Zambia: Mambo yaliyofanya kilichokuwa chama tawala cha Edgar Lungu kuanguka Uchaguzi Mkuu ni haya

SOPINTO

Senior Member
Oct 19, 2020
155
385
Mapema baada ya kupata matokeo ya uchaguzi mkuu nchini Zambia nikasema ngoja nifuatilie nini kimesaidia chama hichi kuanguka baada ya wananchi wa nchini Zambia kuamua , nimefuatilia chanel mbalimbali za mitandao na Tv za ndani ya Afrika na nje ya Afrika kwa lengo la kujua kulikoni chama tawala nchini Zambia kimepinduka miguu juu kichwa chini

Waandishi wengi walikuwa na maswali mbalimbali kwa wazambia ikiwa pamoja na kuwapa fursa ya kuzungumza juu ya demokrasia yao katika uchaguzi ambapo wale wote waliozungumza hasa umri wa vijana ni kama vile walikuwa wameambiana majibu ambapo kila mmoja alisema kuwa Serikali ya Edgar Lungu haikujali mambo mengi ndani ya wazambia huku wakitoa mifano mbalimbali kutoka katika serikali iliyoanguka:
  • Serikali ya Lungu ni kama jina lenyewe yaani Lungu kwa maana haikuwa na demokrasia kwa wazambia unyanyasaji ulikuwa mkubwa sana kwa wazambia kupitia jeshi la polisi.
  • Tatizo la Ajira, Serikali haikujenga mazingira yoyote ya ajira kwa vijana hivyo wakaamua kuiondoa.
  • Mifumuko ya bei hasa katika bidha za chakula . Serikali iliyopita Ilikuwa na mifumuko mingi ya bei ambayo haikujali uchumi wa mzambia hata kidogo hii ni kwasababu binafsi za serikali ya Lungu, wananchi wakasema tunakusubiri katika uchaguzi ujao.
  • Sababu nyingine ni kodi za bidhaa nchini zambia. Nchini Zambia asilimia kubwa ya population ya vijana wamejiajiri , lakini chama kilichoanguka kilikuwa na kodi nyingi ambazo hazikuwa na manufaa yoyote kwa maendeleo ya taifa na wananchi kwa ujumla.
  • Sera nzuri za chama pinzani ambacho kwasasa ndio chama tawala japokuwa serikali kupitia jeshi la polisi walimzuia Rais mteule katika mikutano yake mingi lakini sera za maendeleo zilizokuwa zikitolewa na Hichilema zilikuwa na matumaini makubwa kwa wazambia.
Vyama vya upinzani nchini Tanzania ni vyema mkawa mnajifunza kwa hawa jirani zenu tena jirani kabisa kwani mnafeli wapi? kuweni na mikakati mbona wenzenu wanaweza kwanini nyie , kwasasa mkililia katiba mpya bila kuwa na plan B mtafeli tena , kuweni na plan A,B,C,D.... CHAMA PINZANI KIMEINGIA MADARAKANI TENA BAADA YA KUTESWA SANA NA KILICHOKUWA CHAMA TAWALA , sasa basi jengeni urafiki na Hichilema na chama chake hata kwa kulazimisha mana nao wanajua machungu ya kuwa mpinzania .

Yangu ni hayo tu.

Picha ya Rais Mpya ambaye pia ni mfanyabiashara maarufu nchini Zambia ndugu Haikenda Hichilema , kwa mbalii alitaka kufanana na Majaliwa Kassim Majaliwa

hk.png
 
Tanzania tofauti. Kila uchaFuzi wapinzani wanashinda lakini hawatangazwi. Ni uchaguzi wa 2005 tu ndo ulikuwa huru na haki KK alipoposhinda. UchaFuzi uliopita 2020 ulikua kinyaa hadi SirGodi alishikwa na ghazab ikabidi Jiwe auliwe
 
Funzo kwa Vyama Tawala vya Afrika.

Waje kujifunza CCM inavyojali wananchi wake
 
..Zambia ukiwaudhi wananchi walioko COPPER BELT unaondoka madarakani. Nakumbuka wakati wa Mzee Kaunda mabehewa ya Tazara toka Zambia yaliyokuwa yanachorwa maandishi ya kuipinga serikali.Haukupita muda Mzee Kaunda akaanguka ktk uchaguzi.

..Maana yake ni kwamba chama tawala cha Zambia kikawatibua wapiga kura wa Copper belt basi lazima kiporomoke ktk uchaguzi.

..Kwa hapa Tanzania kidogo kidogo tunaelekea walipo Zambia. Tofauti yetu ni kwamba tutakuwa na "copper belt" zaidi ya moja, na hapa nazungumzia kundi kubwa la vijana walioko mijini bila kazi, au wanakazi zinazolipa ujira mdogo. Kundi hilo ndilo litakalokuja kuipa shida CCM miaka 10 au 15 kuanzia sasa hivi.
 
Bwana Edgar Lungu akiwa kwenye majukumu yake ya kiofisi ya kila siku wakati akiwa Rais wa Zambia🐒🐒🐒
Awsfdl.jpg
 
Back
Top Bottom