comment 13 wanasema Spencer, mshirikina mmoja unasema Buhohela, haya wacha niendelee kuhesabu hizi kura na tarehe 25 mwendo ni huu huu.
Huyu Spencer Lameck anawauma sana CCM. Asante baba mwenye nyumba kwa kutuchagulia kijana machachari
Spencer lameck hana mpinzani
Nimefatilia kwa umakini, nikagundua kuna maripota wanastahili heshima kwenye kazi zao. Hawababaishi, wanaripoti habari na matukio ya kampeni kama yanavyotokea bila upendeleo au kuzidisha chumvi hasa wakati huu tukielekea Oktoba 25.
Naomba nitambue mchango wa Spencer Lameck wa ITV. Dogo yuko vizuri sana, anaripoti kile kinachotokea bila kupindisha ukweli. Kwangu mimi ndio ripota bora kabisa.
Mchumia tumbo tu huyo, fisadi kuiona ikulu ni ndoto ni kama mzinzi kuona ufalme wa Mungu, mtampambaa lkn muda utasema ukweli.