Zaidi ya wabunge 100 wa CCM hawauziki - Msabaha

Nov 1, 2006
73
9
Zaidi ya wabunge 100 wa CCM hawauziki - Msabah

2008-03-28 10:42:04

Na Ahmed Makongo, Bunda

Zaidi ya Wabunge 100 wa CCM wanaotarajia kujitokeza kugombea ubunge katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, majina yao hayatarudi ili kukiepusha chama kushindwa katika majimbo yao.

Kauli hiyo nzito imetolewa juzi kwa nyakati tofauti na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa (NEC), Bw. Salum Msabah, wakati akizungumza na viongozi wa chama hicho, kwenye mikutano ya ndani, katika kata ya Kibara na Nansimo wilayani Bunda.

Bw. Msabah alisema kuwa tayari makao makuu ya chama hicho wamekwishabaini wabunge hao kuwa wakirudi utakuwa mzigo kwa chama hicho na iwapo watagombea tena katika uchaguzi wa mwaka 2010 majina yao hayatapendekezwa na uongozi wa juu wa chama hicho.

``Hilo makao makuu tumekwishaliona na kweli wabunge zaidi ya 100 majina yao inawezekana yasirudi, kwa kuwa tukiyarudisha inawezekana wakasababisha chama chetu kikashindwa katika majimbo yao. Hata hivyo utakuwa ni mzigo kuwanadi kwa wananchi,`` alisisitiza Bw. Msabah.

Alisema kuwa baadhi ya wabunge hao wamekwisha kuwa kero kwa wananchi kwa kuwa wakichaguliwa hawarudi tena kwenye majimbo yao na badala yake wanakuwa watu wa mijini tu.

Kuhusu jimbo la Mwibara ambalo matokeo yake ya uchaguzi yalitenguliwa na Mahakama Kuu, Kanda ya Mwanza na kumvua ubunge, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Bw. Charles Kajege, ambaye amekata rufaa katika Mahakama ya Rufaa, Bw. Msabah, aliwataka wana-CCM, wote kuondoa hofu kwa kuwa hata uchaguzi mdogo ukifanyika jimbo hilo litarudi CCM.

Alisema kuwa chama chao kuanzia ngazi ya juu hadi ya chini, kimejipanga vizuri na kamwe wapinzani wasifikiri kuwa hata kama uchaguzi mdogo ukifanyika watalipata jimbo hilo .

``Hakuna sehemu CCM itashindwa uchaguzi mdogo bwana, tumejipanga vizuri sana kuhakikisha jimbo hili tunalichukua, uchaguzi mdogo ukifanyika wote tutahamia hapa, atakuja Marecela, nitakuja mimi, atakuja Rais wetu, atakuja mzee Makamba na watakuja viongozi wetu wote... Sasa wapinzani watashindia wapi,`` alisema.

``Na sisi tutafanya kampeni kubwa ya nyumba kwa nyumba, kichwa kwa kichwa, kitanda kwa kitanda na shuka kwa shuka...,`` alisema na kushangiliwa na umati mkubwa uliokuwa umehudhuria mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kibara.

Aidha, Bw. Msabah alikiri kuwepo kwa wana CCM., ambao ni wanafiki wanaochangia chama hicho kushindwa katika baadhi ya majimbo, kata, vijiji na vitongoji kwa kuwa wamekuwa hawana msimamo.

Alisema kuwa vyama vya upinzani vilivyoko hapa nchini ni wasindikizaji na kila siku vinazidi kushuka ngazi ya ubora kwa wananchi.

Katika mkutano huo zaidi ya wanachama 60, wa vyama mbalimbali vya upinzani, wengi wao wakiwa ni kutoka TLP, walirudisha kadi za vyama hivyo na kujiunga na CCM.

SOURCE: Nipashe
 
Sounds to be a blessing in disguise. We have a possibility of proving Mwalimu right. 2010 sio mbali sana.
 
Hussein, zinduka baba.
Si kwamba wabunge wa ccm hawafai tu, bali hawa ni kama gunia la mawe, unaujua uzito wa gunia la mawe? usipime mtu wangu, jamaa ndoto zao wakiisha ingia madarakani tuu, wanaanza kujiandaa kwa uchaguzi unaokuja. Baada ya kufikiri jinsi kuwainua wapiga kura wake na kuleta maendeleo,badala yake wao huwaza jinsi ya kujitajirisha.Uzalenzo haupo tena tanzania hii.
 
