Zanzibar haitaendelea na serikali kubwa hivi

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,596
8,738
Ndugu zetu wa Zanzibar hawataweza kuendelea kwa sababu serikali yao ni kubwa sana ukilinganisha na idadi ya watu. Zanzibar ina budget ya $400 million tu na watu wasiozidi 1,500,000!. Zanzibar serikali yao ni kubwa kiasi kwamba inawezekana $200 million inatumika kuwahudumia viongozi tu kuanzia wabunge, mawaziri, ikulu, wakuu wa mikoa, wakuu wa jeshi na polisi. Zanzibar inatakiwa kuwa na serikali ndogo sana. Zanzibar ina watu kama mji wa mwanza lakini angalia ni watu wangapi wanategemea serikali. Je pesa ya shule itatoka wapi?, pesa ya hospitali itatoka wapi wakati hospitali moja ya kisasa ya rufaa inaweza kujengwa kwa hadi $80-$100m hivyo ndugu zangu wa Zanzibar kama kweli tunataka maendeleo tuanza na ukubwa wa serikali.
 
Ushauri wako ni makini lakini kwa utawala wa ccm hilo ni kinyume!hawapo kumfikiria mwananchi wa hali ya chini.
 
Pesa za Muungano zinawalea, subiri siku hiyo gundi ya muunganisho itakapo expire ndio watajua kumbe hata mnyama ni mboga...
 
omba mungu tu? kwa mikakati ya ccm, hamtafurukuta watawapeleka watakavyo na akili zao ndogo. walaaniwe utawala wa ccm amen
 
Siamini nchi ndogo kama Zanzibar kuwa na Makamu wa maraisi 2 hata sijui hao makamu nani atafanya nini. Its one thing kushare madaraka lakini its another thing for them to have big govt for the money they dont have ( We dont have).
 
Siamini nchi ndogo kama Zanzibar kuwa na Makamu wa maraisi 2 hata sijui hao makamu nani atafanya nini. Its one thing kushare madaraka lakini its another thing for them to have big govt for the money they dont have ( We dont have).
Makamu wa 1- kazi yake kuzindua mikutano
Makamu wa 2- waziri kiongozi
 
hivi KWA NINI TULIUNGA NA ZANZIBAR??????????????????, kwa nini SIO KENYA au UGANDA??? ni swali tu Sina maana ya ubaguzi, kwa kuwa naona sababu nilizowahi kuzisiakia SIO ZA MSINGI SAAAAAANA .Naomba SASU ZA MSINGI JIULIZE KABLA YA KUJIBU!!!!!!!!!!!

Nimewasilisha
 
Under ccm Zanzibar will remain the same unless a leader of Salmin's type comes up on power again! Otherwise we will have the same cries every five years!
 
zanzibar ni nchi si mkoa bwana, ebo!

kama kwweli zenji ina budget ys $400mil kwa mwaka, basi wako mbali sana ukilinganisha na huku kwetu! wamepiga hatua kubwa sana basing on its profile
 
wanapewa kama 10% ya pesa ya Tanzania nzima ya budget hivyo sio kwamba wanafanya vizuri ni mgao.Vilevile pesa inaishia kwenye matumizi ya viongozi!!
 
zanzibar ni nchi si mkoa bwana, ebo!

kama kwweli zenji ina budget ys $400mil kwa mwaka, basi wako mbali sana ukilinganisha na huku kwetu! wamepiga hatua kubwa sana basing on its profile

Hiyo pesa wanapewa kama msaada au ni gawio lao kutoka BOT???
 
wanapewa kama 10% ya pesa ya Tanzania nzima ya budget hivyo sio kwamba wanafanya vizuri ni mgao.Vilevile pesa inaishia kwenye matumizi ya viongozi!!

Hiyo pesa wanapewa kama msaada au ni gawio lao kutoka BOT???
 
hivi KWA NINI TULIUNGA NA ZANZIBAR??????????????????, kwa nini SIO KENYA au UGANDA??? ni swali tu Sina maana ya ubaguzi, kwa kuwa naona sababu nilizowahi kuzisiakia SIO ZA MSINGI SAAAAAANA .Naomba SASU ZA MSINGI JIULIZE KABLA YA KUJIBU!!!!!!!!!!!

Nimewasilisha
Akili na mawazo ya waTanganyika ni kuiona Zanzibar ni sehemu yao...kwahiyo huu Muungano ulikuwa kama mtego wa kuichukua tena Zanzibar...Lakini waZanzibari ni watu makini sana, hili wameligundua ndio utaona Zanzibar hawana hamu ya Muungano ila ni sisi Tanganyika.
 
Hivyo Watanganyika hamna la kujadili bali kujadili lisilokuhusuni? Lengo lenu kuiona Zanzibar ikisambaratika lakini wapi!! Mkisema kuwa Wazanzibari hawawezi kuishi kwa amani lakini you were proved wrong! Badala yake ni nyie mliyobaki katika lindi la kukosa amani. Waachieni Wazanzibari kwani si kweli kuwa wanawategemea nyinyi. Natowa changamoto! Waachieni muuone viroho vitakavyowauma kwa maendeleo ya Zanzibar.
 
Zanzibar serikali yao ni kubwa kiasi kwamba inawezekana $200 million inatumika kuwahudumia viongozi tu kuanzia wabunge, mawaziri, ikulu, wakuu wa mikoa, wakuu wa jeshi na polisi. Zanzibar inatakiwa kuwa na serikali ndogo sana.

Ningependa usitumie maneno ya .......huenda......................hivi takwimu za matumizi yao halisi ya kawaida yakiuendeshaji wa serikali si yapo tu hadharani..........ni vyema tukajadili mambo tukiwa na uhakika zaidi........
 
Hivyo Watanganyika hamna la kujadili bali kujadili lisilokuhusuni? Lengo lenu kuiona Zanzibar ikisambaratika lakini wapi!! Mkisema kuwa Wazanzibari hawawezi kuishi kwa amani lakini you were proved wrong! Badala yake ni nyie mliyobaki katika lindi la kukosa amani. Waachieni Wazanzibari kwani si kweli kuwa wanawategemea nyinyi. Natowa changamoto! Waachieni muuone viroho vitakavyowauma kwa maendeleo ya Zanzibar.

Mkuu hata mimi nashangaa hawa jamaa kuisakama Znz kiasi hicho - lakini huu wote ni wivu na choyo kimewakaa kwenye roho zao. Kama ZNZ inawategemea nyinyi kwa nini basi munaendela na Muungano ambao hauna maslahi na nyiyi??? Zanzibar ilikuwepo kabla ya Muungano so kwa nini isiendelee kuwepo bila ya Muungano???. Wacheni hizo nyie
 
Back
Top Bottom