Zanzibar hakukaliki; siri nzito yafichuka fedha zatoka Oman na Uingereza

Kuna jambo moja lipo wazi; kwamba Wazanzibari wengi hususani wale walio nje ya system (hususani Watendaji wakuu CCM) hawautaki muungano. Aidha, Wazanzibar waishio nje nao, kwa uwingi wao ndo hawataki kabisa kusikia lolote kuhusu muungano. Wengi wa hawa, wanaamini kwamba Zanzibar iliburuzwa tu kuingia kwenye muungano na hadi sasa hakuna cha maana wanachofaidika nacho kutokana na muungano huo!

Kama nilivyotangulia kusema hapo awali, Zanzibar iliburuzwa kuingia kwenye muungano. Hali kadhalika, hata Watanganyika nao waliburuzwa na wanaendelea kuburuzwa kuwepo ndani ya muungano huu. Hakuna kura yoyote ambayo ilipata kufanyika ya kuwauliza wananchi wa pande hizi mbili kuhusu kuafiki kwao kuwepo ndani ya ndoa hii ya mkeka.

Pamoja na yote hayo, tofauti na ilivyo huku bara, Zanzibar kwa miaka yote wamekuwa wakitafuta nafasi ya kujipatia Zanzibar yao kama Taifa. Kwa bahati mbaya kabisa, fursa hiyo hawakuipata kutokana na ukweli kwamba Tanzania kwa ujumla ilionekana ni sawa na dhambi ya mauaji kuzungumzia suala la kuvunjwa kwa muungano. Wachunguzi wa mambo wanaamini kwamba, baada ya mifumo mingi ya Nyerere kushindwa; hususani siasa ya ujamaa na kujitegemea pamoja na Azimio la Arusha, CCM walibakiwa na turufu moja tu ya kuaminisha uwezo wao. Nayo ni MUUNGANO! Na kutokana na hilo, MUUNGANO umeonekana kulindwa kwa gharama zozote zile pasipo kuzingatia matakwa ya wananchi.

Baada ya Wazanzibari kusubiria kwa muda mrefu fursa ya kujipatia taifa lao; hatimae wakaamini kwamba fursa hiyo imeshawadia! Waliamini kwamba mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya utawapatia fursa ya kutoa maoni yao kwamba hawapo tayari kuwepo ndani ya muungano!! Inavyoelekea, hawakubaini mapema kwamba rasimu ya katiba mpya ilishatamka wazi kwamba tumetaka tusitake; muungano lazima!

Bila shaka, ni kauli ya JK wakati akiiapisha Tume ya Katiba Mpya ndiyo iliyoamsha ari na ghadhabu za Wazanzibari. Bila kutafuna tafuna maneno na katika hali iliyoonekana kuwapa vijembe wale wote wanaofikiria kuvunja muungano; JK akatamka wazi kwamba kitakachojadiliwa ni aina ya muungano na sio suala la kuendelea ama kutoendelea kwa muungano. Hapo ndipo, baadhi ya Wazanzibari walipokuja kubaini kwamba ndoto ya kuamua mustakabali wa taifa lao imeyyoyoma. Na hapo ndipo wana-Uamsho walipoongeza nguvu ya kuendesha mihadhara dhidi ya muungano. Ni bahati mbaya sana kwamba ingawaje kikundi hiki kina madai ya msingi, wametumia approach ambayo inatia shaka uhalisia wa madai yao.

Hivyo basi, suluhisho la tatizo hili ni kutoa fursa ya kuwepo kwa kura juu ya kama tuendelee na muungano au tusiendelee nao. Haikuwa busara hata kidogo kuweka kizingiti cha wananchi kujadili suala hili. Muungano unaohitajika ni wenye ridhaa za wananchi na sio kushinikizwa na viongozi.
 
Kubalini kutumiwa kupika propaganda na serikali, kwani kufadhiliwa ni stori za leo hizo? mbona hata baadhi ya vyama tulishaambiwa vinafadhiliwa kwa mapesa toka nchi fulani za magharibi na kuna ushauri ulitolewa wa serikali kuwa "makini", au hamjasikia hilo?