Hussein, zinduka baba.
Si kwamba wabunge wa ccm hawafai tu, bali hawa ni kama gunia la mawe, unaujua uzito wa gunia la mawe? usipime mtu wangu, jamaa ndoto zao wakiisha ingia madarakani tuu, wanaanza kujiandaa kwa uchaguzi unaokuja. Baada ya kufikiri jinsi kuwainua wapiga kura wake na kuleta maendeleo,badala yake wao huwaza jinsi ya kujitajirisha.Uzalenzo haupo tena tanzania hii.

Tata Isayamwita nimezinduka sasa na nimekuelewa na sasa nitakaa mkao wa kutoa mimacho .
 
who cares? hata wakileta wendawazimu najua CCM watashinda kwa 99%,acha njaa,umaskini,ufisadi uendelee kama kazi labda wananchi watashtuka lakini kwa sasa nchi yote wamerogwa.
 
who cares? hata wakileta wendawazimu najua CCM watashinda kwa 99%,acha njaa,umaskini,ufisadi uendelee kama kazi labda wananchi watashtuka lakini kwa sasa nchi yote wamerogwa.

Yaani mpaka wafikie hatua ya kula nyasi kama mramba alivyowaambia ndio labda watajua thamani ya kura zao
 
LABDA TURUDI KWENYE HEADING HAPO JUU.......MSABAHA AMESHINDWA KUWATAJA HAO (unsellable goods).....HEBU TUCHUKUE NAFASI HII KWA HEKIMA NA UTULIVU ZAIDI....KUJARIBU KU-GUESS...WHO MIGHT BE........WASIOUZIKA..........STARTING WITH...IBRA MSABAHA,LOWASA,KARAMAGI,KEENJA,MLAKI,LUKUVI(?),.....THE LIST GOES ON...TAJA...TAJA...100 AND MORE.....!
 
who cares? hata wakileta wendawazimu najua CCM watashinda kwa 99%,acha njaa,umaskini,ufisadi uendelee kama kazi labda wananchi watashtuka lakini kwa sasa nchi yote wamerogwa.

koba mimi sijarogwa wala sina mawazo mgando so niondoe kwenye kundi hili .

Kujaribu kudodosa nani anaweza kurudi kwa CCM hata wale wapya wanao omba mwaka huo ni wachafu ambao wamejiandaa kimtandao kuingia hapo sasa tutafanyaje ?
 
LABDA TURUDI KWENYE HEADING HAPO JUU.......MSABAHA AMESHINDWA KUWATAJA HAO (unsellable goods).....HEBU TUCHUKUE NAFASI HII KWA HEKIMA NA UTULIVU ZAIDI....KUJARIBU KU-GUESS...WHO MIGHT BE........WASIOUZIKA..........STARTING WITH...IBRA MSABAHA,LOWASA,KARAMAGI,KEENJA,MLAKI,LUKUVI(?),.....THE LIST GOES ON...TAJA...TAJA...100 AND MORE.....!

List iendelee mimi namjua Mzee Jackson Makweta (ninawahakikishia kama atagombea 2010 Upinzani utashinda hata bila kampeni).
 
List iendelee mimi namjua Mzee Jackson Makweta (ninawahakikishia kama atagombea 2010 Upinzani utashinda hata bila kampeni).

Sarungi kule Rorya maana last time hongo na msaada aliupata toka pale Diamond Motors in return awape tender Jeshini kwamba angali endelea kuwa waziri wa Ulinzi .So naamini niko Rorya sasa wanasema atamwagwa .
 
Sarungi kule Rorya maana last time hongo na msaada aliupata toka pale Diamond Motors in return awape tender Jeshini kwamba angali endelea kuwa waziri wa Ulinzi .So naamini niko Rorya sasa wanasema atamwagwa .

Obvious Mh Dr Jumaa Ngasongwa harudi kama anabusara wala asigombeee kule Malinyi wamemchoka, huwaambia wapiga kura pesa zake ndo zamrudisha bungeni...
 
