nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Siri nzito ya machafuko yanayoendelea mjini hapa, imefichuka.
Habari za kuaminika zilizopatikana jana kutoka Zanzibar, zinasema kuna kundi kubwa la wafanyabiashara wa Kizanzibari wanaoishi katika nchi za Oman na Uingereza, wanadaiwa kutoa fedha nyingi kufadhili vikundi vya kidini na wanaharakati kushinikiza Muungano uvunjwe.
Tunasikitishwa mno na machafuko haya, yameiaibisha Zanzibar, ambayo baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, ilitulia lakini tunasikitishwa na tukio hili ambao linafadhiliwa na Wazanzibari wenzetu wanaoishi Oman na Uingereza.
Watu hawa wanamekuwa wafadhili wakubwa wa kutoa fedha kwenye vikundi vya kidini na wanaharakati, jambo ambalo tunaona ni hatari kubwa kwa amani kisiwani hapa, tunavishauri vyombo vya dola, vichukue hatua, kilisema chanzo chetu.
Aidha chanzo hicho, kinasema kutokana na nguvu kubwa ya fedha, vikundi hivyo vimekuwa na ushawishi mkubwa kwa vijana ambao wengi wao hawana kazi maalum za kufanya.
Utashangaa kuona, baada ya kutokea machafuko haya, wengi walioonekana walikuwa vijana tu, huoni watu wazima, akina baba au akina mama ni wazi utaona fedha zina nguvu kubwa kwa vijana wetu, ukiangalia wale waliondamana juzi ni vijana wenye umri kati ya miaka 18 hadi 24.
Lakini pia tumebaini kwamba, mbali ya vikundi hivi, kuna chama kimoja cha siasa kisiwani hapa, kwa namna moja au nyingine kina mkono wake ndani ya machafuko haya, kimekuwa bingwa wa kuchochea uvunjifu wa amani, kilisema chanzo chetu.
Chanzo hicho kiliiambia MTANZANIA kwamba Wazanzibari hao wamekuwa na ushawishi mkubwa wa kuwashinikiza wananchi waibane Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ili iitishe kura ya maoni.
Issue ya Muungano ni muhimu, lakini hawa jamaa wanafanya hivi ili kuishinikiza Serikali iitishe kura ya maoni ili kuona kama kuna watu wanaukubali Muungano au la! Jambo hili si baya, lakini walitakiwa kupitia njia ambazo ni sahihi, kilisema chanzo chetu.
Kwa upande wake, Mjumbe wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa, Daud Ismail, lisema matatizo yanayoendelea Zanzibar, ni vema Serikali ipitie ripoti mbalimbali zinazohusu kero za Muungano.
Ili kuweza kuondokana na hali hii, ni vema Serikali zote mbili zifanyie kazi ripoti za Hassan Moyo, William Shelukindo, Amina Salum Ally na ya aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), mzee Edwin Mtei, ambazo zote zilieleza wazi tatizo linatotekea sasa Zanzibar.
Leo huwezi kudhibiti hali hii ya machafuko kwa kukaa mezani na Jumuiya ya Uamsho, kufanya hivi ni sawa na kuchochea jambo hili ila kinachotakiwa hapa ni kufanyia kazi jambo hili kwa undani.
Wazanzibari kwa muda mrefu, wamekuwa wakilalamika kuhusu hata namna ya mapato yanavyopendelea upande mmoja wa Tanganyika, na katika kulithibitisha hili, hata ripoti ya mshauri wa Zanzibar ya mwaka 2010, imeeleza wazi, kwa hili ni lazima chama changu cha CCM kitoe tamko na si kunyamaza kimya, alisema Daud.