Zaituni/Zeituni??

furahi

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
945
195
Ndugu wanajamii naomba ufafanuzi kidogo kuhusu hili tunda. Kwa ufahamu wangu siku zote nilifahamu Zeituni ni "Olives", na olives nafahamu ni matunda madogo saizi ya white grapes na mara nyingi huwa naona sura yake inakaribia kufanana na white grapes. Sasa tatizo ni kwamba ktk kipindi cha Dr. Ndodi kinachorushwa EATV alikuja na tunda fulani kubwa la njano lenye umbo la yai akasema ndio zeituni. Sasa nilitaka kujua kuna zeituni nyingine zaidi ya Olive? Na pia lile tunda alilokuja nalo akasema huwa yanapatikana Mbeya na yanaitwa mazeituni kwa Kiingereza linaitwaje?
 
No. Yapo matunda mengine ambayo si peaches kwa Kiswahili yanaitwa zaituni.

Ile rangi ya manjano ni mpaka ndani, na tofauti na peach halina maji ni kavu kavu Kama kiazi kitamu cha kuchoma.
 
No. Yapo matunda mengine ambayo si peaches kwa Kiswahili yanaitwa zaituni.

Ile rangi ya manjano ni mpaka ndani, na tofauti na peach halina maji ni kavu kavu Kama kiazi kitamu cha kuchoma.
Yeah, sasa kiingereza yanaitwaje? Peaches nazifahamu hata kwetu zipo.
 
Yanaitwa peaches
Yale sio peaches. Peaches nazifahamu hata kwetu zipo. Yale aliyoonyesha yana nyama laini sana halafu mbegu yake ndani haina wekundu kama wa peaches. Alikuja na Mtunda kama manne. Peaches, mastafeli, carot, na hayo aliyoyaita mazeituni.
 
Hilo tunda nalifahamu, halina maji ndani, ukila lina-taste kama kiazi kitamu kilichopikwa au kuchomwa. Ni kweli waswahili wanaliita zeituni. Sahihi si sahihi kwa kiswahili, sijui. Ila Olive ambayo nayo ni zaitun, ni tunda lingine kabisa.

Hili zeituni la tanzania kwa kiingereza, linaitwa Canistel, au Yellow sapote au Egg fruit, Scientific name ni Pouteria campechiana. Sina uhakika kama yanapatikana Mbeya, ila nimewahi nunua Morogoro na Dar es salaam

see the pics
 

Attachments

  • Tanzanian Zaitun fruit_Canistel.jpg
    Tanzanian Zaitun fruit_Canistel.jpg
    32 KB · Views: 1,290
Hilo tunda nalifahamu, halina maji ndani, ukila lina-taste kama kiazi kitamu kilichopikwa au kuchomwa. Ni kweli waswahili wanaliita zeituni. Sahihi si sahihi kwa kiswahili, sijui. Ila Olive ambayo nayo ni zaitun, ni tunda lingine kabisa.

Hili zeituni la tanzania kwa kiingereza, linaitwa Canistel, au Yellow sapote au Egg fruit, Scientific name ni Pouteria campechiana. Sina uhakika kama yanapatikana Mbeya, ila nimewahi nunua Morogoro na Dar es salaam

see the pics
Nakushukuru sana Nanren. Bila shaka hilo ndilo jibu nililo hitaji. Thanx
 
Ndugu wanajamii naomba ufafanuzi kidogo kuhusu hili tunda. Kwa ufahamu wangu siku zote nilifahamu Zeituni ni "Olives", na olives nafahamu ni matunda madogo saizi ya white grapes na mara nyingi huwa naona sura yake inakaribia kufanana na white grapes. Sasa tatizo ni kwamba ktk kipindi cha Dr. Ndodi kinachorushwa EATV alikuja na tunda fulani kubwa la njano lenye umbo la yai akasema ndio zeituni. Sasa nilitaka kujua kuna zeituni nyingine zaidi ya Olive? Na pia lile tunda alilokuja nalo akasema huwa yanapatikana Mbeya na yanaitwa mazeituni kwa Kiingereza linaitwaje?
IMG_20210426_082940_208.jpg

Utakuwa unaoongelea tunda hili.
Yanaitwa mazaituni japo tunda hili halitokani na mzaituni (Olive tree).
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom