Zakia Meghji na uuzaji wa Mbuga zetu je atapeta pia ?

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Wataznania
Wote mnakumbuka adha ya Loliondo na watu wa kule , mnakumbuka wanyama kusombwa kwenda Arabuni na Ulaya , mnakumbuka Utalii kukabidhiwa wageni yote haya kwa kiasi kikubwa yalifanywa na Meghji Waziri ambaye aliupata Uwaziri kwa Ubunge wa rais mwenyewe .Hazina mnajua madudu ya kule hata wakawaza kusema tunaweza kutumia a USD pamoja na sisi kuwa huru zaidi ya miaka 40 .

Sasa mimi nauliza si wakati wa kujua kwa Zakia aliamua kutuhujumu na sasa hakuna anayemgusa anakula kwa utulivu huku Nchi ina angamia ?
 
Zakhia Meghji amekaririwa jana na Gazeti la Daily News akisema alikuwa na uhusiano mzuri wa kikazi na Billal. Ina maana alivyo tueleza kwamba alidanganywa na Billal alikuwa anaongopa?

May 21st, 2008, Baada ya Ballal 'kufa.'

Former Minister for Finance, Mrs Zakhia Meghji told the 'Daily News' that Dr Ballali was ailing for the nearly two years she worked with him and that he needed to travel regularly to the US to visit his doctor. She said that they enjoyed a good working relationship, and prayed for his soul to rest in peace.

January 14th, 2008, Kabla Billal 'hajafa'

"I agreed to sign the letter, drafted by the governor himself, because I trusted the governor at that time. It was only later that I realized the payments to Kagoda Agriculture Limited were not related to any government expenditure."

Huyu Mama aidha fisadi, au mwongo mwongo.
 
Kuhani,

Si ndio utamaduni wetu wa marehemu hasemwi huo.

Hata Idd Amin alipokufa alisifiwa kuwa alikuwa mtu mzuri.
 
Zakhia Meghji amekaririwa jana na Gazeti la Daily News akisema alikuwa na uhusiano mzuri wa kikazi na Billal. Ina maana alivyo tueleza kwamba alidanganywa na Billal alikuwa anaongopa?

May 21st, 2008, Baada ya Ballal 'kufa.'

Former Minister for Finance, Mrs Zakhia Meghji told the 'Daily News' that Dr Ballali was ailing for the nearly two years she worked with him and that he needed to travel regularly to the US to visit his doctor. She said that they enjoyed a good working relationship, and prayed for his soul to rest in peace.

January 14th, 2008, Kabla Billal 'hajafa'

"I agreed to sign the letter, drafted by the governor himself, because I trusted the governor at that time. It was only later that I realized the payments to Kagoda Agriculture Limited were not related to any government expenditure."

Huyu Mama aidha fisadi, au mwongo mwongo.



Kuhani haya ni maelezo ya ziada tu na uongo wao wote hawa ila nataka kujua .Are we gonna let her walk free na hasara yote aliyo tutia ? Mbona tunawabana akina Chenge kuanzia mikataba nk lakini huyu na Mbuga zetu tunakaa kimya ? Loliondo ndiyo imeisha sasa wale watu wa kule tuache Mungu awatetee siku ya Kiama?
 
Wataznania
Wote mnakumbuka adha ya Loliondo na watu wa kule , mnakumbuka wanyama kusombwa kwenda Arabuni na Ulaya , mnakumbuka Utalii kukabidhiwa wageni yote haya kwa kiasi kikubwa yalifanywa na Meghji Waziri ambaye aliupata Uwaziri kwa Ubunge wa rais mwenyewe
Hivi unaijua skandali ya Loliondo au unapiga kelele tu hapa? Unakumbuka ni waziri gani hapa Tz ambaye alipewa hata jina la skandali ikiwa mojawapo ya hiyo Loliondo?
Hebu usisushe hadhi ya JF..
 
Hivi unaijua skandali ya Loliondo au unapiga kelele tu hapa? Unakumbuka ni waziri gani hapa Tz ambaye alipewa hata jina la skandali ikiwa mojawapo ya hiyo Loliondo?
Hebu usisushe hadhi ya JF..

Rudia kusoma bandiko langu nadhani baada ya hapo utaelewa .
 
Saa nyingine hizi traditions zetu nyingine ni za kinafiki sana, cha ajabu jamii hata kama inajua uovu wa mtu, akifa basi atamwagiwa misifa kemkem... sasa akina Watson wakiona hivyo wana-conclude... tunaanza kulalama!
 