Obvious Mh Dr Jumaa Ngasongwa harudi kama anabusara wala asigombeee kule Malinyi wamemchoka, huwaambia wapiga kura pesa zake ndo zamrudisha bungeni...

Yule Ngasongwa naye ni mtupu sana . Kuna jamaa aliniambia kwamba yeye alichukua vyeti akaacha akili kwa wahadhiri wake na ndiyo maana akadhani pesa yake ni jibu la kila kitu .
 
Kwahiyo tusogeze majina sasa? Independent wabunge wanaruhusiwa?

Mzee wagombea binafsi CCM na JK wanawakoma vibaya na kesi iko mahakamani nadhani ama bado hawajakata rufaa tupeni status tuje kusimama bila vyama .
 
Sarungi kule Rorya maana last time hongo na msaada aliupata toka pale Diamond Motors in return awape tender Jeshini kwamba angali endelea kuwa waziri wa Ulinzi .So naamini niko Rorya sasa wanasema atamwagwa .

Nilijua utamsema maana najua hata hawezi kuchukua form, kwa kifupi jimbo liko wazi. Vijana wa CCM changamkia tenda lakini sijui kama wapinzani wakihamua kama kweli mtafua dafu.
 
Alisema kuwa chama chao kuanzia ngazi ya juu hadi ya chini, kimejipanga vizuri na kamwe wapinzani wasifikiri kuwa hata kama uchaguzi mdogo ukifanyika watalipata jimbo hilo .

``Hakuna sehemu CCM itashindwa uchaguzi mdogo bwana, tumejipanga vizuri sana kuhakikisha jimbo hili tunalichukua, uchaguzi mdogo ukifanyika wote tutahamia hapa, atakuja Marecela, nitakuja mimi, atakuja Rais wetu, atakuja mzee Makamba na watakuja viongozi wetu wote... Sasa wapinzani watashindia wapi,`` alisema.

.``Na sisi tutafanya kampeni kubwa ya nyumba kwa nyumba, kichwa kwa kichwa, kitanda kwa kitanda na shuka kwa shuka...,`` alisema na kushangiliwa na umati mkubwa uliokuwa umehudhuria mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kibara



Katika mkutano huo zaidi ya wanachama 60, wa vyama mbalimbali vya upinzani, wengi wao wakiwa ni kutoka TLP, walirudisha kadi za vyama hivyo na kujiunga na CCM.

SOURCE: Nipashe
Maneno hayo sio ya kubeza... shauri yenu!


Aidha, Bw. Msabah alikiri kuwepo kwa wana CCM., ambao ni wanafiki wanaochangia chama hicho kushindwa katika baadhi ya majimbo, kata, vijiji na vitongoji kwa kuwa wamekuwa hawana msimamo.

Hawa hata hapa JF wapo... visebusebu na viroho vi papo
 
Kwahiyo tusogeze majina sasa? Independent wabunge wanaruhusiwa?
MI NADHANI THE BETTER WAY TO DO THIS NI KUORODHESHA WOTE WASIOFAA.....AND WHY HAWAFAI.......TUFANYE HIVI ILI KUEPUKA SIASA ZA CHUKI NA KUPAKANA MATOPE......ALIYEFANYA VIZURI JIMBONI KWAKE APEWE SIFA ZAKE..(mf.ndesa,slaa na mkono{japo kafisadi)NA WALIOFANYA VIBAYA VILE VILE PASIPO KUJALI CHAMA WASULUBIWE KWA JINA LA 'UZALENDO/TANZANIA'
TUKITOA MICHANGO YETU KWA TAIFA LETU HATA MUNGU ATATUINUA,KUTUBARIKI,KUTULINDA,ATATUPONYA NA KUTUONGEZA ZAIDI...!
 
Zaidi ya wabunge 100 wa CCM hawauziki - Msabah

2008-03-28 10:42:04

Na Ahmed Makongo, Bunda

Zaidi ya Wabunge 100 wa CCM wanaotarajia kujitokeza kugombea ubunge katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, majina yao hayatarudi ili kukiepusha chama kushindwa katika majimbo yao.