Hili la vijana wa umri wa 18-24 unawadharau hao? hao ndio wana mapinduzi nchi zote (Youth) ndio wapiganaji fuatilia....., kisha mjumbe, Tanzania ni mingoni mwa nchi zenye young population ambapo estimates za sensa iliyopita zinaonyesha kuwa karibu 65% ya total population wapo below 24 years of age.

Serikali ilete hoja, sio propaganda...

Inaboa aisee

Good... Washutumu Waandishi wa Habari na Mfadhili aliyeshikwa akitokea Oman
 
Si hayo tu, bado kuna siri kubwa zaidi chini ya hiyo.
"ukistaajabu ya musa, utaona ya firauni"
MUNGU IBARIKI TANGANYIKA, MUNGU IBARIKI ZANZIBARI, RIP TANZANIA
 

Siri nzito ya machafuko yanayoendelea mjini hapa, imefichuka.

Habari za kuaminika zilizopatikana jana kutoka Zanzibar, zinasema kuna kundi kubwa la wafanyabiashara wa Kizanzibari wanaoishi katika nchi za Oman na Uingereza, wanadaiwa kutoa fedha nyingi kufadhili vikundi vya kidini na wanaharakati kushinikiza Muungano uvunjwe.

"Tunasikitishwa mno na machafuko haya, yameiaibisha Zanzibar, ambayo baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, ilitulia… lakini tunasikitishwa na tukio hili ambao linafadhiliwa na Wazanzibari wenzetu wanaoishi Oman na Uingereza.

"Watu hawa wanamekuwa wafadhili wakubwa wa kutoa fedha kwenye vikundi vya kidini na wanaharakati, jambo ambalo tunaona ni hatari kubwa kwa amani kisiwani hapa, tunavishauri vyombo vya dola, vichukue hatua," kilisema chanzo chetu.

Aidha chanzo hicho, kinasema kutokana na nguvu kubwa ya fedha, vikundi hivyo vimekuwa na ushawishi mkubwa kwa vijana ambao wengi wao hawana kazi maalum za kufanya.

"Utashangaa kuona, baada ya kutokea machafuko haya, wengi walioonekana walikuwa vijana tu, huoni watu wazima, akina baba au akina mama… ni wazi utaona fedha zina nguvu kubwa kwa vijana wetu, ukiangalia wale waliondamana juzi ni vijana wenye umri kati ya miaka 18 hadi 24.

"Lakini pia tumebaini kwamba, mbali ya vikundi hivi, kuna chama kimoja cha siasa kisiwani hapa, kwa namna moja au nyingine kina mkono wake ndani ya machafuko haya, kimekuwa bingwa wa kuchochea uvunjifu wa amani," kilisema chanzo chetu.

Chanzo hicho kiliiambia MTANZANIA kwamba Wazanzibari hao wamekuwa na ushawishi mkubwa wa kuwashinikiza wananchi waibane Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ili iitishe kura ya maoni.

"Issue ya Muungano ni muhimu, lakini hawa jamaa wanafanya hivi ili kuishinikiza Serikali iitishe kura ya maoni ili kuona kama kuna watu wanaukubali Muungano au la! Jambo hili si baya, lakini walitakiwa kupitia njia ambazo ni sahihi," kilisema chanzo chetu.

Kwa upande wake, Mjumbe wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa, Daud Ismail, lisema matatizo yanayoendelea Zanzibar, ni vema Serikali ipitie ripoti mbalimbali zinazohusu kero za Muungano.

"Ili kuweza kuondokana na hali hii, ni vema Serikali zote mbili zifanyie kazi ripoti za
Hassan Moyo, William Shelukindo, Amina Salum Ally na ya aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), mzee Edwin Mtei, ambazo zote zilieleza wazi tatizo linatotekea sasa Zanzibar.

"Leo huwezi kudhibiti hali hii ya machafuko kwa kukaa mezani na Jumuiya ya Uamsho, kufanya hivi ni sawa na kuchochea jambo hili ila kinachotakiwa hapa ni kufanyia kazi jambo hili kwa undani.

