Z - Anto: Bongo Fleva na maisha binafsi ngoma droo

minda

JF-Expert Member
Oct 2, 2009
1,068
65

(nb: these pics are links; kindly click them)
mwanzoni nilipomuona huyu selebu akitoa 'shooting' ya nguvu na sara 'binti kiziwi' [ kwenye wimbo maarufu wa 'binti kiziwi' alimshirikisha msanii pingu], nilidhani mchezo uliishia kwenye kupiga picha (shooting) ya wimbo huo maarufu uliowashika vibaya vijana wa tanzania.


Lakini kumbe z-anto na sara, mambo yakafuata ile kanuni ya “kazi na dawa” kulikopelekea huyu selebu kumbinafsisha huyo binti mwenye ulemavu wa kutosikia ( sio mlemavu tafadhali; ana ulemavu tu!).


Lakini cha sana mambo yakawa “easy come easy go”, mshkaji akamwaga wino huko bakwata (sio mahakama ya kadhi!!!). Ikumbukwe huyu z-anto ni ustaadh wa kutupwa!!!




khaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaahhhhh!!
sasa mshkaji ametoa 'singo' nyingine iitwayo kisiwa cha malavidavi ambapo imenenwa ya kuwa jamaa 'anamsomesha' tena huyo tausi kwa maneno laini kiaina na inavyosemekana ndege huyo ameshaanza kuelewa 'ishara zake' na kwa mujibu wa mtandao wa kizabizabina wa gpl, huyo binti yuko bize kumpigia simu mshkaji ili wamalizane wakalee familia; na hasa ikasemwa kwamba sababu kuu ni wimbo huo uliokopa maneno ya kihindi?




Sasa ninachoshangaa ni kwamba huyu z-anto akitoa wimbo basi tujue ndo hali halisi ya maisha yake?
Ama kweli kwake bongo fleva na maisha binafsi ni ngoma droo.
Lakini je, inashaurika kwa selebu ku-expose maisha yake kiasi hicho?
 
sasa si keshaoa .............au mke wa pili?

sijakuelewa hapo kidogo mkuu
 
sasa si keshaoa .............au mke wa pili?

sijakuelewa hapo kidogo mkuu



yaani alimuoa huyo aliyepiga naye shooting kisha baada ya muda akampa talaka.
sasa ametoa wimbo mpya huku akionekana kuomba msamaha.

scenario;

  • wimbo wa kwanza- 'binti kiziwi'
wakati anafanya shooting ya wimbo huu; dating na courtship ikawa hapo hapo wakaishia kuoana.
baada ya muda akampa talaka.



  • wimbo wa pili; 'Kisiwa cha malavidavi' unatamba kwa sasa kwenye vituo vya redio.
ikadaiwa kwamba katika wimbo huu ndio anaomba msamaha warudiane.
 
Msanii wa Bongo Flava Ally Mohamed ‘Z-Anto' ameibuka na kudai kuwa, aliyekuwa mke wake Sandra Khan ‘Binti kiziwi' amekuwa akimpigia simu akiomba warudiane, Hemed Kisanda anaripoti.

Akiongea na Amani Z-Anto alisema kuwa, tangu aliporejea kwenye gemu amekuwa akisumbuliwa na ‘x-wife' wake huyo akiomba wasahau yaliyopita wagange yajayo.

"Sina hakika na maisha anayoishi huko aliko sasa lakini ni mara nyingi amekuwa akinipigia simu kuomba turudiane kabla na hata baada ya kutoka kwa wimbo wangu unaotesa kwa sasa," alisema Z-Anto.

Baada ya Z-Anto kutoa habari hizi, Amani lilimwendea hewani Binti Kiziwi ili kusikia kutoka kwake ambapo alipopatikana alikiri kumpigia simu mumewe huyo wa zamani lakini kwa mazungumzo ya kawaida na si kumuomba warudiane.

"Ni kweli huwa nampigia mara kwa mara lakini sijawahi kumwambia turudiane, huwa tunazungumza kama marafiki wa kawaida," alisema Binti Kiziwi.

Hata hivyo mwisho wa mahojiano hayo Binti Kiziwi alisema kuwa, bado anampenda Z-Anto ingawa hakuweka wazi kama yupo tayari warudiane.


source: global publishers
 
Maisha Noma Ngoma ikivuma lazima itapasuka Z-Anto chali anaemea pua moja(source:Itafahamika remix) Binti kiziwi ameungana na shosti wake wa macau wapo nyuma ya nondo(behind bars)!! Z katoa cngo mpya ni nzuri ajirudi kwa OSATA(Wazee wa fitna) atatoka tena.
 
Back
Top Bottom