Nyaka-One
JF-Expert Member
- Oct 27, 2013
- 4,312
- 5,979
Jamani huko vijijini watu wamekuwa wakitumia ulimbo kuwategea ndege wadogo mashambani au sehemu za vichaka ndege wengi wanapotua. Huo ulimbo unatokana na utomvu mzito wa miti fulani ambao uchemshwa na kupatikana ulimbo ambao uweza kutumika kunasia ndege kwa siku kadhaa.
Sasa mwenzenu nina shamba langu ambapo kuna sehemu italimwa lakini sehemu nyingine ambayo ina vichaka vichaka itabaki hadi hapo baadae. Kila niendapo shambani naona kuna ndege wadogo wadogo ambao huruka kwa makundi makubwa makubwa kiasi na kutua kwenye hivyo vichaka. Kwa uzoefu wangu hao ndege uliwa.
Hivyo napenda kujua kutoka kwenu ni mbinu gani ya kisasa zaidi mbadala wa ulimbo ambayo naweza kuitumia kuwatega hao ndege wadogo wadogo kwa usalama na kuniwezesha kupata kitoweo na hivyo kunifanya niongeze upendo kwenye safari zangu za kwenda huko shambani. Je, huko kwenye maduka ya kilimo na mifugo naweza kupata vifaa vya kuwatega?
Sasa mwenzenu nina shamba langu ambapo kuna sehemu italimwa lakini sehemu nyingine ambayo ina vichaka vichaka itabaki hadi hapo baadae. Kila niendapo shambani naona kuna ndege wadogo wadogo ambao huruka kwa makundi makubwa makubwa kiasi na kutua kwenye hivyo vichaka. Kwa uzoefu wangu hao ndege uliwa.
Hivyo napenda kujua kutoka kwenu ni mbinu gani ya kisasa zaidi mbadala wa ulimbo ambayo naweza kuitumia kuwatega hao ndege wadogo wadogo kwa usalama na kuniwezesha kupata kitoweo na hivyo kunifanya niongeze upendo kwenye safari zangu za kwenda huko shambani. Je, huko kwenye maduka ya kilimo na mifugo naweza kupata vifaa vya kuwatega?