"Wazanzibari kwa muda mrefu, wamekuwa wakilalamika kuhusu hata namna ya mapato yanavyopendelea upande mmoja wa Tanganyika, na katika kulithibitisha hili, hata ripoti ya mshauri wa Zanzibar ya mwaka 2010, imeeleza wazi, kwa hili ni lazima chama changu cha CCM kitoe tamko na si kunyamaza kimya," alisema Daud.
Kumbe kuitwa Mzee mpaka uwe Chadema?:ranger:
 
The way forward ni kuruhusu muungano ujadiliwe kwenye katiba mpy

Nadhani tulipofikia ni kuuvunja ili kuruhusu tujadiliane kama tunauhitaji. Yaani kwanza usiwepo halafu tuone kama kuna mtu atam miss mwenzie.
 
Wauvunje tu..nitakuwa nauza k.moto huko kwa dollar ya marekani.wapumbavu kabisa hawa
 
ungana na msumbiji ,,,zambia ,,,,malawi,,,,,,,imarisha mafia iwe zanzibar yetu ,,,kuku kuku tu jogoo jina,,,kama visiwa ni mali ,,,tuna mafia na ukerewe,,,,,,
 
Jamani, si tuna TISS au?? yani hadi waandishi wa habari waseme ndio reactions zianze?
 
kwani kuna ubaya gani wazanzibar popote walipo wakachangia harakati za kuidai zanzibar huruu sasa ule udini unao ingizwa na serekali ya tanganyika unajulikana ushauri wangu kwa wakristo wanotumiliwa kuwagawa wazanzibar ninawaomba wawache tabia hiii kwani iko siku watakuja kup[ata tabu bora wakae kimya tu wasikubali kutumiliwaa
 
Sasa Muungano ukivunjika wazanzibari wataacha kuja Dar? au watatumia Pasipoti itabidi wawe na Ubalozi Dar
 
Ndugu yangu tanganyika mwaka 1964 ulikuja (nyerere) na wazo la kuungana na mimi karume sikuona vibaya nikakubali bila hata ya kuwashirikisha wenye nchi na hata viongozi wenzangu..tulikubali tukidhani ndani ya muungano tutapata maendeleo zaidi lakini kumbe ni kinyume zanzibar kama nchi imekua ikididimia kiuchumi,
sasa nia njema kabisa tunaona hatuna haja ya kuendelea na muungano huu, bora turejee katika hali yetu kabla ya muungano, na sisi tutashirikiana kama zamani, kwenye kombe la gosage, tutajiunga na jumuiya ya afrika mashariki,tutakua memba wa saddc, pia tutakua memba wa au, common wealth na united nation.
Pia tukipata mafuta kama yapo basi kwa vile ni memba wa east africa basi tutawauzia kwa bei za jirani,
kwa heshima turudi kama zamani, kabla ya 1964 ,unakumbuka wakati huo kina ali hassan mwinyi, jumbe,issack sepetu,mwakanjuki,karume,agustine ramadhan,lewis makame walisoma zanzibar bila ubaguzi? Basi hali hii ya udugu haitabadilika....alakini tunataka kuwa huru..tuwachieni..

Haya ndio madai yetu na si oman wala uk...sisi ni nchi mbili zilizo ungana tofauti kama moshi wakitaka 'uhuru' wao ..
 

Siri nzito ya machafuko yanayoendelea mjini hapa, imefichuka.

Habari za kuaminika zilizopatikana jana kutoka Zanzibar, zinasema kuna kundi kubwa la wafanyabiashara wa Kizanzibari wanaoishi katika nchi za Oman na Uingereza, wanadaiwa kutoa fedha nyingi kufadhili vikundi vya kidini na wanaharakati kushinikiza Muungano uvunjwe.

"Tunasikitishwa mno na machafuko haya, yameiaibisha Zanzibar, ambayo baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, ilitulia… lakini tunasikitishwa na tukio hili ambao linafadhiliwa na Wazanzibari wenzetu wanaoishi Oman na Uingereza.

