Yusuph Makamba: Tusimfundishe Rais Samia kufanya kazi, hatumtendei haki

kalacha mateo

Senior Member
Sep 27, 2021
118
237
Wakati serikali ya awamu ya sit chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu ikianza kuchukua hatua kutokana na mapungufu yaliyoainishwa katika ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)watu mbalimbali wametoa mitazamo yao ikiwemo Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuph Makamba anasema Rais Samia Suluhu asifundishwe kufanya kazi aachwe kwani tayari hatua alizochukua ni sahihi.

Ni vyema kumpa nafasi mkuu wa nchi afanye kazi, kwa kuwa hadi sasa kila mmoja ameona na kusikia kuhusu uwezo wake katika utendaji wa juu kwa namna anavyoisimamia serikali na nchi kwa utashi, usikivu na kuwa na uamuzi wenye tija kwa maslahi ya Taifa.

"Tusimfundishe namna ya kufanya kazi hatumtendei haki....niulize kwa haya yanayoendelea je kuna mwenye mashaka tena na uwezo wake hadi sasa? Rais Samia kwetu watanzania ni kiongozi bora anatosha na kwa CCM tunaamini ndicho chama bora, wakae watulie sasa.

"Muhimu tumuombee kwa kuwa ni kiongozi makini anayeamua mambo kwa busara, msikivu na anajua hapa niseme nini, nifanye nini, angeamua kukaa kimya kwa hii ripori kufanywaa kwa kificho tusingejua, lakini kutokana na uchungu alionao kwa nchi akiwa kiongozi anayejiamini ameweka wazi na anaendelea kuchukua hatua bila kumuonea mtu." -aliongezea Mzee Yusuph Makamba.

ccm-2-pic.jpg
 
Hivi kweli nyie watu mlikuwa hamjui kabisaaa kwamba fedha za Serikali zinaibiwa kila siku na karibu kila idara? Yaani mpaka mmeletewa report ya CAG ndio mnakuja kwa kushangaa? Halafu mnataka sijui Katiba Mpya, sijui mfumo! Hizi Sheria zitawasaidiaje ikiwa nyie wenyewe hamuoni wala hamjui kama mlikuwa mnaibiwa!
 
Mshamba huyu mzee hajui mama anasikiliza ushauri wa JF members at all ina maana mama akikubali ishu za ushoga tusimnange kwa maamuzi mabovu? Yeye atuache na yetu atukome kabisa aendelee kula asali atuche tuendelee kula masega na nyuku.
 
Ameona hii taja taja itamkumba mwanawe. Na kama samia atakuwa anasikia haya maneno na kuyafanyia kazi basi mwanawe hatokuwa salama.
 
Kumwambia Rais awashughulikie wezi sio kumfundisha kazi, ni kumkumbusha atimize wajibu wake kwasababu anaonekana amelala.

Huyu Makamba anataka Rais aachwe tu aendelee kuwatazama wezi, kwasababu inawezekana nae ni mnufaika wa huo wizi kwa namna moja au nyingine.
 
Back
Top Bottom