Zaidi ya wakazi 2000 hatariri kuugua magonjwa ya mlipuko kwa kuchangia maji ya kunywa na mifugo

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275
maji%2823%29.jpg


Wakazi zaidi ya 2,000 wa kijiji cha Chembeli kata ya Didia wilayani Shinyanga wako hatarini kukumbwa na magonjwa ya mlipuko kufuatia mradi wa maji uliojengwa mwaka 2014 kuwekwa mabomba mabovu hali inayosababisha wakazi hao kuchangia maji ya kunywa na mifugo katika mabwawa yasiyo rasmi.

Wakizungumzia hali hiyo baadhiya wakazi wa kijiji hicho ambacho kinadaiwa hakijawahi kutembelewa na mkuu wa wilaya yeyote tangu kianzishwe wamesema licha ya mradi huo kujengwa na kukamilika mwaka 2014 mabomba yaliyowekwa yamekuwa yakipasuka mara kwa mara na kusababisha maji kukosekana hali inayowalazimu wanawake na watoto kutumia muda mrefu kutafuta maji.

Sylivester Mpemba ni mkandarasi anayelalamikiwa na wananchi kujenga mradi huo na kuweka mabomba mabovu amesema mradi umezingatia viwango lakini kwa sasa anafuatilia sababu zinazosababisha changamoto ya mabomba kupasuka

Kufuatia malalamiko ya muda mrefu ya wananchi mkuu wa wilaya ya shinyanga Bi.Josephone Matiro akalazimika kuingilia kati na kumuagiza mkurugenzi wa Halmashauri ya Shinyanga DC kuunda timu ya wataalamu na kuchunguza mradi huo ndani ya siku 30 na kurudisha majibu.



Chanzo; ITV
 
Back
Top Bottom