minda
JF-Expert Member
- Oct 2, 2009
- 1,068
- 65
(nb: these pics are links; kindly click them)
mwanzoni nilipomuona huyu selebu akitoa 'shooting' ya nguvu na sara 'binti kiziwi' [ kwenye wimbo maarufu wa 'binti kiziwi' alimshirikisha msanii pingu], nilidhani mchezo uliishia kwenye kupiga picha (shooting) ya wimbo huo maarufu uliowashika vibaya vijana wa tanzania.
Lakini kumbe z-anto na sara, mambo yakafuata ile kanuni ya kazi na dawa kulikopelekea huyu selebu kumbinafsisha huyo binti mwenye ulemavu wa kutosikia ( sio mlemavu tafadhali; ana ulemavu tu!).
Lakini cha sana mambo yakawa easy come easy go, mshkaji akamwaga wino huko bakwata (sio mahakama ya kadhi!!!). Ikumbukwe huyu z-anto ni ustaadh wa kutupwa!!!
khaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaahhhhh!!
sasa mshkaji ametoa 'singo' nyingine iitwayo kisiwa cha malavidavi ambapo imenenwa ya kuwa jamaa 'anamsomesha' tena huyo tausi kwa maneno laini kiaina na inavyosemekana ndege huyo ameshaanza kuelewa 'ishara zake' na kwa mujibu wa mtandao wa kizabizabina wa gpl, huyo binti yuko bize kumpigia simu mshkaji ili wamalizane wakalee familia; na hasa ikasemwa kwamba sababu kuu ni wimbo huo uliokopa maneno ya kihindi?
Sasa ninachoshangaa ni kwamba huyu z-anto akitoa wimbo basi tujue ndo hali halisi ya maisha yake?
Ama kweli kwake bongo fleva na maisha binafsi ni ngoma droo.
Lakini je, inashaurika kwa selebu ku-expose maisha yake kiasi hicho?