"Watu hawa wanamekuwa wafadhili wakubwa wa kutoa fedha kwenye vikundi vya kidini na wanaharakati, jambo ambalo tunaona ni hatari kubwa kwa amani kisiwani hapa, tunavishauri vyombo vya dola, vichukue hatua," kilisema chanzo chetu.

Aidha chanzo hicho, kinasema kutokana na nguvu kubwa ya fedha, vikundi hivyo vimekuwa na ushawishi mkubwa kwa vijana ambao wengi wao hawana kazi maalum za kufanya.

"Utashangaa kuona, baada ya kutokea machafuko haya, wengi walioonekana walikuwa vijana tu, huoni watu wazima, akina baba au akina mama… ni wazi utaona fedha zina nguvu kubwa kwa vijana wetu, ukiangalia wale waliondamana juzi ni vijana wenye umri kati ya miaka 18 hadi 24.

"Lakini pia tumebaini kwamba, mbali ya vikundi hivi, kuna chama kimoja cha siasa kisiwani hapa, kwa namna moja au nyingine kina mkono wake ndani ya machafuko haya, kimekuwa bingwa wa kuchochea uvunjifu wa amani," kilisema chanzo chetu.

Chanzo hicho kiliiambia MTANZANIA kwamba Wazanzibari hao wamekuwa na ushawishi mkubwa wa kuwashinikiza wananchi waibane Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ili iitishe kura ya maoni.

"Issue ya Muungano ni muhimu, lakini hawa jamaa wanafanya hivi ili kuishinikiza Serikali iitishe kura ya maoni ili kuona kama kuna watu wanaukubali Muungano au la! Jambo hili si baya, lakini walitakiwa kupitia njia ambazo ni sahihi," kilisema chanzo chetu.

Kwa upande wake, Mjumbe wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa, Daud Ismail, lisema matatizo yanayoendelea Zanzibar, ni vema Serikali ipitie ripoti mbalimbali zinazohusu kero za Muungano.

"Ili kuweza kuondokana na hali hii, ni vema Serikali zote mbili zifanyie kazi ripoti za Hassan Moyo, William Shelukindo, Amina Salum Ally na ya aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), mzee Edwin Mtei, ambazo zote zilieleza wazi tatizo linatotekea sasa Zanzibar.

"Leo huwezi kudhibiti hali hii ya machafuko kwa kukaa mezani na Jumuiya ya Uamsho, kufanya hivi ni sawa na kuchochea jambo hili ila kinachotakiwa hapa ni kufanyia kazi jambo hili kwa undani.

"Wazanzibari kwa muda mrefu, wamekuwa wakilalamika kuhusu hata namna ya mapato yanavyopendelea upande mmoja wa Tanganyika, na katika kulithibitisha hili, hata ripoti ya mshauri wa Zanzibar ya mwaka 2010, imeeleza wazi, kwa hili ni lazima chama changu cha CCM kitoe tamko na si kunyamaza kimya," alisema Daud.

YALIANZIA 1993 NAMNA HIVI

MJADALA unaendelea nchini kote juu ya kuundwa kwa serikali ya Tanganyika na muundo wa Muungano wa Zanzibar na Tanganyika. Inavyoelekea yapo matatizo, dosari na sababu za msingi zilizopelekea wananchi kuhoji muundo wa sasa wa Muungano na kuleta hoja ya kuundwa kwa serikali ya Tanganyika ni yenye kuundwa kama si leo kesho.

Lakini wapo pia wanaopinga kabisa kuundwa kwa serikali ya Tanganyika.


Aliyejitokeza kwa nguvu na kwa ukali hadharani kupinga hoja hiyo ni Mwalimu Julius Nyerere, katika kupinga hoja hiyo Mwalimu anatoa hoja zifuatazo:


Hoja ya kuundwa kwa serikali ya Tanganyika imeletwa kwa kuwachoka Wazanzibari na Waislamu. Ufupi wa maneno Mwalimu Nyerere anadai hoja ya kuundwa Serikali ya Tanganyika imetokana na chuki za kidini - Wakristo kuwachukia Waislamu.



Hoja haipo katika sera za CCM na taratibu zimekosewa.


