Zaidi ya Suti: WikiLeaks yafunua mgongano kati ya JK, Kapuya na Gen. Waitara...

Mambo mengine hata kuanza kuyafikiria ni aibu. Lakini pia yanatudokeza mambo mengine ambayo yameendelea baadaye. Kuna watu siku moja watatakiwa kujibu walipolifikisha taifa hili hapa.

Kuna mapungufu makubwa sana ya 'thinkinig' katika safu ya political elite hapa nchini. Hii cable inaonesha ni jinsi gani wakubwa wanashindwa am kuungaisha dots au wamedhamiria kuwa 'darling' wa nchi zingine. Tanzania sasa hivi inapiganiwa na nchi za kadhaa zenye mrengo tofatuti. Lakini Marekani na Wachina na Canada ndio vinara wa kuchanja mbuga. Kupita American Peace Corps, hawa wakubwa wametuma utitiri wa watu wao. sasa hivi wako kila mahali, kuanzia Kigoma, mpaka Arusha. Mafunzo ya kijeshi nayo yanaendelea both marekani na wachina.

Na swali nilalojiuliza bila kupata jibu hata kidogo ni hili; viongozi wetu wanafanya haya yote kwa sababu wanataka kujenga Tanzania ya namna gani?
 
Duh, yaaani kumbe hali iko hivi? sijui ikulu itatoa press release ngapi hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu! haya yetu macho

Mkuu Eli
RWEYMAMU/S atatoa Press Release hata mia litatoa ili mradi kulinda kibarua chake ni moja ya jinga lilipewa fadhila na rais kwa kumsaidia kwenye uchaguzi
samahani kuwaita wote makenge Maana wana fadhila kama kenge
 
I wish jamaa wa wikileaks wangetoa na ile ya uvumi wa Gen. Abdurahman Shimbo .

muda ukifika utaiona tu mkuu kuwas mpole kijana akurupuki anafanya uchunguzi yakinifu kwanza ajue alizipataje sio tu kujua kiasi mpwa
usiache kuendelea kutembelea mtandao wwetu wa kila siku w..........l...................s
 
Kwa nini Kapuya "mtiifu" naye baadaye akaondolewa wizara hii na kisha kutupwa kabisa nje ya Cabinet?
 
Binafsi naona kuwa hakuina haja ya kujibu,

Watasema nini wakati hawana majibu....Bora wakae kimya kwa sababu wale 80% wanaopeperushwa na upepo hawatajua!!
 
Comment: An Easy Calculation
-----------------------------
The Kikwete administration finds itself in a
difficult position: President Kikwete publicly committed to
peacekeeping training but is being blatantly hamstrung by his
own Chief of Defence Forces. Yet President Kikwete has made
an easy calculation, which we, in fact, agree with. The cost
of waiting 12 weeks until General Waitara retires appears a
small price to pay compared to open confrontation with
Tanzania's most senior military officer whose attitude is,
"ACOTA over my dead body."
END COMMENT.
RETZER

My take:
Kwa nia njema kabisa nashauri Salva na timu yake Ikulu wavute pumzi ya nguvu (deep breath) kabla hawajatoa ufafanuzi kwenye haya madai ya Wikileaks na waepuke kutoa majibu ya jazba kama yale ya shopping za suti. Nasema hivyo kwa sababu kwa jinsi mambo yanavyozidi kufumuka kupitia Wikileaks, Rais wetu anaonekana kama 'ameajiriwa' na serikali ya Marekani.

Haya madai kwamba alikuwa anasubiri Waitara 'astaafu' ndio aweze kufanyia kazi matakwa ya wamerakani kama ni kweli italeta picha mbaya sana kwa ofisi ya rais kama 'taasisi' na kwa Tanzania yote. Na pia madai kuwa Prof Kapuya (wakati huo akiwa Waziri wa Ulinzi) anaomba msamaha kwa sababu wanashindwa kufanya kama wamarekani wanavyotaka na kwa muda waliokuwa wanatarajiwa kwa sababu Waitara aligoma kama kweli nayo ni fedheha kubwa kwa nchi.