Wataznania
Wote mnakumbuka adha ya Loliondo na watu wa kule , mnakumbuka wanyama kusombwa kwenda Arabuni na Ulaya , mnakumbuka Utalii kukabidhiwa wageni yote haya kwa kiasi kikubwa yalifanywa na Meghji Waziri ambaye aliupata Uwaziri kwa Ubunge wa rais mwenyewe .Hazina mnajua madudu ya kule hata wakawaza kusema tunaweza kutumia a USD pamoja na sisi kuwa huru zaidi ya miaka 40 .

Sasa mimi nauliza si wakati wa kujua kwa Zakia aliamua kutuhujumu na sasa hakuna anayemgusa anakula kwa utulivu huku Nchi ina angamia ?

Lunyugu uechemka hakuwa Zakhia kwenye kashfa hiyo kumbuka kulikuwa kun mtu anaitwa skandali
 
tumekuwa ni watu tunaobururwa sana kimawazo!!

wakuu wametutaka tuimbe wimbo wa ufisadi basi bila ya kuvuta pumzi na kujiuliza tumekuwa wa kuhemkwa tu.


akisemwa Mwatumu fisadi hufikiri unaruka kweli fisadi.

zakia mwanamme wake rostam kweli na vipambio tuengeze kama vile tunajua sana.

JF makini lazima tuipiganie irudi na ni ile yenye kuja na data za uhakika halafu ndio tunafanya analysis kwadata sio kukurupula tu
 
tumekuwa ni watu tunaobururwa sana kimawazo!!

wakuu wametutaka tuimbe wimbo wa ufisadi basi bila ya kuvuta pumzi na kujiuliza tumekuwa wa kuhemkwa tu.


akisemwa Mwatumu fisadi hufikiri unaruka kweli fisadi.

zakia mwanamme wake rostam kweli na vipambio tuengeze kama vile tunajua sana.

JF makini lazima tuipiganie irudi na ni ile yenye kuja na data za uhakika halafu ndio tunafanya analysis kwadata sio kukurupula tu



Mtu wa pwani wewe si mtu wa data bali kubeza kama hapo ulipo beza .hapa watu tuna uliza Maliasili wakati wa Meghji kuna mengi yametokea.Tunataka kuweka rekodi straight na ibaki iko siku tutakuja kutafuta data hizi .Mtu wa pwani data zako zimekuwa ni utetezi na vijembe na labda kuhamisha data na kupeleka huko unako husika wacha kutukana watu .Hapa haimbishwi mtu na mambo huwa yanaanza namna hii .Tunataka kujua mambo wakati yanaenda mrama kule Maliasili na Utalii yeye alifanya nini .
 
Hili alina ubishi mariasili kumeoza sana wakati wa zakia, nafikiri hawa mawaziri wakifika wanapewa mafundisho na makatibu wa wizara maana uozo umeanza siku nyingi na unaongezeka kila siku, ila wakati wa zakia nafikiri ulifika kiasi ambacho kilikuwa kinatisha zaidi kulinganisha na vipindi vingine.
 
Mtu wa pwani wewe si mtu wa data bali kubeza kama hapo ulipo beza ..
Wewe ndie huna data, kama unataka kuweka rekodi, basi Loliondo na Meghji futa hiyo kwanza, Kama hujui kitu usione aibu kuuliza na sio kuandika kitu ambacho hakipo...
 
Mtu wa pwani wewe si mtu wa data bali kubeza kama hapo ulipo beza .hapa watu tuna uliza Maliasili wakati wa Meghji kuna mengi yametokea.Tunataka kuweka rekodi straight na ibaki iko siku tutakuja kutafuta data hizi .Mtu wa pwani data zako zimekuwa ni utetezi na vijembe na labda kuhamisha data na kupeleka huko unako husika wacha kutukana watu .Hapa haimbishwi mtu na mambo huwa yanaanza namna hii .Tunataka kujua mambo wakati yanaenda mrama kule Maliasili na Utalii yeye alifanya nini .

Kwani mambo yameacha kwenda mrama huko Maliasili na Utalii? Haya yanayoendelea Serengeti (ujenzi wa airstrip, mahoteli), Ngorongoro (ujenzi wa mahoteli) na Ziwa Natron (ujenzi wa kiwanda) hatuyaoni? Au ndio tunasubiri mpaka yatakapoharibika ndiyo tuanze kuwashughulikia wahusika!
 