Kuundwa kwa serikali ya Tanganyika kutavunja Muungano na kutavunja Tanganyika pia.

Ukizingatia sifa nyingi ambazo Nyerere alijilimbikizia wakati wa utawala wake na sasa si vigumu kuelewa kwa nini anapinga kuundwa kwa serikali ya Tanganyika.

Mambo yake yote aliyoyaanzisha kwa vishindo huku akisifiwa kuwa zidumu fikra zake, yamekuwa yakiporomoka moja baada ya jingine huku mwenyewe akiona. Lililosalia ni Muungano; nao ukiporomoka haitaleta picha nzuri katika historia yake katika siasa.



Lakini lililo gumu kueleweka ni hatua ya Mwalimu Nyerere kutumia Turufu ya udini kuwagawa Wabunge; wana-CCM na Wa-Tanzania kwa ujumla katika suala hili. Kauli hiyo ingesemwa na Muislamu ingepewa mtizamo tofauti na labda isingeeleweka hasa miongoni mwa Waislamu.

Lakini kusemwa na Mwalimu Nyerere kunaleta mkanganyiko zaidi. Kwanini; (udini ulikuwa umejengeka). Hali hiyo ilipelekea Masheikh kumlalamikia lakini akawanyamazisha kwa kuwashutumu kuwa wanachanganya dini na siasa. Miongoni mwa Masheikh hao wapo waliofukuzwa nchini; waliowekwa kizuizini, waliofukuzwa katika chama na kadhalika.



Sheikh Hassan bin Amir katika waraka wake kwa Waislamu mwaka 1963 aliutaja udini uliokuwa unajengwa Tanzania kwa kutoa mifano ifuatayo:



Kuingizwa nchini Tanganyika mara tu baada ya uhuru vimedali vidogo vidogo vyenye picha ya bendera ya Tanganyika usoni na katikati ya bendera hiyo amesimama Mama Maria na mtoto mchanga na nyuma yake maandiko 'MARIA MTAKATIFU ULINDE UHURU WA TANGANYIKA'.



Gazeti la KIONGOZI la tarehe 1/8/1963 lilimuonyesha Bwana George Kahama akipewa cheo cha dini na Pope kwa kuwakilisha serikali ya Tanganyika katika mkutano wa Makanisa ya Roma.



Mwaka huo huo wa 1963, mnamo tarehe 24 mwezi wa nane, Baraza Kuu la Makanisa ya Kilutheri Tanganyika lilitoa matangazo kuwa Uhuru wa Tanganyika ulikuwa 'Chini ya Msalaba'.
 
Hii ni kujielewa au ni kutokujielewa kwa wazanzibari. Kwani mpaka sasa hivi hakujakuwa na hoja
sahihi ya kudai kuvunjwa kwa muungano zaidi ya udini, vurugu na kauli chafu.
Matabaka katika ujazo wa raia wa unguja ndio ulioshika kasi, kutaka kuwageuza wengine kurudia
katika hali ya utumwa. Hatusemei kiubaguzi bali hali halisi ya mambo ndio inavyokwenda, sasa
tujiulize, wazanzibari ni kina nani ? jibu ni mchanganyiko wa watu kutoka Bara, Oman, Iran (Washirazi)
na hata wangazija kutoka Comoro. Kwa kila hali ilivyo kauli za kupinga muungano zimeshaeleweka
zinatokea wapi, lile neno la kusema Unguja kuna mafuta na gas, ndio limetenda kosa la kuwainua
na kuwageuza mioyo ya matamanio ya utajiri, na kuwageuza wengine ambao bado awajajielewa
kuwa watumwa. Mategemeo ya sultani wa Oman kuja kutawala tena Zanzibar, ni matumaini ambayo
hayawezi kugeuka kuwa kweli, na zaidi ya wananchi Zanzibar kuamua aina ya muungano wanaoutaka.
 
YALIANZIA 1993 NAMNA HIVI

MJADALA unaendelea nchini kote juu ya kuundwa kwa serikali ya Tanganyika na muundo wa Muungano wa Zanzibar na Tanganyika. Inavyoelekea yapo matatizo, dosari na sababu za msingi zilizopelekea wananchi kuhoji muundo wa sasa wa Muungano na kuleta hoja ya kuundwa kwa serikali ya Tanganyika ni yenye kuundwa kama si leo kesho.

