeren sana wazenj.
 
Kama watu wanaweza kuvunja Katiba ya nchi ambayo wameapa kuitetea na kuilinda watashindwa vipi kuvunja au kudharau Kanuni za Halmashauri? Au sheria nyingine?

Zanzibar ni nchi kamili! Hili suala la Muungano ni historia. Ni ndoa ambayo ipo kwa ajili ya watoto na jamii kuona lakini chumbani kila mtu analala kitanda chake! Wanandoa (Tanganyika na Zanzibar) wanaogopa talaka kwa sababu watagawana mali!! Sheria ya mgawanyo wa mali ni 50 - 50 hata kama mke alikuwa mama wa nyumbani! Kwa mfano huo mtajua wenyewe mke nani mume nani!
 
Mie mkishajitenga nitakuja kuomba kazi wazanzibar mtanikataa? Maana mie mtanganyika yakhe na huku bara karibuni tutashikana mashati!!
 
0>-10000 (yaani sifuri ni kubwa kuliko hasi 10,000)caf zamani ilikuwa ziro sasa hivi ni-10000
 
Hii ni nzuri na mbaya pia. Kwamba wanandoa wanatakiwa walale kitanda kimoja na kufanya mambo pamoja zaidi ili kukoleza mapenzi. Hili ni jambo zuri litakalodumisha ndoa ya ccm na cuf huko znz.

Lakini, wananchi wamefulia! Kwa kuwa wanandoa wameamua kuimarisha mahusiano yao, watafanya mambo pamoja na kusifiana ili kukoleza mapenzi. Watafanya ufisadi pamoja, watabweteka kwa sababu hakuna Mke/mume mwenza. Na kwa kuwa katika nchi yao hakuna mtu aliyevunja ungo/ aliyebalehe basi hawatahitaji kuhofia ushindani.

Nani atawasemea wananchi wenye mtazamo tofauti wa mambo? Nani ataikosoa serikali iwapo utendaji wake ni mbaya? Wananchi watapata wapi taarifa za ukweli kuhusu utendaji wa serikali?

Najaribu kusema, what is the incentive for gov to be effective? What is the incentive for citizens to participate in politics? Have we gone back to single party system? Did cuf decide to merger with ccm or join the gov? Are zanzibaris going to organize another strong opposition party?

What the fate of cuf bara?
 
Hii ni nzuri na mbaya pia. Kwamba wanandoa wanatakiwa walale kitanda kimoja na kufanya mambo pamoja zaidi ili kukoleza mapenzi. Hili ni jambo zuri litakalodumisha ndoa ya ccm na cuf huko znz.

Lakini, wananchi wamefulia! Kwa kuwa wanandoa wameamua kuimarisha mahusiano yao, watafanya mambo pamoja na kusifiana ili kukoleza mapenzi. Watafanya ufisadi pamoja, watabweteka kwa sababu hakuna Mke/mume mwenza. Na kwa kuwa katika nchi yao hakuna mtu aliyevunja ungo/ aliyebalehe basi hawatahitaji kuhofia ushindani.

Nani atawasemea wananchi wenye mtazamo tofauti wa mambo? Nani ataikosoa serikali iwapo utendaji wake ni mbaya? Wananchi watapata wapi taarifa za ukweli kuhusu utendaji wa serikali?

Najaribu kusema, what is the incentive for gov to be effective? What is the incentive for citizens to participate in politics? Have we gone back to single party system? Did cuf decide to merger with ccm or join the gov? Are zanzibaris going to organize another strong opposition party?

What the fate of cuf bara?

Good point mkuu na mie nililiona hiyo pia kwamba hakuna mtu atakayeuliza maamuzi ya serikali maana wote wamo ndani. Hivi niulize Chadema, TLP, Jahazi asilia wako wapi?
 
Power Sharing kills and buries democracy. It is pointless to have CUF in Zanzibar (and mainland). Whats the point? What (and who) is CUF opposing? They are a government and so they will remain for the next five years-!
 
Tatizo ambalo liko likely kutokea nikwamba Baraza la Wawakilishi litakuwa na kazi moja tu ya kupiga muhuri maamuzi ya serikali. Serikali ya mseto ilikuwa vyema ikizingatiwa hali halisi ya kisiasa Zbar ilivyokuwa lakini kuna hatari ya serikali kulala zaidi hasa katika siku za usoni baada ya ari ya "tuonyesheni mabadiliko" kufifia kama ilivyo ada ya serikali nyingi.
 
Haya yote yametokea kwa vile chama kimoja hakikubali kushindwa na chama kingine hakikubali kushinda...!!!!
 
Power Sharing kills and buries democracy. It is pointless to have CUF in Zanzibar (and mainland). Whats the point? What (and who) is CUF opposing? They are a government and so they will remain for the next five years-!

CUF wakikusikia?
 
Back
Top Bottom