singidadodoma
JF-Expert Member
- Nov 11, 2013
- 4,394
- 1,531
Mwenyekiti wa club ya Yanga bwana Yusuf Manji amemtaka Mengi kuacha kumsakama na badala yake aendelee na shughuli zake, Manji anamtaka bwana Mengi kuacha kutumia vyombo vyake vya habari vya IPP kumsakama kwani yeye anamuheshimu kama babu yake.
Katika kipindi hicho kinachoendelea kurushwa live na TBC muda huu ambao Mengi alialikwa ili authibitishie umma ufisadi wa Manji lakini hakutokea, hata hivyo Manji amesema kuwa yupo tayari kipindi kama hicho kiandaliwe tena na Mengi aalikwe tena ili aje kuthibitisha madai yake.
Manji amesema kuwa ni kwa miaka kumi sasa amekuwa akindikwa vibaya na magazeti na vyombo vya habari vya IPP vya bwana Mengi, alifika mbali zaidi kuvishangaa vyombo vingine vya habari pamoja na kuwa mara nyingi amekuwa akiita vyombo vya habari kujibu shutuma hizo lakini anashangaa asubuhi hakuna hata chombo kimoja kinachoandika.
Manji pia ametangaza kugombea udiwani kata ya Mbagara Kuu.
Chanzo: TBC
Katika kipindi hicho kinachoendelea kurushwa live na TBC muda huu ambao Mengi alialikwa ili authibitishie umma ufisadi wa Manji lakini hakutokea, hata hivyo Manji amesema kuwa yupo tayari kipindi kama hicho kiandaliwe tena na Mengi aalikwe tena ili aje kuthibitisha madai yake.
Manji amesema kuwa ni kwa miaka kumi sasa amekuwa akindikwa vibaya na magazeti na vyombo vya habari vya IPP vya bwana Mengi, alifika mbali zaidi kuvishangaa vyombo vingine vya habari pamoja na kuwa mara nyingi amekuwa akiita vyombo vya habari kujibu shutuma hizo lakini anashangaa asubuhi hakuna hata chombo kimoja kinachoandika.
Manji pia ametangaza kugombea udiwani kata ya Mbagara Kuu.
Chanzo: TBC