Lakini wapo pia wanaopinga kabisa kuundwa kwa serikali ya Tanganyika.


Aliyejitokeza kwa nguvu na kwa ukali hadharani kupinga hoja hiyo ni Mwalimu Julius Nyerere, katika kupinga hoja hiyo Mwalimu anatoa hoja zifuatazo:


Hoja ya kuundwa kwa serikali ya Tanganyika imeletwa kwa kuwachoka Wazanzibari na Waislamu. Ufupi wa maneno Mwalimu Nyerere anadai hoja ya kuundwa Serikali ya Tanganyika imetokana na chuki za kidini - Wakristo kuwachukia Waislamu.



Hoja haipo katika sera za CCM na taratibu zimekosewa.


Kuundwa kwa serikali ya Tanganyika kutavunja Muungano na kutavunja Tanganyika pia.

Ukizingatia sifa nyingi ambazo Nyerere alijilimbikizia wakati wa utawala wake na sasa si vigumu kuelewa kwa nini anapinga kuundwa kwa serikali ya Tanganyika.

Mambo yake yote aliyoyaanzisha kwa vishindo huku akisifiwa kuwa zidumu fikra zake, yamekuwa yakiporomoka moja baada ya jingine huku mwenyewe akiona. Lililosalia ni Muungano; nao ukiporomoka haitaleta picha nzuri katika historia yake katika siasa.



Lakini lililo gumu kueleweka ni hatua ya Mwalimu Nyerere kutumia Turufu ya udini kuwagawa Wabunge; wana-CCM na Wa-Tanzania kwa ujumla katika suala hili. Kauli hiyo ingesemwa na Muislamu ingepewa mtizamo tofauti na labda isingeeleweka hasa miongoni mwa Waislamu.

Lakini kusemwa na Mwalimu Nyerere kunaleta mkanganyiko zaidi. Kwanini; (udini ulikuwa umejengeka). Hali hiyo ilipelekea Masheikh kumlalamikia lakini akawanyamazisha kwa kuwashutumu kuwa wanachanganya dini na siasa. Miongoni mwa Masheikh hao wapo waliofukuzwa nchini; waliowekwa kizuizini, waliofukuzwa katika chama na kadhalika.



Sheikh Hassan bin Amir katika waraka wake kwa Waislamu mwaka 1963 aliutaja udini uliokuwa unajengwa Tanzania kwa kutoa mifano ifuatayo:



Kuingizwa nchini Tanganyika mara tu baada ya uhuru vimedali vidogo vidogo vyenye picha ya bendera ya Tanganyika usoni na katikati ya bendera hiyo amesimama Mama Maria na mtoto mchanga na nyuma yake maandiko 'MARIA MTAKATIFU ULINDE UHURU WA TANGANYIKA'.



Gazeti la KIONGOZI la tarehe 1/8/1963 lilimuonyesha Bwana George Kahama akipewa cheo cha dini na Pope kwa kuwakilisha serikali ya Tanganyika katika mkutano wa Makanisa ya Roma.



Mwaka huo huo wa 1963, mnamo tarehe 24 mwezi wa nane, Baraza Kuu la Makanisa ya Kilutheri Tanganyika lilitoa matangazo kuwa Uhuru wa Tanganyika ulikuwa 'Chini ya Msalaba'.

Yeah, Unajua Dini zote za kikristo na kiislamu zilianzia Zanzibar na Pwani wakati ule ikiwa chini ya Sultani na kuingia Bara kwa idhini ya Sultani?

Unajua kuwa George Kahama pamaja na hiyo ana wake wanne, na hiyo haitakiwi kwa Dini ya Kiroma? kwahiyo kiuhalali wangemtelekeza? Angepokelewa karibu na Waislamu kwa kuoa wake wanne zaidi ya waroma.