Nirudie, Ikulu wajipange vizuri na waelewe ni nini hasa tasfiri ya haya madai ya Wikileaks kabla hawajatoa Press Release nyingine. Hii imekaa vibaya mno kuliko ile ya suti maana inaongelea mambo ya ulinzi wa nchi na hivi majuzi ndege ya kivita ya Qartar imetua, ikapakia wanyama na kuondoka zake na Wizara ya ulinzi wamekaa kimya hadi sasa. Na swali ambalo inabidi wawe nalo kichwani wakati wanaandaa majibu ni hili, 'how are safe as a nation?

Mambo mengine hata kuanza kuyafikiria ni aibu. Lakini pia yanatudokeza mambo mengine ambayo yameendelea baadaye. Kuna watu siku moja watatakiwa kujibu walipolifikisha taifa hili hapa.


Mnajua najaribu sana kuvumilia lakini mmejiuliza kwa nini INVISIBLE alifunga ile thread nyingine ya WIKILEAKS?

Couple of issues:

1. Mimi niko kwenye cable page ya 9 lakini kujua background ya maneno ya huyu balozi inabidi uzisome kwa makini hizi cables ndio utaelewa why wamarekani walikuwa hawampendi Waitara.

2. Kuna picha naipata kuwa wa Marekani of all state organs walikuwa wanapata tabu sana kudeal na watu wa Foreign na Mama Malamula in particular. Kule foreign walikuwa hawapewi blank cheques kama kwingine

3. Je mmesoma kwa nini hawa wamarekani walikuwa wana ngangania article 98?
 
nasikitika kusema kuanzia sasa, where my passport is not involved i will act up as a non tanzanian! najisikia aibu kuwa mtz kwa kweli. yaani kapuya wake zake na vimada wanajua hayakweli? kuwa anaenda kuomba radhi 'repeatedly'? nna bahati mweusi,manake blushing yake sijui ingekuwaje,dah!
 
Jama alivyosema mtoa mada ni kwamba ikulu wajipange vizuri na ametoa muda waje na hoja siyo mipasho na spelling error na sidhani kama mkuu wa majeshi ana kichaa hata kumkatalia amiri jeshi jambo muhimu kama lina masilahi kwa Taifa lakini kama halina masilahi kwa ila kinachoonekana alipuuzwa kwa masilahi ya wachache ambayo wanayajua wao wenyewe na kuhakikisha anastaafu ili wafanye wanavyotaka nataka tu kuwaambia hivi. KAMA HAWA WASTAAFU WAKIULIZWA KUNA MIKATABA MINGAPI AMBAYO WAMEIPGA CHINI KWA MASILAHI YA TAIFA NA WALIVYOONDOKA IMETIPITISHWA WANAOGOPA KUSEMA YASIJE KUWAKUTA YALIMKUTA DG. MSTAAFU KOMBE WANGESEMA MENGI SANA NA MASIKIO YANGETUWASHA.
 
uzuri wa uongozi wetu wa sasa hawapendi ku-address issues serious. za suti na kubembea ndo watajibu chapchap! they might nt be the foolish ones,rather labda sie ndo fools!
Binafsi naona kuwa hakuina haja ya kujibu,
Watasema nini wakati hawana majibu....Bora wakae kimya kwa sababu wale 80% wanaopeperushwa na upepo hawatajua!!
 
Kuna mapungufu makubwa sana ya 'thinkinig' katika safu ya political elite hapa nchini. Hii cable inaonesha ni jinsi gani wakubwa wanashindwa am kuungaisha dots au wamedhamiria kuwa 'darling' wa nchi zingine. Tanzania sasa hivi inapiganiwa na nchi za kadhaa zenye mrengo tofatuti. Lakini Marekani na Wachina na Canada ndio vinara wa kuchanja mbuga. Kupita American Peace Corps, hawa wakubwa wametuma utitiri wa watu wao. sasa hivi wako kila mahali, kuanzia Kigoma, mpaka Arusha. Mafunzo ya kijeshi nayo yanaendelea both marekani na wachina.

Na swali nilalojiuliza bila kupata jibu hata kidogo ni hili; viongozi wetu wanafanya haya yote kwa sababu wanataka kujenga Tanzania ya namna gani?

Haya yalikuwepo hata zama za Mwalimu JK na yeye akiwa ndie Muasisi wa mfumo huo,ambao ndio bora katika mbinu na mikakati ya kijeshi kwa Taifa hili kwa kuwa tungekuwa tunahudumiwa na Taifa moja kati ya hayo Mawili hakika kuhujumiwa ingekuwa lahisi sana.

Na kwa kuwa hatuna waatalamu wazuri wa kuanza kutayarisha mbinu na mikakati ya kuielimisha jamii katika lugha lahisi kuhusu mahusiano ya kimataifa ya kiulinzi na kiuslama huku waliopo wakijificha na kulazimisha jamii kuona maswala ya ulinzi wa nchi ni jukumu la wachache na kumbe ni jukumu la kila mwananchi wa Taifa hili.

Tunamataifa mengi sna tunayoshrikiana katika Ulinzi nyanja tofauti tofauti,na mikakati hiyo Tanzania katika swala la majeshi ya Ulinzi imebaki kuwa ni Nchi yenye kuaminika kwenye vikosi vyake.Yote hayao ni kwa sababu ya kuwa na mbinu na maarifa tofauti tofauti katika vikosi vyetu huku wanaofaidika ni Watanzania kwa kuwa wanapata technolojia toka pande mbili na nyingine nyingi za mahasimu wa mbinu za kijeshi kama China,Marekani, Russia, Cuba, Israel,Ufaransa, South Africa,Misri na Nchi Kadha wa Kadha.

Hivyo kukubali au kukataa kwa kiongozi husika ni swala tu la kimtazamo wa umuhimu au mahitaji ya wakati huo wa kipi kitangulie kwa kimikakati [Strategies Priorities] kwake. Je watangulie Wachina na kisha wengine wafuate au Watangulie Wamerikani kisha Wengine wafuate kwa hiyo kila kiongozi haswa katika huu mfumo wetu wa pilamid kuna kuwa na mambo kama hayo.

Pia hawa jamaa wote watatu yaani Marekani,China na Russia bado kijeshi huwa wanafanya lobbing kwa viongozi wetu wa kisiasa kukubalika sera zao za kijeshi kupewa support na Taifa letu.Kwa kuwa wanaimani kuwa wakipata support ya kijeshi na Taifa letu ni hakika na lahisi kwao kuwin kisiasa na kiuchumi katika kanda ya Afrika.

Kwa hilo hilo la Waitara na Kapuya ndio moja ya itikadi ya kikundi,japo historia nayo ya yaliopita kati ya mtu na mtu uzaa hisia na mitizamo ambayo kwa namna kubwa pia uchangia matokeo ya aina fulani ya kitu kipya ambacho ndio kinaweza kuwa kufanikisha au kushindwa kwake.Kama Mwalimu alivyopata kusema Serikali zitaendeshwa na binadamu na si malaika ambao Mungu anawashusha kuja kutuendesha hapa duniani.Migongano ya wakubwa mingine ikiwa imekaa zaidi kutofautina kitaaluma na kiitikadi ndiyo vitu vinavyozaa msuguano COI [Confrict of Interst] na hivyo kuzaliwa zana [thesis] mpya kulingana na nyakati na muda.

Kwa wanazuon waliopita chuo kikuu wanawajua watu kitivo ch Uhandisi haswa Jiolojia na Umeme jinsi wanavyokuwa na msuguano wa kitaaluma na kada nyingine za kitaaluma kwa kuziona kama ni kada za lelemalelema vile,uku wakiwa na kiburi cha kitaaluma kuwa wao ndio wasomi wenye kuumiza kichwa na hivyo hawa wengine ni wapiga polojo.Hivyo tafouti hizo zinapoingia katika uhalisia wa Maisha wale wa kada lelema lelema nao wana mchango wao mkubwa sana kwa mhandisi huyu katika kuweka sawa maisha yake kwa mustakabari wa life cycle.
 
