Phillemon Mikael
Platinum Member
- Nov 5, 2006
- 10,531
- 8,616
JF - BROKE NEWS OF THE BELOW APPOINTMENTS WHICH WENT INTO NEWS ..karibuni kwa uchambuzi....
Kikwete awapandishwa vyeo maofisa JWTZ
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 9th September 2011
AMIRI Jeshi Mkuu na Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete amewapandisha cheo maafisa wakuu 13 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), sita kutoka Brigedia Jenerali na kuwa Meja Jenerali huku wengine saba wakipandishwa kutoka Kanali na kuwa Brigedia Jenerali.
Kwa mujibu ya taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano, Makao Makuu ya Jeshi, Upanga, maofisa hao wamepandishwa vyeo kuanzia Septemba 2, mwaka huu. Waliopandishwa cheo kuwa Meja Jenerali ni pamoja na Leonard Elifariji Mndeme, Samwel Albert Ndomba, Paul Ignance Mella, Nicholas Fulko Miti, Hassan Vuai Chema na Salum Mustafa Kijuu.
Waliopandishwa cheo kutoka Kanali na kuwa Brigedia Jenerali ni Matata Mohamed Juma Mangwamba, Edwin Victor Milinga, Loth Peter Kilama, Emmanuel Edward Maganga, Josia Mwita Makere, Issa Suleiman Nassoro na Leila Chando.
Aidha, Rais Kikwete pia amemteua Kamanda Brigedi ya Nyuki - Zanzibar Meja Jenerali Kijuu kuwa Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu. Ofisa Mkuu huyo anashika nafasi iliyoachwa wazi na Meja Jenerali Wynejones Kisamba ambaye amepewa madaraka ya kuwa Naibu Kamanda wa Vikosi vya Umoja wa Mataifa nchini Sudan.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange amewavisha cheo Maafisa Wakuu hao kwa niaba ya Rais Kikwete. Wote wanabakia na madaraka yao isipokuwa kwa Meja Jenerali Salum Mustafa Kijuu
Kikwete awapandishwa vyeo maofisa JWTZ
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 9th September 2011
AMIRI Jeshi Mkuu na Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete amewapandisha cheo maafisa wakuu 13 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), sita kutoka Brigedia Jenerali na kuwa Meja Jenerali huku wengine saba wakipandishwa kutoka Kanali na kuwa Brigedia Jenerali.
Kwa mujibu ya taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano, Makao Makuu ya Jeshi, Upanga, maofisa hao wamepandishwa vyeo kuanzia Septemba 2, mwaka huu. Waliopandishwa cheo kuwa Meja Jenerali ni pamoja na Leonard Elifariji Mndeme, Samwel Albert Ndomba, Paul Ignance Mella, Nicholas Fulko Miti, Hassan Vuai Chema na Salum Mustafa Kijuu.
Waliopandishwa cheo kutoka Kanali na kuwa Brigedia Jenerali ni Matata Mohamed Juma Mangwamba, Edwin Victor Milinga, Loth Peter Kilama, Emmanuel Edward Maganga, Josia Mwita Makere, Issa Suleiman Nassoro na Leila Chando.
Aidha, Rais Kikwete pia amemteua Kamanda Brigedi ya Nyuki - Zanzibar Meja Jenerali Kijuu kuwa Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu. Ofisa Mkuu huyo anashika nafasi iliyoachwa wazi na Meja Jenerali Wynejones Kisamba ambaye amepewa madaraka ya kuwa Naibu Kamanda wa Vikosi vya Umoja wa Mataifa nchini Sudan.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange amewavisha cheo Maafisa Wakuu hao kwa niaba ya Rais Kikwete. Wote wanabakia na madaraka yao isipokuwa kwa Meja Jenerali Salum Mustafa Kijuu