Wataznania
Wote mnakumbuka adha ya Loliondo na watu wa kule , mnakumbuka wanyama kusombwa kwenda Arabuni na Ulaya , mnakumbuka Utalii kukabidhiwa wageni yote haya kwa kiasi kikubwa yalifanywa na Meghji Waziri ambaye aliupata Uwaziri kwa Ubunge wa rais

Mkuu
Hapa sijui kama watu wanalielewa hili som kwani limetokea kipindi kirefu kidogo!

Ni kweli kipindi kile kampuni ya uwindaji ya Kiarabu ilipopewa kibali cha kuendesha shughuli za uwindaji Loliondo Bi. Zhakia alikuwa waziri wa maliasili na Utalii.

Kampuni hiyo ilipatiwa kibali cha kuendesha shughuli zake kwa muda mrefu (sikumbuki vizuri, walipewa miaka mingapi) kitendo ambacho kiliwashangaza wadau wautalii, mpaka yakatokea manung'uniko ya chini kwa chini. Lakini sababu Mke wa mzee Ruksa alikuwemo ndani yake, mambo yalikubalika na shughuli ikaendelea.

Serikali iliamua kustisha mkataba wa kampuni hiyo kabla ya muda walipewa kumalizika, baada ya kugundua kuwa wanaibiwa, wale jamaa walikuwa na uwanja wao wa ndege, kwa hiyo wakichukua wanyama wanaruka moja kwa moja toka Loliondo kwenda kwao nani atajua kuwa kile kilichochukuliwa ndicho walichokubaliwa kuchukua.

Nakumbuka walipofunga shughuli zao hawakuondoka na kitu chochote, vifaa vyao vyote walivyokuwa akivitumia walivitoa zawadi kwenye kikosi cha jeshi ambacho kiliendesha oparesheni ya kuwasaka wasomalia waliokuwa wakifanya uporaji sehemu za Loliondo na Ngorongoro wakifadhiliwa na matajiri wauza mirungi wa Kenya

kwa vipindi 2 ambavyo Zakia amekuwa waziri wa maliasili na utalii, kulikukuwa na mambo kibao ya kimauza -uza.
 
Mkuu
Hapa sijui kama watu wanalielewa hili som kwani limetokea kipindi kirefu kidogo!

Ni kweli kipindi kile kampuni ya uwindaji ya Kiarabu ilipopewa kibali cha kuendesha shughuli za uwindaji Loliondo Bi. Zhakia alikuwa waziri wa maliasili na Utalii.
Mwaka 1992 sehemu ya Loliondo(LGSA) ilikodishwa kwa asasi ya uarabuni kwa ajili ya uwindaji na ubebaji wa wanyama kwa kipindi cha miaka 10. Mwaka mmoja baadae (1993) Waziri wa utalii wakati huo Abubakar Mgumia alijiuzuru kutokana na kashfa ya LGSA...

Sasa huyo Meghji anahusika vipi na hili... Hebu fafanueni
 
unakumbuka huyu mmama alitaka kuuza hata ule msitu wa Tanga wa selikali kwa shs.7billion, wakati walipokuja kufanya tathmini ulikuwa halali uuzwe kwa shs.60bill., kuna daktari mmoja hivi wa mazingira kule morogoro(nikipata jibu nitawaambia)ndo alikuwa repsonsible na misitu akapinga sana. mpaka leo huyo Dr.hapatani na zakia. huyu mmama ni mama mmoja fisadi sana..anatisha. mimi niliumia sana hata kipindi kile alipochaguliwa kuwa W.wa fedha. yaani tz wakati mwingine kama hatuna macho vile. tunaweka uchafu kwenye uongozi, hivi wasomi wameisha kweli mpaka tunaendelea kuhangaika na mafisadi madarakani? hivi wewe unaesoma hii msg, ukipewa madaraka uwe waziri, utashindwa kufanya kazi bora kuliko hawa? sasa kwanini wasipigwe chini wakapewa watu waadilifu, mbona wasomi waadilifu tunao wengi tu hapa tz. inauma sana kwakweli.
 
Jamani, hivi huyu mmama anakanyagwa na nani,nana anamchukua huyu mama. naelewa kuwa mmewake alishakufaga. au anachukuliwa na fisadi mmoja hivi. naombeni nambieni mme wa huyu mama. ila siamini kama Rostam ndo anaemkanyaga.kama ingekuwa hivyo, basi tungesema yuko kwenye mfereji wa makambare yanayotisha, yanayotakiwa kuendewa na msumeno, sio kiwembe.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom