Idd Ninga
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 5,136
- 4,298
1.Kweli ulitupa tabu,tena tabu kubwa sana
Tabu zilo na sababu,hasa ulipo tuchana
Uliwasema vibabu,wazee hata vijana
Mapoti na mabawabu,uliwaponda mchana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
2.Sasa tutakula bata,kwa siasa kuachana
Ingawa ulitusuta,na matusi kutukana
Ukatupeleka puta,kwa mwendo wa kukazana
Na pengine tulijuta,kwanini tulijuana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
3.Hakika ulitutesa,na vichwa tukagongana
Mambo yetu kuyanasa,pale tulipolumbana
Ukafunua mikasa,visa vilofichikana
Sasa tutakupa visa,uje hatuto kubana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
4.Siasa uwache kweli,isiwe twataniana
Uje kuzamisha meli,tena tuanze chimbana
Useme kusema ngeli,haijui yule bwana
Hapo kusema ukweli,kifwatacho kuuwana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
5.Ukitaka kutusema,kwanza tuje ambiana
Tushituwane mapema,ili mambo fichiana
Tusije shindwa kuhema,mengine kuzibiana
Mwisho tuka kata pema,maneno kurushiana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
6.Umesha ule wakati,wakti wa kukimbizana
Sasa mipya mikakati,mwaka le tutaonana
Tuzifaidi chapati,na keki tulogawana
Ukikipata kibuti,twanze kwanza konyezana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
7.Dada na kwaga kwa heri,kwa kheri ya kuonana
Nakuacha u buheri,hakuna tena banana
Zile zahama na shari,sasa tutasikizana
Tupige tari zimari,tutakutana kabana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
SHAIRI-DADA KAACHA SIASA
MTUNZI-Idd Ninga,Tengeru Arusha
+255624010160
iddyallyninga@gmail.com
Tabu zilo na sababu,hasa ulipo tuchana
Uliwasema vibabu,wazee hata vijana
Mapoti na mabawabu,uliwaponda mchana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
2.Sasa tutakula bata,kwa siasa kuachana
Ingawa ulitusuta,na matusi kutukana
Ukatupeleka puta,kwa mwendo wa kukazana
Na pengine tulijuta,kwanini tulijuana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
3.Hakika ulitutesa,na vichwa tukagongana
Mambo yetu kuyanasa,pale tulipolumbana
Ukafunua mikasa,visa vilofichikana
Sasa tutakupa visa,uje hatuto kubana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
4.Siasa uwache kweli,isiwe twataniana
Uje kuzamisha meli,tena tuanze chimbana
Useme kusema ngeli,haijui yule bwana
Hapo kusema ukweli,kifwatacho kuuwana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
5.Ukitaka kutusema,kwanza tuje ambiana
Tushituwane mapema,ili mambo fichiana
Tusije shindwa kuhema,mengine kuzibiana
Mwisho tuka kata pema,maneno kurushiana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
6.Umesha ule wakati,wakti wa kukimbizana
Sasa mipya mikakati,mwaka le tutaonana
Tuzifaidi chapati,na keki tulogawana
Ukikipata kibuti,twanze kwanza konyezana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
7.Dada na kwaga kwa heri,kwa kheri ya kuonana
Nakuacha u buheri,hakuna tena banana
Zile zahama na shari,sasa tutasikizana
Tupige tari zimari,tutakutana kabana
Dada kuacha siasa,wazee tutapumua.
SHAIRI-DADA KAACHA SIASA
MTUNZI-Idd Ninga,Tengeru Arusha
+255624010160
iddyallyninga@gmail.com