Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
- Thread starter
- #41
Mzee wewe mkali
Lakini sijakubali
Mbona meliweka mbali
Swali langu la awali?
Kupenda sio hisia
Bado hujaniambia
Vipi linajisikia
Kisu kinapoingia?
Kupenda sio kuhisi
Ni tendo lenye kiasi
Lizukalo kwa wepesi
Kati ya wenye nafasi
Doriani lapendeza
Machoni linaliwaza
Hebu puani sogeza
Harufuye taiweza?
Moyoni utalipenda
Na mti utaupanda
Mwenyewe utajipinda
Hisia zitakushinda
Mwenye kula hujilamba
Sasa jibu naliomba
Mwenye kuliwa ni rumba
Au ni ngoma ya Pemba?
Nimetafuta majibu
Kuhusu hizo zabibu
Naona napata tabu
Kujalipata jawabu!
Labda yanapata raha
Pale ninapotafuna
Hakika siyo karaha
Yanaiva tunaona