Taarifa hii inaelea mno chanzo cha yote hayo ni nini waitara alikataaa nini na kwa nini madhara ni nini, manufaa ni nini na hasara ni nini uamuzi wa wa jk kumsubiri asitaafu kwa nini jeshi lingeasi au ulikuwa na maslahi binafsi tungependa kujua ila kwa sababu inagusa jeshi habari yake itaishia hapa mambo ya jeshi la watanzani hayajadiliwi na watanazania ni rahisi kuambiwa ukweli ukiwa mmarekani nakumbuka vizuri jibu la muheshimiwa waziri mkuu bungeni kuhusiana na meremeta.
 
Kwa nini Kapuya "mtiifu" naye baadaye akaondolewa wizara hii na kisha kutupwa kabisa nje ya Cabinet?
Ili mambo yaende vizuri lazima kufanya kazi kama timu na invyoonekana katika timu hii kulikuwa na mashauriano na mapendekezo ambayo kwa kawaida yule mhusika mkuu ambaye ni mkuu wa majeshi lazima ayatoe kabla ya kuukubali mpango wowote unaotaka kupitishwa na wakubwa wake kwa usalama wa Taifa kwanza ili asije kulaumiwa baadaye lakini inaonekana kama mapendekezo aliyoyatoa Waitara yalikuwa sawa na Kapuya alikubaliana naye ila alishindwa kuwa na msimamo zaidi tu ya kupewa maagizo na mkulu kwamba afuate lakini Waitara akagoma kwa kutumia uzoefu wake wa ndani na nje ya jeshi na kujua tabia halisi za wamarekani zikoje na alikuwa tayari kupoteza kazi yake lakini sidhani kama alhaji Akudo alikuwa tayari maana inanekana alikuwa mguu ndani mguu nje hajui afanye nini mpaka alivyopelekwa kutukanana na wakina Mgaya wa Tucta.
 
Of all the friends to choose, kweli tunawachagua wamarekani? Tena kwenye mambo ya jeshi!!! Gen Waitara knows better!! Hakutaka siku moja jina lake lisike kwamba ndio alifungulia mlango wa Taifa lenye nguvu kama lile ndani ya jeshi.
I hope sitamsikia mtu anakimbilia kutoa press release na kusema ni uongo maana mambo kama haya yanatutia aibu na kuonyesha ni jinsi gani tulivyo sasa hivi.
 
Nimeisoma hii topic vizuri sana, mi nipo tofauti kidogo na wachangiaji wengine. Ningependa kujua kwanini Waitara aligoma, na serikali ikaheshimu na kusema inasubiri kwanza astaafu then ndo program ianze. Kama mkuu wa majeshi amegoma, maana yake kuna sababu za msingi na bila shaka alizitoa na serikali ilimuelewa. Kinachonishangaza kama mtu ana sababu za msingi na amezitoa (Kama alifanya hivyo) na serikali kama serilkali akazielewa, kweli dawa yake ni kumsubiri huyo mkuu wa majeshi astaafu????

Hatuna uhakika kama CDF alitoa sababu za kusisitiza kuwa ni muhimu wakasaini Status of Forces Agreement (SOFA) kabla ya kuanza African Contingency Operations Training and Assistance (ACOTA). Inaonekana wamarekani walikuwa wakisisitiza kuwa sio lazima kusaini SOFA kabla ya kuanza mafunzo kitu ambacho CDF alikuwa hakubaliani nacho. Labda tujiulize kwa nini CDF aliona ni muhimu kuwa na makubaliano ya SOFA kabla ya kuanza utaratibu wa mafunzo wa ACOTA? Na kwa nini wamarekani walikuwa wanataka kuharakisha mafunzo kabla ya kusaini huo mkataba?
 
What goz araund kamz araund,hii ni faida ya siasa za magumash ambazo wanamtandao walizianzisha
ʞontɹact Sniper;2460673 said:
<b><font size="4">atakayeweza japo kuhisi ni kwanini haya yanaibuka sasa hivi........itabidi nimfahamu vizuri, na hakika huyo atakuwa ni......<br />
Just give a try and me will pm you....</font></b>if....
<br />
<br />
 
Back
Top Bottom