Yeah, Ulisema hivyo lakini wakati huo huo Machifu wote waliofuata hiyo dini ya Kilutheri waliondolewa wadhifa wao Mfano
Chief Mareale wa Marangu, alikuwa Mlutheri powerful kweli na Kahawa, Nyerere alimvua cheo chake na kukichukua Chama
Cha Ushirika cha KNCU kwa sababu wachaga wachache walikuwa Matajiri na kutosikiliza serikali.

Nyerere alifanya Mengi Machungu kwa Wakristo pia Wakristo sio kundi Moja kuna madhehebu Mbalimbali; Hapa Tanganyika Waislamu wetu wengu ni Sunni; lakini kwa Wakristo tuna Roma, Walutheri nakadhalika na wote waliathirika
Kwa kutaifishiwa ghuzo zao za kiuchumi kama walutheri hospitali ya KCMC au wa ROMA bugando hospitali au Mashule kibao; walimchukia kwa hayo pia lakini katika Dini za kikristo biblia inaongelea kusaidia Masikini. Sasa Nyerere aliyasema hayo, kwahiyo hata kama hawakupenda jinsi alivyochukua mali zao alisema ni kusaidia kila masikini nchini awe mkristo au muislamu. Hapo kweli hakubagua Mkristo na Muislamu walienda hizo shule na hospitali na kupata matibabu bila shida yoyote.

Sasa kama ni Chuki ya Nyerere, kweli sawa lakini wapo au tupo tuliofanikiwa na aliyoyatenda kuna watu tusingeona elimu ya Juu, au Kidato cha kwanza au kusomeshwa nje ya nchi na serikali angalia Kenya hawana hayo.

Chuki hii ni Ignorance, wengi wao ukiwauliza kuna faida tatakuambia ya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ya Nyerere
Lakini kama ni Muda Umefika wa Zanzibar kujitenga ni lazima Udini Uwekwe ili ijiondoe? Kuna Wazanzibari UK; wanaishi kwa Amani huko UK unadhani hata siku moja watachoma Kanisa huko? Hata siku Moja watamtukana Mkristo huko UK?
 
1.Je!Ni kwanini watanganyika tunajifanya sana kuwajali hawa wazanzibar kuliko wao wanavyojijali?Kama wanahitaji nchi yao kwa nini tusiwaachie ili kama wanataka kuwa kama Somalia na basi wawe?
Thank you!

Mkuu, umeliona hilo? That is the biggest conundrum there is. Kwa nini Watanganyika ndio tunajifanya tunawapenda saaaana Wazanzibar kiasi cha kuwakatalia wasijitoe eti wataumia?


3.Kumekuwa na hii propaganda kuwa Muungano wetu ni kwa ajiri ya usalama zaidi ,hivi naomba niulize tena kabla ya 1964 mbona usalama wa tanganyika ulikuwa sawa?[/SIZE]
Basi kama hiyo ndio concern ina maana Watanganyika sisi ni waongo na wanafiki, sio kweli kwamba tunawapenda Wazanzibar kihiiivyo kwmba wakijitoa wataumia bali the real concern ni kwamba sisi ndio waoga, Zanzibar wakijitoa sisi ndio tunaogopa tutavamiwa!

Which is so mindless. I mean, issue hii ya usalama, jamani hivi mtemi mwenye ma zana ya kivita ya kileo akitaka kukutungua from wherever he is jamani does it matter kama umeungana na Zanzibar au la? Ni lazima hayo ma warhead yake ayalete Zanzibar kabla hajakutungueni? Kwa hiyo tuseme nchi zote zinazopakana na bahari bila visiwa pembeni yake ni militarily unreachable?? It is so incredibly absurd to say that Zanzibar is protecting us, so ridiculous!

Halafu Tanzania tuna bifu na nani tunaemwogopa ambae anataka kuchukua Zanzibar ili atuchape, Sultani wa Oman? hahahahhaha...
 
Kwa hicho kinachotokea Hapo Mjini Magharibi ni ishara tosha kuwa Zanzibar Can not take care of itself!!!
 
Watu badala ya kufadhili ujenzi wa shule,vyuo,hospitali nk, wanafadhili vikundi vya 'wahuni'...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom