Zanzibar 2020 Zanzibar: Hali ilivyo mapokezi ya Mgombea Urais Kupitia ACT- Wazalendo, Maalim Seif na Bernard Membe. Ni Mafuriko

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
May 5, 2014
602
1,526
Leo Mgombea Urais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad na Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bernard Membe, watapokelewa asubuhi hii na Wazanzibar wa Unguja.

Matukio mbalimbali na picha za mapokezi tutawawekea hapa.

IMG-20200809-WA0002.jpg
IMG_20200809_083139_927.jpg
IMG_20200809_082936_523.jpg
IMG_20200809_084342.jpg
IMG_20200809_121217_622.jpg
IMG_20200809_121221_104.jpg


IMG_20200809_122312_779.jpg
 
Washaaaaaa washaaaa act wazalendo. Ndio chama pekee kikubwa cha upinzani ninachokiamini. Kina watu wasomi wenye kuujua uongozi. Watanzania tunawapenda sana act wazalendo. Membe Mungu akubariki uwe rais mupate wabunge wengi sana.
 
Ivi jaman kwa mgawanyiko huu kweli tutaiweza ccm kweli??
Wapinzani huwa mnatuangusha sana wananchi au mna ajenda ya makusudi kubuy time ccm akiendelea kutawala?

Bila kuungana nawahakikishia hamtaing'oa ccm, mnatupotezea mda wapiga kula.
tena ni afadhali wkt ule tukiwa na ukawa ulituunganisha na ccm kama alikufa japo tume NEC iliwanusuru lkn kwa hali hii ya sasa mnajua mnapoteza mda tu ccm hamtaiweza.

KUMBUKENI,
UMOJA NI NGUVU UTENGANO NI UDHAIFI.

KIDOLE KIMOJA HAKIVUNJI CHAWA.

NDG WAKIGOMBANA CHUKUA JEMBE UKALIME WAKIPATANA CHUKUA KAPU KAVINE, MAANAKE NI HERI TUSHUGULIKE NA MAMBO YETU NYIE NI WASANII TU.

AHYA MTATWAMBIA..
Nyie tatizo lenu mnapokea puppet ili Chadema tusiende ikulu ila mjue unafiq utawaponza.
 
Zanzibar sawa nakunga mkono na kimuombea sana Maalim seif awamu hii aichukue SMZ ila bara lzm waungane atleast na chadema, hacha kujidanganya huku bara bado pagumu ndg yangu
Washaaaaaa washaaaa act wazalendo. Ndio chama pekee kikubwa cha upinzani ninachokiamini. Kina watu wasomi wenye kuujua uongozi. Watanzania tunawapenda sana act wazalendo. Membe Mungu akubariki uwe rais mupate wabunge wengi sana.
 
Ndugu yangu tusubiri. Muda bado na hata hizo fomu za ugombea hazijarudishwa na zaidi hazijapitishwa. Hata kampeni bado. Bado muda upo. Haraka haraka haina baraka. Wapinzania siyo wajinga na wanajua wanachokifanya.

Tena basi kumbuka: muda mzuri wa kuungana ni baada ya kampeni kuanza na kujua yupi amepitishwa na NEC kugombea nini. Nadhani unajua kabisa hili tawi la CCM linavyoweza kufanya lolote iwapo wataungana mapema na wagombea rasmi kujulikana.
 
Zanzibar sawa nakunga mkono na kimuombea sana Maalim seif awamu hii aichukue SMZ ila bara lzm waungane atleast na chadema, hacha kujidanganya huku bara bado pagumu ndg yangu
Act anaweza kua chama kikuu cha upinzani kama akipata wabunge wachache bara na Zanzibar akapata wengi. Chadema kwa Zanzibar hapati hata diwani. Lakini kwa huku bara kumbuka wabunge alionao ilikua ni nguvu kubwaa sana ya lowassa ingawaje nao chadema walikua na vinguvu vyao lakini ile nguvu kubwa ya lowassa na ukawa ndio ilifanya wakawa na wabunge wengi sana.

Je chadema wana mtu mwenye nguvu na ushawishi wa kisiasa kama ule wa lowassa?.
Kwasasa chadema nzima mwenye vinguvu ni lissu tena huyu anajulikana sana mitandaoni na baadhi ya watu walioelimika.
 
Ivi jaman kwa mgawanyiko huu kweli tutaiweza ccm kweli? Wapinzani huwa mnatuangusha sana wananchi au mna ajenda ya makusudi kubuy time ccm akiendelea kutawala?...
Wapinzani waungane wasiungane ushindi wa kishindo wa CCM upo pale pale
 
Hivi ndivyo hali ilivyo kwasasa huko Zanzibar, wananchi walio jitokeza kwenye mapokezi ya viongozi wa ACT wazalendo visiwani humo.
MAALIM SEIF mgombea urais Zanzibar na BERNARD MEMBE mgombea urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania wanao wasili leo visiwani Zanzibar.

Picha hizi ni kutoka bandarini ambapo wazanzibar wamejitokeza kwaajili ya mapokezi ya viongozi hao.

Swali: Je, nini kipo nyuma ya kiu kubwa ya madaraka aliyo nayo MAALIM SEIF? Kugombea zaidi ya Mara tano bila mafanikio si sababu sahihi ya kuwaachia wengine?

IMG_20200809_103113.jpg

IMG_20200809_103108.jpg

IMG_20200809_103103.jpg
 
46 Reactions
Reply
Back
Top Bottom