Kauli hiyo nzito imetolewa juzi kwa nyakati tofauti na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa (NEC), Bw. Salum Msabah, wakati akizungumza na viongozi wa chama hicho, kwenye mikutano ya ndani, katika kata ya Kibara na Nansimo wilayani Bunda.

Bw. Msabah alisema kuwa tayari makao makuu ya chama hicho wamekwishabaini wabunge hao kuwa wakirudi utakuwa mzigo kwa chama hicho na iwapo watagombea tena katika uchaguzi wa mwaka 2010 majina yao hayatapendekezwa na uongozi wa juu wa chama hicho.

``Hilo makao makuu tumekwishaliona na kweli wabunge zaidi ya 100 majina yao inawezekana yasirudi, kwa kuwa tukiyarudisha inawezekana wakasababisha chama chetu kikashindwa katika majimbo yao. Hata hivyo utakuwa ni mzigo kuwanadi kwa wananchi,`` alisisitiza Bw. Msabah.

Alisema kuwa baadhi ya wabunge hao wamekwisha kuwa kero kwa wananchi kwa kuwa wakichaguliwa hawarudi tena kwenye majimbo yao na badala yake wanakuwa watu wa mijini tu.

Kuhusu jimbo la Mwibara ambalo matokeo yake ya uchaguzi yalitenguliwa na Mahakama Kuu, Kanda ya Mwanza na kumvua ubunge, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Bw. Charles Kajege, ambaye amekata rufaa katika Mahakama ya Rufaa, Bw. Msabah, aliwataka wana-CCM, wote kuondoa hofu kwa kuwa hata uchaguzi mdogo ukifanyika jimbo hilo litarudi CCM.

Alisema kuwa chama chao kuanzia ngazi ya juu hadi ya chini, kimejipanga vizuri na kamwe wapinzani wasifikiri kuwa hata kama uchaguzi mdogo ukifanyika watalipata jimbo hilo .

``Hakuna sehemu CCM itashindwa uchaguzi mdogo bwana, tumejipanga vizuri sana kuhakikisha jimbo hili tunalichukua, uchaguzi mdogo ukifanyika wote tutahamia hapa, atakuja Marecela, nitakuja mimi, atakuja Rais wetu, atakuja mzee Makamba na watakuja viongozi wetu wote... Sasa wapinzani watashindia wapi,`` alisema.

``Na sisi tutafanya kampeni kubwa ya nyumba kwa nyumba, kichwa kwa kichwa, kitanda kwa kitanda na shuka kwa shuka...,`` alisema na kushangiliwa na umati mkubwa uliokuwa umehudhuria mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kibara.

Aidha, Bw. Msabah alikiri kuwepo kwa wana CCM., ambao ni wanafiki wanaochangia chama hicho kushindwa katika baadhi ya majimbo, kata, vijiji na vitongoji kwa kuwa wamekuwa hawana msimamo.

Alisema kuwa vyama vya upinzani vilivyoko hapa nchini ni wasindikizaji na kila siku vinazidi kushuka ngazi ya ubora kwa wananchi.

Katika mkutano huo zaidi ya wanachama 60, wa vyama mbalimbali vya upinzani, wengi wao wakiwa ni kutoka TLP, walirudisha kadi za vyama hivyo na kujiunga na CCM.

SOURCE: Nipashe

Kwa maoni yangu hii ni idadi ndogo sana, mimi nilidhani 98% ya wabunge wa CCM haiuziki kwa kipi walichokifanya mpaka 100 tu ndio hawauziki? Asilimia kubwa wanachapa usingizi tu ukiondoa wachache ambao ni watendaji wazuri lakini hawana sauti ndani ya bunge au CCM.
 
Kwa maoni yangu hii ni idadi ndogo sana, mimi nilidhani 98% ya wabunge wa CCM haiuziki kwa kipi walichokifanya mpaka 100 tu ndio hawauziki? Asilimia kubwa wanachapa usingizi tu ukiondoa wachache ambao ni watendaji wazuri lakini hawana sauti ndani ya bunge au CCM.

CCM ni maneno ya majukwaani bwana hawana lolote .Watawapata wapi wasafi wa kubakia majimboni ?Yeye mwenyewe kwao haendi leo anaongea nini?
 
Back
Top Bottom