Yu wapi Waziri William Lukuvi?!

MTK

JF-Expert Member
Apr 19, 2012
8,927
6,850
Ni muda sasa Waziri wetu wa Ardhi, Nyumba na Makazi hayuko mubashara, haonekani kwenye vyombo vya habari, hasikiki Anafanya Nini au nini kimemsibu Waziri Lukuvi?!

Binafsi nimeufuatilia utendaji kazi wake pale wizarani kipindi chote Cha nginjanginja za Mwendachato, alinikosha kwa kweli

Ni Waziri jasiri asiyependa kujipendekeza hata kwa JPM Jambo ambalo halikuwa la kawaida, mawaziri wengi wakiwemo kina Palamagamba Kabudi kufikia kutamka kwamba katolewa jalalani, Jaffo huyo ndio usiseme Ili mradi mawaziri wengi walikuwa ni mwendo wa kudemka tu.

Narudia Yu wapi Waziri Lukuvi?
 
Lukuvi alianza kupunguza kasi baada ya kuambiwa na "Mungu mdogo" kua hawezi kupewa uraisi amezeeka.hata kabudi pale ndo aligeuzia gia angani
Na huyu ndio anamtesa Mama na chochoko zake ndani ya Chama nadhani JPM hakuwa mnafiki yeye alikuwa akiletewe habari za ndani anawalipua tu hadharani kwa hili JPM nilikuwa nampendea, kuona mpaka siku ile JPM kamlipua basi ujuwe alikuwa na taarifa 100% na hili linamtesa huyu waziri maana sio 2025 tena itabidi asubiri 2030 ila Mama nadhani time ya kumpoteza huyu mtu ndani ya Chama ni hatari sana huyu jamaa.
 
Aisee huyu nimoja ya ma-state shriners wa ngazi za juu kabisa, alipata kusema 95% ya wazanzibari ni Waislam, mnataka watuletee serikali ya Kiislam Kule? ....waarabu watakuja kutusumbua ahahaha nkajua wazee wa ndevu watamuandama waapi kimyaaa!

Mtu hatari sana huyu,huwa anashirikiana na akina Membe, na kifaru mmoja hivi kupenyeza mambo yao. Mama wochit
 
Yeye sio parish worker, au unataka atoke nje aende sokoni kununua kunde na mtama ?

Yupo ofisini kwake anachapa kazi, yupo imara !
 
Bunge limeisha washughulikie Migogoro ya ardhi Kinondoni mwenye kustahili haki yake apate kama Rais alivyosema leo.

Kule Mbopo Waziri Lukuvi Mbona hamtoi ufumbuzi?

Cc: DC Gondwe

J. Gwajima (PM)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom